Tanzania ndio nchi yenye mzigo mdogo wa deni Afrika Mashariki kwa sasa

Tanzania ndio nchi yenye mzigo mdogo wa deni Afrika Mashariki kwa sasa

OffOnline

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2022
Posts
644
Reaction score
478



Wale wanaopiga kelele kwamba Tanzania tunakopa na tumekopa Sana msikilize huyu Mwamba vizuri ndio utaelewa kwanini Mungu alimleta Rais Samia wakati huu,

Mkuu wa mkoa wa Simiyu akihojiwa na kituo cha redio cha E-FM amedadavua kwa undani Sana swala hili la deni la Taifa,

RC Kafulila anasema "tuangalie mjadala kuhusu ukubwa wa deni na afya ya kukopa.

Nianze kwa angalizo tu kwamba masuala ya kupima ukubwa wa deni na afya ya uchumi wa nchi kukopa ni sayansi ya uchumi na zipo kampuni 75 kimataifa (Global Credit Rating Agency). Maarufu ni3( MOODY'S, S&P na Fitch) ambazo zinamiliki zaidi ya 90% ya kazi hizi duniani.

Lakn kubwa kuliko zote ni MOODY'S. Ambayo inamiliki karibu 45% . Kwa mujibu wa Ripoti ya MOODY'S ya Agust30,2021, Tanzania imepewa daraja la B2 (stable) kwa afya yake ya kukopesheka( creditworthiness) ikiwa juu ya Kenya, Namibia, Msumbiji, Ghana, Ivorycoast, Senegal na nchi nyingi ukanda wa kusini, mashariki na magharibi ya Afrika.

Taasisi hii ya MOODY'S inapima uchumi wa USA, nchi za Ulaya, Asia na kote duniani, inatupa daraja hilo, ni kielelezo kwamba tupo imara na thabiti ktk usimamizi wa deni na uchumi.

Bank ya Dunia Juni2022, tathimini yake imeonesha mzigo wa deni kwa uchumi (GDP), Tanzania ni 31% wakati Kenya ikiwa na mzigo mkubwa wa 64% huku Rwanda 49.8% na Uganda 49.7%.

Nikweli deni ni changamoto kwa nchi nyingi za Afrika. Lakn bado afya ya Tanzania eneo hilo inaonekana imara kwa ulinganisho huo na vipimo vya taasisi zinazoheshimika kwa weledi wa kupima mambo haya dunaini."

#Tanzania tuko vizuri Sana, hongera Rais Samia, asante Kafulila kwa kulifungua Taifa kimtazamo.
 
Tatizo sio kukopa ila hiyo mikopo kama nchi inanufaikaje? Au ndio zinaishia kulipana posho za safari, vikao na mishahara?

Mpaka sasa mama ameshakopa karibia tr 10. Ila haiendani na thamani ya hiyo miradi anayokopea. Hapo ndipo changamoto. Hao wengine tusijifananishe nao sababu kwao maendeleo yanaonekana.
 
Inategemea unakopa kufanya nini?
Hata katika mazingira ya kawaida tu tabia ya kukopa kopa inamshushia mtu heshima yake.

Sisi kama Taifa hii tabia imekua sugu.

Na inasikitisha mno badala ya kiongozi kupendekeza namna ya kupunguza kuwa tegemezi naye anasifia matatizo.

Huyo ndugu Mkuu wa Mkoa kabisa anasifia mikopo?? Ni jambo la kuhuzunisha mno.
 
Eeeh,Leo Kafulila uko vizuri,

Tatizo Watanzania hasa Upinzani na Sukuma Gag walikimbia shule,

I like this, Hongera Rais wangu Samia uko njema lete hela tufanye kazi sisi
Mama hakukosea kumteua huyu jamaa anajua Sana vitu
 
Hata katika mazingira ya kawaida tu tabia ya kukopa kopa inamshushia mtu heshima yake.

Sisi kama Taifa hii tabia imekua sugu...
Tumekuwa Sugu tukijifananisha na nani?
 
Stroke, Namna nzuri ya kufanya maendeleo ni kutumia pesa zisizo zako zenye gharama amabayo miradi yako inaweza kurudisha na kukuachia faida. Kama una access ya fedha jaribu hili.
Kibiashara ndio ila sio kama Taifa tena kwa nchi Changa kama hii.

Tatizo kubwa ni usimamizi mzuri. Hatuna.

Nchi nyingine wanakopa na wanafanya miradi ya kimkakati ya kuwaondoa katika hali hiyo ya utegemezi.

Sasa sisi tunakopa hata kwa mambo yasiyohitaji kukopa na bado mikopo hiyo haisimamiwi vizuri, watu wanajipigia tu.

Hivyo mikopo kwa nchi yetu ni matatizo tu.
 
Kibiashara ndio ila sio kama Taifa tena kwa nchi Changa kama hii.

Tatizo kubwa ni usimamizi mzuri. Hatuna...
Hivyo basi kwa hoja yako Usimamizi ndo tatizo. Raia wanapaswa wawe wakali na usimamizi pale mkopo unapochukuliwa.
 
Naona Kafulila kaajiri PR maana Kila siku ni media coverage kumpa sura ya kitaifa.

Anyway kukopa hakuna ubaya kama unawekeza kwenye miradi itakayokupa returns huko mbeleni. Mfano tukikopa kumaliza SGR, Kupanua bandari, Barabara, mashule n.k then hakuna ubaya.

Changamoto nayoiona ni vipaumbele mfano tunataka kujenga bwawa la Nyerere wakati huo huo tunataka Kutanua upatikanaji wa umeme wa gesi so unakuta mnakopa kufanya miradi inayofanana!! Hii haina afya ni bora mfanye kimoja kwanza kingine kije baadae.

Hata Suala la mafuta unakuta tunakopa Ili kuweka Ruzuku kwenye mafuta huku Bado sensa itaenda kula Mabilion, kuna wakati inabidi mchague kimoja kingine mkiweke kando kwa miezi kadhaa.
 
Naona Kafulila kaajiri PR maana Kila siku ni media coverage kumpa sura ya kitaifa.

Anyway kukopa hakuna ubaya kama unawekeza kwenye miradi itakayokupa returns huko mbeleni. Mfano tukikopa kumaliza SGR, Kupanua bandari, Barabara, mashule n.k then hakuna ubaya...
Noted mkuu,
 
Shida ya Watanzania hawajibidiishi kufahamu haya mambo, kumbe Tanzania tuko vizuri kiasi hiki. Naunga mkono mikopo iendelee
 
View attachment 2299582
Wale wanaopiga kelele kwamba Tanzania tunakopa na tumekopa Sana msikilize huyu Mwamba vizuri ndio utaelewa kwanini Mungu alimleta Rais Samia wakati huu...
Hiyo tathmini ni kabla ya deni babu kubwa toka IMF la sh trilioni 2.4. Ukiliweka hilo tayari tunawapiku uganda na rwanda!! Labda uipongeze "nchi" ya Zanzibar ambayo deni lake linasoma "sifuri"!!!
 
Back
Top Bottom