Naomba tukatendee haki haka katoto!. Mwenye mamlaka ya kutaja chanzo cha kifo ni daktari, na mwenye mamlaka ya kumtaja mhusika ni jeshi la polisi!.
Nashauri subirini taarifa ya dakitari kuhusu chanzo cha kifo. Mpaka sasa hakuna uthibitisho kuwa Lulu alimsukuma, inawezekana kwenye purukushani hiyo, ni Kanumba mwenyewe ali bugi step akateleza na kuanguka bila kusukumwa na yoyote!.
Hata kama ni kweli Lulu alimsukuma, chanzo cha kifo sio lazima kiwe kimetokana na kusukumwa!. Inawezekana Kanumba alikuwa na heart problem, pressure etc, hivyo alipokasirika pressure zikapanda, au akapata heart failure ndipo akaanguka!.
Hata kama ni kweli alijigonga, subirini madaktari wathibitishe chanzo cha kifo ndipo tuendelee kujadili!.
Najua msiba huu ni huzuni kubwa, lakini nawaombeni sana, lets not be judgemental kwa Lulu!.
Mimi ni miongoni mwa waumini wakubwa wa the doctrine of "karma", kuwa there is nothing new under the sun, hakuna coincidence wala bahati mbaya, lolote ambalo limetokea, lilikuwa litokee tuu, yaani siku ya mpendwa wetu Kanumba ndio ilikuwa imefika, saa ilipotimia Mungu akamuita, hata asingesukumwa, angefia usingizini!.
After all, there is life after life and life before life!, death ni change tuu ya life form from physical body to spiritual body!.
Rip Kanumba.
Pasco