Tanzania tuhifadhi akiba yetu kwa Dhahabu badala ya Dollar

Tanzania tuhifadhi akiba yetu kwa Dhahabu badala ya Dollar

Kipindi cha mzee Ruxa, benki kuu ilianza kununua dhahabu na kuhifadhi,, [emoji16],kilichotokea sasa... Wabongo ni wezi sana,,
Hata nchi nyingine kubwa hawawezi hifadhi dhahabu kwa usalama,, huwa wanapeleka Fort Knox, US,,
Hata hapo mwisho wa siku mmarekani akitaka anakudhulmu,, kama ilivyotokea kwa dhahabu za venezuela, silizokuwa zimehifadhiwa, US
New York Federal Reserve Bank ndo yaongoza kwa kuwa na dhahabu nyingi za nchi nyingi.

Venezuela dhahabu zake zilikuwa London,
 
kudhibiti soko kama ilivyoagizwa kwenye sheria ya mwaka 2017.

SHERIA YA MADINI MABADILIKO HOTUBA YA PROF. KABUDI

HOTUBA YA MHESHIMIWA PROF. PALAMAGAMBA J.A.M.
KABUDI, WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA AKIWASILISHA
MUSWADA WA SHERIA YA MAREKEBISHO YA SHERIA
MBALIMBALI WA MWAKA 2017 (THE WRITTEN LAWS
(MISCELLANEOUS AMENDMENTS) ACT, 2017)
________________________________
1.0 Utangulizi
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Kanuni ya 86 ya Kanuni
za Kudumu za Bunge, Toleo la Mwaka 2016, naomba kutoa
hoja kwamba Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya
Sheria Mbalimbali ya Mwaka 2017 (The Written Laws
(Miscellaneous Amendments) Act, 2017) sasa usomwe kwa
Mara ya Pili na Bunge lako Tukufu lijadili na hatimaye
lipitishe Muswada huu na kuwa sehemu ya sheria za
Kuweka masharti yatakayowezesha kuunzishwa kwa .........
vyombo mbalimbali vitakavyohusika katika shughuli
za madini kwa niaba ya serikali. Vyombo hivyo ni
pamoja na:
(i) Hifadhi ya dhahabu na vito chini ya Benki Kuu
(Establishment of the National Gold and Gemstone Reserve); Rejea ibara ya 27 C

(ii) Maeneo maalumu ya masoko ya dhahabu na
vito (Gem and Minerals Houses); Rejea kifungu kipya kinachopendekezwa cha 27B

(iii) Maghala ya Serikali ya kuhifadhia madini
(Government Mineral Warehouses); Rejea kifungu
kipya kinachopendekezwa cha 27D ......
 
Wazalendo wa CCM mpya tangu mwaka 2017, wakiongozwa na Mh. Rais, John Pombe Joseph Magufuli na kina Prof. John Aidan Mwaluko Kabudi wamejaribu lakini inaonekana jaribio hilo la kuweka hifadhi ya dhahabu ktk benki kuu ya Tanzania lineshindwa,hata kabla ya kuanza.

Tatizo ni nini nchi kushindwa kununua dhahabu au ni kwa vile dhahabu yote inachimbwa na kumilikiwa na wadau wa maendeleo kutoka nje hivyo mikataba ni migumu kuibadilisha ili dhahabu hiyo inunuliwe na BoT kwa shilingi ya kiTanzania badala ya dolari za marekani maana wawekezaji hao kwa kufuatana na mkataba wa, uwekezaji hawakubali fedha za madafu yaani Shilingi ya kiTanzania ! Na mkataba huo unalindwa,kwa masharti na vigezo vya Tribunal ya Kimataifa iliyo huko France , Netherlands na siyo vyombo kama Mahakama Kuu ya Tanzania pale panapotokea ulalamishi wowote .
Tumesaini mkataba wa MIGA na wa ICSID. Tutashtakiwa kwa kuvunja mikataba kienyeji kinyume na makubaliano yaliyosainiwa hapo awali baina ya wawekezaji na serikali ya CCM - Tundu Lissu
Investment: The Role of the World Bank, with. Particular Reference to ICSID and MIGA ....
 
Kav

Kavulata tusubiri end game.Waliotuingiza in this mess wanashangilia mafanikio yao,wakati sisi tuonajua what is going on behind the curtain tunalia.The World is very unfair.
Shida hatujui kuwa hatujui. Hebu ona mfano huu rahisi tu. Kenya wanajua kiingereza vizuri, Uganda wanaongea kiingereza vizuri, Rwanda, Burundi, Congo, Mali na nchi zilizotawaliwa na ufaransa wanajua kuongea kifaranza vizuri TU hata wachezaji wao wanajua lugha. Tanzania tumetawaliwa na Uingereza na ujerumani lakini hatujui kiingereza kabisa pamoja kwamba tunasoma kiingereza tokea shule ya msingi hadi chuo kikuu. Walimu na wanafunzi wote hawajui lugha ya kufundishia na kujifunzia. Inategemea nini hapo.
 
TOKA MAKTABA :

MIFANO YA MIKATABA MIBOVU YA MADINI

Mwaka 2017

Mawaziri na maofisa waandamizi walihusika kusaini mikataba mibovu ya madini


Ripoti hiyo iliyosomwa jana na baadaye kukabidhiwa kwa Spika Job Ndugai na baadaye kwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, pia imetaka wajumbe wa bodi ya mgodi wa Williamson Diamond Limited (WDL) waliohuhusika katika uingiaji wa mikataba ya uendeshaji mgodi huo wa almasi, wahojiwe na kuchukuliwa hatua stahiki.

Dodoma. Profesa Abdulkadir Mruma, ambaye alitikisa nchi kwa kutaja mawaziri na maofisa waandamizi serikalini waliohusika kusaini mikataba mibovu ya madini, ametajwa katika ripoti ya kamati maalum ya Bunge iliyoundwa kuchunguza biashara ya madini ya almasi .....

Alipoulizwa inakuwaje mtu msomi na aliyepewa dhamana na taifa kulinda rasilimali asaini nyaraka bila ya kuzisoma, alijibu kuwa anawaamini watu walioziandaa

......mmoja mkubwa, akisema thamani yake kwa sasa ni dola 200 milioni za Kimarekani (sawa na zaidi ya Sh400 bilioni za Kitanzania).

Pia alisema katika uchunguzi wao kwa siku mbili walizokaa mgodini hapo wameona makinikia ya almasi tani 1.5 ambayo yanaweza kutoa madini yenye thamani ya Sh2.3 trilioni.

Alisema hiyo inawafanya wahisi gharama za uchimbaji bado zimewekwa katika makinikia hayo kwa kuwa yalichimbwa miaka 50 na marehemu Wiliamson.

Petra inamiliki asilimia 75 wakati Serikali ya Tanzania asilimia 25 na utafiti uliopo hadi sasa unaonyesha kuwa mgodi wa Mwadui unaweza kuzalisha almasi hadi mwaka 2033, ingawa kuna uwezekano wa kuendelea kuzalisha miaka mingi ijayo.

Kwa mujibu wa ripoti ya fedha ya mwaka 2016, Petra ilipata dola 78.9 milioni za Kimarekani. Katika migodi yake yote duniani, Petra ilitoa mrabaha wa jumla ya dola 27 milioni za Kimarekani. Uzalishaji ulipanda kwa asilimia 5 mwaka 2016 hadi kufikia carrat 212.869 kutoka carrat 202, 265.

Mapato pia yaliongezeka kwa asilimia 27 hadi kufikia dola 78.9 milioni za Kimarekani kutoka dola 62.1 milioni Kwa mujibu wa ripoti hiyo, ongezeko hilo lilitokana na kuuzwa kwa almasi aina mbili za kipekee za rangi ya waridi.
 
Hatuwezi kupiga hatua kwa kuagiza kila kitu.

Hakika ni lazima tujitegemee pakubwa kwa kutumia akili ili tuweze kubadilisha jiwe la Mchuchuma n.k kuwa engine ya magari, reli, mitambo ya viwanda vikubwa na vidogo ili hata mazao yote kama nyanya, maembe, viazi, ndizi, mananasi ,nyama za mifugo pia dagaa, samaki n.k zisindikwe badala ya kuoza mashambani na ktk masoko ili bidhaa hizo zijae ktk maduka na supermarket zetu
 
Mkuu, kwa mfano Toyota Tanzania ina mkataba na serikali kuimport magari ya serikali, makampuni mengine pia yana mikataba kuhakikisha biashara zinafanyika. Unadhani hapo suala unalosema litawezekana kweli?
Kila mkataba lazima uwe na muda wa kwisha na muda wa kufanyiwa marejeo, tunaweza kununua magari Yao kwa dhahabu yetu badala ya dollar. Lengo kuu liwe kupunguza utegemezi wa dollar unaoua uchumi wetu.

Kama watawala na wachumi wetu wengekuwa na elimu sahihi ya kutosha wangeshatoa Amri ya kusema, kuanzia mwaka 2025 madaladala yote, na magari madogo yote lazima yafumie gesi badala ya mafuta ya petroleum. Tutakosa Kodi za mafuta lakini tutaokoa manunuzi ya mafuta kwa dollar.
 
TOKA MAKTABA :

MIFANO YA MIKATABA MIBOVU YA MADINI

Mwaka 2017

Mawaziri na maofisa waandamizi walihusika kusaini mikataba mibovu ya madini


Ripoti hiyo iliyosomwa jana na baadaye kukabidhiwa kwa Spika Job Ndugai na baadaye kwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, pia imetaka wajumbe wa bodi ya mgodi wa Williamson Diamond Limited (WDL) waliohuhusika katika uingiaji wa mikataba ya uendeshaji mgodi huo wa almasi, wahojiwe na kuchukuliwa hatua stahiki.

Dodoma. Profesa Abdulkadir Mruma, ambaye alitikisa nchi kwa kutaja mawaziri na maofisa waandamizi serikalini waliohusika kusaini mikataba mibovu ya madini, ametajwa katika ripoti ya kamati maalum ya Bunge iliyoundwa kuchunguza biashara ya madini ya almasi .....

Alipoulizwa inakuwaje mtu msomi na aliyepewa dhamana na taifa kulinda rasilimali asaini nyaraka bila ya kuzisoma, alijibu kuwa anawaamini watu walioziandaa

......mmoja mkubwa, akisema thamani yake kwa sasa ni dola 200 milioni za Kimarekani (sawa na zaidi ya Sh400 bilioni za Kitanzania).

Pia alisema katika uchunguzi wao kwa siku mbili walizokaa mgodini hapo wameona makinikia ya almasi tani 1.5 ambayo yanaweza kutoa madini yenye thamani ya Sh2.3 trilioni.

Alisema hiyo inawafanya wahisi gharama za uchimbaji bado zimewekwa katika makinikia hayo kwa kuwa yalichimbwa miaka 50 na marehemu Wiliamson.

Petra inamiliki asilimia 75 wakati Serikali ya Tanzania asilimia 25 na utafiti uliopo hadi sasa unaonyesha kuwa mgodi wa Mwadui unaweza kuzalisha almasi hadi mwaka 2033, ingawa kuna uwezekano wa kuendelea kuzalisha miaka mingi ijayo.

Kwa mujibu wa ripoti ya fedha ya mwaka 2016, Petra ilipata dola 78.9 milioni za Kimarekani. Katika migodi yake yote duniani, Petra ilitoa mrabaha wa jumla ya dola 27 milioni za Kimarekani. Uzalishaji ulipanda kwa asilimia 5 mwaka 2016 hadi kufikia carrat 212.869 kutoka carrat 202, 265.

Mapato pia yaliongezeka kwa asilimia 27 hadi kufikia dola 78.9 milioni za Kimarekani kutoka dola 62.1 milioni Kwa mujibu wa ripoti hiyo, ongezeko hilo lilitokana na kuuzwa kwa almasi aina mbili za kipekee za rangi ya waridi.
Wote tunakubaliana kuwa elimu yetu ni mbovu, hata maprofesa wetu pia wamepitia elimu hiyohiyo mbovu. Kuna ubaya gani kumlipa mwanasheria kutoka Urusi, au N Korea au Israel au south Africa kutusaidia kwenye kuingia mikataba na makampuni ambayo sisi hatuna uelewa kwenye maeneo tunayoingia mkataba?
 
Wazalendo wa CCM mpya tangu mwaka 2017, wakiongozwa na Mh. Rais, John Pombe Joseph Magufuli na kina Prof. John Aidan Mwaluko Kabudi wamejaribu lakini inaonekana jaribio hilo la kuweka hifadhi ya dhahabu ktk benki kuu ya Tanzania lineshindwa,hata kabla ya kuanza.

Tatizo ni nini nchi kushindwa kununua dhahabu au ni kwa vile dhahabu yote inachimbwa na kumilikiwa na wadau wa maendeleo kutoka nje hivyo mikataba ni migumu kuibadilisha ili dhahabu hiyo inunuliwe na BoT kwa shilingi ya kiTanzania badala ya dolari za marekani maana wawekezaji hao kwa kufuatana na mkataba wa, uwekezaji hawakubali fedha za madafu yaani Shilingi ya kiTanzania ! Na mkataba huo unalindwa,kwa masharti na vigezo vya Tribunal ya Kimataifa iliyo huko France , Netherlands na siyo vyombo kama Mahakama Kuu ya Tanzania pale panapotokea ulalamishi wowote .

Investment: The Role of the World Bank, with. Particular Reference to ICSID and MIGA ....
Tanzania ina wachimbaji wadogo wengi sana. Hata ingeamua kununua kutoka kwa hao bado ingepeta dhahabu ya kutosha. Hao hawahitaji dola. Na pia ingeweza kuongea na makampuni makubwa ya uchimbaji labda kuchukua 10% ya dhahabu wanayozalisha kwa madafu.
 
Kila mkataba lazima uwe na muda wa kwisha na muda wa kufanyiwa marejeo, tunaweza kununua magari Yao kwa dhahabu yetu badala ya dollar. Lengo kuu liwe kupunguza utegemezi wa dollar unaoua uchumi wetu.

Kama watawala na wachumi wetu wengekuwa na elimu sahihi ya kutosha wangeshatoa Amri ya kusema, kuanzia mwaka 2025 madaladala yote, na magari madogo yote lazima yafumie gesi badala ya mafuta ya petroleum. Tutakosa Kodi za mafuta lakini tutaokoa manunuzi ya mafuta kwa dollar.
Mkuu, hizi option zilishapitiwa ila hicho unachosema ni sawa na kujifungia kutokana na resources zetu ila zikiisha huna msaada kwingine na ndio maana Tanzania ina opt kukopa fedha kwa ajili ya miradi na kuinject katika mzunguko wa fedha lengo likiwa kuleta maendeleo kwa haraka.
 
Hakika ni lazima tujitegemee pakubwa kwa kutumia akili ili tuweze kubadilisha jiwe la Mchuchuma n.k kuwa engine ya magari, reli, mitambo ya viwanda vikubwa na vidogo ili hata mazao yote kama nyanya, maembe, viazi, ndizi, mananasi ,nyama za mifugo pia dagaa, samaki n.k zisindikwe badala ya kuoza mashambani na ktk masoko ili bidhaa hizo zijae ktk maduka na supermarket zetu
Kaka umeshawahiona wapi nchi Haina samaki wakati imezunguukwa na bahati, maziwa makubwa na mito? Elimu yetu ni ndogo sana kupitiliza, watu hawakopesheki
Mkuu, hizi option zilishapitiwa ila hicho unachosema ni sawa na kujifungia kutokana na resources zetu ila zikiisha huna msaada kwingine na ndio maana Tanzania ina opt kukopa fedha kwa ajili ya miradi na kuinject katika mzunguko wa fedha lengo likiwa kuleta maendeleo kwa haraka.
Kukopa sio kuzuri sana, maana kunatengeneza vicious cycle ya utegemezi kwa mtu huyohuyo anaekudai. Ni kweli resources zinaisha ndio maana lazima Sasa uzitumie katika kuhamia kwenye vyanzo vingine vya mapato kama elimu, huduma, viwanda mama au jeshi kubwa linalotumika kama mercenary kulipwa hela nyingi. Hata Uingereza Kulikuwa na wanyamapori hapo zamani lakini maendeleo yaliwamaliza wanyama wao wote lakini wakahamia kwenye aina nyingine ya maendeleo
 
Kaka umeshawahiona wapi nchi Haina samaki wakati imezunguukwa na bahati, maziwa makubwa na mito?

Ndiyo maana elimu na akili kubwa mfano Japan hawana madini lakini akili kubwa wanaunda injini zote za vifaa / vyombo mbalimbali vya kisasa sisi hata mashine ndogo ya kusindika nyanya au mananasi n.k kijijini wasomi wetu na wavumbuzi wetu hawawezi.
 
Dhahabu inahifadhiwa kama "reserves" toka muda sana. Be informed according.
 
Ndiyo maana elimu na akili kubwa mfano Japan hawana madini lakini akili kubwa wanaunda injini zote za vifaa / vyombo mbalimbali vya kisasa sisi hata mashine ndogo ya kusindika nyanya au mananasi n.k kijijini wasomi wetu na wavumbuzi wetu hawawezi.
Kaka shida yetu ni kubwa sana kuliko tunavyodhani, akili zetu kubwa hazikimo kweñye watu wanaofanya maamuzi kuhusu taifa. Sehemu za kufanya maamuzi wamejaa watoto wa wapigania Uhuru wetu, watoto wa viongozi wa zamani na wajanja wajanja wanaojua kusifia sana viongozi na jamaa zao. Wale wenye akili kubwa wanaonekana maadui, wametumwa, wasalti, wapinzani, nk.

Hebu ona mfano rahisi tu huu, sisi tuna dhahabu, tanzanite, Ruby, silver, copper, korosho, mbao, nk, lakini vipato vyetu ni vidogo sana kiasi Cha kushindwa kuvinunua vitu vyetu wenyewe na kuvitumia, tunalipatana kiasi kidogo sana Cha ujira kwa kazi kubwa tunazofanya, yaani kima Cha chini ni laki 2…5 na professor mkubwa analipwa 4.0 m kwa mwezi, house girl aalipwa 50,000 kwa mwezi, kibarua anaejenga analipwa 3000 kwa kutwa, Wakulima ndio hawajui soko la mazao Yao na hawajui bei ya Kuku wao. Hii maana yake nini? Maana yake watanzania hatuwezi kuyanunua madini yetu wenyewe na kuyavaa shingoni, vidoleni, masikioni, puani, miguuni Wala viunoni ingawa tunayo, hatuwezi kununua korosho zetu na kuzitafuna siisi wenyewe kwanza, hatuwezi kukunua kwa wingi bidhaa za viwanda vetu kwa wngi sisi wenyewe. Maana yake tunategemea zaidi soko la nje, duniani kote hakuna uchumi unaoendeshwa hivyo. Kenya uchumi wao ni mkubwa kukuwa uwezo wao wa kulipana ni mkubwa hivyo na uwezo wao wa kununua vitu vyao ni mkubwa pia. Yaani, mkilipana zaidi mtakatana Kodi kubwa zaidi, mtanunua vitu vyenu zaidi, mtazalisha zaidi na mtaongeza morali zaidi ya kufanya kazi na mtapunguza udokozi zaidi. Wanafanya hivyo Marekani, Ulaya, Asia na kote kasoro Africa na sanasana Tanzania.

Hii ni akili ya kawaida TU ya kuzaliwa nayo. Madini yetu tulipaswa kuyavaa sisi wenyewe kwanza lakini hatuwezi kuyanunua.
 
Ni kweli mkuu,ndio maana wakamua.They new aki-back the Dinar with Gold,in principle uchumi utakuwa imara sana,inflation will be history,na realistically the US $ will be threatened na Africa haitaihitaji tena Ulaya au Marekani for loans,so Africa will be trully independent.Oh my my,that was hard to swallow.
Kaka watu huwa hawajui kuwa World Bank, IMF na World Trade Organization ni mali kamili ya Marekani. In fact hata UN inamilikiwa na Marekani. Watu wanaoweka amana (dhahabu) kule marekani ndio wanaoweza kukopeshwa kwa urahisi na IMF na WB maana wana collateral zao kule kuliko wewe ambae huna. Wakiamini kwamba kama hutalipa deni lako au utakuwa mkorofi na adui wa marekani utapoteza mali yako yote.

Hatuhitaji viongozi wanaogopa kufa kwa kusema ukweli na kufanya mambo mema kwaajili ya nchi zao na watu wao. Kuna viongozi alijitoa mhanga kwaajili ya taifa na watu wake, akasema anajitoa sadaka kwaajili ya taifa lake kuliko kuwasikiliza mabeberu na akaamua kufanya mambo makubwa sana.

Viongozi wengi wa Afrika wanaahidi kutenda makubwa kwa nchi zao wakati wanaomba kura, lakini baada ya kupata kura hawatendi kama walivyoahidi. Hawafanyi walivyoahidi wananchi wao sio kwa kupenda bali wanakutana na maagizo, makakatazo, makalipio, vitisho na vikwazo vinavyotishia hata maisha yao binafsi kutoka kwa mabeberu. Ndio maana hata vya upinzani vilivyofanikiwa kuviangusha vyama tawala vinafanya yaleyale na pengine vibaya zaidi kuliko vyama vilivyoangushwa. Mtu asikudanganye kuwa kama CCM itaanguka basi maisha yetu yatakuwa bora sana kuliko hivi, sio kweli. Itakuwa tu sawa na kuacha kunywa chai ukanywa kahawa au kuacha safari larger na kunywa Serengeti larger, zote zitakulevya tu. Kiongozi atakaelisaidia taifa lake ni yule tu atakaekubali kutofautiana na ushauri, amri, njama na hila za mabeberu.
 
Back
Top Bottom