Tanzania na Uganda zapigwa marufuku na Ulaya kuendeleza Miradi ya Mafuta na Gesi

Tanzania na Uganda zapigwa marufuku na Ulaya kuendeleza Miradi ya Mafuta na Gesi

Sijui chochote,ila nauliza "hivi uaribifu wa mazingira unaathili vipi nchi za EU"?
Sioni sababu ya msingi ya Nchi za EU kupinga miradi wa Nchi nyingine.
Labda wangelijiondoa kwenye ufadhili kama upon,lakini sio kutumia kichaka Cha uaribifu wa Mazingira.
Huo ni ukoloni mamboleo.
 
Pamoja ya kuwa Mh. John Magufuli kumtumia mwanadiplomasia namba mbili Prof. Palamagamba Kabudi waziri wa mambo ya nje katika dili nyingi kimataifa za kibiashara ikiwemo korosho na bomba la mafuta, lakini imeshindikana.

Inabidi sasa serikali kutumia uzoefu wa kina Rostam Aziz, Juma Volter Mwapachu, Jumanne Kishimba , Omari Issa kutoa ushauri jinsi biashara na madili ya kimataifa yanavyofanikishwa badala ya kwenda kisiasa tu ktk madili haya.

View attachment 2358638
Picha : Rais wa benki ya Maendeleo Afrika-AfDB (kulia)Dr. Akinwumi "Akin" Adesina akiwa na mfanyabiashara Rostam Aziz


6 September 2019

Magufuli : Bomba liitwe Museveni Pipeline, sifurahishwi na ucheleweshaji


Rais John Magufuli amemshauri Rais wa Uganda Yoweri Museveni kuwa mkali kwa watendaji wake ambao wanakwamisha kuanza kwa mradi wa ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi kutoka Hoima Uganda mpaka Tanga Tanzania.

 
Hakuna Vita ya Uchumi duniani.
Tatizo letu Afrika ni kukosa msimamo unaoungwa mkono na Wananchi wetu.
Ni nani huku kwetu anayejua miradi inayofanyika huko Ulaya na athari zake kimazingira?
Jibu ni kwamba, hakuna.
Kama hatujui kinachofanyika kwao, kwa nini tunawasikiliza wanapozungumzia yanayofanyika kwetu?
Jibu ni moja tu. Hatujiamini.
Ni nini chanzo cha kutojiamini kwetu?
Umasikini na kukosa focus..yani kiufupi viongozi hawajui nini wanataka na niwaoga sana mbele ya mataifa makubwa..ila ni makatiri dhidi ya wananchi wao.

#MaendeleoHayanaChama
 
Hii inaashiria uchuro kwa miradi mikubwa inayoendelea.

Je tulifanya tathmini sahihi pia bwawa la JNHPP Stiegler's Gorge Rufiji, SGR Reli mpya, ATCL shirika la ndege n.k miradi ya matrilioni ya shilingi za kiTanzania au tutakwama njiani kama mradi huu wa EACOP Bomba la Mafuta Hoima - Tanga ?
 
Hii inaashiria uchuro kwa miradi mikubwa inayoendelea.

Je tulifanya tathmini sahihi pia bwawa la JNHPP Stiegler's Gorge Rufiji, SGR Reli mpya, ATCL shirika la ndege n.k miradi ya matrilioni ya shilingi za kiTanzania au tutakwama njiani kama mradi huu wa EACOP Bomba la Mafuta Hoima - Tanga ?
Mfano ATCL na SGR nayo inachafua mazingira?
 
Sijui chochote,ila nauliza "hivi uaribifu wa mazingira unaathili vipi nchi za EU"?
Sioni sababu ya msingi ya Nchi za EU kupinga miradi wa Nchi nyingine.
Labda wangelijiondoa kwenye ufadhili kama upon,lakini sio kutumia kichaka Cha uaribifu wa Mazingira.
Huo ni ukoloni mamboleo.
Africa tushakwama Hadi Sasa, nilitegemea baada ya 2020 pengine tutakua bara lenye uchumi mkubwa Ila ishashindikana.

Ulaya na Marekani Wana miradi ya kila aina yenye athari kubwa kwa mazingira kuliko miradi iliyopo Africa. Ila hakuna wa kusema chochote.

Bomba Kama hili huko ulaya yapo mengi yenye miles kubwa ila wote tupo kimya
 
27 November 2021

January Makamba - Mradi wa bomba la mafuta UGANDA-TANZANIA , kazi imeanza

Wadau waelezea matumaini makubwa juu ya faida za kiuchumi zitakazomiminika Tanzania na Uganda. Mnyororo wa faida wa mradi huu wa bomba la mafuta ghafi utakuwa na mguso mpana sana kwa nchi zote mbili bila kusahau wananchi wake pia.
Source : wasafi media
 
Mavi yake!! Angewajibu kwani yeye ndiye mwenye mafuta? Huyu Magufuli mnamu over estimate sana. Alikuwa pimbi tu na asingefanya lolote.

Alishindwa kuuza korosho kupitia TPDF mpaka sasa kuna baadhi hawajalipwa ndiyo mnafananisha na mafuta??
Uzi mzima umetafuta alipotajwa Magufuli. ***** mpaka ujifungue mwaka, nasemaje kunya boga Kama umechukia.
Pumbafffff zako
 
Mfano ATCL na SGR nayo inachafua mazingira?

Hapo ni kuangazia je ilikuwa sahihi kutumbukiza fedha nyingi ktk miradi hiyo au itakata roho kama mradi huu wa bomba la mafuta ghafi hivyo nchi kupoteza fedha nyingi mno kutokana na kutofanyika upembuzi yakinifu wa kutosha kama ambavyo sasa tunaona kupuuziwa suala la mazingira kumesababisha mradi kuyumba na pengine hasara kubwa.

Soma zaidi : MRADI WA SGR RELI

 
Hapo ni kuangazia je ilikuwa sahihi kutumbukiza fedha nyingi ktk miradi hiyo au itakata roho kama mradi huu wa bomba la mafuta ghafi hivyo nchi kupoteza fedha nyingi mno kutokana na kutofanyika upembuzi yakinifu wa kutosha kama ambavyo sasa tunaona kupuuziwa suala la mazingira kumesababisha mradi kuyumba na pengine hasara kubwa.

Soma zaidi : MRADI WA SGR RELI

Kuwa na akili basi, Reli inajengwa kwa phase. Ni Kama ilivyo mwendokasi, kaanza nayo kikwete, kaja, Magufuli na Sasa anayo mama Samia.

Ulitaka reli kutoka Dar, Dom, Tabora, kigoma, mwanza, Kahama ijengwe ndani ya mwaka mmoja??

Huwa mnatumia nini kufikiria?

Mkienda Dubai kupiga picha kwenye flyovers na burj khalifa mnaona raha. Kuna watanzania ni wapumbavu mmoja wapo ni wewe. Nchi haiweze kuendelea bila miradi.
 
Africa tushakwama Hadi Sasa, nilitegemea baada ya 2020 pengine tutakua bara lenye uchumi mkubwa Ila ishashindikana.

Ulaya na Marekani Wana miradi ya kila aina yenye athari kubwa kwa mazingira kuliko miradi iliyopo Africa. Ila hakuna wa kusema chochote.

Bomba Kama hili huko ulaya yapo mengi yenye miles kubwa ila wote tupo kimya

Wao mabeberu huko ulaya, marekani ya kaskazini, China , Korea ya Kusini na Australia wanajitegemee kwa fedha, utaalamu, mitambo, vifaa, kuyeyusha chuma na kikubwa ujuzi.

Tatizo sisi mfano mradi huu fedha mkopo toka huko kwa mabeberu, utaalamu pia ujuzi tunawaajiri mabeberu maana hatuna vitu hivyo, mabomba yanatengenezwa huko kwa mabeberu sisi tunasubiri kuelekezwa jinsi ya kuchomelea mabomba n.k n.k

Hilo ndilo tatizo la nchi za kiAfrika wakati wa kuanzisha miradi mikubwa.
 
Salaam Wakuu,

Bunge la Umoja wa Ulaya limeazimia Azimio linalozitaka Tanzania na Uganda kusitisha mara moja uendelezaji wa Miradi ya mafuta na Gesi katika Ukanda wa Afrika Mashariki.

Wanadai miradi hiyo inaharibu mazingira.

Wakati Bunge la Tanzania likiwa kimya, Bunge la Uganda limelaani azimio hilo walilodai ni kiwango cha juu cha Ukoloni Mamboleo na ubeberu dhidi ya Uhuru wa Uganda na Tanzania.

View attachment 2358292

Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) kutoka Kabaale – Hoima Nchini Uganda kwenda kwenye peninsula ya Chongoleani Mkoani Tanga Nchini Tanzania, ni Mradi wenye urefu wa jumla ya kilomita 1443 kati ya hizo kilomita 296 zipo Uganda na kilomita 1147 zipo Tanzania.

Bomba linapita katika mikoa 8 ya Tanzania Bara ambayo ni Kagera, Geita, Shinyanga, Tabora, Singida, Dodoma, Manyara na Tanga, vilevile linapita katika wilaya 24, kata 134 na vijiji zaidi ya 180.

Matokeo ya utafiti uliofanywa na kampuni za kimataifa za utafutaji na uchimbaji wa mafuta na gesi za TOTAL, TULLOW na CNOOC ulibaini uwepo wa mafuta ghafi takribani mapipa bilioni 6.5. Kutokana na ugunduzi huo imebainika uwezekano wa kuvuna mapipa kati ya bilioni 1.2 hadi 1.7. Kutokana na mahusiano ya ushirikiano ya muda mrefu na faida za kupitisha bomba nchini Tanzania Serikali ya Uganda na wawekezaji wa mkondo wa juu waliamua kujenga mradi huu kupitia Tanzania kutoka Hoima Uganda hadi Bandari ya Tanga.

Lengo la Mradi
Lengo la mradi huu ni kuwezesha mafuta yatakayozalishwa Uganda kusambazwa katika soko la ndani na sehemu inayobaki kuuzwa nje kwenye soko la kimataifa kupitia bomba la mafuta.

Gharama za kukamilisha ujenzi wa mradi wa bomba zinatarajia kufikia takribani Shilingi Trilioni 8 za Kitanzania. Bomba hili lilitarajiwa kujengwa na kuendeshwa na kampuni za TOTAL ya Ufaransa, CNOOC ya China na TULLOW ya Uingereza, kwa ubia na Kampuni ya Taifa ya Mafuta ya Uganda (UNOC) na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).
Huku wanatudai pesa zao,wakatulazimisha tuweke tozo Ili tulipe madeni!sasa wametoa hiyo,tukigoma hawatupi mikopo!!hapa shangazi wa ccm macho yatazidi kurembua kama amekula kungu gunia Zima.
 
Kwani mazingira yakiharibika si ya kwetu kwani yao???mbona urusi anabomba la mafuta refu linafika hadi ujerumani huko na walikua kimya,,,hapa lengo lao ni kuidumaza Africa tuendelee kuwategemea,,,hawataki kabisa Africa iendelee!
 
Pamoja ya kuwa Mh. John Magufuli kumtumia mwanadiplomasia namba mbili Prof. Palamagamba Kabudi waziri wa mambo ya nje katika dili nyingi kimataifa za kibiashara ikiwemo korosho na bomba la mafuta, lakini imeshindikana.

Inabidi sasa serikali kutumia uzoefu wa kina Rostam Aziz, Juma Volter Mwapachu, Jumanne Kishimba , Omari Issa kutoa ushauri jinsi biashara na madili ya kimataifa yanavyofanikishwa badala ya kwenda kisiasa tu ktk madili haya.

View attachment 2358638
Picha : Rais wa benki ya Maendeleo Afrika-AfDB (kulia)Dr. Akinwumi "Akin" Adesina akiwa na mfanyabiashara Rostam Aziz

Hayo ndiyo maneno. Kazi za wataalamu zifanywe na wataalamu tu.

Watanzania walikuwa wanapenda kusikia tu Domo la Magufuli likiropoka huku athari zikiwarudia wao wenyewe bila kujua. Nchi Ina wajinga wengi
 
Mama anafungua nchi. Kwa Fitna za Kenya utasikia Mradi umepangwa kupitia Kenya ili kulinda mazingira. #mama anafungua nchi.
Sasa Mama anausika nini hapo wakati mradi ni wa Uganda?
 
Back
Top Bottom