Tanzania yazuia ndege za Kenya Airways kutua nchini. Ni baada ya Kenya kutoruhusu ndege za Tanzania kubeba mizigo Kenya

Tanzania yazuia ndege za Kenya Airways kutua nchini. Ni baada ya Kenya kutoruhusu ndege za Tanzania kubeba mizigo Kenya

Angalau hapa mwanasheria nguli wa TCAA msomi Hamza Johari amefanya uzalendo unaukubalika, kutetea maslahi ya Tanzania.

Na katazo hili liwe siyo tu baina ya Nairobi na Dar es Salaam tu bali Kenya na viwanja vyote vikubwa vya kimataifa vya nchini Tanzania.

Tanzania blocks Kenya Airways flights in reciprocity dispute​

thecitizen.co.tz
https://www.thecitizen.co.tz › national
Tanzania blocks Kenya Airways flights in reciprocity dispute | The Citizen

37 minutes ago — Tanzania blocks Kenya Airways flights in reciprocity dispute. Monday, January 15, 2024.
Missing
 
View attachment 2872704



Taarifa ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania imeeleza kuwa kwa niaba ya Mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imeamua kufuta vibali vya Shirika la Ndege la Kenya (KQ) kuendesha safari za abiria kati ya Nairobi na Dar es Salaam kuanzia 22 Januari 2024

Taarifa hiyo imedai hatua hii ni baada ya uamuzi wa mamlaka ya anga ya Jamhuri ya Kenya kwenda kinyume na Kifungu cha 4 cha Mkataba wa Maelewano kuhusu Huduma za Ndege, kati ya Tanzania na Kenya yaliyotiwa saini Novemba 24, 2016 Jijini Nairobi

Kufuatia Uamuzi huu, hakutakuwa na safari za ndege za abiria kwa KQ kati ya Nairobi na Dar es Salaam kuanzia tarehe 22 Januari 2024
Hao Punda wa Kunyaland ni kwenda nao hivyo hivyo.

Wana chuki sana na Tzn sijui Huwa yakoje
 
Kumekucha.
Kama kupata tupate wote, kwa nini unazuia ATCL isinlbebe mizigo Tanzania na kutua Kenya.

Nadhani kuna haja ya kutumia forum za kidiplomasia za EAC. Vinginevyo tuambiwe EAC imeshindwa kukutanisha viongozi wake ili kutatua mambo yao kwa amani.
View attachment 2872698
Sababu wao walijiandaa kutufungia, basi hata wakitufungulia itabidi na sisi tutumie angalau mwaka hivi tukijiandaa kuwafungulia...wangese sana hawa wakenya.
 
EAC ni muungano wa kihuni sana na utasambaratikaga kihuni sana,Rwanda na Burundi wana bifu,Rwanda na Congo bifu,Uganda na Kenya bifu ya biashara ya mafuta na sasa Kenya na Tanzania tena. Muungano kama EU wana mashariti magumu sana kupokea wanachama,ndio maana huwezi sikia wanakwaruzana wao kwa wao.EAC ni muungano wa kihuni
Huwezi kuunganisha mabomu madogo madogo kadhaa halafu utegemee usalama. Hizi nchi za EAC zote zina matatizo ya ndani makubwa tu. Sahihi ilitakiwa wa-draft sheria na kanuni (tena wawape third party kufanya hii kazi) halafu kuwe na ulazima wa kila nchi ku-adhere to them. Kwa mfani kuwe na kanuni kuwa kila nchi ni lazima uchaguzi uwe baada ya miaka mitano na kuwe na ukomo wa urais bila kusahau uchaguzi huru na wa haki.
 
Safi sana hiyo kitu kwenye diplomasia ya kimataifa inaitwa scratch my back I Scratch yours

Safi sana Raisi Samia uko vizuri sana kwenye hili

Nipongeze na wataalamu walioshauri uamuzi huo uchukuliwe wako vizuri kichwani

Serikali iendelee kuajiri walio vizuri sana vichwani kushika nafasi nzito Raisi hawi na kazi nzito sana

Wataalamu wamenifurahisha sana Kwa hili limeenea kiusomi,kiutaalamu na kiuzalendo
 
Kenya hufanya hujuma sana za kichini chini kufanya abiria wanaokuja Tanzania kupitia JKIA Jomo Kenyatta International Airport Nairobi kwa kuwaweka masaa kibao ili abiria hao waseme usafiri kwenda Tanzania ni mgumu sana hivyo kama masuala ya kiutalii, biashara n.k bora wamalizie Nairobi Kenya badala ya kwenda 'shamba kijijini' Tanzania ambapo usafiri wa ndege ni mgumu sana...
 
Kumekucha.

Kama kupata tupate wote, kwa nini unazuia ATCL isinlbebe mizigo Tanzania na kutua Kenya.

Nadhani kuna haja ya kutumia forum za kidiplomasia za EAC. Vinginevyo tuambiwe EAC imeshindwa kukutanisha viongozi wake ili kutatua mambo yao kwa amani.

======
Taarifa ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania imeeleza kuwa kwa niaba ya Mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imeamua kufuta vibali vya Shirika la Ndege la Kenya (KQ) kuendesha safari za abiria kati ya Nairobi na Dar es Salaam kuanzia 22 Januari 2024

Taarifa hiyo imedai hatua hii ni baada ya uamuzi wa mamlaka ya anga ya Jamhuri ya Kenya kwenda kinyume na Kifungu cha 4 cha Mkataba wa Maelewano kuhusu Huduma za Ndege, kati ya Tanzania na Kenya yaliyotiwa saini Novemba 24, 2016 Jijini Nairobi

Kufuatia Uamuzi huu, hakutakuwa na safari za ndege za abiria kwa KQ kati ya Nairobi na Dar es Salaam kuanzia tarehe 22 Januari 2024
View attachment 2872698


Badala ya kufungua mjadala mnazuia, wanajua connection za KQ kuja Tanzania zilivyo muhimu?
 
Wakenya hata mipakani kwao wana wasumbua sana watanzania, maafisa wana kuta wana shout unakwenda Kenya kufanya nini? Sema tu kama una kwenda kwa mchumba wako, mambo useless kuuliza vitu vya kijinga kijinga kama mtu ambae hana elimu, EAC inatakiwa irahisishe biashara na muungiliano wa watu.

Ujinga mwingine ni kuzuia kitu cha mwenzio kisiingie nchini mwako wakati wewe unapeleka katika nchi nyingine.

Hii hatua ni nzuri ambayo serikali imechukua.
 
Angalau hapa mwanasheria nguli wa TCAA msomi Hamza Johari amefanya uzalendo unaukubalika, kutetea maslahi ya Tanzania.

Na katazo hili liwe siyo tu baina ya Nairobi na Dar es Salaam tu bali Kenya na viwanja vyote vikubwa vya kimataifa vya nchini Tanzania.

Tanzania blocks Kenya Airways flights in reciprocity dispute​

thecitizen.co.tz
https://www.thecitizen.co.tz › national
Tanzania blocks Kenya Airways flights in reciprocity dispute | The Citizen

37 minutes ago — Tanzania blocks Kenya Airways flights in reciprocity dispute. Monday, January 15, 2024.
Missing
Hongera sana Johari kusimamia taaluma,utaalamu na uzalendo vyote Kwa mpigo wengine waige kwako
 
Back
Top Bottom