Tanzania tujipange kupokea wazungu watakaokimbia baridi kali kwao

Tanzania tujipange kupokea wazungu watakaokimbia baridi kali kwao

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Hali sio nzuri nchi za Ulaya na Marekani, mfumko wa bei ya mafuta, gesi na chakula umevuruga mipango ya serikali na raia ya wazungu. Hivi karibuni majira ya baridi yataikuta Ulaya ikiwa na uhaba wa gesi na umeme kupashia nyumba joto. Hii itawafanya wazungu wengi kuja kujisalimisha nchi za joto tukiwemo Tanzania.

Tusije kuuchanganya ugeni huu na Royal tour movie yetu. Watakuja wengi kwaajili ya kujisalimisha kwa baridi na unafuu wa maisha hapa kwetu.

Serikali, utalii na wajasiliamali tukae mkao wa kula, maana bahati ni pale fursa inapokutana na maandalizi katika sehemu na wakati mmoja. Tujipange.
 
Waziri wa utalii,ndo muda wake wa kujibrand kwa MAMA.
 
Mtoa mada punguza porojo. North America wana hifadhi ya kutosha ya mafuta na gas kwa sababu ni wazalishaji wa gas asilia na mafuta..
 
Waziri wa utalii,ndo muda wake wa kujibrand kwa MAMA.
Waziri awe tayari kuyaainisha makundi 3 ya wazungu wanaokuja wakati huu, yaani atofautishe kati ya:
1. wanaokuja kitalii
2, wanaokuja kukimbia baridi na njaa lakini watafanya utalii mdogomdogo, na
3. Wanaokimbia baridi na njaa tu basi.

Ni muhimu sana kuweka rekodi zao maana huenda wakahitaji treatment tofauti kabisa. Usije ukaona ndege kutoka Ujerumani, Italy, UK zimejaa ukadhani wote ni watalii, lahsha, fumbua macho yako na ubongo.
 
Wanatumia gharama kubwa kuendesha vita badala ya kupambana na changamoto za kimazingira........hiyo vita wanayoendesha hapo Ukraine ina manufaa yapi hasa kwa ustawi wa watu, akili nyingi huondoa maarifa..
Vita hii ina manufaa kwa marekani na kidoogo Uingereza. Uingereza itanufaika zaidi kwa Ujerumani, Ufaransa na Italy mataifa mihimili ya EU kuanguka kiuchumi, maana baada ya Brexit ya UK mihimili ya Umoja wa Ulaya ni German, France na Italy, zikianguka hizi kiuchumi na EU itaanguka pia. Solz ni kama pandikizi la Marekani na UK
 
Hali sio nzuri nchi za Ulaya na Marekani, mfumko wa bei ya mafuta, gesi na chakula umevuruga mipango ya serikali na raia ya wazungu. Hivi karibuni majira ya baridi yataikuta Ulaya ikiwa na uhaba wa gesi na umeme kupashia nyumba joto. Hii itawafanya wazungu wengi kuja kujisalimisha nchi za joto tukiwemo Tanzania.

Tusije kuuchanganya ugeni huu na Royal tour movie yetu. Watakuja wengi kwaajili ya kujisalimisha kwa baridi na unafuu wa maisha hapa kwetu.

Serikali, utalii na wajasiliamali tukae mkao wa kula, maana bahati ni pale fursa inapokutana na maandalizi katika sehemu na wakati mmoja. Tujipange.
Narudia kali ilosubiria Royal tour ndio iwalazimishe wazungu kuja?

Royal tour is real
 
Hali sio nzuri nchi za Ulaya na Marekani, mfumko wa bei ya mafuta, gesi na chakula umevuruga mipango ya serikali na raia ya wazungu. Hivi karibuni majira ya baridi yataikuta Ulaya ikiwa na uhaba wa gesi na umeme kupashia nyumba joto. Hii itawafanya wazungu wengi kuja kujisalimisha nchi za joto tukiwemo Tanzania.

Tusije kuuchanganya ugeni huu na Royal tour movie yetu. Watakuja wengi kwaajili ya kujisalimisha kwa baridi na unafuu wa maisha hapa kwetu.

Serikali, utalii na wajasiliamali tukae mkao wa kula, maana bahati ni pale fursa inapokutana na maandalizi katika sehemu na wakati mmoja. Tujipange.
Usisahau kutuambia mahotel na viwanja watakavyokua wanatembelea
 
Mtoa mada punguza porojo. North America wana hifadhi ya kutosha ya mafuta na gas kwa sababu ni wazalishaji wa gas asilia na mafuta..
unaifahamu bei ya gallon moja ya mafuta kule Marekani hivi sasa? wazungu kaka wanaishi kwa bajeti zinazofanywa mwanzoni mwa mwaka, kule kwao bei haziyumbi mara kwa mara, sasa hivi wanatumia nje ya bajeti zao.
 
Kicheko kwa yule Bwana ataongeza usajili wa wachezaji
 
Usisahau kutuambia mahotel na viwanja watakavyokua wanatembelea
Aaa kaka hawa wanaokimbia baridi wanaojifanya wanakuja kutalii wanakaa nyumba na mtaa wowote, hata kule Tandale, kwamtogole na mnyamani wanakaa tu, hawachagui. Kule Zanzibar wale jamaa wa Ukraine sasa hivi wanaishi hata kule vijijini shambani kabisa.
 
Aaa kaka hawa wanaokimbia baridi wanaojifanya wanakuja kutalii wanakaa nyumba na mtaa wowote, hata kule Tandale, kwamtogole na mnyamani wanakaa tu, hawachagui. Kule Zanzibar wale jamaa wa Ukraine sasa hivi wanaishi hata kule vijijini shambani kabisa.
Dah! Wacha nijichanganye tu labda ntakutana nao
 
Mbususu za kizungu zinamiminika.......huku kigamboni walishaanza mapema kutiririka
 
Back
Top Bottom