Nikiwa kwetu kasulu-BUHA sijuwahi kujua utani ni nini. Siku moja bana nikiwa dsm ukatokea musiba, aliyefariki muha, watani wakaja mfipa tena mwanamke na mkurya mmoja. Wacha waanze kuponda, eti ninyi waha mimi siwaelewi. Leo mnachanga hapa hata hela inayotakiwa haijatimia, kama hamjajiandaa si mngetoa matunzo na matibabu kwa marehemu? Mkurya na mfipa wakatangaza hakuna kuchimba hadi tupate hela yote iliyohitajika. Tulijichanga wala haikufika, ili shughuli ziendelee ilibidi tumfunge kamba mkurya, yule mama wa kifipa yeye tulimdhibiti.
Nikauliza, kwa nini wanafanya hivi, nikajibiwa ni watani na musiba wa juzi tuliwamwagia maji wakiwa wamelala