Tanzania opposition Chief Whip Tundu Lissu shot

Tanzania opposition Chief Whip Tundu Lissu shot

Mimi kwa hili linanitoa hadhi ya kuwa Mwafrika kabisa, Mbona sijivunii tena.

Yani mbona viongozi wa Afrika wawe hivi?? Aah! Inaudhi kweli
 
Don't conflate one violent prone tribe from one small region to mean all Kenyans involve in bloodthirsty electioneering.I've never seen Merus,Taitas ,Giriamas,Samburus ,Turkanas ,Kikuyus,Kambas or a bunch of other tribes start bloody violence due to politics.You're fusing one fight-prone tribe to mean all Kenyans .
Many killings took place in Nairobi suburbs and western part of the country, but for outsiders Kenya is one thing, anything happening in Kenya is for Kenya, many best marathon winners in Kenya come from specific tribes, but they represent Kenya as a country, so if there is one or two tribes that are troublesome, still they represent Kenya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi kwa hili linanitoa hadhi ya kuwa Mwafrika kabisa, Mbona sijivunii tena.

Yani mbona viongozi wa Afrika wawe hivi?? Aah! Inaudhi kweli
Japo ni mapema sana kusema ni serikali imehusika lakini kuna dalili zote kwamba serikali ina mkono wake, wameahidi kwambamlazima wawakamate na Magufuli mwenyewe amemuagiza IGP ahakikishe kwamba wamekatwa, hicho ndicho kitakuwa kipimo cha kujua kama ni serikali inahusika au hapana, wasipokamatwa, basi serikali itakuwa inahusika

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe unauhakika gani kama nyerere hakuuliwa, au Kawawa hakuuliwa?, kwa sababu umeamua kuishi maisha ya kusikiasikia bila kukubaliana na ripoti zilitolewa basi tuishi hivyo hivyo, kila anayekufa tuseme kauliwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nyerere mbona aliuliwa,wee hujui,muulize cga nkapa.Alifika airport anatembea mzima akarudi kwenye jeneza,jiulize.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Professor Chachage alikuwa mwalimu wangu na tulimuuguza hadi siku yake ilipofika, acha kuishi maisha ya udaku kusikiliza habari za vijiweni

Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe ni muongo humjui chachage,chachage alifia semina Kibaha,acha uongo. Chachage mbali na mengine yote tukikutana Sisimizi bar na vikao vya chama fulani.Mkuu ulimuuguza Chachage lini na hispital gani? Haya dk Mvungi je?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Many killings took place in Nairobi suburbs and western part of the country, but for outsiders Kenya is one thing, anything happening in Kenya is for Kenya, many best marathon winners in Kenya come from specific tribes, but they represent Kenya as a country, so if there is one or two tribes that are troublesome, still they represent Kenya.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mtanzania mgani wewe unaelewa kizungu sana hivi?
 
Some how you are right, but that is changing very fast my friend, Kenya is old story, Tanzania is changing that equilibrium very fast, try to go to Tanzania you will see for yourself, economy is booming, roads are far much better, manufacturing industry is picking up education system is undergoing major reforms

Sent using Jamii Forums mobile app
wacha kujiliwaza mkuu...huwez ukawadanganya waafrika mashariki wote...the Rwandese guy is just telling you the truth...ila naona ni ngumu kumeza...
 
'Unataka kucheza wewe na ushike firimbi'...duh! mwambieni huyo jamaa wenu aheshimu opposition leaders...na pia aheshimu demokrasia...aende na wakati aache mambo ya uchwara mambo zamani
 
Mkuu wa Mkoa anapiga marufuku mikusanyiko anasahau hata kutoa pole!!!
 
wacha kujiliwaza mkuu...huwez ukawadanganya waafrika mashariki wote...the Rwandese guy is just telling you the truth...ila naona ni ngumu kumeza...
Nimegundua uzalendo, hasira za kuona Tanzania inaendelea kwa kasi na flustrations za maisha zinakusumbua zaidi kuliko kujenga hoja zenye mashiko, huo ndio ukweli ulio wazi japo ni uchungu kumeza, ukiondo GDP ambayo Kenya iliifikia zamani, kwanza kwa sababu Kenya iliendelezwa na wakoloni wa kiingereza ikilinganishwa na nchi zingine za EA, na baada ya uhuru Kenya iliendelea na kasi ya kujenga uchumi wake haikusima kufanya marekebisho yoyote ya kimuundo wa kisiasa wala kijamii, ilipokea kijiti toka kwa mabepari na kuendelea na ubepari(soma the Wako report ya Kenya).

Tanzania ilipowekwa chini yw uangalizi wa waingereza baada ya vita kuu ya kwanza toka kwa mjerumani, waingereza waliitumia kama sehemu ya kuzalisha mali ghafi za mazao kwa ajili ya viwanda vyao vilivyokuwepo Nairobi, hawakushughulika kuweka miundombinu yoyote kwa kujua kwamba ipo siku wataondoka wakati wowote, na baada ya kupata uhuru, Nyerere hakuanza kujenga uchumi kwanza, yeye aliamua kujenga umoja wa taifa kwanza, alitaka kuunganisha nchi iwe moja na kuondoa tofauti za matabaka ya watu yaliyowekwa na wakoloni, kusitokee mtu kujiona bora kutokana ama na rangi yake, kabila au dini yake, kipato au elimu yake, au cheo chake. Tulifundishwa maneno mengi kama vile; binadamu wote ni sawa, rushwa ni adui wa haki sitopokea wala kutoa rushwa, cheo ni dhamana, watanzania wote ni ndugu zangu na africa ni moja.

Katika kipindi hiki cha kujenga utaifa, sio tu kwamba tulikua hatuzalishi bali tulitumia fedha chache tulizopata kugharimia shughuli hii ya kujenga utaifa na uzalendo kwanza, Nyerere aliamini bila umoja wa kitaifa hakutokua na amani wala uzalendo wa kweli, vitu ambavyo ni muhimu sana katika kujenga uchumi imara na endelevu.

Msumari wa mwisho katika kusambaratisha uchumi wa Tanzania ni pale Nyerere alipoanza vita vya ukombozi kusini mwa Afrika na kumalizia vita vya Uganda, kumbuka kipindi chote hiki Kenya iliyokua mbele tokea enzi za ukoloni ilikua inaendelea kujenga uchumi wake, haijawahi kusimama kupitia lolote lililopunguza kasi ya uchumi wake(Soma article ya Dr. David Ndii).



Sent using Jamii Forums mobile app
 
'Unataka kucheza wewe na ushike firimbi'...duh! mwambieni huyo jamaa wenu aheshimu opposition leaders...na pia aheshimu demokrasia...aende na wakati aache mambo ya uchwara mambo zamani
Katika hili la demokrasia ninakubaliana na wewe kwa kiasi fulani, Magufuli is one among the best presidents in the world at the moment, ila ana upungufu katika eneo hilo, chimbuko lake sio mwana siasa ni mtendaji zaidi. Japo sio mtu mbaya sana kama watu wanavyomsema, ni kama vile kununua shati jeupe sana kwa hiyo hata ukiweka doti la kalamu linaonekana, nadhani utakua umenielewa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani hawa jirani zetu imebaki nawaonea huruma. Naona ni kama wanachapa hatua mbili nyuma kila tukichapa hatua mbili mbele! Yaani juzi juzi tu si ndo J.K alikuwa anakenua kenua, si ni hii hii Tanzania?
Hahaha wanaochapa hatua 10 nyuma ni nyie na uchaguzi wenu wa kipumbavu
 
Hiyo ni wakati ule hata Tz Hanga,Sadala,Abdala majura,Nk waliuawa.Kenya ya leo demokrasia imetamalaki,vinginevyo jaluo asingekuwepo.HuyubMsando ni issue binafsi zaidi.
PAKA baada ya kumaliza ya mchungaji sasa kaikamata nchi ,tuko safarini tunaenda Rwanda.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hivi unajua zaidi ya watu 30 wameuliwa na polisi Kenya tangu siku ya kupigwa kura hadi sasa ?
 
wakora....ila huwezi ukapata waziri ama kiongozi wa opposition wamepigwa risasi hata siku moja...isitoshe huwez ukapata kiongozi wa opposition amekamatwa na polisi au kukandamizwa kwa hali yoyote ile...yaani Tanzania=Zimbabwe=Rwanda=Uganda=Somalia=DR Congo=dictatorships
Yule Saitoti alikufa kwa kipindupindu?
 
Mtanzania mgani wewe unaelewa kizungu sana hivi?
Bwana Tony254 mimi ninapata taabu sana kumuona mkenya anashindwa kuitumia lugha yake ya taifa kiufasaha, ninachanganyikiwa zaidi nikiona viongozi wakubwa serikalini na shughuli za kiserikali kama Bunge, mahakama na Rais anahutubia nchi kwa kiingereza, nijuze tafadhali what is going on over there?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom