Tanzania: Nyumba nyingi dining room zinajengwa, ila hazitumiki

Tanzania: Nyumba nyingi dining room zinajengwa, ila hazitumiki

Tatizo kubwa ni uchumi wa kati. Baba na mama wanakuwa hawapo karibu ili wale na watoto. Wanakuwa busy kutafuta fedha.

Kuna jamaa aliniambia nchi ya uswisi inaheshimu familia kula pamoja na ndiyo maana muda wa jioni maduka yanafungwa ili kulipisha hilo zoezi. Sina uhakika kama ni kweli.
wale mliofika ulaya si mnasemaga kule hakuna mambo ya kudeka deka kila mtu anaishi kivyake? kumbe wanaheshimu mambo ya familia? sasa mbona tunadanganyana huku Mpanda.
 
Cha kushangaza baba anasema nileteeni chakula changu hapa huko watoto wako wanasumbua sana. Wakati watoto uliwazaa mwenyewe na wanauliza maswali ili waelewe dunia.
daah. kuna wakati nafika nyumbani niko hoi bin taabani vibarua huko nilikotoka vinataka kunitoa roho. mara vingine vimebuma na vingine nimepigwa hasara na faini. sasa napofika nyumba watoto wanaanza kuuliza hiki na kile nachanganyikiwa. nachofanya naoga fasta chakula kitanikuta chumbani nalia chini kwenye mkeka, mto nashusha hapo hapo hata kitandani sipandi nalala kama nyoka.

haya maisha bwana we acha tu.
 
Kula pamoja kama ni dining au nje kwenye mkeka ni jambo zuri kwa familia. Ni muda wa kupiga stori ya yaliyotokea kutwa nzima. Hapo unaweza kugundua mabadiliko ya tabia ya mtoto kama utakua makini na stori zake. Pia ni namna nzuri ya kufanya watoto wawahi kurudi nyumbani. Kwa mfano kama mnakula saa mbili usiku, mtoto atafanya jitihada zote awahi muda huo awe nyumbani.
Kuwasema watoto wakati wa chakula sio vizuri. Upatikane muda tofauti wa kumkanya mtoto, sio wakati wa kula.
 
Wakuu,

Nimefanya utafiti usio rasmi.

Ndani ya Tanzania yetu. Nyumba nying Sana zinajengwa zikiwa na sehemu ya dinning room.

Cha kushangaza, nyumba nyingi Sana Dinning room zimegeuzwa eneo la wazi na lisilotumika kwa ajili chakula Kama ilivyokusudiwa.

Wengi Sana Nmeona bado wana utamaduni wa kulia chakula sebleni (living room).

Hii imekaaje, nini MTIZAMO Wako kuhusu ili suala.

My take:
Kama mtu hapendi kulia chakula dinning room, ni Bora tu kwenye ramani yake asiijenge.

Ni upotezaji wa rasilimali fedha kujenga kitu usichokua na matumizi nacho.
Sio kwamba na dining room pawe na TV! Huko living room wengi wanafuata TV!! Kama ni aina ya viti, basi viwekwe dining pia ingawaje sio sehemu yake!
 
Sehemu hii kwangu inaheshima kubwa lzm Nile pamoja na watoto

Akina mama wanakamtindo watoto kueatengea peke Yao huko nje au jikoni kwangu nshapiga marufuku chakula kinatengwa sehemu moja tunakula wote hata heshima iwepo
 
Kabisa,
hapo umenigusa hata Mimi pia.

Nlipokua mdogo Nlkua sipendi kula chakula dinning pamoja na familia.

Sababu kubwa ilkua kumkwepa mama,

yaani MDA wa kula pale dinning hasa Usiku,
Ndo MDA unaanza kusemwa makosa yako Yote uliofanya siku nzima.

Na Kama majibu hayaridhishi, baaada ya chakula Ni stiki.
Wakati wa kula ni muda wa Aman sana kwangu hakuna kuongea makosa Nani kafanya nn au kipi kimekuaje tukimaliza tunapeana abc za baadaye, kama ni usiku ibada inafuata

Lzm kama mwanaume udhibiti mambo ya nyumba yako
 
Sebuleni kuna tv wengi wanasave time. Anakula while anaangalia movies...habari...ila hii ni tabia mbaya maana muda wa kula hutakiwi kufanya chochote hata kuzungumza.
ila leo nikila mkono mmoja nina simu....
Kula huku utani wa mbali mzuri sana au unashusha kastori kazuri yaaan watoto watatamani kula na ww kila muda
 
Sebuleni kuna tv wengi wanasave time. Anakula while anaangalia movies...habari...ila hii ni tabia mbaya maana muda wa kula hutakiwi kufanya chochote hata kuzungumza.
ila leo nikila mkono mmoja nina simu....
Falsafa ya modern architecture imeegemea towards "open" structures and spaces majumbani na ofisini .majumbani kwa mfano Kitchen,living,na dining inakaribia a single space mnaonana na kupiga gumzo .Pia maofisini idara zote zipo single open space badala vyumba vyumba. Hiii inachochea team work kutimiza malengo na mahusiona mazuri idara na idara.

1620644204732.png
 
Wanaume hawatakiwi kukaa pamoja na wanawake kwenye meza ya chakula.

Nyumba lazima itenganishe sebule ya wanawake na wanaume.

Mtoto wa kiume afundishwe ya kiume kwenye kikome na mtoto wa kike afundishwe ya kike huko jikoni na mama zake.
Ni jamii na jamii

Kwangu kula pamoja wote ni muhimu kamaa Baba lazima niwafundishe wote kazi zote lzm wajue

Kuna occasion tu nitakaa na wa kiume kuwafunda pia nitakaa na wa kike kuwafunda

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Yani upike tembele na ugali uhangaike kupeleka dinning room!?
unapiga juu kwa juu
Hata kama ni makande Tu mkuu lazima iwe hivyo

Kula pamoja kunaleta upendo na kumisi misi hivi kwa mtoto unamjengea kitu chema kwenye subconscious yake hata atakapokuwa mkubwa ndiyo maana wanawake wajaliwa na watoto wao kwa kuwa tu kwenye subconscious ya watoto waliwekeza

Ni Jambo la msingi sana kula na watoto wako na kupiga Stori nao wakati wa kula
 
Kula pamoja mezani na kusali pamoja ni vitu muhimu ambavyo vinasahaulika katika jamii. Mnapo sali pamoja ni rahisi watoto kukumbuka sala hata wakiondoka nyumbani. Kula pamoja kunafundisha watoto table manners.

Tatizo linaanza pale uhusiano wa wazazi unapoanza kuyumba. Baba na mama hawako vizuri na hawawezi kukutana mezani.

Wakati mwingine baba anaangalia mpira na chakula chake apelekewe sebuleni. Mama anaangalia Instagram na yeye anataka chakula chake kiachwe jikoni atakula atakapokua tayari.
Facts tupu nimekuoenda bure
 
Pana maswali mengi baba ana kwepa au watoto wanakwepa city room Kuna TV watu wanakuwa bz
 
Nyumba bila dinning kwangu ni sawa na bure,napenda sana kupanga chakula kwenye dinning table halafu vile mnakaa kama familia kila mtu anajisevia msosi basi burudani tu!
 
Back
Top Bottom