Tanzania ya sasa ni ile aliyoona Oscar Kambona, Mwalimu Nyerere alikosea sana

walikua close kana kwamba hakuna mtu aliyeweza kusimama mbele ya mwalimu na kumuambia unachofanya sio, inasemekana the rest walikua ni wazee wa ndio mzeee

Mkuu shukrani kwa huu uzi.

Hata kama ukweli wa Oscar Kambona hautajulikana vizuri leo au kesho, bado historia ni mwalimu mzuri na kuna mengi ya kujifunza katika huu uzi na michango ya wadau.

Moja ya hayo ni kutenganisha majukumu ya uongozi wa umma na mahusiano binafsi kama urafiki, undugu wa damu, mapenzi n.k
 
kwenye vijiji vya ujamaa watu walifanyishwa kazi kwa nguvu...mbona mafanikio hayapo?
 

Nyerere alikuwa scholar wa kitu gani?
 
Hizi comments zindhihirisha namna gani Watanzania wengi tulivyojaa upumbavu.

Wengi humu wala hawajawahi kufuatilia historia yoyote, na wanarukia tu hoja zinazotolewa humu na kuzitolea hisia zao.

Inashangaza kuna mengi yaliyokuwa yanavumishwa tu na Watu wenye malengo yao na bado kuna Watu leo hii wanayarudisha na yakisomwa na kizazi kipya chenye upeo finyu wanaishia kuhemuka....kuna moja ya hotuba Mwalimu aliongea kwa hisia sana kuhusu uvumi uliokuwa unazuka kila kukicha nchini wakati huo na haswa kiini kikiwa hapo Dar es salaam.....alitoa mfano wa uvumi wa kuwa yeye anajiuzulu na kuhamia Uingereza na Wavumi walitoa hata safu mpya ya Uongozi.

Kiufupi kuna ombwe kubwa sana kwenye historia yetu na hii inawapa fursa wapotoshaji kuingiza fikra zao wakitumia vibaya ufahamu haba wa kizazi kilichopo.
 
Watu kushangilia kufeli kwa siasa za Mwalimu ni ushahidi tosha kuwa Waafrika/Waswahili hawakuwa/hatuko tayari kujitegemea.

Mwalimu aliamini kuwa chochote anachoweza kufanya Mzungu basi na Mswahili anaweza....kumbe hakuwa sahihi maana asili ya Mtu mweusi ni Mvivu, tegemezi na hana ubunifu.

Hivi kweli kuna Kizazi kinacholalama kwamba kwa nini Mwalimu alifunga milango tusipate sabuni na colgate zilizotengenezwa na Wazungu?, kabla ya Wazungu tuliishije?, yaani kuonjeshwa tu vya Wazungu basi tukawehuka?.... hivi hatuoni aibu kuishi Dunia ambayo tuna Mjomba wa kumtegemea kwa mahitaji yetu? Hivi huyo Mzungu wakati anaanza yeye alimtegemea nani?

Hivi kweli tunampiga vita Mtu aliyejitoa kwa hali na mali kutaka kumjengea Mswahili imani ya kuwa anaweza kuishi bila Mzungu?.

Kuna hotuba moja Mwalimu anatoa mfano wa Raisi wa Korea aliyeitwa na Vijana wake wakamuoneshe Trekta walilotengeneza na kwa bahati mbaya wakati wanamuonesha Trekta lilirudi nyuma badala ya kwenda mbele...Raisi yule aliwapa moyo na kuwaambia endeleeni maana mkirekebisha kidogo tu Trekta litaenda mbele...Mwalimu alimalizia kama utani kwa kuomba na yeye Vijana watengeneze Trekta linalorudi nyuma....sasa nani angetengeneza Trekta ikiwa vichwa vyote vinamuangalia Mzungu?.

Hivi inahitaji elimu gani kujua maono ya Mwalimu yalikuwaje kwa Mtu Mweusi?

Baadhi ya comment humu zinatia simanzi sana kwa Mtu yeyote anayejithamini na kuamini kuwa naye ameumbwa na Mungu kama wengine na hakuja duniani kuwa Mtumwa wa mwingine.

Wakati anaomba uhuru Mwalimu alijigamba kwa Wakoloni kwamba baada ya miaka kumi warudi waone Mswahili alivyofanya makubwa, huku nao wakimkebehi kwamba hakuna chochote kitafanywa na Mtu asiyeweza kutengeneza hata sindano. Hivi leo tunashangilia kufeli kwa hilo?, sasa hiyo ni aibu ya Mwalimu au sisi wote?, hivi kweli tunaona fahari kumpa Mzungu ushindi wa kucheka na kuuliza "kikowapi Watumwa tu nyie?"

Hivi ni nini haswa dhambi ya ujamaa?, kwamba Watu mna imani za dini lakini hamtaki kuamini kwenye kuishi pamoja kupendana na kufanya kazi pamoja, kuvuna pamoja na kula pamoja?, kufeli kwa Ujamaa sio kufeli kwa Mwalimu bali ni kufeli kwa utu miongoni mwa binaadamu...hivi kuamini kwamba ni vibaya wewe ule ushibe na jirani yako alale njaa nalo ni kosa?.

Baada ya uhuru na wakati anataka kujenga umoja Mwalimu aliweka wazi kuwa hawezi kujenga taifa ambalo limegawanyika, ambapo sehemu ndogo ya Watu wake wanamiliki mali huku wengi waliobaki ni hohe hahe...tena wachache hao wenye uwezo walikuwa ni wa ngozi nyeupe....kwamba Wahindi waendelee na maisha yao kama kikundi fulani maalumu na bado Mwalimu ajigambe kuwa anaongoza nchi moja na huru? .

Hivi wangapi wanafahamu kuwa baada ya uhuru kulishaanza kuzuka fukuto kuhusu wasio na asili ya Tanzania?. Kuna Waswahili walianza kuhoji kuwa kama hawa nao ni Wenzetu mbona hatuwaoni kwenye shughuli mbali mbali kama maandamano n.k... na nani kama sio Mwalimu aliyesimama kidete kuhakikisha hilo jambo halipati nafasi?.

Na kama Wanalalamika kunyang'anywa majumba yaliyovunwa hapa hapa kwenye ardhi yetu, hivi si huyo huyo Mwalimu pia aliyewanyang'anya taasisi za dini shule zao ili tu hata wasio waumini wa dini hizo wakasome huko?.

Mfano hapa Arusha ile shule ya msingi Meru ilikuwa ni ya Wahindi tu, wakati sisi tunaanza shule ndio tulikuta kidogo kidogo kunaanza kuwa na uwiano wa Waswahili na Wahindi huku idadi ya Wahindi ikienda ikipungua kadri siku zilivyokuwa zinaenda...sasa je hivyo ndio tulitaka Mwalimu atawale taifa likiwa na hayo matabaka?.

Hivi ni kizazi gani cha kulaumiwa haswa, ni kile cha enzi ya Mwalimu au hiki cha sasa?. Marehemu Mzee wangu pamoja na kuwa Daktari alikuwa pia anajua useremala, nyumbani alikuwa ana cherehani na alikuwa ananunua kitambaa na anatushonea nguo Watoto wake...nyie kizazi cha sasa mnaoimbiana nyimbo za "binuka nipachike" na mnashangiliana kama Mazuzu ndio mnakaa chini na kuanza kulaumu nyakati za Mwalimu?.

Ni kama uingie kwenye nyumba iliyojengwa na mwingine na kuwekwa samani zote, wewe Mswahili unachotaka ni kuketi tu kwenye sofa laini miguu uweke juu na remote control ya TV ya inchi 60 mkononi, huku Mwenye nyumba Mzungu anakuhudumia chochote unachotaka, maziwa, mayai, Kuku n.k....na kweli bado unadhani hapo upo salama?

Na akijitokeza Mswahili Mwenzako kukwambia hivi sio sawa turudi kwenye ile nyumba yetu ya Msonge tushirikiane tuitengeneze iwe kama hii unaanza kumtukana kwa kukukatisha starehe na kukupeleka kwenye taabu?.
 
ni kweli ,tufungue macho mkuu kama una chochote unachokifahamu kwasababu sisi tulishakuta mambo yamefanyika na sasa tunauliza kwanini hiki kilikua hivi? we need the answers
 
Eti Tanzania ilikuwa moja, unamjua Thomas Marealle wewe?
Mifumo hiyo ya ulinzi ina misingi ya ujamaa (nyumba kumi kumi).
 
Msingi wa yanayoendelea leo Tanzania kiuchumi na kisiasa mwanzo wake ni jinsi Nyerere alivyomfanyia Kambona. Kambona alikuwa kiongozi mwenye upeo mkubwa sana na aliona mbali sana kuwa Sera za Nyerere sizingeweza kuzalisha Tanzania waliyokuwa wanaipigania dhidi ya Mkoloni.

Kiburi cha Nyerere na watu wake ndo mwanzo wa Tanzania yetu kuanguka vibaya kiuchumi na kuwa na mfumo mbovu zaidi wa utawala unaotengeneza watu wanafiki wanaomzunguka mtawala mkuu ambao kazi yao sio kumwambia mtawala mkuu ukweli bali kumlisha maneno ya uongo ili matumbo yao yaendelee kushiba.

Kambona aliona mbali sana. Alipinga kabisa uanzishwaji wa Azimio la Arusha na akajiuzuru nafasi zake zote. Waliokuwa wanampinga na kumuungua mkono Nyerere ndo walioshuhudia nchi ilivyoanguka vibaya kiuchumi kutokana na sera mbovu za ujamaa, na Nyerere alipoondoka tu walizitupilia mbali sera za ujamaa na kuanzisha soko huria.

Kama Tanzania Leo tusingekuwa na ujamaa Leo Tanzania ingeweza kuwa nchi yenye uchumi mkubwa zaidi Africa maana kwa miaka ya 60 Tanzania ilikuwa na wakulima vijijini waliokuwa wakilima kwa tractors. Sasa hali ingeendelea kuwa vile hadi leo tungekuwa wapi???

Ukweli lazima usemwe, ipo siku lazima tutamkumbuka Kambona kama shujaa wa Taifa hili na ukweli utasemwa kweli kuwa Nyerere ndo chanzo cha hii Tanzania mbovu tuliyokuwa nayo leo.
 
Eti Tanzania ilikuwa moja, unamjua Thomas Marealle wewe?

Mifumo hiyo ya ulinzi ina misingi ya ujamaa (nyumba kumi kumi).

Nimeongelea kusini tena kipindi cha maji maji mbona umemleta Mangi wa kaskazi tena kipindi cha harakati za uhuru 1950s??

Tukirudi kwenye mada, hata habari za Thomas nyingi ni propaganda za kijima ili ionekane tupo sehemu salama huyu hana mbadala, hawezi kuzibika nafasi yake, yule na yule hawafai. Upuuzi fulani wakirusi enzi ya Stalin
 
nyerere aliingiza mambo binafsi kwenye maslahi ya taifa
 
Ni kweli mwl hakufanya kazi peke yake lazima wasaidizi kama hawa wawepo.. hii ni kawaida hata katika makampuni makubwa na taasisi zote zenye mafanikio rekodi huwekwa kwa maCEO licha ya kwamba hawa hufanya kazi kwa ushauri wa watu wachache nyuma yao. Leo hii microsoft imemfanya BillGate atambulike duniani kote ila tafuta historia yake utajua waliokuwa nyuma yake... Hata mpirani historia itamkumbuka sana Leonel Messi ila wapishi wake wakuu akina Iniesta, Xavi hawatakumbukwa kwa muda mrefu... Ndivyo ilivyo
 
nchi nyingi kua na changamoto nyingi kuliko TZ haimanishi tupo nafasi nzuri, Tungeweza kufanya vizuri zaidi ya hapa lakini tulifeli kwasababu ya mtu mmoja
Miaka 35 sasa tangu aachie ngazi, wote waliofuata nn wamekifanya cha maana... kitu kikubwa ambacho nyerere alitujengea na ni cha kujivunia ni amani tuliyonayo..... ukitembelea nchi nyingi za kiafrika utagundua mipasuko mikubwa iliyomo miongoni mwa raia wake.. nenda cameroon,nigeria, ethiopia, sudan, rwanda, SA hata tu hapo kenya utagundua hili....
 
Nimeongelea kusini tena kipindi cha maji maji mbona umemleta Mangi wa kaskazi tena kipindi cha harakati za uhuru 1950s??
Umoja huo wa kusini haukuwa wa kitanzania bali wa vikundi vidogo vidogo. Na hii ndiyo sababu Mjerumani aliweza kututawala, alipiga hapa leo, kesho akapiga pale, kidogo kidogo akaichukua nchi. Na hii ndiyo sababu ya Nyerere kuondoa uchifu ili kubadilisha mfumo ulioshindwa na kuweka mfumo madhubuti ambao hauingiliki kirahisi.

Uchifu ulikuwa unaangalia himaya ndogo sana ambayo kwa sasa ni sawa na eneo la kata au wilaya mmoja tuu. Nadharia ya nchi ya mamilioni ya watu hatukuwanayo waafrika. Nyerere alifahamu hilo na kuhakikisha anajenga utaifa ili nchi isije ingilika kirahisi kama walivyofanya wajerumani.
 

Mkuu hivi unaifahamu vyema historia ya vita vya Maji Maji?

Kwa Tanzania hivi ndio vita vya kwanza vyenye mwelekeo wa kitaifa, na havikupiganwa ndani ya himaya ndogo kama unavyodhani vilipiganwa mikoa zaidi ya minne kuanzia mikoa ya kusini hadi baadhi ya sehemu za mkoa wa Pwani.

Kitendo cha watawala wa enzi zile kuungana ili kumtoa mkoloni ilikuwa ni kielelezo cha utaifa kama haujui hilo mkuu.

Soma historia vizuri achana na historia ya sekondari ya kuunga unga.

Mwl. Nyerere alifuta uchifu ili aweze kutawala atakavyo yeye.

Uganda wanashindwa na Uchifu kwa sababu ya rushwa na viongozi corrupt walafi wa madaraka, hii haimaanishi na sisi tungeshindwa na mfumo wetu ule
 
Naona vitu vingi ulivyouliza vipo katika uzi hapo juu
 
Hujazuiwa kumuandika Kambona na historia yake badala ya MS na wale wazee wa mjini waliowatoa tongotongo washamba.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…