Tanzania National Identities (Vitambulisho vya Taifa)

Tanzania National Identities (Vitambulisho vya Taifa)

Ndugu yangu Nungwi nimekusoma na sipati shida sasa kuelwa kwamba kumbe wewe ni wakala wa nani. Kinachonisikitisha tena na kule kuendelea kuishushia hadhi JF. Mimi hoja yangu ni rahisi sana: Kwamba hakuna chcochote kinachounga mkono hoja ya kugombea vitambulisho na majadala wako hapa umedhihirisha kwamba hapa vita siyo ID ni urais na ndiyo maana sasa umeamua kuwa wazi kueleza kwamba Membe hafai kuwa rais na kwa nini. Lakini huko ni kupoteza muda bure kujadili kitu ambacho yeye mwenyewe amekwishasema kwamba hana mpango nacho. Whether sababu za kusema hana mpango nacho ni sababu ulizzotoa au sababu nyingine hatujui lakini ni vema ukajua kwamba unapigia kelele na unakerwa na kitu ambacho yeye si mshindani.

Ndugu yangu naomba nikuarifu kwamba fikra kwamba Mbopo ni Membe ni case ya mistaken identity. Mbopo ni Mbopo na wala si Membe na kwa hiyo kama wewe una ugomvi naye basi unayemtukana humu si Membe. Narudia tena kwamba hoja na tuhuma za ugomvi wa ID ilichochewa na hofu ya urais tu na si vinginevyo. lakini pia ninaomba nikuonye hapa kwamba wewe kama mtu msomi na mwenye utashi kwamba hoja haiwi bora kwa kumtukana mtu au kumvunjia mtu heshiam yake. Mimi kama mfuatiliaji wa mijadala mbalimbali ya JF nimeona kwamba hoja zilizoshinda ni zile ambazo mijadala yake ilikuwa ya kistaarabu na yenye ushahidi makini na si kukurupuka kwa ajili ya kulipa deni ya kutumiwa kama mpambe. Simfahamu sana Membe na sihitaji yeye kunifahamu kuweza kujua kwamba hapa anpigwa vita kwa vitu visivyo vyake.Kwanza hata huo mradi wenyewe kandarasi yake haijatolewa.

Ndugu yangu, mimi nakushauri ufuate mfano wa watu kama mwanakijiji ambaye hushusha hoja zake bils jazba na huchukua muda kutafiti kila anachopanga kusema na ndiyo maana nyingi ya hoja zake huenda hata kwenye magazeti na kusisimua wasomaji. Ukweli unabaki palepale kwamba mzee unalazimisha hoja na kila anyejaribu kuwa objective kama mimi na Masatu tunakoga matusi na kashfa zako mzee. NARUDIA KUSEMA MZEE MMECHEMSHA NA SASA HOJA IKO WAZI, NI URAIS NA HOFU YA WALIOKUTUMA. LAKINI WAAMBIE WASIHOFU, MEMBE HAYUKO KWENYE RACE, WALALE TU VIZURI MZEE.


Matusi sidhani kwamba ni majibu ya hoja bali nayachukulia kama Ubabe ambao Sitta anatuletea Tanzania na baadhi ya wana CCM kama Ditopile mbabbe na analindwa na serikali ya Kibabe.

Mbopo naona na wewe umeingia katika mkumbo wa one on one attack ama majibizano na name calling . Mtoa hoja ama leta hoja ni GT. This guy huwa naamini ni smart sana . Narudia kuomba tena.

Popote ulipo GT jitokeze Mbopo kawaka na kutangaza ushindi .Hoja ni ID na fraud yake .Urais si hoja ila mawazo ya watu kama wanavyo zipata habari hizi .Hili ndilo kubwa hapa.

ID tunazitaka sana ama waache kila Mtanzania apewe PP ambazo tayari zipo si not a big deal lakini sasa mgogoro wa nani apewe tenda ama kaanza kuhangaika na tenda bado si issue ila issue itakuwa pale kwamba billions of money ya walala hoi.

Hilo ndilo nadhani limemsukuma GT kuleta hoja kuwa alert kwamba we are watching na kwangu si Urais wa Membe wala nini ila namna mwisho wa siku hizo ID zitakavyo tugharimu.

Now your part I think is over kwamba umesha tetea kwamba Membe hayuko katika huo mpango na Urais ni mawazo ya mtu . Let us now wait and see
 
Hapa Hakuna hoja kwani yote hapa yamejaa ni majungu tupu, mpaka sasa hakuna hata mmoja anaejua ukweli wa mambo, ni majungu tupu.

Hakuna tenda ya kutengeneza vitambulisho iliotangazwa bali iliowahi kutangazwa ni tenda ya consultant wa vitambulisho mwaka 2002, sasa kama mnadhani kuna anaefaa kufanya kazi hio mwambieni ajiandae kucompite
 
Bado sijafahamishwa hao Gotham wasifa wao ni upi? Wamefanya kazi gani ambazo zimewafanya washinde hiyo tenda? Hofu yangu ni kuwa kama consultants hawa mabwana au mabibi ndio watakao tayarisha hizo terms of reference zitakazotumika kumpata mkandarasi wa mradi!

Kama hawa ni bomu tumekwisha. Kama wana uwezo kweli basi watuondoe wasiwasi kwa kuuweka wazi.
 
Huyo GT alieanzisha hiki kitim tim kaingia mitini, tunaweza kuhitimisha kwa kusema hili ni jungu la kufungua mwaka na hapa hakuna kitu tunajadili speculations tu.

Bahati sasa tushajua kumbe issue sio ID bali ni kinyang'anyiro cha 2015!
 
Wasiingie mitini mchezo kwi kwi kwii. Nawe Nungwi..masikini ndio maana.....

Huwezi jujenga hoja bila names calling? jibu swali: Tupe jina la kampuni na wanahisa wake. La sivyo nyamaza au nami ninauwezo wa kwenda personal...
 
FD wewe na Mbopo wako ndio mtakao kimbia naona unataka kumponza MBOPO.

MBOPO mheshimiwa Lowassa amesemwa sana humu kwenye JF kuliko wewe.najua FD na Mbopo wote mmetoka chuo kisicho na hadhi Tz.

FD ulikaenda tena Canada mkawa na Mbopo mkamfanyia fitina Kitine.

Mbopo jiandae kujibu hoja usije kukimbia au kumpa kazi Assah Mwambene kuja hapa badala ya kufanya kazi ya wizara.

Mbopo hongera kwa kuchaguliwa mkuu wetu AU.

Kweli we mropokaji!, Humjui hata Mbopo ni nani unarukia rukia tu: This theory fits you exactly:

1 Nungwi (Ngw) is the quantity of stupidity in 1000 mature people who have lost 63.3% or (1-exp(-1)) of their reasoning power. The level of stupidity in a normal person is between 2 to 10 microNungwis and it is normally unnoticeable. People start showing abnormal behavior when their stupidity level reaches abot 100 microNungwis and it becames alarming when it reaches 1 milliNungwi. It is advised to stay away from whoever records stupidity level of above 1 milliNungwi. Sporadically people with stupidity levels of up to 1 full Nungwi have been observed but they are very rare, appearing once in about 100 years per continent.
 
Tz priotization ya vitu ni issue mtu akishaset percent zake anakomaa mradi uanze bila kujali kwamba tuna mambo ya msingi zaidi ya kudeal nayo.
To me whether jina limetajwa au la,i dont care mambo mengine yanauzi.

Uzalendo alikufa nao mwalimu waliobaki hawana ata uchungu na taifa maskini kama Tz
 
Ndugu yangu Nungwi nimekusoma na sipati shida sasa kuelwa kwamba kumbe wewe ni wakala wa nani. Kinachonisikitisha tena na kule kuendelea kuishushia hadhi JF. Mimi hoja yangu ni rahisi sana: Kwamba hakuna chcochote kinachounga mkono hoja ya kugombea vitambulisho na majadala wako hapa umedhihirisha kwamba hapa vita siyo ID ni urais na ndiyo maana sasa umeamua kuwa wazi kueleza kwamba Membe hafai kuwa rais na kwa nini. Lakini huko ni kupoteza muda bure kujadili kitu ambacho yeye mwenyewe amekwishasema kwamba hana mpango nacho. Whether sababu za kusema hana mpango nacho ni sababu ulizzotoa au sababu nyingine hatujui lakini ni vema ukajua kwamba unapigia kelele na unakerwa na kitu ambacho yeye si mshindani.

Ndugu yangu naomba nikuarifu kwamba fikra kwamba Mbopo ni Membe ni case ya mistaken identity. Mbopo ni Mbopo na wala si Membe na kwa hiyo kama wewe una ugomvi naye basi unayemtukana humu si Membe. Narudia tena kwamba hoja na tuhuma za ugomvi wa ID ilichochewa na hofu ya urais tu na si vinginevyo. lakini pia ninaomba nikuonye hapa kwamba wewe kama mtu msomi na mwenye utashi kwamba hoja haiwi bora kwa kumtukana mtu au kumvunjia mtu heshiam yake. Mimi kama mfuatiliaji wa mijadala mbalimbali ya JF nimeona kwamba hoja zilizoshinda ni zile ambazo mijadala yake ilikuwa ya kistaarabu na yenye ushahidi makini na si kukurupuka kwa ajili ya kulipa deni ya kutumiwa kama mpambe. Simfahamu sana Membe na sihitaji yeye kunifahamu kuweza kujua kwamba hapa anpigwa vita kwa vitu visivyo vyake.Kwanza hata huo mradi wenyewe kandarasi yake haijatolewa.

Ndugu yangu, mimi nakushauri ufuate mfano wa watu kama mwanakijiji ambaye hushusha hoja zake bils jazba na huchukua muda kutafiti kila anachopanga kusema na ndiyo maana nyingi ya hoja zake huenda hata kwenye magazeti na kusisimua wasomaji. Ukweli unabaki palepale kwamba mzee unalazimisha hoja na kila anyejaribu kuwa objective kama mimi na Masatu tunakoga matusi na kashfa zako mzee. NARUDIA KUSEMA MZEE MMECHEMSHA NA SASA HOJA IKO WAZI, NI URAIS NA HOFU YA WALIOKUTUMA. LAKINI WAAMBIE WASIHOFU, MEMBE HAYUKO KWENYE RACE, WALALE TU VIZURI MZEE.

Mheshimiwa Mbopo unajichanganya kuwa humjiu vizuri MEMBE, halafu unasema hawezi kugombea urais ina maana unamjua vizuri sana kiasi cha kumsemea moyo wake,unayajua ya moyoni mwake na future plans zake.

Nungwi hakuanzisha mjadala huu hivyo usiseme kuwa anatumiwa kwa ajili ya kukuzuia wewe kuwa rais, hivi wanaosemwa humu wote watakuwa marais 2015? MBOPO acha utoto?

Mbopo mwezi mtukufu wa Ramadhan bwana MEMBE alifuturisha na kuita wafanyabiashara toka mikoa yote na si waislamu. jee hiyo sio kampeni ya urais?

MBOPO unapata aibu kujibizana na watu humu GT humuwezi utaumia.
 
hii midanganyika kweri haifanyagagi mikazi. mumerifunguwa rikijiwe rakupishana humu kwenye hii mi ngamuzi sijuigi munayaitaga aje haya mafitu. simwendege kwenye maparaza ya kahawa.

munaumwa namiroho mukiwaonaga wanatengenezaga mipesa. simukatengenezege yenu badiri ya kukaaga kubishaga. si munapotezaga miwakati purepure. kwani yakitengesaga mifitamburisho si watawausiga na mutatowaga mipesa na mipesa watagawanaga na ire mifaransa.

kwani murifiki mitamburisho inatenegezwaga na mijani ya mugomba. rroo. siwatairetaga kutoka kwa mifaransa na mijerumani. murifikirigi wao watapataga mipesa mingimingi ni riasirimia tatu tu. rrooo,
 
Nachukua jembe naenda zangu kondeni kulima, Let me know wen its all over pls....
 
Ndugu washirika wa JF. Mimi ni msomaji mzuri na wa muda mrefu sana wa mtandao huu. Kwa kiasi kikubwa huwa navutiwa sana na michango mbali mbali inayotolewa na washirika wa JF kwani huwa inaleta changamoto ktk hoja zinazoendelea nyumbani.

Hivi karibuni kuna mshirika mmoja alituletea hoja kuhusu mradi wa vitambulisho vya uraia wa watanzania wenye kicha cha habari, "Membe na Lowassa Wagombania Mradi wa ID."

Watu wengi walitoa mchango wao wa mawazo kwa kile ambacho wao wanakiamini kuwa ni sahihi. Ghafla mjadala huu uligeuka toka kwenye dhana ya ufisadi ktk mradi, ukahamia kwenye siasa, na hasa ktk nafasi ya urais kwa muhula ujao.

Mimi nadhani ni mapema sana kuanza kujadili nafasi ya kiongozi wa juu ktk nchi wakati huyu aliyeko hajamaliza muda wake, lakini la msingi zaidi, ningependa kuwashauri ndugu zangu kuwa, tunapoletewa taarifa ya jambo fulani, ni vema tukalifanyia utafiti wa kutosha kabla hatujaliweka hadharani. Madhara ya kukurupuka na kuweka mambo ktk mtandao bila ya kuyafanyia utafiti wa kina yanatpunguzia hadhi iliyojengwa kwa muda mrefu sana.

Tunamuomba mtoa hoja atualetee jina la kampuni ya Membe anayodai imesajiliwa Marekani na kuongozwa na Mwikalo. Tayari Mwikalo kupitia mtandao wa Tanzanet amekanusha kumiliki kampuni yeyote hapa duniani, je mtoa hoja hii mbona hajaleta ushahidi wa hiyo kampuni?

Tahadhari: Tusikubali kutumiwa na viongozi wachache kuchafua majina ya watu kwa maslahi yao binafsi. Tulinde heshima ya JF kwa kuandika mambo ya ukweli kwa manufaa ya nchi yetu.

Assalam Alleykhum...
 
Ndugu washirika wa JF. Mimi ni msomaji mzuri na wa muda mrefu sana wa mtandao huu. Kwa kiasi kikubwa huwa navutiwa sana na michango mbali mbali inayotolewa na washirika wa JF kwani huwa inaleta changamoto ktk hoja zinazoendelea nyumbani.

Hivi karibuni kuna mshirika mmoja alituletea hoja kuhusu mradi wa vitambulisho vya uraia wa watanzania wenye kicha cha habari, "Membe na Lowassa Wagombania Mradi wa ID."

Watu wengi walitoa mchango wao wa mawazo kwa kile ambacho wao wanakiamini kuwa ni sahihi. Ghafla mjadala huu uligeuka toka kwenye dhana ya ufisadi ktk mradi, ukahamia kwenye siasa, na hasa ktk nafasi ya urais kwa muhula ujao.

Mimi nadhani ni mapema sana kuanza kujadili nafasi ya kiongozi wa juu ktk nchi wakati huyu aliyeko hajamaliza muda wake, lakini la msingi zaidi, ningependa kuwashauri ndugu zangu kuwa, tunapoletewa taarifa ya jambo fulani, ni vema tukalifanyia utafiti wa kutosha kabla hatujaliweka hadharani. Madhara ya kukurupuka na kuweka mambo ktk mtandao bila ya kuyafanyia utafiti wa kina yanatpunguzia hadhi iliyojengwa kwa muda mrefu sana.

Tunamuomba mtoa hoja atualetee jina la kampuni ya Membe anayodai imesajiliwa Marekani na kuongozwa na Mwikalo. Tayari Mwikalo kupitia mtandao wa Tanzanet amekanusha kumiliki kampuni yeyote hapa duniani, je mtoa hoja hii mbona hajaleta ushahidi wa hiyo kampuni?

Tahadhari: Tusikubali kutumiwa na viongozi wachache kuchafua majina ya watu kwa maslahi yao binafsi. Tulinde heshima ya JF kwa kuandika mambo ya ukweli kwa manufaa ya nchi yetu.

Assalam Alleykhum...

Huyu Mwikalo ndiye inabidi aje hapa na sio kukimbilia kwa huko kujieleza. Na pia usitumia jina la wingi kuwa Tusikubali maana hakuna maamuzi ya jumla hapa!
 
Nadhani tunachojadili hapa ni ufisadi na sio kujigeuza sie kuwa chombo cha sheria na kutoa hukumu.

Unaonaje kama tukimuomba mtoa hoja hiyo atuletee majina ya kampuni ya Lowassa na ya Membe/Mwikalo ili tuangalie kama kweli makampuni hayo yameorodheshwa ktk mchakato huo wa zabuni ya vitambulisho?

Maana tusipokuwa na ushahidi basi kila mmoja atakuja na stori zake za kusadikika na hivyo kupotosha ukweli
 
Ndugu washirika wa JF. Mimi ni msomaji mzuri na wa muda mrefu sana wa mtandao huu. Kwa kiasi kikubwa huwa navutiwa sana na michango mbali mbali inayotolewa na washirika wa JF kwani huwa inaleta changamoto ktk hoja zinazoendelea nyumbani.

Hivi karibuni kuna mshirika mmoja alituletea hoja kuhusu mradi wa vitambulisho vya uraia wa watanzania wenye kicha cha habari, "Membe na Lowassa Wagombania Mradi wa ID."

Watu wengi walitoa mchango wao wa mawazo kwa kile ambacho wao wanakiamini kuwa ni sahihi. Ghafla mjadala huu uligeuka toka kwenye dhana ya ufisadi ktk mradi, ukahamia kwenye siasa, na hasa ktk nafasi ya urais kwa muhula ujao.

Mimi nadhani ni mapema sana kuanza kujadili nafasi ya kiongozi wa juu ktk nchi wakati huyu aliyeko hajamaliza muda wake, lakini la
msingi zaidi, ningependa kuwashauri ndugu zangu kuwa, tunapoletewa taarifa ya jambo fulani, ni vema tukalifanyia utafiti wa kutosha kabla hatujaliweka hadharani. Madhara ya kukurupuka na kuweka mambo ktk mtandao bila ya kuyafanyia utafiti wa kina yanatpunguzia hadhi iliyojengwa kwa muda mrefu sana.

Tunamuomba mtoa hoja atualetee jina la kampuni ya Membe anayodai imesajiliwa Marekani na kuongozwa na Mwikalo. Tayari Mwikalo kupitia mtandao wa Tanzanet amekanusha kumiliki kampuni yeyote hapa duniani, je mtoa hoja hii mbona hajaleta ushahidi wa hiyo kampuni?

Tahadhari: Tusikubali kutumiwa na viongozi wachache kuchafua majina ya watu kwa maslahi yao binafsi. Tulinde heshima ya JF kwa kuandika mambo ya ukweli kwa manufaa ya nchi yetu.

Assalam Alleykhum...

Kinyaba karibu,

JK alianza pilika miaka zaidi ya kumi kabla ya wakati wenyewe so sitoshangazwa na Mh. Membe naye kuanza pilika sasa hivi.

Alafu inaonekana Mh. Membe anaingia hapa ama ana katask force kake kakumbrief kila kinacholenga MoF na yeye binafsi. Sie yetu macho.
 
Icadon,

Mwaka 1995 JK alijitumbukiza ktk kinyang'anyiro cha Urais, hivyo hakukuwa na kificho ktk harakati zake. Kwa kigezo hicho, mimi nadhani kama tunataka kuwa "fair" ni vema tukawajadili wale waliovuka mpaka ktk nafasi 3 za mwisho na kumfanya JK kuibuka mshindi kwa kishindo.

HAPA KAMA TUMEAMUA KUJADILI MAMBO YA SIASA ZA NYUMBANI, lakini naomba tusitoke nje ya mada yenyewe, "MEMBE NA LOWASSA WASHINDANIA MRADI WA ID" Hebu tujaribu kuwa makini kidogo na suala lenyewe kwanza, maana kwangu mimi nauchukulia mradi wa vitambulisho nauona kama ni "nyeti" sana
 
Nadhani tunachojadili hapa ni ufisadi na sio kujigeuza sie kuwa chombo cha sheria na kutoa hukumu. Unaonaje kama tukimuomba mtoa hoja hiyo atuletee majina ya kampuni ya Lowassa na ya Membe/Mwikalo ili tuangalie kama kweli makampuni hayo yameorodheshwa ktk mchakato huo wa zabuni ya vitambulisho? Maana tusipokuwa na ushahidi basi kila mmoja atakuja na stori zake za kusadikika na hivyo kupotosha ukweli

Unatumia sana wingi mkuu,

"Karibu sana jamvini" na chukua muda "kusoma" maoni ya watu uone kuwa ni wachache sana wanatumia wingi hapa. Simamia hoja zako mwenyewe na huyo Mwikalo inabidi aje hapa mwenyewe na sio kutuma wasemaji wake hapa!
 
Icadon,

Mwaka 1995 JK alijitumbukiza ktk kinyang'anyiro cha Urais, hivyo hakukuwa na kificho ktk harakati zake. Kwa kigezo hicho, mimi nadhani kama tunataka kuwa "fair" ni vema tukawajadili wale waliovuka mpaka ktk nafasi 3 za mwisho na kumfanya JK kuibuka mshindi kwa kishindo. HAPA KAMA TUMEAMUA KUJADILI MAMBO YA SIASA ZA NYUMBANI, lakini naomba tusitoke nje ya mada yenyewe, "MEMBE NA LOWASSA WASHINDANIA MRADI WA ID" Hebu tujaribu kuwa makini kidogo na suala lenyewe kwanza, maana kwangu mimi nauchukulia mradi wa vitambulisho nauona kama ni "nyeti" sana

Jambo la busara lingekuwa ni kutumia creteria waliyotumia Tume ya Uchaguzi kuwapa Digimarc tenda ya voters ID.
 
Ndugu washirika wa JF. Mimi ni msomaji mzuri na wa muda mrefu sana wa mtandao huu. Kwa kiasi kikubwa huwa navutiwa sana na michango mbali mbali inayotolewa na washirika wa JF kwani huwa inaleta changamoto ktk hoja zinazoendelea nyumbani.

Hivi karibuni kuna mshirika mmoja alituletea hoja kuhusu mradi wa vitambulisho vya uraia wa watanzania wenye kicha cha habari, "Membe na Lowassa Wagombania Mradi wa ID."

Watu wengi walitoa mchango wao wa mawazo kwa kile ambacho wao wanakiamini kuwa ni sahihi. Ghafla mjadala huu uligeuka toka kwenye dhana ya ufisadi ktk mradi, ukahamia kwenye siasa, na hasa ktk nafasi ya urais kwa muhula ujao.

Mimi nadhani ni mapema sana kuanza kujadili nafasi ya kiongozi wa juu ktk nchi wakati huyu aliyeko hajamaliza muda wake, lakini la msingi zaidi, ningependa kuwashauri ndugu zangu kuwa, tunapoletewa taarifa ya jambo fulani, ni vema tukalifanyia utafiti wa kutosha kabla hatujaliweka hadharani. Madhara ya kukurupuka na kuweka mambo ktk mtandao bila ya kuyafanyia utafiti wa kina yanatpunguzia hadhi iliyojengwa kwa muda mrefu sana.

Tunamuomba mtoa hoja atualetee jina la kampuni ya Membe anayodai imesajiliwa Marekani na kuongozwa na Mwikalo. Tayari Mwikalo kupitia mtandao wa Tanzanet amekanusha kumiliki kampuni yeyote hapa duniani, je mtoa hoja hii mbona hajaleta ushahidi wa hiyo kampuni?

Tahadhari: Tusikubali kutumiwa na viongozi wachache kuchafua majina ya watu kwa maslahi yao binafsi. Tulinde heshima ya JF kwa kuandika mambo ya ukweli kwa manufaa ya nchi yetu.

Assalam Alleykhum...

Kibvaba karibu sana . Nadhani kuna mahali umeguswa hadi kukaamua kujitoa hapa kusema kwa kuwa umekuwa miongoni mwa wasomaji tu.Sasa umeanza kwa kuhukumu kwamba mtoa hoja alikurupuka.

Ni kosa ila nakubaliana nawe kwamba Mwikalo kesha kanusha tena mara kadhaa na kwa taarifa nilizo nazo katoa hata pesa kama kutakuwa na ushahidi kapanda dau la dolla 200.Ni wakati sasa wa mtoa hoja kuja kusema kusema aliyo nayo. Siamini kama mtu mzima anaweza kukurupuka kama amavyo kurupuka Samwel Sitta kule kwenye genge lake Dodoma.

Hapa ni mahala makini na naamini GT is matter of time hawezi kuingia mtini ila anaweza kuwa kachelewa kuendeleza mjadala .
 
Nadhani kuna mgogoro kdogo wa lugha hapa. Wewe unapotuma ujumbe unategemea kusomwa na wengi, na sio mtu mmoja.

Suala hili linajadiliwa na watu wengi, sasa sidhani kama nitakuwa sahihi kujisemea mwenyewe tu. Hivi kuna tabu gani kwa mtoa hoja kutuletea majina ya hayo makampuni ya Lowassa na Membe/Mwikalo? Tatizo ni nini? Ni kweli alikuwa anataka kufichua ufisadi au alikuwa ana mambo yake na akataka kuyapitishia JF? Nasikia Mwikalo ametoa offer ya USD. 200 kwa mtu atakayemletea jina la kampuni yake hiyo, je mtoa hoja hazitamani hela hizo?

Mbona kaingia "mitini" bila kutuaga? Hapa ndipo ninapokuwa na mashaka na usahihi wa taarifa zake hizo. Kama hana basi ajitokeze aseme tu kuwa naye alidanganywa, aombe radhi kwaMwikalo basi yaishe, huo ndio uungwana jamani
 
Mjadala huu una muda ktk mtandao huu. Mtu anapotoa shutuma dhidi ya mtu mwingine huwa ninaamini kuwa ana ushahidi au vielelezo vya ushahidi wake. Ninachokiomba hapa ni jina la kampuni ya Mwikalo/ Membe na Lowassa.

Jamani hivi hata hili linahitaji kwenda darasani kweli? GT, nakuomba utuletee jina la kampuni ya Mwikalo/Membe iliyosajiliwa huko Marekani, na ukiweza tupe jina la kampuni ya Lowassa pia.
 
Back
Top Bottom