Tanzania ukiajiriwa Serikalini ni raha kuzidi kujiajiri kwa kipato sawa na mshahara wa aliyeajiriwa

Tanzania ukiajiriwa Serikalini ni raha kuzidi kujiajiri kwa kipato sawa na mshahara wa aliyeajiriwa

Mimi kwa experience yangu ya maisha naona wafanyabiashara wengi maisha nyumbani mazuri, wakati tupo wadogo ukiingia tu sebuleni kwa mfanyabiashara una notice utofauti na kwenu au nyumba za waajiriwa, nyumba za wafanyabiashara huwa zina vitu excess yani sebuleni kuna accessories ambazo muajiriwa ngumu kuwa nazo, nje usafiri wa kutosha alafu mara nyingi nyumba huwa wamejenga wao sio kupanga. Watoto wapo private schools

Tuseme tu ukweli wafanya biashara wengi japo wanaweza kuishi na stress sana ila maisha yao ndio hasa maisha ya mtanzania wa kipato cha kati, watumishi wengi (sio wote) sebuleni utakuta Tv nchi 32-43 , fridge na radio, sofa set moja na nje gari sana sana moja,wachache wana mbili basi, lakini nyumba za wafanya biashara madude mengi, huko nje gari nne na kuendelea
Mimi dingi mkubwa alikuwa mtumishi akafikia level ya ukuu wa idara, baadae akawa professor kabisa anapigisha mapindi chuo na kuandika miradi akastaafia huko. Ila maisha yalikuwa mazuri sana tu mbona gari 5 uwani watoto kasomesha shule za maana kisha chuo kasomesha Canada wote hakuna aliesoma chuo cha umatumbini 🤣🤣🤣 so inategemea ni level gani mtu kaajiriwa. Ajira sio mbaya ukiwa upo kwenye level zenye maslahi.

Ni mbaya tu kama uko kwenye level za laki 3 kwa mwezi.
 
Ni wapuuzi tu na wivu kudhani kuajiriwa ni Utumwa.

Huko Marekani CIA na FBI woote na Masenator na wakurugenzi wote mamilioni kwa mamilioni pale NewYork na New Jersey wameajiriwa ila mpuuzi mmoja amepaya jiko moja la kuuza Chips anaanz akunanga watu walio ajiriwa😆😆
🤣🤣🤣🤣🤣🤣 waliojiajiri na wanakula bata bongo hii sio wale wauza maji, ice cream za bhakresa, wakaanga viazi na mihogo na wabangaizaji wote waliojazama barabarani. Yani kiufupi kama hufanyi huduma na mtaji wako ni chini ya 2M huwezi kusema unainjoy kujiajiri maana wewe ni sehemu ya kuhangaika na huko kujiajiri. 🤣
 
🤣🤣🤣🤣🤣🤣 waliojiajiri na wanakula bata bongo hii sio wale wauza maji, ice cream za bhakresa, wakaanga viazi na mihogo na wabangaizaji wote waliojazama barabarani. Yani kiufupi kama hufanyi huduma na mtaji wako ni chini ya 2M huwezi kusema unainjoy kujiajiri maana wewe ni sehemu ya kuhangaika na huko kujiajiri. 🤣
Hahahh
 
Mkuu, wafanyabiashara wenye assets kama Ardhi nk hawawezi kupata mkopo kiurahisi ? Tuchukulie mfanyabiashara wa kipato cha kawaida anayeingiza faida milioni 3 kila mwezi, huyu atapata ugumu kupewa mikopo ?
Hizi zote ni dalili za kutaka urahisi, dunia hii mambo haya hayapo tena, chagua kuwa tajiri kwa kupitia njia ngumu ya kujiajiri au kuwa masikini kwa kupenda vitu virahisi, mara nyingi watu wanapenda ajira za serikalini kwa sababu hamna kuumia akili, kila kitu kimepangwa wewe ni kutekeleza tu na ndiyo maana waajiriwa wengi hususani wa serikali wakistaafu ndiyo mwisho wao. Unashangaa profesa wa uchumi au biashara anastaafu na bado anafia kazini kwa mikataba ya kufundisha. unaweza ukadhani alikuwa anawadanganya wanafunzi wake kuhusu biashara lakini ukweli ni kutokupenda kujishughulisha!
 
Mtu akimiliki nyumba Vigwaza na gari IST anaona maisha kayamaliza hahaha

Sent from my Pixel 5 using JamiiForums mobile app
Lazima aone kayamaliza mkuu,jua ni kali,maisha yamebadilika sana,hali ni ngumu.
Mtu kwao katoka familia duni kapambana kafikia hali hio,hakuwaza hata angekuja kumiliki gari
Katoboa huyo,acheni utani nyie 😀😀

Mambo yanakaba sana 😄
 
Hizi zote ni dalili za kutaka urahisi, dunia hii mambo haya hayapo tena, chagua kuwa tajiri kwa kupitia njia ngumu ya kujiajiri au kuwa masikini kwa kupenda vitu virahisi, mara nyingi watu wanapenda ajira za serikalini kwa sababu hamna kuumia akili, kila kitu kimepangwa wewe ni kutekeleza tu na ndiyo maana waajiriwa wengi hususani wa serikali wakistaafu ndiyo mwisho wao. Unashangaa profesa wa uchumi au biashara anastaafu na bado anafia kazini kwa mikataba ya kufundisha. unaweza ukadhani alikuwa anawadanganya wanafunzi wake kuhusu biashara lakini ukweli ni kutokupenda kujishughulisha!
Sio kwamba watu hawapendi kua matajiri

Ingekua hivo hapa jf kila mtu angekua safi,kua tajiri ni ngumu, pia inachangiwa na bahati na connections,hard work pekee haitoshi 🙆
 
Lazima aone kayamaliza mkuu,jua ni kali,maisha yamebadilika sana,hali ni ngumu.
Mtu kwao katoka familia duni kapambana kafikia hali hio,hakuwaza hata angekuja kumiliki gari
Katoboa huyo,acheni utani nyie 😀😀

Mambo yanakaba sana 😄
mtu wa kwanza kwenye ukoo kumiliki IST na mjengo ndani ya miaka 5 ya ajira tu. Utasemaje hajafanikiwa?
 
Mimi dingi mkubwa alikuwa mtumishi akafikia level ya ukuu wa idara, baadae akawa professor kabisa anapigisha mapindi chuo na kuandika miradi akastaafia huko. Ila maisha yalikuwa mazuri sana tu mbona gari 5 uwani watoto kasomesha shule za maana kisha chuo kasomesha Canada wote hakuna aliesoma chuo cha umatumbini 🤣🤣🤣 so inategemea ni level gani mtu kaajiriwa. Ajira sio mbaya ukiwa upo kwenye level zenye maslahi.

Ni mbaya tu kama uko kwenye level za laki 3 kwa mwezi.
Huyo dingi yako mkubwa mfananishe na sanga store,vunja bei na sandaland usiwafananishe na wauza chips.
Wauza chips wafananishe na walimu wa Certificate diploma wanaopokea chini ya laki 5
 
"Mahakimu" wa mahakama za mwanzo wana ratiba yao ya J'3,J'5 na Ijumaa tu.

Siku mbili wapo off kila wiki
katika kazi nazidharau na kuziogopa ni hizo za kuingia kwenye maisha ya watu binafsi , hakimu, polisi. .nk ni watu ambao maisha yao baada ya kustaafu kazini yanakuwaga ya hovyo na kujificha sana!
 
Ukweli ni kuwa Kuna walio ajiriwa lakin wanaishi kama wako motoni pamoja na hizo job securities zao .Na Kuna wengine wamejiajiri lakin kama wapo motoni vile vile kwa wanachokipitia.

All in all unaweza ukaajiriwa na bado ukafanya biashara zako pembeni mambo yako yakakuendea vizuri

Pia unaweza kujiajiri ukatusua vizuri sana na ukahisi kuajiriwa ni kupoteza muda na nguvu.

Kuna kipindi nilikuwa nafanya mishe zangu mwenyewe nilikuwa sipati changamoto kutoka kwa ndugu kutaka pesa Kila muda na ilikuwa naishi tu maisha fresh kabisa.

Ila sasa nimeajiriwa simu hazikati kwa ndugu kwa sababu wanaona uko serikalini inalipwa vizuri kumbe mshahara ni wakaida na ukisema utumie hiyo Hadi mwisho WA mwezi basi mshahara wako utakuwa haukutani na mwezi unaofuata.

Mwisho nimekuja kuconclude ni kuwa kujiajiri ni Bora x 10 KULIKO hizo job securities ZENU mnazozitolea macho na kiinua mgongo baada ya kufanya kazi miaka 30 .Ndio uje upate nssf ili uanze biashara ya daladala na mwisho WA siku ununue gari mbovu ufe kwa presha Bure !!!!!!

Ushauri wangu ni kuwa hata kama upo kwenye ajira tafuta any side hustle na utakuja kunishukuru baadae.!
 
Back
Top Bottom