Pre GE2025 Tanzania tunaongozwa na Watanzania? Yanayotokea ni bahati mbaya? Asante CDF

Pre GE2025 Tanzania tunaongozwa na Watanzania? Yanayotokea ni bahati mbaya? Asante CDF

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ukisoma historia ya Tanzania, Mwalimu J.K Nyerere alipata tabu sana kuwafundisha Watanzania dhana ya uraia.

Nyerere alisimamia uraia wa Tanzania kama kitu ambacho mtu ambaye hata si mzawa anaweza kuwa nacho, kwa kiapo.

Jambo hili lilimletea upinzani mkubwa kutoka kina Christopher Kassanga Tumbo, na hata jeshini.

Mpaka akaletewa jaribio la mapinduzi na wanajeshi mwaka 1964. Akavunja jeshi na kuliunda upya kwa aibu kubwa.

Mpaka Nyerere akafanyiwa uasi na wanajeshi ambao hawakutaka kuongozwa na watu wasio wazawa.

Professor Paul Bjerk kaandika vizuri sana katika "Building a Peaceful Nation: Julius Nyerere and tge Establishment of Sovereignty in Tanzania, 1960 -1964".

Ukisoma utaona kabisa Nyerere alivyopigania uraia wa Tanzania uwe na maana kubwa zaidi ya uzawa, na jinsi Watanzania wengi walivyokuwa hawajaeleea hilo somo.

Na mpaka leo, bado hawajaelewa hilo somo.

Wanaona mtu akizaliwa nchi nyingine, au akiwa na wazazi waliozaliwa nchi nyingine, hawezi kamwe kuwa raia wa Tanzania.

Xenophobia tu.
Nchi inahitaji wazalendo, ukiona watu wamelalamika kaa ukijua hao watu ambao ni wakimbizi walio kwenye nafasi za maamuzi si wazalendo , kitendo wao kuwa si wazalendo kwa nchi yao ndo kimefanya tuwashitukie ila kama wangekuwa wazalendo Wala tusinge jua kama si watanzania.
 
Sifa mojawapo ya mtu masikini ni wivu uliopitiliza. Sasa kama mtu kawa raia hata wa kuomba tu, kunashida gani akipata uongozi?

Embu acheni xenophobia, ingekuwa nyadhifa kama ya urais kweli tungeongea lakini hayo mengine hamna shida.

Dunia kwa sasa inakwenda kasi, kama bado waishi kama mkoloni lazima itakushinda.

Tunapoelekea miaka ya mbele kutakuwa na uraia pacha ni suala la muda tu. Nahisi tukifikia hiyo steji utajirusha ghorofani kuona mtu anauraia wa Gambia na Tanzania halafu kawa waziri.

Nadhani tujikite kwenye kuangalia taaluma na uwezo wa mtu katika kufanya kazi ndio tutapata maendeleo ya kweli na sio kuweka viraza kwenye position fulani kisa tu ni Mtanzania wa kuzaliwa.
Jamii forum Kuna wakimbizi wengi sana
 
Unataka kuniambia mtu aliyezaliwa hapa ana uzalendo kuliko aliyezaliwa kwingine akachukua uraia WA TZ. hivi mafisadi wote waliozaliwa TZ na wakafilisi nchi hii(bila kutaja majina) ni wazalendo?

Mwenzenu Kagame ana mawaziri wengi na government workers waliokuwa naturalized citizens na Mambo yanaenda vizuri.
Hoja ni mapandikizi wa Kagame Tanzania, wanachukua uraia huku kutengeneza njia ya M23
 
Rais akusaidie kwa utumbo uliouandika bila datails? Kutaja majina ya nchi ndiyo kwako imeshakuwa ukweli?

Kwanza muelewe ile kazi top pale kama siyo system huzipati kabisa.
Mapandikizi hadi USA wapo
Na USA ni watu makini
sasa nchi yako hii ambapo cv ni kujuana tu
Unadhani ni nini kinaweza kushundikana
Watu wanakupa tu miaka mitano au mitatu ya kudeal na wewe basi unamuona huyu ni rafiki wa kweli kama ndugu basi anakupa mwanae ambaye amesoma na hana kazi unamuweka mahali
Huyo unaemuweka sehemu Kwasababu wewe labda ni waziri na umempeleka pale dogo kwenye taasisi flani na anaonekana ana ukaribu na wewe waziri basi mambo yake yanakuwa rahisi na kuogopwa na wafanyakazi wenzake na hiyo ni njia ya kwenda mbele zaidi
 
Kwenda wewe. Mnajifanya mnajuwa kumbe hamjuwi lolote.

Nyinyi ni watu ambao hazicharge kabisa vichwani mwenu, hata CDF hamjamuelewa kwanini kayasema yale.
Mwambieni Mama Samia Mwalimu Nyerere mwaka 1964 Jeshi la Tanganyika lilitaka kumpindua baada ya kulazimisha Wazungu kuendelea kushika nyadhifa za kijeshi wakati siyo Watanganyika na leo tena Rais anaambiwa na Jeshi kuna watu ambao si raia wamekamata nyadhifa za kimaamuzi.
Endeleeni na uchawa JWTZ siyo Jeshi la Polisi!

Sent from my V2111 using JamiiForums mobile app
 
Marekani inawageni kibao kwenye system hadi vyombo nyeti. Biden shughulikia hilo.
 
Faiza Kaa kimya 🤐 chutama chutama. Bora ukaye kimya tu.
Acha Mkuu Apumzike Mmemziba Pumzi Anahema Kwa Tabu
20240120_155935.jpg
 
Mipaka ya bara la Afrika ilichorwa na wakoloni wakiwa wameketi kwenye meza huko Berlin Ujerumani bila kutia mguu Afrika. Matokeo ni kwamba mipaka haikizingatia jamii husika. Si ajabu kule Ngara , Kigoma , Mtwara, Karagwe nk baadhi ya familia zilitenganishwa.
Baba mdogo akajikuta yuko Uganda , baba mkubwa Tanzania, Shangazi Rwanda, Mjaomba Tanzania.
Laiti waliochora mipaka wangekuwa field hizo changamoto zisingetokea.
 
Nchi inahitaji wazalendo, ukiona watu wamelalamika kaa ukijua hao watu ambao ni wakimbizi walio kwenye nafasi za maamuzi si wazalendo , kitendo wao kuwa si wazalendo kwa nchi yao ndo kimefanya tuwashitukie ila kama wangekuwa wazalendo Wala tusinge jua kama si watanzania.
Basi pigieni kelele tatizo la kukosekama uzalendo, sio tatizo la kukosa wazawa katika uongozi.

Kwa sababu, mzawa pia anaweza kukosa uzalendo na asiye mzawa anaweza kuwa na uzalendo.

Uzawa na uzalendo si lazima viende pamoja.

Kwani madudu yote yaliyofanyika nchi hii yamefanywa na watu wasio wazawa?

Mbona mnatolewa relini kwa hoja ambazo hazina mashiko?
 
Idara ya uhamiaji ya Tanzania inadaiwa wamejaa Wakenya! How come tunaruhusu haya..afu Wakenya wenyewe waliopo wengi ni TOP. (But Anna ni mtu wa kusini).

Idara ambayo ni mama ya inchi kama uhamiaji wanadaiwa wameajiri Wakenya tena top position. Ndiyo maana unakuta kazi hata ndogo km hotel wapo wao hapo EAC ni wao tu.

Ebu tufukirie yatuatayo!

Namba 4 Kuna tetesi siyo wa kwetu..wanasema anatoka Kwa MR Pk. Hata namba 2 kiasili siyo wetu. Ulikuwaje hadi mfumo ukampitisha namba 2 wakati siyo wetu...Je mfumo nao upo compromised.

Namba 4 aliongoza madini je madini yetu yapo salama? Namba 4 leo yupo umemeni Je imekuaje?

Mh. Rais tafadhali fanyia kazi haya. Kuna watu wanajifanya ni wahaya au wasukuma kwenye cabinet ila ni wa Kule.

leo umeme hamna..SGR inapelekwa Rwanda badala ya Kongo? How .! Kwann tusiimarishe bandari yetu ya Kigoma. Mzigo ukitoka Dar unaenda Kigoma unapitia lake Tanganyika unafika Kongo why lazma upite Rwanda.
Hivi why kila siku kesi tunashitakiwa na kushindwa.. why.?

CDF Asante sana.

Rais tusaidie.
We ni mbeya ndiyo maana unaogopa kuwataja maana hauna ushahidi zaidi ya kusikia kwenye vijiwe vya kashata.
 
Back
Top Bottom