Tanzania National Identities (Vitambulisho vya Taifa)

Tanzania National Identities (Vitambulisho vya Taifa)

Sijaisoma hiyo hotuba ila kama ni kweli ninachokisoma kwenye magazeti ni sahihi kuwa rais amewapa mafisadi wa EPA muda mpaka tarehe 31 kurudisha fedha au kupelekwa mahakamani kwa sababu za haki za binadamu basi JK ni rais bomu kuliko wote waliopata kutokea Tanzania!!! double standards tupu! mafisadi wangapi wanapewa muda wa kurudisha fedha walizoiba? anapeleka ujumbe gani kwa wananchi katika vita dhidi ya rushwa? hii kali sijawahi kuisikia sehemu yeyote duniani.
 
JK is a joker!! sijawahi kusikia serious president ana negotiate na mafisadi!! haki za binadamu -upuuzi mtupu.
 
Amegusa kila eneo kadri alivyoweza na kwa kuzingatia mstakabali wa kisiasa kwa nchi yetu kwa sasa,

namuunga mkono.
 
asikudanganye mtu hotuba ilikuwa nzuri sana tena sana,hasa ukizingatia summary aliyotoa ya juhudi za kujenga barabara kuunganisha mikoa yote (na kuna tangible results) na juhudi za kupeleka umeme kila makao makuu ya wilaya nchi nzima.siku zote siri ya maendeleo ni kujenga infrastructure na kuacha wajasiriamali wawekeze kwa raha zao.halafu you could feel his sincerelity na utu wa kutotaka ku abuse powers.let us give credit where it is due na kwa hili la hotuba tumpe haki yake.

Bishanga hebu tupe hizo tangible results ambazo mwenzetu unaziona. Kama infrastructure aliahidi toka wakati wa kampeni lakini mpaka sasa hakuna kinachoendelea. Speed ya ujenzi wa barabara enzi za Mkapa zilikuwa ni nzuri lakini toka JK na serikali yake waiingie madarakani hamna kitu, ujenzi barabara unasuasua au umesimama.

Halafu kwa nini rais aseme watachukuliwa hatua baada ya miezi miwili, je ina maana baada ya miiezi hiyo miwili ndiyo watuhumiwa watakuwa na makosa? Je wakirudisha pesa ina maana watakuwa wamesalimika na uhujumu waliolifanyia Taifa?? Labda mwenzetu umenyweshwa maji ya bendera ndiyo sababu unatetea zidumu fikra sahii za mwenyekiti wa CCM.
 
Someni thread ya Hotyba Ya Jk Bungeni. Waliopost walikwa live na upupu alioongelea umechambuliwa fresh tu.
 
Kwakeli kwa hili Six nampa kumi, yale maneno yake japo mafupi lakini ujumbe wake ni mzito sana! JK unachezea shilingi wenye tundu la choo.., mwizi ni mwizi, iweje hawa wa EPA wawe wezi juu ya sheria?? Let them be where they deserve...
 
Nashukuru wapo ambao waliokuwa wameona kuwapeleka mahakamani ilikuwa njia ya kuwazawadia na wangetoka na kutamba baada ya kifungo kwa kuwa bado wangekuwa matajiri.

Hii inatosha kujua kwamba huna hoja hapa isipokuwa unaslazimisha upuuzi ambao hauna maana kabisa.
Labda utuambie kuwa umewasiliana na majaji na wamekuhakikishia kuwa hao mafisadi wa EPA wakishitakiwa hawatafungwa zaidi ya miaka miwili na kulipa faini si zaidi ya milioni tano!!!!
Lakini ukweli ni kuwa nyie(unaonekana nawewe umo??) wezi wa fedha za EPA mkifikishwa mahakamani ndipo mtakapoacha kuihujumu nchi hii.

Na kwa taarifa yako hao unaosema wanakubaliana na kutowapeleka mahakamani ndio njia bora ni wachache sana tena ni mafisadi wa akili na mawazo, mtu asiye fisadi wa akili hawezi kutetea kutoheshimu kanuni, taratibu na sheria hususan mahakama ambacho ndicho chombo pekee chenye mamlaka ya kutafsiri sheria kwa mujibu wa sheria na katiba.

Vibaka wakikwapua cheni, hereni, simu na mikoba ya akina dada wakachomwa moto mitaani, mnasimama kuwatetea eti wangepelekwa polisi ili wafikishwe mahakamani.Vibaka wenzao wakiiba BOT na serikali ikawakingia kifua
wasipelekwe mahakamani mnawatetea tena?

AMA KWA HAKIKA KIZAZI CHA UFISADI UTAKITAMBUA TU!!!!!
 
Hoja nzuri!!!!

2. Mwenye akili timamu yeyote anajua huyo aliyefaidika na EPA tayari choka mbaya. hii ni adhabu kubwa sana... kuliko ukimpeleka mtu gerezani... kwa miaka miwili au faini... mil. 5, ambazo huenda ndio ziko kwenye sheria kama adhabu... kumbuka sheria nyingi zina adhabu za juu..... jamaa wangeweka fedha zao kwenye Hisa mfano za NMB. wakitoka kifungo baada ya mwaka au miezi... kwa kuwa hawakutumia silaha misamaha mingi inge-apply kwao... wange-endelea kuwa mamilionea...

.


Sasa kwa mfano huyo mtu wa EPA alikuwa choka mbaya sana kabla inakuwaje.
Kwamba adhabu yake ni kumrudisha kwenye hali yake ya zamani,au sio?

Kwa hio wale wezi wa simu,vitumbua,kuku wanaosota jela kumbe walitakiwa warudishe na wasingefungwa?
Si tunasema hii nchi inatawaliwa kwa misingi ya sheria,mimi nilijua kwenye sheria mwizi ni mwizi tu.

Sasa,hawa jamaa wa EPA wanarudisha pesa walizochukua,bila interest.Sasa kama mtu alichukua mfano bilioni 10 akafanyia biashara,hata kama faida yake ni 10%,tayari anakuwa ametengeneza bilioni 1! Hapo kweli utasema umemfilisi? Acheni jama.....
 
Kuna mtu ana uthibithisho wa mali za watuhumiwa zilizochukuliwa na Serikali?
 
Date::8/21/2008
Spika Sitta ampa tahadhari Rais Kikwete kuhusu wahujumu uchumi

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Tanzania, Samuel Sitta, amemkumbusha Rais Kikwete kuwa wahujumu uchumi hawastahili kuneemeka kwa madai ya haki za binadamu.

Na Ramadhani Semtawa
Mwananchi

WAKATI Rais Jakaya Kikwete, akionyesha huruma kwa watuhumiwa ufisadi wa mabilioni ya shilingi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu (BoT), Spika wa Bunge Samuel Sitta, amemkumbusha kuwa ni makosa kusimamia haki za binadamu kwa wahujumu uchumi.

Spika alitoa kauli hiyo muda mfupi baada ya hotuba ya Rais Kikwete bungeni, ambayo pamoja na mambo mengine iliwapa ahueni mafisadi wa EPA kwa kuwaongezea muda wa kuzilipa hadi Oktoba 31, mwaka huu.

Baada ya hotuba ya rais, Spika alimtaka kuongeza ukali kidogo katika masuala ya rushwa na ufisadi na kwamba Bunge litasaidia kuiweka nchi sawa.

"Hongera sana mheshimiwa Rais, umetoa hotuba nzuri, tumesikia, kuna mambo ya msingi, kuna hili la utawala bora, ukiongeza ukali kidogo basi sisi wabunge tutakusaidia. Lakini, wakati mwingine haya mambo ya kuweka visingizio vya haki za binadamu kwa wahujumu uchumi, yanakwamisha maendeleo ya nchi," alisema Sitta huku Rais akitabasamu.

Spika Sitta alifafanua kwamba, wakati mwingine kushindwa kushughulikia wahujumu uchumi kwa kisingizio cha haki za binadamu hurudisha nyuma maendeleo ya nchi.

Alisema nchi za Asia Mashariki zimeweza kupiga hatua kutokana na kuwa makini katika masuala ya rushwa na kwamba kama zingeendekeza visingizio hivyo zisingefanikiwa.

Spika Sitta ambaye chini ya uongozi wake, Bunge limetoa maamuzi mazito dhidi ya uhujumu uchumi, ikiwemo mkataba wa umeme wa dharura kwa Kampuni ya Richmond, alisema kuwapo kwa ufisadi katika Mfuko wa Uagizaji Bidhaa nchini (ICF) ni ishara kwamba zinahitajika juhudi za kusafisha nchi.

Alisema hivi sasa mwananchi wa kawaida hawezi kuelewa akisikia eti wahujumu uchumi mabilionea hawakamatwi kwani kuwakamata ni vigumu.

Mh.Speaker aliamua kufanya hivyo baada ya kugundua kuwa JK hajafanya kile watanzania walichotarajia kusikia toka kwake.

Ukweli ni kwamba miongoni mwa mambo ya muhimu sana ambayo watanzania walitegemea JK ayazungumzie na kuyatolea maamuzi kwa manufaa yao ni suala la wizi wa EPA.

Cha kustaajabisha ni kuwa JK anawabembeleza wezi warudishe fedha zetu walizokwiba!!
Na pamoja na kupiga danadana kuwa amewaongezea kipindi kingine cha neema hadi october 31, sisi tunae tu hadi mwisho tujue JK ana maslahi gani ndani ya EPA?

Sio jambo la kawaida rais ashindwe kuwajali wapiga kura wake na kuwakumbatia wanyang'anyi!
 
Ni kama bado nangoja hotuba ya mkuu wa kaya vile, alichoongea 6 ni cha kupongeza, au ndio speed and standards?
 
Mh. Bishanga. Whether aliyoyasema ni kweli au sio kuna mambo ya muhimu hapa:
1. Raisi siyo msemaji mkuu wa serikali, tunataka afanye maamuzi.
- Kuhusiana na epa riport ya wakaguzi aliipata siku nyingi, mpaka leo hakuna uamuzi! By the way maamuzi yenyewe hayako within his will, kama ukaguzi umebaini majambo, then we have a court of law.
2. Speech kama ile haina hadhi ya president mara 3hrs
3. Kama si kipofu, basi hajui kusoma nyakati, la he hasn't played his cards well.
He needs to regain peoples confidence, i think he lost one big shot!

Mh. Bishanga suala la miundo mbinu na kwerekwere zingine ni majukumu yake ya kila siku si lazima tuyajue, we entrusted him with all resources to do that, by the way he has a minister to attend that staff. sidhani kama ilikuwa busara kuongea vitu trivial au obvious bungeni.

Kwa kweli sijaridhika kabisa.

Ushauri wangu kwa wote tunaompenda rais wetu, ikifika 2010 tumpigie makofi Prezda wetu, sio ya kampeni! ila kwamba Imetosha.
 
Hakika ni bora na heri Sita ndo angekuwa President wetu, uliona wapi rais mwenye dola anabaki kusikitika na kukosa cha kufanya wakati sheria na kanuni zinakuwepo kulingana na mazingira ya wakati huo.


Napata tabu sana namna nchi hii inavyopata waziri mkuu. Ingekuwa bomba sana wananchi wamchague Sitta leo hii hii awe waziri mkuu.

Mabadiliko ya katiba hayaepukiki!



.
 
Mkuu Kasheshe,

Usijiangushe kwa kutetea upuuzi huo wa kuwalinda mafisadi. Watu wanauliwa TZ kwa kuiba shilingi elfu moja, eti watu waliochota mabilioni wanapewa muda wa kuzirudisha?

Hapo sio sawa kabisa na najua hata CCM walio wengi wanaona sio sawa kabisa.

Haki ya binadamu iko kwa kila mtu, iko kwa wanafunzi wanaotaabika kwa kukosa posho zao, iko kwa watoto na akina mama wanaokufa kwa kukosa dawa. Tena hawa wanataabika sio kwa mapenzi yao, akitabika fisadi ambaye kwa tamaa yake aliamua kutuibia, sioni ubaya wake kabisa.

JK anajiangusha sana kwa kuendelea kuwalinda hawa majambazi, kinachotakiwa TZ sasa ni leadership lakini bahati mbaya JK kashindwa kabisa kutuongoza Watanzania kuelekea kwenye maendeleo ya maana.

Hata ukiangalia mapesa yote anayosema amemwaga kwenye sectors mbalimbali, ukweli ni kwamba mafanikio yake ni madogo mno. Kuna haja gani ya kumwaga pesa ambazo hata hujui kama kweli zinatumika ipasavyo?
 
Six maneno yake ya dk kama 10 yamezidi hotuba ya JK ya masaa 3. Ila wabunge wako bado wanafiki, eti wanaifagilia hotuba, sijui kwa lipi? Labda kwa sababu wameahidiwa posho zaidi. they are after maslah.
 
kwa maneno ya dakika tano aliyoyatoa spika yakuwa bora kuliko maneno ya rais ya karibia masaa manne!!!
 
Sipati picha kama tangu uhuru tungekuwa na viongozi wa sampuli ya Kikwete. Kwa hotuba yake ya jana amedhihirisha kuwa hana jipya na hafai kuwa kiongozi wa vita hivi dhidi ya ufisadi.

Hapa ndipo ninapokubaliana na watu wengine wasemao kuwa kwa Kikwete kushughulikia mafisadi na sawa na kukata tawi la mti uliokalia kwani yeye ni mafisadi wa nchi hii lao moja. Kuna usemi usemao UKITAKA KUMJUA MTU TAZAMA MARAFIKI ZAKE.

Hotuba ya rais ilisheheni porojo tupu bila hata kutoa maamuzi ya msingi juu ya masuala mbalimbali yanayolikabili taifa hususani EPA.
 
Sasa tungojee sokomoko kati ya 6 na wadau pinzani ndani ya SISIEM. Na huyu hawamuachi kipindi kijacho, wamegundua kimbembe cha kumpa kichaa rungu!
 
Kama ndiyo hayo, kweli kazi ipo!!!!! Na afadhali asihutubie kwa sababu hii itakuwa sawa na kung'ang'ania kuzoa maji yaliyomwagika! Nchi inayumba kama washauri ndio wanamshauri rais hivi! Labda anahotuba yake ataitoa mfukoni, siyo hiyo rasmi

NINI...Chunga sana kauli zako...
 
Kama ndiyo haya anayotaka kuzungumzia kweli
Je tukimwita ZeCommedy kuna tatizo
Hivi huyu President kwa akili yake nyepesi tu amabzo hakuna hata mtanzania mmoja ambaye hizo statistics hazimuingii hakilini yeye inakuwaje akubali jamani??

Lakini kwa Rais Kikwete sishangai mambo yake
Maana aliagiza kamati aliyounda kuchukua hatua za kisheria na pesa zirudishe, wao wakaja na riport vitu viwili tofauti na akapokea

Report yenyewe hata hajaisoma na kuona ndani yake kuna nini, anawapongeza kwa kazi ngumu na nzuri sana walioifanya

Hivyo kwa mtu kama huyu kwenda kuliutubia Bunge na watanzania wote kwa kupmba kama hizo si ajabu ndugu!!

anyway simkubali hata kidogo na nina mengi sana ya kumuelezea huyu mtu
tusubili hiyo kesho

jamani hili si fala tu..au mnasemaje!!
 
Back
Top Bottom