Tanzania ni nchi ngumu sana kutoboa bila shortcut, hakuna uwazi

Tanzania ni nchi ngumu sana kutoboa bila shortcut, hakuna uwazi

sasa mnataka tuwe marajiri wote nani ataosha magari yenu na kupiga deki nyumba zenu? hayo ma sufuria mtadugua na mikucha yenu hiyo mirefu watoboe wachache tu ili maisha yaende kila mtu akimiliki mzigo wa pesa ni sawa na kuwa maskini wa kutupwa sababu nani sasa atakaye tumwa? [emoji1787] yaani hivi tulivyo ndivyo tunavyo takiwa kuwa ni lazima kundi fulani li nyonywe tu tofauti na hapo maisha yana weza kuwa magumu sana [emoji22]
 
.

Screenshot_20220118-221901_Instagram.jpg
 
Mkuu hujui kua tunatofautiana? Hujui kuna watu wameridhika na hayo unayoyaongea, kuna watu wanapambana kwa nguvu nyingi sana kua maskini na akina sisi tunapambana kwa njia zozote kua MATAJIRI..ikiwezekana kukaa sehemu moja na Lucifer kufanya mkataba.
Wee jamaa hujapata connection bado?
 
Tanzania hatuchukii ufisadi ila huwa tuna chuki wale waliopo kwenye channel wakati huo.Kila Mtanzania anapenda kuwa fisadi amini kwamba.
Asante mkuu,kwa ugumu huu ni lazima kila mtu atamani kuwa fisadi tu.
 
Tuseme ulikiwa unafanya biashara maeneo yasiyo rasmi (machinga) ukatolewa na serikali.

Ukatoka na msingi wako wa 2ml kwenda mtaani kuanza biashara unaamua kuuza kiduka cha vitu vidogo vidogo labda na gas za kupikia majumbani.

Kutokana na msingi kuwa mdogo na hali ya biashara mauzo yako yanakuwa hayazidi 60k kwa siku moja.

Kwa kawaida huwa maduka ya mtaani ukiuza 10,000 faida buku, kwa hiyo mauzo yako wastani ni 50k ina maana faida ni 5k tu.

Kodi ya pango ni 30k kwa mwezi umeme ni zaidi ya 10k

Manispaa inakuja kukukamata ukachukue leseni 80,000 kwa mwaka na city service levi 50,000.
TRA wanataka ukachukue TIN ya mlipa kodi kwa mwaka 150k makadirio ya chini kabisa.

Hujakaa sawa serikali ya mtaa inakuja inatakiwa kulipa ulinzi shirikishi 2000 na takataka 15,000 kwa mwezi.
Kama hutaki usifanye biashara

Weka matumizi yako ya kawaida kila siku ya lazma, kuna kutoboa kweli hapo?
Tatizo wa Tanzania tunavipaji vya kulalamika sana,mnahisi kuna watu wanakodi nyingi kama marekani kila siku watu wanafilisiwa,mfano mdogo angalia wasanii wakubwa na waliobaki nikilio hatari huko.Tujifunze kulipa kodi na michango mengine kwa serikali
 
Tatizo wa Tanzania tunavipaji vya kulalamika sana,mnahisi kuna watu wanakodi nyingi kama marekani kila siku watu wanafilisiwa,mfano mdogo angalia wasanii wakubwa na waliobaki nikilio hatari huko.Tujifunze kulipa kodi na michango mengine kwa serikali
Mkuu Africa ndiyo bara pekee ambalo viongozi wake wanakamua ng'ombe maziwa bila kuwalisha vizuri. Huko Marekani ng'ombe wanalishwa vizuri kwanza halafu ndiyo wanakamuliwa maziwa.

Wafanya kazi wanalipwa mishahara mizuri kisha ndiyo wanakatwa kodi. Wafanya biashara wanaandaliwa mazingira mazuri na sera nzuri za biashara kisha ndiyo wanakatwa kodi.

Hatukatai pengine watanzania tunapenda sana kujilalamisha lakini pia serikali yetu imejisahau sana. Kuajiri hawataki watu wakijiajiri wanawabebesha mizigo ya kodi kuzidi vipato vyao.
 
Tatizo wa Tanzania tunavipaji vya kulalamika sana,mnahisi kuna watu wanakodi nyingi kama marekani kila siku watu wanafilisiwa,mfano mdogo angalia wasanii wakubwa na waliobaki nikilio hatari huko.Tujifunze kulipa kodi na michango mengine kwa serikali

Kwahio ndo tuseme rushwa imekuja kutuokoa kiasi fulani sio?

Sent from my TECNO CE9 using JamiiForums mobile app
Rushwa ni tamu ukiitoa wewe ila akutolee mtu ndio utaona ubaya wake
 
Back
Top Bottom