Tanzania ukiajiriwa Serikalini ni raha kuzidi kujiajiri kwa kipato sawa na mshahara wa aliyeajiriwa

Namba mbili na tatu inategemea umejiajiri vipi?
Mfano una daladala zako kadhaa mjini unasubiri jioni uletewe hesabu wala hautakua involved na kua kazini 7days a week.
Mtoa mada nadhani ni muajiriwa aliyekata tamaa na ametoa thread kama njia ya kujifariji.
 
Mmiliki wa daladala kaajiri madereva na kondakta.
Hao ndio wanaozungumziwa.
 
Wengine humu mnasema biashara sio ngumu wakati mmekuta alishakufungulia baba yako kafanya kukuachia urithi. Umekuta foundation imekaa vizuri we kazi kusugua kisigino tu Mtupishe
Sasa hapo ndio uone faida ya kujiajiri maana unawaachia urithi watoto mpaka wajukuu,wewe uliyeajiriwa ukifa unadhani kazi yako na mshahara wako wataurithi watoto wako?? Zaidi familia itapata msongo wa mawazo tu maana tegemezi umeshakufa.
NB:Baba/mama aliyeajiriwa ikitokea akifa anaiacha familia katika wakati mgumu sana maana yeye ndiye aliyekuwa tegemezi
 
1. Kila mtu akifanya biashara nani atakua mteja?

2. Nlishaandika huko juu. Una uhakika gani ukifa watoto wako watakua na uelewa wa biashara yako au watagain interest ya biashara yako. Umesomesha mtoto aje kuwa pilot ukimwambia akasimamie machine za kukobolea mahindi atakuelewa?

Endeleeni na nadharia zenu za madaftari ila asikwambie mtu serikalini kuna security kubwa sana.
Hata usiende mbali ile bima ya afya tu, imagine una watoto sita, wewe na mkeo wote mjikatie bima ya najali afya uone milioni zitakazokudondoka. Ila serikalini sio gharama kubwa.

Biashara hata ikiyumba vipi serikalini utapokea mshahara ila wajasiriamali wanayumba kweli.

Endeleeni kukaza fuvu ila wanaokula asali ni walioko serikalini na wana vitega uchumi. I rest my case
 
Sawa ana njaa lakini kumbuka sisi tunafanya kazi zetu, hatupangiwi na mtu nini cha kufanya ratiba zote tunazipanga wenyewe

Popote ambapo tunaona kuna mzunguko mzuri wa kupiga pesa tunawekeza

Tunafunga mahesabu ya mwaka mzima mwezi huu
 
Acheni kufananisha kuajiriwa na kujiajiri, kamwe mtu aliyeajiriwa hawezi kuwa sawa financially na mtu aliyejiajiri. Mtu aliyejiajiri ni lazima tu atakuwa juu siku zote
 
Na hakuna mtumwa tajiri sasa raia mil 61 wote watafute kazi serikalini? Mtu anaewaza kuajiriwa fkira zake ni za kimasikini

Sent from my PRA-LA1 using JamiiForums mobile app
 
Kujiajiri si rahisi kama mnavosimuliana kwenye vijiwe au uko chuoni kwenye course ya entrepreneurship. Sifa ya kwanza ya kutoboa Kwa kujiajiri ni uwe na roho ngumu na ukubali muda mwingine utapita njia za panya utoboe. Wengi ambao hawapiti njia za panya wako hivi mpaka leo, wengine wanaanguka.
 
Wengi hujipa moto majority ni majanga.

Wanaoacha ajira wakafanikiwa ni wale wenye nidhamu ya kazi kama akina Bill Gate.

Madoja hata wakienda kujiajiri wanaangukia pua au kwenye biashara haramu.
Hakuna atakaejitoa ajiran kama mvivu. Mana kujiajiri hakuhitaji relax hata second. Watu wanaopambana kwenye kujiajiri wanafanikiwa sana. Hii nimeona kwa mzee moja hiv amejiajiri Ana kampuni 3 lakin kulala kwake kwa machale pampja na kuwa na wafanyakaza zaid ya 50
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…