Tanzania Premier League 'TPL' Singida United Vs Simba SC Uwanja wa Namfua Singida

Tanzania Premier League 'TPL' Singida United Vs Simba SC Uwanja wa Namfua Singida

Nimemwona Refarii amepigwa mpira na mchezaji wa singida na madaktari wa simba waliwahi kumtibu nataka sana.
 
Hvi Tff si watupe kombe letu siku ya mechi na Valencia tu!?

Tutawasusia kombe Lao maana hata mwakani tuna uhakika wa kulichukua tena.
 
Kuelekea kumalizika msimu wa Ligi Kuu Tanzania TPL, Patashika hiyo kushika kasi kwa viwaja tofauti kupigwa ambapo kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mbao FC wanamenyana na KMC, huku Uwanja wa Namfua mkoani Singida wanyeji Singida United wanapapatuana na Mabingwa watetezi Simba SC.

Mchezo wa Singida United dhidi ya Simba SC, unatarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua kwa muda wote wa dakika tisini

Msimu uliopita Simba SC walitangaza ubingwa rasmi kwenye uwanja huo huo wa Namfua Stadium, wakati walipopepeta na Singida United na wenyeji hao kukubali kipigo cha 1-0

Na leo tena Mei 21, 2019 Mabingwa hao wanahitaji ushindi muhimu ili kuweza kutangaza rasmi ubingwa msimu 2018/2019. Je historia itajirudia au Singida United wanaweza kumsimamisha Simba SC kwa muda?

Usikose ukaambiwa..Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 10:00 jioni na utakuwa mubashara kupitia Azam Sports 2.View attachment 1103721View attachment 1103722

Naaaaaaam mpira umeanza uwanja wa Namfua mkoani Singida TPL..

Singida United 0-0 Simba SC

02' Mchezo umeanza kwa kasi kwa Simba kuliandama lango la wenyeji na kupata kona mbili ambazo hazikuzaa matunda.

05' Singida United, wanajaribu kujibu mashambulizi ambapo shuti la Maganga limetoka nje sentimita chache lango la Simba.

09' Goooooooooooooooooooaaal gooooooooaaal.. Maddie Kagere anaipatia Simba SC bao la kwanza baada beki wa Singida United kushindwa kuondosha mpira wa hatari ulipigwa na Mohammed Hussein

Singida United 0- 1 Simba SC

14' Singida wanaokoa mpira wa hatari ambao ungeweza kuipatia Simba bao la pili.

Mchezo umechangamka kwa pande zote mbili, Singida wakijihakikishia kusalia TPL, huku Simba wakihitaji ushindi.

15' Singida United 0-1 Simba SC

Kinyombo anakwenda lango la Simba lakini mwamuzi anasema umejiangusha na mpira wanachukua Simba

20' mpira umetawaliwa na Simba, japo Singida ni wenyeji

Free kick kuelekea Simba.Inapigwaaaaa lakini Munishi anadaka bila wasiwasi.

24' mpira umesimama baada ya mwamuzi mpira kumpiga kichwani, madaktari wanaitwa kumpatia matibabu..

Haya mpira unaendelea, TPL uwanja wa Namfua baada ya mwamuzi kupata rabsha na kutibiwa

26' Okwi anapata nafasi safi anapiga lakini mpira unatoka nje na kuwa goal kick

30' Inapigwa free kick kuelekea Simba, sio mbali, inapigwaaa lakini mpira unakuwa hafifu na kudakwa na Munish

35' Singida wapiga pasi za hapa na pale kujaribu kulifikia lango la Simba, anatokea mchezaji wa Singida anapiga nje na kuwa goal kick

Bocco anaambaa na mpira, na anapiga kwake Kagere..Lakini mwamuzi anasema mpira ulitoka nje kabla ya kupiga

40' Singida United 0-1 Simba SC

Simba wanasogea langoni mwa Singida anachukua Okwi mpira anapiga lakini mpira unapaa na kutoka nje na kuwa goal kick

45+2' kuelekea kuwa mapumziko

Naaaaaaam Mpira ni mapumziko uwanja wa Namfua, ambapo Simba wanatoka mbele kwa bao moja bila goli la Maddie Kagere

Singida United 0-1 Simba SC
Simba Bingwa
 
Back
Top Bottom