Tanzania National Identities (Vitambulisho vya Taifa)

Tanzania National Identities (Vitambulisho vya Taifa)

Kijakazi.....By the way utawatofautisha vipi na wale waTZ waliochanganya na wakenya..Waganda...Waburundi...Wanyarwanda....ambao wengine wamejaa mabenk hadi ......? maana wale uliowataja umewatofatutisha kwa Rangi zao.....!!!!

Pia inaonesha kuwa Hata mambo ya Kimataifa wewe yamekupiga Chenga..ni Juzi tu Kumekufanyika Mkutano MKUBWA juu ya UBAGUZI WA RANGI......labda googling utaona resolutions zake....!!!
 
kama hao wandugu ambao hawana asili ya Tanzania wameshakuwa rais wa Tanzania, kwa nini waanze kubaguliwa? Kumbuka ili kuupata uraia, aidha wamezaliwa hapa au waliamua kuukana uraia wao wa awali, sasa mtu mwenye mapenzi na Tanzania kiasi cha kuamua kuukana uraia wake wa awali kwa nini abuguliwe na kuonyeshwa kuwa si Mtanzania halisi?
 
Ndugu watanzania wenzangu kutokana na hali ya kwamba ktk nchi yetu sasa tunakaribia kuanza kutoa vitambulisho kitu ambacho mimi binafsi naona nicha muhimu sana kwetu kama nchi, nemekuwa na pendekezo moja ambalo nnaona ni lazima tulifwate ktk zoezi hili la utoaji wa vitambulisho nalo ni kwamba ni lazima tutoe vitambulisho tofauti kwa watu tofauti nikimaanisha kwa mfano watu ambao hawana asili ya Tanzania (waarabu, wahidi, wazungu, wasomali, n.k) tuwape vitambulisho tofauti na sisi wenye asili ya hapa nchini kwetu lengo ni kwamba kuweza mwishowe kutoa tofauti kati yetu sisi na wazaliwa wageni. Je sijui ninyi mna mawazo gani juu ya hilo...

ILLEGAL, Discrimination, Apartheid, Segregation.

Unaposema vitambulisho tofauti una maana gani?. Mi ninavyojua vitambulisho vyote vitakuwa tofauti, huwezi kufananisha kitambulisho chako na cha mwingine ni lazima vitakuwa tofauti kuanzia details zote (eg picture, date of birth, jina n.k) huo ndiyo utofauti. Kinachotofautisha ni data na si rangi wala ukubwa, hoja hii kidogo haijakamilika hebu idadavue ieleweke
 
Kijakazi ktk Mawazo ya Kibaguzi haya no.1....

Haya mawazo yako yalikuwepo wakati wa Tanganyika under MKOLONI...na yalifutwa chini ya Tanganyika Huru. Wakati hao ulio wataja walikuwa 1st Class citizen. na walikuwa na shule zao....

Kijakazi baada ya mawazo yako kufanyiwa kazi unataka nini next...?wawe na shule zao? maduka yao?...Masoko yao?....mitaa yao?

Tukimaliza hayo itabidi tuje 2nd Phase "Wakuja wote warudi kwao Mikoani" kila mmoja arudi Mkoani kwake...kwani mmekuja kuwanyonya wenyeji..."wazawa wa Dar es Salaam"...

Baada ya hapo itabidi tuvunje Muungano, maana wenzetu wa Zenj wao Mixing yao na rangi yao sijui utasemaje..."baada ya hapo tutarudi like Rwanda/Burundi tukiona wakuja hamuwezi kuondoka mijini kwetu...."...wataka twende Huku...?

Hivi ni nini hasa kinachokukera kuwaona watu wa sampuli uliotaja?
Kwanza sijui kwa ubaguzi unamaanisha nini, kama ubaguzi maana yake upendeleo kwetu sisi na watu wetu basi unaweza kuuiita hivyo kama unapendelea.

Hiyo hatua ya pili uliyoisema haiwezekani kwani hao watu wa mikoani ni watanzania asilia kwa hiyo tutakuwa na vitambulisho vya aina moja TOFAUTI na vitambulisho vya raia wenye asili ya nje kwa hiyo hoja ni batili! na ni sehemu kubwa ya propaganda inayoenezwa na watu wanaopenda kuendelea kutunyonya ndani ya nchi yetu na hayo madai nimekuwa nikiyasikia tangu nipo shule ya msingi

Hoja ya tatu kuhusu Unguja na Pemba au Zanzibar kama ulivyopendelea kupaita napo pia ni vizuri tungefanya hatua hiyo kwamba watu wenye asili ya kwetu tuwape vitambulisho sawa na na wenye asili ya kigeni tuwape vyao. Na hilo kwa maon yangi litakuwa limetatua sehemu kubwa sana ya tatizo lilopo huko!

Kwa kifupi ninachotaka kusema hapa ni kwamba hao watu woote unaowatetea hawana uchungu wowote na nchi yetu na popote pale wanapoonyesha uchungu ni pale wanaponufaika kwa hiyo ni zuga toto tuu, sasa swali langu ni kwamba ni kwanini watu ambao hawana uchungu na nchi yetu wawe na haki sawa na sisi? na ninaandika hivi sio kutoka hewani ni mambo tunayashuhudia kila siku hapa Tanzania ukitaka kuthibisha hili subiri siku ya uchaguzi halafu uangalie watu wanaojaribu kuondokea nchi za jirani kwa maana nyingine kukimbia karibu wote na ninaweza kusema wote sio watanzania asili bali ni wenye asilia ya nje.
 
Kijakazi.....By the way utawatofautisha vipi na wale waTZ waliochanganya na wakenya..Waganda...Waburundi...Wanyarwanda....ambao wengine wamejaa mabenk hadi ......? maana wale uliowataja umewatofatutisha kwa Rangi zao.....!!!!

Pia inaonesha kuwa Hata mambo ya Kimataifa wewe yamekupiga Chenga..ni Juzi tu Kumekufanyika Mkutano MKUBWA juu ya UBAGUZI WA RANGI......labda googling utaona resolutions zake....!!!
Ndio manake mambo ya kimataifa mimi siyajui na wala sihitaji kuyajua kwa maana linalomata hapa ni sisi na nchi yetu... kumbuka mimi sijaongelea Ubaguzi hapa bali UPENDELEO kwetu sisi.

Kuhusu hao wengine wakenya, burundi... hiyo sio ngumu sana kwani tutakuwa na vitambulisho kwa hiyo ili kupata kazi ni lazima uonyeshe kitambulisho chako, kwa hiyo ikitokea kama mkenya mkikuyu amezaliwa nchini kwetu hamna tabu atachukuliwa kama sisi kwani yupo kama sisi...
 
Ndio manake mambo ya kimataifa mimi siyajui na wala sihitaji kuyajua kwa maana linalomata hapa ni sisi na nchi yetu... kumbuka mimi sijaongelea Ubaguzi hapa bali UPENDELEO kwetu sisi.

Kuhusu hao wengine wakenya, burundi... hiyo sio ngumu sana kwani tutakuwa na vitambulisho kwa hiyo ili kupata kazi ni lazima uonyeshe kitambulisho chako, kwa hiyo ikitokea kama mkenya mkikuyu amezaliwa nchini kwetu hamna tabu atachukuliwa kama sisi kwani yupo kama sisi...

MKUU Kumbe mgumu kuelewa...ENDELEA NA UBAGUZI WAKO....NAFIKIRI KTK DINI YAKO UBAGUZI UMERUHUSIWA!!!!
 
Watanzania asilia ni kina nani?

Wahindi na Waarabu ambao babu zao waliokuja mika 200 ilopita wamezaliwa hapa hawjawahi kuvuka mipaka ya Tanzania kwenda nchi yeyote wao wako kwenye kundi gani?

Mtu mwenye ngozi Nyeusi kama ya waTanzania walio wengi na anaongea Kinyamwezi fasaha lakini asili yake ni Sudan au Morocco;alikuja hapa akiwa kijana wa miaka 23 baada ya vita kuu ya pili ya Dunia na ana wajuu na bado anakwenda kwao kuhiji kila mara huyu ni Mtanzania asilia?

Mtanzania asilia ndiyo nani?
 
Hivi kwani huu ufisadi wa vitambulisho bado unaendelea? mi nilidhani ulizimika kwa jinsi tulivo upigia kelele sana, tujuvyenu wajameni!
 
any progress?

nakumbuka nilipoanzisha hii thread nilishambuliwa ile kichizi

Pole sana GT, hakuna progress yote. Hili limegubikwa na ufisadi wa hali ya juu. Vitambulisho vya Taifa vitavyogharimu shilingi bilioni 200 wakati tuna vipaumbele vingi muhimu kuliko hili la vitambulisho.
 
Na Boniface Meena
Mwananchi
Jan/9/2010

RAIS Jakaya Kikwete ameingilia kati sakata lililoibua mjadala mkubwa mwaka jana la mradi wa vitambulisho vya taifa kwa kuagiza lishughulikiwe kwa haraka.

Kitendo cha Rais Kikwete kuingilia suala hilo kimetuliza kwa muda mzuka wa mbunge wa Kilindi (CCM), Beatrice Shellukindo, ambaye katika Bunge la mwaka jana alimpa miezi sita Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha kushughulikia suala hilo nyeti.

Shellukindo aliiambia Mwananchi kuwa uamuzi wa Kikwete umemfanya aamue kutowasilisha tena hoja binafsi ya kutokuwa na imani na Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha ambaye mbunge huyo alidai kuwa ndiye anayekwamisha mradi huo mkubwa wa vitambulisho vya taifa unaotarajiwa kuligharimu taifa takribani dola 160 milioni za Kimarekani.

Hata hivyo, Shellukindo alisema uamuzi wake wa kuwasilisha hoja hiyo utabaki palepale endapo agizo hilo la rais halitatekelezwa ipasavyo.

Mwaka jana, Shellukindo alidai kuwa alipanga kuwasilisha hoja hiyo, lakini Waziri Masha alimuwahi kwa kuahidi kuwa mradi wa vitambulisho ungeisha mwaka jana na hivyo kuamua kumpa miezi sita kukamilisha mradi huo, la sivyo ataendelea na hoja yake.

Kwa mahesabu ya haraka, Shellukindo alitakiwa kuwasilisha hoja hiyo katika Bunge la mwanzoni mwa mwaka huu.

Lakini jana, Shellukindo aliibuka na hoja mpya wakati alipoeleza kuwa ameamua kusitisha msimamo wake huo kwa muda baada ya rais kuingilia kati.

"Hilo suala nimekuwa nikilifuatilia na wakati wa kamati za Bunge tuliambiwa rais ameagiza suala hilo la vitambulisho vya taifa lifanyiwe kazi haraka," alisema Shellukindo.

"Nimefuatilia mwenyewe NIDA na wizarani na nimeona kazi inaendelea vizuri, lakini kama kutakuwa na kitu kimeenda tofauti, msimamo wangu utabaki palepale," alisema mbunge huyo machachari.

Alisema uchunguzi wake umebaini kuwa baada ya Rais Kikwete kutoa agizo hilo, mchakato wa vitambulisho vya taifa unaendelea vizuri na zabuni zinaendelea kushughulikiwa.

Masha anatuhumiwa kuchelewesha mradi huo kutokana na kudaiwa kuingilia mchakato wa zabuni kwa kuhoji sababu za kampuni ya Sagem Securite kuachwa kwenye hatua za awali na tuhuma kwamba kampuni ya ushauri wa kitaalamu ya Gotham International kupewa tena katika mazingira tata.

Kitendo cha Masha kinaelezewa kuwa ni kukiuka taratibu za Sheria ya Manunuzi ya Umma ya mwaka 2004.

Masha ameshakana tuhuma zote na pia kueleza kuwa alichofanya ni kutaka malalamiko ya kampuni zilizokuwa kwenye zabuni yasikilizwe.

Gotham International nayo ilijitokeza na kujitetea kwamba haikupendelewa wala kupata kazi hiyo katika mazingira tata.

Katika mahojiano na gazeti hili mjini Dodoma, Shellukindo ambaye alihoji ni lini mradi huo utakamilika, alisema hana tatizo na Waziri Masha, lakini msukumo wake mkubwa unalenga kuona mradi huo nyeti unakamilika.

Shellukindo alisema wakati huo mjini Dodoma kuwa Waziri Masha hawezi kukwepa lawama kwamba anakwamisha mradi huo, kwani hana sababu za msingi kuingilia mchakato wake wakati Sheria ya Manunuzi ya Umma haimtambui.

Kwa mujibu wa Shellukindo, kutokana na kuwa waziri mwenye dhamana, Masha hakupaswa kuingilia mchakato huo hasa baada ya kupitishwa na Baraza la Mawaziri, badala yake alitakiwa kupata maelezo kutoka kwa katibu mkuu wa wizara ambaye ndiye mwenyekiti wa mchakato.

Shellukindo alidai kuwa mgogoro unaogubika mchakato wa vitambulisho ni wa kimaslahi na kumtuhumu Waziri Masha kuwa angependa mzabuni aliyepatikana na kupitishwa na Baraza la Mawaziri, Gotham asifanye kazi hiyo.

"Yeye anasema haridhiki na Gotham wakati amepitishwa na baraza la mawaziri. Kuna hasara nyingi ambayo taifa linaweza kupata kwa kumuondoa Gotham: Anaweza kuweka kizuizi cha mradi huo mahakamani, kujitoa katika mikataba mingine yote na kuomba fidia kwa usumbufu," alieleza Shellukindo.
 
Wana JF,

Kama inavyotamkwa kuwa swala la Raia wa Tanzania wataanza kupata vitamburisho vya Uraia a.k.a Kipande mwishoni mwa mwaka huu, Ningelipenda kushauri katika kipindi hicho mtanzania nani raia(mwenye urai) wa Tanzania anye paswa kupewa kitamburisho apige sahihi ya kidole gumba cha mkono wa kushoto na kulia (Electronic finger print should be taken both left and right thumb).

Na wakati huu tukiwa twasubili hilo zoezi kutekerezwa napenda kuliomba Jeshi la Police lije na mikakati mipya ya kuanzisha Database system kwa ajiri ya storage ya izo records na itawasaidia kwa ajiri ya kuchunguza uharifu kwa kuchukua izo finger print na kuzitumia kuchunguza matukio mbalimbali ya uhalifu, pia waandaae Investigative tools and equipments eg Forensic Lab, Law Enforcement, na Police Department ijigawe katika vitengo maarumua kwa ajiri ya Crime Scene Investigation.

Maana Bila hivyo utasikia wizara ya mabo ya ndani imekuja na hoja nyingine bungeni ati wametenga Budget nyingine kabisaaaa ooh tulisaha wakati twatengeneza vitamburisho hatu ku introduce hii system ya finger print kwa Jeshi la Police kwa ajiri ya security yetu hawakawii kusema hayo.

Ni yaho tu.
Wana JF mwaweza pia toa maoni yenu.
 
vitamburisho, uharifu, kutekerezwa, kwa ajiri..... duh, tobaa!!!

mtazamo wangu ni kuwa, wanaosimamia hii project kwa sasa wanaangalia ku'print na kusambaza tu! Long-term goals/implications hazipo katika fikra, ili mradi watu wakusanye mabilioni yao watie mfukoni mambo mengine baadaye.
 
kwanini tusitumie pasport kama vitambulisho.Hii biashara ya vitambusho does not work.
 
Sijapata kuona watu wanaopenda makubwa kutokana na kipato chao kidog kama serikali ya Tanzania. Haya and then?

Wengine wamesha anza kutuletea nuksi hata kuja ma-holiday haya wenye nchi jifaidieni labda bwana KOBA aje hatuelezee faida zake hapa maana ni mshabiki maradufu wa hizi sera.
 

Kama inavyotamkwa kuwa swala la Raia wa Tanzania wataanza kupata vitamburisho vya Uraia a.k.a Kipande mwishoni mwa mwaka huu, Ningelipenda kushauri katika kipindi hicho mtanzania nani raia(mwenye urai) wa Tanzania anye paswa kupewa kitamburisho apige sahihi ya kidole gumba cha mkono wa kushoto na kulia (Electronic finger print should be taken both left and right thumb).

Na wakati huu tukiwa twasubili hilo zoezi kutekerezwa napenda kuliomba Jeshi la Police lije na mikakati mipya ya kuanzisha Database system kwa ajiri ya storage ya izo records na itawasaidia kwa ajiri ya kuchunguza uharifu kwa kuchukua izo finger print na kuzitumia kuchunguza matukio mbalimbali ya uhalifu, pia waandaae Investigative tools and equipments eg Forensic Lab, Law Enforcement, na Police Department ijigawe katika vitengo maarumua kwa ajiri ya Crime Scene Investigation. Maana Bila hivyo utasikia wizara ya mabo ya ndani imekuja na hoja nyingine bungeni ati wametenga Budget nyingine kabisaaaa ooh tulisaha wakati twatengeneza vitamburisho hatu ku introduce hii system ya finger print kwa Jeshi la Police kwa ajiri ya security yetu hawakawii kusema hayo.

Ni yaho tu.
Wana JF mwaweza pia toa maoni yenu.

ni wazo zuri tatizo utekelezaji wa hii serikali yetu na sio kwamba hawalijui hilo
 
kwanini tusitumie pasport kama vitambulisho.Hii biashara ya vitambusho does not work.

labda waanzishe utaratibu wa kuwapatia wananchi wote passport..........vinginevyo itakuwa ngumu, ni asilimia kidogo sana ya wananchi wa Tanzania wenye passport
 
Back
Top Bottom