Tanzania yakubali ombi la Kenya kuwapatia madaktari 500

Tanzania yakubali ombi la Kenya kuwapatia madaktari 500

..asante kwa mchango wako mzuri.

..nakubaliana na wewe kwamba serikali yetu kushindwa kuajiri madaktari ni uzembe.

..natofautiana na wewe kuhusu suala la kuhamia Dodoma.

..kama tunataka Central corridor na Dodoma ziendelee basi tulenge kwenye sekta ya uchumi ambayo inashirikisha wananchi wengi wa maeneo hayo.

..kwa mfano, tungeweza kuwekeza ktk sekta ya zabibu na uzalishaji wa wine/mvinyo. Au, tungeweza kuwekeza ktk sekta ya mifugo kwa kuanzisha viwanda vya ngozi na kusindika nyama. Nakumbuka zamani kulikuwa na nyama toka Kongwa Dodoma, ukienda bucha unanunua kongwa steak.

..kwa hiyo maoni yangu, kuongeza thamani ya mazao yanayozalishwa Dodoma na Central corridor ni njia bora zaidi ya kujenga uchumi wa eneo hilo na kuinua kipato cha wananchi kuliko kujenga ikulu na kupeleka makao makuu ya wizara za serikali.

NB:

..nimeangalia miji mikuu kama Washington DC, Berlin,Ottawa, Moscow, New Delhi, yote haiko katikati ya nchi zao. Kwa hiyo dhana kwamba mji mkuu ukiwa katikati ya nchi tunapeleka serikali/huduma karibu na wananchi inawezekana haina mashiko sana.
Nimekuelewa mkuu

point yako ya mwisho ni kweli kabisa kwa sababu hata mimi niliona kuwa dodoma itahitajika kutumia nguvu nyingi ili kuisukuma kimaendeleo ukilinganisha na mikoa mingine kutokana na uchache wa rasilimali kulinganisha na mikoa mingineyo kama mwanza

Makao makuu yakiwekwa dodoma ni dhahiri kuwa watu wengi watahamia zaidi na hivyo kutengeneza soko kwa bidhaa zozote zitakazozalishwa na hii itakuwa na impact kubwa kwa wakazi wa mji huo kutokana na kukua kwa mzunguko wa pesa...

Ongezeko la watu huvutia uwekezaji na hupelekea eneo husika kukua, uwekezaji unaouhitaji waweza kufanywa na sekta binafsi kama eneo lenyewe litaonesha uwepo wa mazingira stahiki ya faida kutengenezwa...

Naliongelea hili kwa kuwa mimi nimeshakaa dodoma na hata sasa huwa ni mpitaji hivyo, nimeona hali ya muamko wa kiuchumi kutokana na hamisho hilo la makao makuu

Kwa sasa construction kwa dodoma ni kubwa sana na uwekezaji unaonekana kukua sana...
central corridor ni lazma itakua kwa uharaka kwa kutegemea serikali na sekta binafsi
 
Suala la madaktari lina kahistoria yake, ndio maana mwaka jana waliajiri baadhi kwa vituo vyote vipya vya afya kama Mlonganzila, vile vile serikali imeshasema itachukua madaktari 450 mwaka huu, ila hii haiwezi kuondoa surplus iliyopo mtaani.

Tatizo la sekta ya afya si la leo na wala haliwezi tatuliwa kwa siku moja na naona kama linaanzia kwenye sera huko, watanzania walio na bima ya afya bado ni wachache sana, sekta binafsi ndio inabidi iwe kiungo mkubwa kwa afya kwa mijini. Hauwezi kuajiri madaktari wakati hauna sehemu ya kuwapeleka, kuwaruhusu kwenda Kenya ni uamuzi wa busara kwa muda huu.

..Kenya wana export ma barmaid kuja Tz.

..sisi waTz tunasomesha MADAKTARI na kuwa export kwenda Kenya.

..halafu baadhi ya ndugu zetu waTz wanafurahia na kujivunia hali hiyo.

..mimi nasema hii ni HASARA kwa TANZANIA.

CC MK254, Nguruvi3, Tobaa
 
..Kenya wana export ma barmaid kuja Tz.

..sisi waTz tunasomesha MADAKTARI na kuwa export kwenda Kenya.

..halafu baadhi ya ndugu zetu waTz wanafurahia na kujivunia hali hiyo.

..mimi nasema hii ni HASARA kwa TANZANIA.

CC MK254, Nguruvi3, Tobaa

JokaKuu Hehehehe
Yaani ina maana sisi tunaokuja huko Tanzania na utaalam wetu wote huu unatuona bar maids.....

Anyway nimefuatilia hoja zako na pakubwa nakubaliana na wewe, lakini kila kitu kina immediate and long term solutions, leo hii mna vijana waliosomea taaluma ya udaktari wamejaa kitaa, ilhali serikali yenu inadai haipo tayari kuwaajiri wote kwa mpigo, halafu sisi jirani wenu Kenya, vijana wetu wananyakuliwa wote kila wakimaliza chuo, na tunahitaji kuongeza idadi ya mdaktari, sasa tumewaomba wenu hao ambao badala ya kupoteza muda kitaa angalau wapate ajira na ujuzi, wakirudi kwenu watakua wamebobea.

Kumbuka madaktari Kenya wameongezwa mshahara, hivyo hao vijana wenu watalipwa kitita cha mshahara hata zaidi ya madaktari wenu wazoefu. Hivyo wale watarudi nyumbani kama wana akili watawekeza pamoja na kuwa na ujuzi. Hili jambo sio la kuponda kaka yangu Joka Kuu, unafaa kuliangalia kwa jicho la pili na la tatu.

Kuna wakati inabidi kuwaacha wataalam kufuata ajira za nje pamoja na kwamba nchi yao inawahitaji. Wengi huwekeza nyumbani, hurudi kama wamejipanga, huboresha na kupanua wigo na mawazo yao. Mimi binafsi nimetoka mara kadhaa ndani ya nchi yangu, sio kwamba utaalam wangu hauhitajiki nyumbani, lakini kuna wakati inabidi maana unakuta nimepata deal nzuri nje kwa mfano huko huko Tanzania, naifuata na kuwekeza nyumbani.

Najua utasema yale ya uwanja wa Chato, uhamaji wa kwenda Dodoma na mengineyo, hayo sijui tija yake kiuchumi lakini kwa hili la sasa na immediate solution, wacha vijana wenu wachangamkie hii fursa.
 
..Kenya wana export ma barmaid kuja Tz.

..sisi waTz tunasomesha MADAKTARI na kuwa export kwenda Kenya.

..halafu baadhi ya ndugu zetu waTz wanafurahia na kujivunia hali hiyo.

..mimi nasema hii ni HASARA kwa TANZANIA.

CC MK254, Nguruvi3, Tobaa
Cha muhimu ni well being ya wataalamu wetu, ya wakenya sio matatizo yetu. Hawa vijana wamekaa mtaani muda wote kwenu haikuwa tatizo, kusikia wanaenda Kenya sasa imekuwa tatizo kubwa kwenu, hiyo ni ishara unaendeshwa na siasa na si uhalisia. Njoo kwenye uhalisia, je serikali ina uwezo wa kuajiri madaktari 2000 kwa mpigo mwisho wa mwaka. Acha vijana wakapate chochote na wao.
 
Back
Top Bottom