Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Unataka lini nikuletee ushahidi wa Membe na kampuni yake?
Unataka lini nikuletee ushahidi wa Membe na kampuni yake?
Masatu naona umemkalia kidedea Mtalii...Hageuki...
Mtalii hatutaki tukuulize lini ushahidi uulete..ushahidi unahitaji studies, usikurupuke....Kaa chini tulia uweke mambo..
Akina Masatu watumishi wa serikali hichi kijiwe wakione Kibaya...
Vitambulisho vya Uraia bomu jingine
Mwandishi Wetu Machi 12, 2008
Raia Mwema
Tayari zimevutwa 200m/=
MRADI mkubwa wa vitambulisho vya Taifa uliomo mbioni kuanza ni kashfa nyingine mithili ya zile za kampuni hewa ya Richmond na EPA, Raia Mwema imeelezwa.
Mradi huo ulioanza kuzungumzwa miaka ya katikati ya 1970 na ambao utagharimu kiasi cha Sh. bilioni 250, unaelezwa kwamba umo katika hatua za mwisho za kutaka kutekelezwa japo taarifa zinaonyesha kwamba ni mpango mwingine mkubwa wa ulaji fedha za umma.
Shaka hiyo inatokana na ukweli kwamba tangu mwanzo mradi huo umesimamiwa na maofisa wa Serikali kutoka Wizara za Mambo ya Nje na Ofisi ya Rais (Utumishi) kama washauri na ambao sasa inaaminika tayari wamekwisha kulipwa kwa kazi yao hiyo.
Taarifa zinasema pia kwamba sasa washauri hao kutoka serikalini wamejipanga katika nafasi za asasi zitakazokuwa zikisimamia mradi huo.
Raia Mwema imefanikiwa kuona orodha ya washauri mbalimbali wa mradi huo ambao baadhi yao wako karibu na vigogo serikalini. Orodha ya washauri hao ni pamoja na Profesa Damas Muna, Jaffar Buyogera, John Kyaruzi, Dickson Maimu, Jack Gotham, Salum Mpugusi, Donald Carriere, Coen Kleinhans, Kenneth Roko, Robert Alexander, Balozi Richard Butler, Anthony Githua, Rama Mwikalo na Robert Stewart.
Baadhi ya nyaraka ambazo Raia Mwema imefanikiwa kuona zinaonyesha kwamba wazo la mradi huo lilidakwa na kampuni ya Gotham International ambayo iliingia ubia na kampuni ya FootPrint Africa Business Solutions ya Afrika Kusini na kwa pamoja zikaingia katika mkataba na Wizara ya Mambo ya Ndani wa kuzifanya kampuni hizo mbili kuwa meneja wa mradi baada ya kukamilisha kazi ya utafiti wa awali.
Inasema sehemu ya nyaraka hizo: Pande zote zilikuwa na mazungumzo mjini Dar es Salaam kati ya Novemba 13 na 18, 2004 kuelekea utekelezaji wa Mpango wa Vitambulisho vya Taifa kwa kipindi cha 2004 hadi 2014, kwa ajili ya utekelezaji wa mfumo, ilikubalika kwamba kundi la makampuni hayo liwe na jukumu la kuwa Washauri katika Menejimenti ya Mradi.
Kwamba timu ileile iliyoshiriki kutafiti uwezekano wa mradi kufanyika ndiyo inayopendekeza pia kuwa mameneja wa mradi, ni jambo ambalo limeufanya mradi wenyewe kuonekana dhahiri kuwa mpango mahususi wa ulaji.
Kinachotia shaka kingine, kwa mujibu wa takwimu, ni wigo wa mradi wenyewe. Inapendekezwa kwamba watakaopewa vitambulisho hivyo ni makundi ya umri kati ya miaka 0-14 ambao wanakadiriwa kuwa asilimia 44 ama watu 16, 174,387 ya kundi lote la raia wa Tanzania wanaokadiriwa kufikia milioni 37.
Kundi jingine ni la umri wa kati ya miaka 15-64, kiasi cha asilimia 53, wanaokadiriwa kuwa 19,629,729. Kuna pia kundi la miaka 65 na kuendelea, kiasi cha asilimia 2.6, wanaokadiriwa kufikia watu 962,240.
Wataalamu waliozungumza na Raia Mwema wanahoji upana wa wigo huo hasa katika kundi la kwanza kwamba kwa nini watoto ambao ndiyo kwanza wanazaliwa waingizwe katika mpango huu ilhali kimsingi ni bado tegemezi na hawawezi kuwa na kumbukumbu zote za kiuchumi au vinginevyo; achilia mbali kwamba hata kupiga kura au kufungua akaunti benki hawawezi.
Watafiti/mameneja wa mradi huo wanapendekeza kwamba vitambulisho aina ya smart card, ambavyo ni ghali, ndivyo vitumike.
Ni ughali huo ambao miaka ya nyuma ulisababisha wafadhili kadhaa kujitoa katika mradi baada ya kubaini kwamba huu haukuwa mradi halisi wa Taifa bali mradi wa watu wachache kuvuna fedha za umma.
Inafahamika kwamba nchi kama China, Korea na Sweden zilipata kuonyesha nia ya kutaka kuufadhili mradi huo lakini ikashindikana, hiyo ikiwa ni pamoja na Benki ya Dunia, kuuacha mradi sasa ukiamuliwa kutekelezwa kwa fedha za ndani ambazo kimsingi wafadhili hawawezi kuhoji matumizi yake.
Gharama za sasa za mradi huo zinakadiriwa kuwa Sh. bilioni 250 zikiwa zimekua kutoka Sh. 152 za makisio ya awali, ambazo zinakifanya kitambulisho hicho kuwa ghali kuliko hata vya nchi zilizoendelea kama Sweden,
Raia Mwema ina taarifa kwamba Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia aliyekuwa anamaliza muda wake mwaka jana, Judy OConnor wakati akiaga alihoji ughali wa vitambulisho hivyo na inaaminika kwamba ofisa mmoja mwandamizi wa Serikali, Mambo ya Ndani, wakati huo ambaye alikuwa na maslahi katika mradi alifoka akisema kama Benki ya Dunia inataka kujitoa ijitoe. Kweli Benki ya Dunia ikajitoa.
Kwa sababu ya mradi kuwa dhahiri wa fedha nyingi, mara kadhaa kumetokea migongano miongoni mwa wakubwa, kila mmoja akivutia upande wa kampuni yenye maslahi naye, huku wengine wakitaka mradi huo uendeshwe kwa uwazi kama ambavyo taratibu za Serikali zinataka.
Migongano ya aina hiyo imeripotiwa kujitokeza Wizara za Mambo ya Ndani, Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara ya Mambo ya Nje.
Aidha, Raia Mwema imetaarifiwa kwamba hitilafu nyingine, kama ilivyokuwa kwa mkataba wa ile kampuni hewa ya kufua umeme ya Richmond, ni kuwa mradi huu wa vitambulisho nao haukupita katika chekecheke la Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA).
Tangu mwaka 2004 zimekuwapo safari za vigogo kadhaa serikalini kwenda nje ambako wamekuwa wakikutana na kampuni za huko kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo.
Wakati hayo yakiwa hivyo, Mkurugenzi Msaidizi wa Uhamiaji, anayeshughulikia sheria, Magnus Ulungi, aliliambia Raia Mwema, juzi, kuwa Mradi wa Vitambulisho vya Taifa sasa umeanza kutekelezwa, na kwa kuanzia tayari Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mradi ameteuliwa.
Suala la vitambulisho vya Taifa sasa liko kwenye process (mchakato) tayari, na kwa kuanzia Chief Executive Officer ameteuliwa.
Ofisi za mradi huu zitakuwa chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani, ingawa mradi pia utakuwa chini ya usimamizi wa mawakala, na gharama zitatolewa na Serikali, ambayo ndiyo itajua vyanzo vya fedha, kama ni kutoka serikalini au kwa wahisani, alisema Ulungi.
Alipoulizwa kuhusu gharama kubwa za mradi huo, Ulungi alisema kwamba gharama halisi zitajulikana baada ya wazabuni wa mradi kujulikana mara tu baada ya kushindanishwa, kauli ambayo ni ya kushangaza na kutilia shaka; hasa kwa kuwa tayari ameshateuliwa Ofisa Mtendaji Mkuu
Kuhusu umuhimu wa mradi kupita katika tararibu za PPRA, Ulungi alisema kwamba mambo ndiyo kwanza yanaanza, na lazima mradi ufuate tararibu hizo zilizowekwa na Serikali.
Hata hivyo, hatua ya serikali kumteua Ofisa Mtendaji Mkuu inaleta utata wa mradi huo kupita katika chekecheo la PPRA.
Akizungumza bungeni mwaka jana kuhusu mradi huo, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Joseph Mungai alisema: Mheshimiwa Spika, katika Bunge la bajeti la mwaka wa fedha 2006/2007 nililiahidi Bunge lako tukufu kwamba baada ya kukamilisha zoezi la upembuzi yakinifu Wizara yangu ingeanza utekelezaji wa Mradi wa Vitambulisho. Napenda kulijulisha Bunge hili kuwa Wizara imeanza utekelezaji wa mradi kwa kununua jengo kwa ajili ya Ofisi anzilishi ya mradi. Hali kadhalika Wizara yangu ikishirikiana na Wizara ya Menejimenti ya Utumishi wa Umma pamoja na Asasi nyingine zinaendelea na mchakato wa kuundwa kwa Wakala (Agency) itakayosimamia na kuendesha zoezi la utoaji wa Vitambulisho vya Taifa.
Wizara inakamilisha Andiko la Maelezo ya Mradi (Project Design Document) ambalo ndiyo litatoa dira ya mwelekeo wa utekelezaji wa mradi hatua kwa hatua. Aidha, zoezi la kuwatambua na kuwaorodhesha wageni wanaoishi vijijini na mijini linaendelea katika Mikoa ya Kagera, Kigoma, Rukwa, Mbeya, Ruvuma, Mtwara, Mwanza, na Mikoa ya kati. Hii ni hatua muhimu ya maandalizi ya utoaji vitambulisho. Lengo la Serikali ni kukamilisha Mradi wa Vitambulisho ifikapo Desemba, 2009.
Kama kuna ID lakini hakuna ZIP CODE system kama ya marekani ID zitakuwa kama karatasi tu. Nilazima waanzishe zip code system ili watu wawe na anwani za makazi.Utaratibu kabla ya kuanzishwa kwa hizo ID haujakamilika
Vitambulisho vya Uraia bomu jingine
Mwandishi Wetu Machi 12, 2008
Raia Mwema
Tayari zimevutwa 200m/=
MRADI mkubwa wa vitambulisho vya Taifa uliomo mbioni kuanza ni kashfa nyingine mithili ya zile za kampuni hewa ya Richmond na EPA, Raia Mwema imeelezwa.
Mradi huo ulioanza kuzungumzwa miaka ya katikati ya 1970 na ambao utagharimu kiasi cha Sh. bilioni 250, unaelezwa kwamba umo katika hatua za mwisho za kutaka kutekelezwa japo taarifa zinaonyesha kwamba ni mpango mwingine mkubwa wa ulaji fedha za umma.
Shaka hiyo inatokana na ukweli kwamba tangu mwanzo mradi huo umesimamiwa na maofisa wa Serikali kutoka Wizara za Mambo ya Nje na Ofisi ya Rais (Utumishi) kama washauri na ambao sasa inaaminika tayari wamekwisha kulipwa kwa kazi yao hiyo.
Taarifa zinasema pia kwamba sasa washauri hao kutoka serikalini wamejipanga katika nafasi za asasi zitakazokuwa zikisimamia mradi huo.
Raia Mwema imefanikiwa kuona orodha ya washauri mbalimbali wa mradi huo ambao baadhi yao wako karibu na vigogo serikalini. Orodha ya washauri hao ni pamoja na Profesa Damas Muna, Jaffar Buyogera, John Kyaruzi, Dickson Maimu, Jack Gotham, Salum Mpugusi, Donald Carriere, Coen Kleinhans, Kenneth Roko, Robert Alexander, Balozi Richard Butler, Anthony Githua, Rama Mwikalo na Robert Stewart.
Baadhi ya nyaraka ambazo Raia Mwema imefanikiwa kuona zinaonyesha kwamba wazo la mradi huo lilidakwa na kampuni ya Gotham International ambayo iliingia ubia na kampuni ya FootPrint Africa Business Solutions ya Afrika Kusini na kwa pamoja zikaingia katika mkataba na Wizara ya Mambo ya Ndani wa kuzifanya kampuni hizo mbili kuwa meneja wa mradi baada ya kukamilisha kazi ya utafiti wa awali.
Inasema sehemu ya nyaraka hizo: Pande zote zilikuwa na mazungumzo mjini Dar es Salaam kati ya Novemba 13 na 18, 2004 kuelekea utekelezaji wa Mpango wa Vitambulisho vya Taifa kwa kipindi cha 2004 hadi 2014, kwa ajili ya utekelezaji wa mfumo, ilikubalika kwamba kundi la makampuni hayo liwe na jukumu la kuwa Washauri katika Menejimenti ya Mradi.
Kwamba timu ileile iliyoshiriki kutafiti uwezekano wa mradi kufanyika ndiyo inayopendekeza pia kuwa mameneja wa mradi, ni jambo ambalo limeufanya mradi wenyewe kuonekana dhahiri kuwa mpango mahususi wa ulaji.
Kinachotia shaka kingine, kwa mujibu wa takwimu, ni wigo wa mradi wenyewe. Inapendekezwa kwamba watakaopewa vitambulisho hivyo ni makundi ya umri kati ya miaka 0-14 ambao wanakadiriwa kuwa asilimia 44 ama watu 16, 174,387 ya kundi lote la raia wa Tanzania wanaokadiriwa kufikia milioni 37.
Kundi jingine ni la umri wa kati ya miaka 15-64, kiasi cha asilimia 53, wanaokadiriwa kuwa 19,629,729. Kuna pia kundi la miaka 65 na kuendelea, kiasi cha asilimia 2.6, wanaokadiriwa kufikia watu 962,240.
Wataalamu waliozungumza na Raia Mwema wanahoji upana wa wigo huo hasa katika kundi la kwanza kwamba kwa nini watoto ambao ndiyo kwanza wanazaliwa waingizwe katika mpango huu ilhali kimsingi ni bado tegemezi na hawawezi kuwa na kumbukumbu zote za kiuchumi au vinginevyo; achilia mbali kwamba hata kupiga kura au kufungua akaunti benki hawawezi.
Watafiti/mameneja wa mradi huo wanapendekeza kwamba vitambulisho aina ya smart card, ambavyo ni ghali, ndivyo vitumike.
Ni ughali huo ambao miaka ya nyuma ulisababisha wafadhili kadhaa kujitoa katika mradi baada ya kubaini kwamba huu haukuwa mradi halisi wa Taifa bali mradi wa watu wachache kuvuna fedha za umma.
Inafahamika kwamba nchi kama China, Korea na Sweden zilipata kuonyesha nia ya kutaka kuufadhili mradi huo lakini ikashindikana, hiyo ikiwa ni pamoja na Benki ya Dunia, kuuacha mradi sasa ukiamuliwa kutekelezwa kwa fedha za ndani ambazo kimsingi wafadhili hawawezi kuhoji matumizi yake.
Gharama za sasa za mradi huo zinakadiriwa kuwa Sh. bilioni 250 zikiwa zimekua kutoka Sh. 152 za makisio ya awali, ambazo zinakifanya kitambulisho hicho kuwa ghali kuliko hata vya nchi zilizoendelea kama Sweden,
Raia Mwema ina taarifa kwamba Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia aliyekuwa anamaliza muda wake mwaka jana, Judy OConnor wakati akiaga alihoji ughali wa vitambulisho hivyo na inaaminika kwamba ofisa mmoja mwandamizi wa Serikali, Mambo ya Ndani, wakati huo ambaye alikuwa na maslahi katika mradi alifoka akisema kama Benki ya Dunia inataka kujitoa ijitoe. Kweli Benki ya Dunia ikajitoa.
Kwa sababu ya mradi kuwa dhahiri wa fedha nyingi, mara kadhaa kumetokea migongano miongoni mwa wakubwa, kila mmoja akivutia upande wa kampuni yenye maslahi naye, huku wengine wakitaka mradi huo uendeshwe kwa uwazi kama ambavyo taratibu za Serikali zinataka.
Migongano ya aina hiyo imeripotiwa kujitokeza Wizara za Mambo ya Ndani, Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara ya Mambo ya Nje.
Aidha, Raia Mwema imetaarifiwa kwamba hitilafu nyingine, kama ilivyokuwa kwa mkataba wa ile kampuni hewa ya kufua umeme ya Richmond, ni kuwa mradi huu wa vitambulisho nao haukupita katika chekecheke la Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA).
Tangu mwaka 2004 zimekuwapo safari za vigogo kadhaa serikalini kwenda nje ambako wamekuwa wakikutana na kampuni za huko kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo.
Wakati hayo yakiwa hivyo, Mkurugenzi Msaidizi wa Uhamiaji, anayeshughulikia sheria, Magnus Ulungi, aliliambia Raia Mwema, juzi, kuwa Mradi wa Vitambulisho vya Taifa sasa umeanza kutekelezwa, na kwa kuanzia tayari Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mradi ameteuliwa.
Suala la vitambulisho vya Taifa sasa liko kwenye process (mchakato) tayari, na kwa kuanzia Chief Executive Officer ameteuliwa.
Ofisi za mradi huu zitakuwa chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani, ingawa mradi pia utakuwa chini ya usimamizi wa mawakala, na gharama zitatolewa na Serikali, ambayo ndiyo itajua vyanzo vya fedha, kama ni kutoka serikalini au kwa wahisani, alisema Ulungi.
Alipoulizwa kuhusu gharama kubwa za mradi huo, Ulungi alisema kwamba gharama halisi zitajulikana baada ya wazabuni wa mradi kujulikana mara tu baada ya kushindanishwa, kauli ambayo ni ya kushangaza na kutilia shaka; hasa kwa kuwa tayari ameshateuliwa Ofisa Mtendaji Mkuu
Kuhusu umuhimu wa mradi kupita katika tararibu za PPRA, Ulungi alisema kwamba mambo ndiyo kwanza yanaanza, na lazima mradi ufuate tararibu hizo zilizowekwa na Serikali.
Hata hivyo, hatua ya serikali kumteua Ofisa Mtendaji Mkuu inaleta utata wa mradi huo kupita katika chekecheo la PPRA.
Akizungumza bungeni mwaka jana kuhusu mradi huo, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Joseph Mungai alisema: Mheshimiwa Spika, katika Bunge la bajeti la mwaka wa fedha 2006/2007 nililiahidi Bunge lako tukufu kwamba baada ya kukamilisha zoezi la upembuzi yakinifu Wizara yangu ingeanza utekelezaji wa Mradi wa Vitambulisho. Napenda kulijulisha Bunge hili kuwa Wizara imeanza utekelezaji wa mradi kwa kununua jengo kwa ajili ya Ofisi anzilishi ya mradi. Hali kadhalika Wizara yangu ikishirikiana na Wizara ya Menejimenti ya Utumishi wa Umma pamoja na Asasi nyingine zinaendelea na mchakato wa kuundwa kwa Wakala (Agency) itakayosimamia na kuendesha zoezi la utoaji wa Vitambulisho vya Taifa.
Wizara inakamilisha Andiko la Maelezo ya Mradi (Project Design Document) ambalo ndiyo litatoa dira ya mwelekeo wa utekelezaji wa mradi hatua kwa hatua. Aidha, zoezi la kuwatambua na kuwaorodhesha wageni wanaoishi vijijini na mijini linaendelea katika Mikoa ya Kagera, Kigoma, Rukwa, Mbeya, Ruvuma, Mtwara, Mwanza, na Mikoa ya kati. Hii ni hatua muhimu ya maandalizi ya utoaji vitambulisho. Lengo la Serikali ni kukamilisha Mradi wa Vitambulisho ifikapo Desemba, 2009.
Naamini sio coincident kwamba mradi uanze 2009 bali ni njia nyingine ya kutafuta fedha za kampeni za chama, na pia kujipa ujiko kwamba tumeanza tupeni muda tumalizie.
Kama alivyosema Kamundu, bila Zip Code system ni ngumu kujua mtu anapoishi(Adress, house number, street, town)n.k
Kwa nini wasimpe kila mmoja passport na kuachana na hizo smar cards maana ni wizi wa mchana .Kama kuna passport na watu wananyimwa je hizo card nani atanunua wakati hata pesa ya kula watu hawana?
Naamini sio coincident kwamba mradi uanze 2009 bali ni njia nyingine ya kutafuta fedha za kampeni za chama, na pia kujipa ujiko kwamba tumeanza tupeni muda tumalizie.
Kama alivyosema Kamundu, bila Zip Code system ni ngumu kujua mtu anapoishi(Adress, house number, street, town)n.k
Smart Cards au kwa jina lingine lolote bei yake ni ya chini ukilinganisha na passport. Nchi nyingi sana ulimwenguni wanatoa national ID ambayo data zake zinakuwa tayari tangu unapozaliwa. Cha muhimu ni kufanya hiyo kazi properly bila urichimondulian au ukaramagis etc.
MIMI NAITWA mr.KAIZA TWALIPO, LEO NI SIKU YANGU YA KWANZA KUANDIKA MESSAGE HAPA JAMBO FORUM..BAHATI MBAYA AU NZURI NIMEZALIWA TAREHE 09 MWEZI 12 MWAKA 1961,SIKU YA UHURU WA TANGANYIKA, NA NINAISHI NCHINI MAREKANI...ANWANI 2079 JUBILEE CT, COLUMBIA MD 21046...EMAIL NI TWALIPO1961@YAHOO.COM...
MY FORMAL INTRODUCTION...HIYO NA ANATASEMA NIMEPEWA HELA KUFUATA COMMON SENSE ASEME TU..USHENZI MTUPU KWA WANA JF...HIZO PESA KWANGU SIZIHITAJI...LAKINI UPUUZI WA WATU FULANI KATIKA HII FORUM HAUWEZI KUPUUZIWA UENDELEE, ...SAID KUBENA HAWEZI KUWA GODFATHER WA JF NA MEDIA TANZANIA..I LOVE THIS FORUM BUT I HAVE TO SAVE IT FROM STUPIDITY FROM A FEW JOB, INBALANCED CONTRIBUTORS FROM CHAOS & UCHOCHEZI...THE TANZANIA TABLOID IS GETTING OUT OF HAND, MAKING PESA BECAUSE RUMORS ARE NEWS, SOME UNFOUND BASELESS NA HATA MIRADI YA KAWAIDA UMEKUWA NI KASHFA...
STOP THE STUPIDITY, UCHOCHOZI WA LEO KUFANYA KUSOMA KWOTE WATANZANIA WA NJE WENGINE MNA FAMILIA ETI SOURCE YENU NI GAZETI LA MWITA GACHUMA NA SAID KUBENA, NDIO MNATAKA KULETA UCHOCHEZI WA HABARI ZINGINE ZA KISHENZI
KUSHABIKIA UFISADI NA KUENEZA RUMORS HAKUWEZI KUTUSAIDIA SISI WATANZANIA KAMA NCHI MASIKINI, SASA HATA MAKANISANI NI HILO TU NDIO ISSUE...MUACHE USHENZI NA ANATAKA AJE KWANGU KWA KUTETEA UJING ETI MTAJE JINA, HILO HAPO NA ANWANI NIMETOA FOR THAT...UTEMI WA INTERNET NAO UTEMI (ushIROMBO)...PONGEZI KWA SHY & COMMON SENSE PEOPLE LIKE FM ES & SHY, HAMUWEZI KUPATA OPINION ZINGINE. TOLERANCE IKO WAPI, USHABIKI WA KITOTO MUACHE WABONGO