Tanzania tupate High Speed Train, Wachina watajenga!

Kama kusukuma maji ni issue na train je? So unataka WA tz wore kifo Chao kiwe train. Tusifanye test kwenye life za watu

Kipi kinachoshindikana chini ya jua ambacho binadamu wengine wamefanya Watanzania washindwe mbaya zaidi kunanchi zingine wamefanya makubwa wakiwa na rasilimali chache zaidi yetu sisi Watanzania tuwaoga hasa ktk kujaribu mambo mapya na hili limesababishwa na MFUMO MBOVU WA ELIMU ndo maana we unahisi kuwa na Train ya Umeme ni kuongeza vifo !!nikupe moyo yote yanawezekana usikate tamaa kwa unayoyaona leo
 
Kwa hiyo wewe unafkr mwandishi sio muelewa? Punguani weweee hivi vitu ni vya kawaida na vinawezekana hata hapa Tz. Acha kufkr kama kizamani

Hapo ndipo uwelewa wake ulipofika chukua kijiti cha uwelewa wake changanya na za kwako kusongesha safari ya maarifa kwake na kwa wengine badala ya kulaumu na kukaa kimya

Rudini kwanza shule muelewe teknolojia itumikayo kwenye usafirishaji kwa njia ya treni za umeme na hizi treni tutumiazo.

Kwa kuanzia anza kusoma alichoandika huyu mdau hapa chini:
Gauge ya rail zetu ni ya zamani,haifai kwa mitambo ya kisasa. maana yake tunapaswa tufumue tujenge upya SGR (Standard Gauge Rail), maelfu ya kilometres. .. Hivyo si shughuli ya kitoto,ni matrilioni mengi. pia hata mabehewa yake ni tofauti kabisa.

Mkimaliza hapo pia fuatilieni aina ya mabehewa na injini zitumiazo umeme na zile zitumiazo mafuta ghafi.

Mkishatambua utofauti wa hayo rudi tena hapa jamvini halafu msome hoja ya mleta mada ni ipi.

Jengeni hoja sio mnaropoka vitu msivyojua...
 

Soma kwa umakini na acha uoga!,usihisi wote wanaomuunga mkono mtoa hoja kwa kila alichoandika na wala hawasemi wachukuwe mawazo yake kama yalivyo wayapeleke kwenye utekelezaji bali tunamuunga mkono kwamba anahoja ambayo inaweza fanyiwa kazi na kuboresha Maisha ya Watanzania,wahisi hatujui mifumo ya reli inatakiwa mipya? wahisi hatujui kwamba treni zenye miundo tofauti na hizi za mkoloni? wahisi hatujui kunahitajika mifumo dhabiti ya nishati? lakini kwa waona mbali haya yote na mengine yanawezekana kwenye nchi yetu kama tutaweka vipaumbele vyetu vizuri na kutumia rasilimali tulizonazo vizuri
 
Khaa!!! Wazo zuri ila umekurupuka. Mipango ya nchi hupangwa na wanasiasa tena majukwaani. Mara elimu itakuwa bure hadi chuo kikuu, mara cement itakuwa buku 5 nk nk. Mawazo kama haya ya uwekezaji wa mudamrefu hawana. Hebu tuachane na mawazo magumu kutekelezeka kamahayo. Tuboreshe barabara hadi kule kijijini tumuokoe mkulima anayeharibikiwa na mazao kisha tuboreshe reli zetu zifanye kazi kwa 100% halafu ndiyo tuangalie hiyo reli ya kwenda kasi tunaihitaji? Kama tunaihitaji tuijenge. Tukiishaijenga basi na sisi tumpeleke mtanzania mwezini mbona wenzetu wanafanya hivyo??
 
Mkuu mleta mada nimemsoma kwa makini na hoja yake nimeielewa.

Kwanza lazima utambue kuwa kuna challenges nyingi kwenye uwezeshaji wa mawazo yake, challenges hizo ni za kiteknolojia, kiutendaji na uendeshaji (kimfumo).

Pia lazima utambue kuwa treni za umeme hizo anazoongelea huyu ndugu ni mahsusi kwa ajili ya usafirishaji wa watu na sio mizigo.

Hao Wachina anaowalilia mizigo yao inasafirishwa na treni kama hizi hizi tulizonazo na wala sio fast trains.

Kwa hoja zangu tu hizo mbili ukiacha zile za kiufundi za mwanzo bado utagundua hoja ya ndugu yangu bado haina tija.

Muhimu labda tujadili namna ya kuboresha huu mfumo tulionao kwanza...

 
Nasikia zitajengwa Pemba
acha utoto, umeshakua. Hivi unadhani hatuna uchumi wa kuwa na treni za aina hiyo. Acha kuwaza kinafiki au una hofu malori/mabasi yako yatakosa wateja

Ndiyo nyie mnaofanya kila jitihada treni zisiwe barabarani kwa ajili ya matumbo yenu
 
Lakini pale mwanzoni ulijifanya hamnazo kwa kile ulichopost, Kiongozi. Pale uliteleza. Hoja yake ina tija ndg yangu. Hivi wewe kwa mtazamo wako unakubaliana na hali iliyopo ya kutokuwa treni ambayo inafanya kazi kwa ufanisi, wakati katk mataifa yaliyoendelea ziko on, sisi tunaziua

tuna safari ndefu kama wasomi ndiyo mnawaza hivi basi tuna safari ndefu sana kufika kwenye neema
 

Kwa umeme upi? Kwanza tuwe na umeme wa kutosha na pili miundombinu iwe katika hali ambayo umeme hautakatika ovyo.
Baada ya kuweka sawa hayo, ndiyo ndoto za treni za haraka zije
 
Umeme wa kuwashia taahamna utatoka wap wa kuendesha Ttain Dar-Kigoma?
 
Hii 2014 bado una akili za kuomba-omba?...
 

Ukubwa(muundo) wa reli tuliyonayo sasa nchi nyingi duniani wameshaacha kuutumia kwani inalazimu treni zinazopita juu yake kubeba mizigo ya uzito mdogo na kasi ndogo mtoa mada anadadavua matatizo makubwa anayokabiliwa/wanayokabiliwa watu wa hali ya chini yawezekana hajayaeleza kwa kiasi ambacho wewe ulitaka aeleze ila ametoa mawazo murua ambayo yakifanyiwa kazi yataleta mafanikio chanya kwa Taifa letu,badala ya kumlaumu ebu anzia pale alipoishia kwenye hoja yake fanyia marekebisho ya msingi kisha yalete kwa mtazamo wa kujenga taifa badala ya kumkatisha tamaa.......
 
Mkishamaliza kubishana na watu8 mnipigie namba yangu ni ile ile ili nami nitoe mawazo yangu maana mnafahamishwa kitu chenye uhakika lakini mnaandamana. Hapa cha muhimu ni kuipiga tu chini CCM dunia hii tangu uhuru hadi leo maisha yale yale!!?
 
Kama kusukuma maji ni issue na train je? So unataka WA tz wore kifo Chao kiwe train. Tusifanye test kwenye life za watu

Acha ushamba wewe watakufaje? Sasa nkt umeme utawekwa kwa juu ya treni..mpk huko juu unaenda kutafuta nin sasa??
 
Vitu vingine mnapoamua kuandika mbele ya kadamnasi kama JF hakikisheni mna uelewa wa kutosha kwanza...

Mkuu uko sahihi! Inaelekea mleta mada hana uelewa wo wote kuhusu suala analozungumzia.

Mleta mada anadhani kuwa kitu muhimu kwa high speed train ni umeme tu!

Haelewi kwamba njia imara ya reli ndiyo muhimu kuliko vyote.

Kwa taarifa yake, sehemu nyingi za reli tuliyo nayo sasa haziwezi kuhimili mwendo zaidi ya 50kph, kutokana na wepesi wa reli na udhaifu wa tuta zinapokalia reli.
Sasa hata ukiweka treni za umeme zitakwenda mwendo gani?!

Kama reli iko imara, kuna injini za mafuta zenye uwezo wa kwenda hadi 200kph. Kwa wakati huu Tanzania tunahitaji zaidi ya mwendo huu?! Lets be realistic!
 
Tz we are not serious at all, kwa hiyo kwa sasa sitashauri kutumia umeme. Train za umeme zinahitaji watu waliomakini sana na utendaji wao, sio sisi labda baadaye , otherwise mtaua msmis ya wananchi. Vitu vidogo tu unaona serikali haichukui maamuzi, leo umeme unakatikankila bada ya dakika kadhaa...tutafika kweli? Hata kujenga miji yenu mnashindwa hadi mnaomba msaada China, sembuse na hili? Mmh
 
Ingewezekana kama wanene wangetilia mkazo upatikanaji wa umeme wa maji ambao gharama zake ni poa. Tatizo la wanene wetu ni politiki kuwa ndio kipaumbele huku wakijikita kwenye umeme wa mafuta.
 
Yani ndugu yangu ulivyoandika ni kama unamuandikia mtu mmoja msikivu kwelikweli.
SERIKALI SIKIVU HUENDA IKALIONA HILI.TUNGOJE.
 
Vitu vingine mnapoamua kuandika mbele ya kadamnasi kama JF hakikisheni mna uelewa wa kutosha kwanza...

Ndiyo maana ya jf, huo ndiyo uelewa wake mleta mada na wewe weka uelewa wako na mwingine ataweka uelewa wake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…