Kabende Msakila
JF-Expert Member
- Oct 7, 2020
- 1,809
- 1,692
Wana JF,
SALAAM!
Nawauliza kuna tatizo gani nchini KWETU hususan kwa hawa wanaojiita watetezi wa wananchi kupitia forums za vyama vya siasa. Naona kila jambo linaloanzishwa na Serikali liwe zuri au baya linapita bila kikwazo.
Mfano:-
(a). Tozo. - hizi zimeanzishwa kimzahamzaha lkn mwisho wake zimepenya na kuwa mwiba kwa wananchi. Hakuna uhalali wa kuanzia rundo la vikodi ktk mazingira ambayo uchumi unakumbwa na anguko;
(b). Miamala ya simu - hii nayo imeingiziwa na wachumi uchwara kwa madai ya kuongeza mapato ya Serikali lkn wakati huo mzigo ukibebwa na walalahoi. Watu wamepiga yowe lkn vyama viko kimya, SASA MBONA SIONI DHIMA YA KUANZISHWA KWA VYAMA VINGI!
(c). Miamala ya benki - hii imepita na watumiaji wa benki kuanza kukatwa fedha isivyo halali kwa kuwa fedha hizo kwa mfanyakazi anakuwa ameshakatwa kodi, kwa mfanyabishara anakuwa ameshalipa kodi - SASA vyama vimefyata mkia as if hili jambo ni zuri;
(d). Kikokotoo - kimeletwa kikilenga watumishi wa umma zaidi. Mtu afanye kazi hadi at age ya 60 halafu pension yake uikate na kubaki nayo huku ukimlipa mafungu mafungu. Hili ni unyanyasaji na ukilitimba dhidi ya watumishi. SASA VYAMA VINGI VYA SIASA NCHINI VINA MSAADA GANI KWA WANANCHI?
Nimeandika haya nikipenda vyama vijitathmini na kujikosoa vinginevyo ruzuku zetu wanazokula ni moto wa laana utakaowalamba.
Msakila M Kabende
Kakonko - Kigoma.
SALAAM!
Nawauliza kuna tatizo gani nchini KWETU hususan kwa hawa wanaojiita watetezi wa wananchi kupitia forums za vyama vya siasa. Naona kila jambo linaloanzishwa na Serikali liwe zuri au baya linapita bila kikwazo.
Mfano:-
(a). Tozo. - hizi zimeanzishwa kimzahamzaha lkn mwisho wake zimepenya na kuwa mwiba kwa wananchi. Hakuna uhalali wa kuanzia rundo la vikodi ktk mazingira ambayo uchumi unakumbwa na anguko;
(b). Miamala ya simu - hii nayo imeingiziwa na wachumi uchwara kwa madai ya kuongeza mapato ya Serikali lkn wakati huo mzigo ukibebwa na walalahoi. Watu wamepiga yowe lkn vyama viko kimya, SASA MBONA SIONI DHIMA YA KUANZISHWA KWA VYAMA VINGI!
(c). Miamala ya benki - hii imepita na watumiaji wa benki kuanza kukatwa fedha isivyo halali kwa kuwa fedha hizo kwa mfanyakazi anakuwa ameshakatwa kodi, kwa mfanyabishara anakuwa ameshalipa kodi - SASA vyama vimefyata mkia as if hili jambo ni zuri;
(d). Kikokotoo - kimeletwa kikilenga watumishi wa umma zaidi. Mtu afanye kazi hadi at age ya 60 halafu pension yake uikate na kubaki nayo huku ukimlipa mafungu mafungu. Hili ni unyanyasaji na ukilitimba dhidi ya watumishi. SASA VYAMA VINGI VYA SIASA NCHINI VINA MSAADA GANI KWA WANANCHI?
Nimeandika haya nikipenda vyama vijitathmini na kujikosoa vinginevyo ruzuku zetu wanazokula ni moto wa laana utakaowalamba.
Msakila M Kabende
Kakonko - Kigoma.