Tanzanian traditional local foods

Tanzanian traditional local foods

Umekuwa mtu wa kwanza kwenye uzi huu kuutambua ugali huu, tafadhali tuelezee kama unafahamu maandalizi yake mpaka kupelekea muhogo huo kuwa na rangi hiyo, pia unaweza kututanabaisha ugali huu ni maarufu kwa wenyeji wa mkoa gani.
Ugali wa muhogo usiokuwa mweupe kabisa(Nyange/Makopa),utokana na njia moja ya kutengenezwa.
Kwanza ni aina ya muhogo wenyewe,mara nyingi muhogo unaotengezwa unga huwa ni muhogo mchungu usioweza kuchemshwa na kuliwa ukitolewa tu shambani.
Ugali huu wa muhogo wenye rangi za weusi,utengenezwa kwa njia ya KUVUNDIKA.
Muhogo utolewa shambani na kumenywa na kisha kuwekwa juani kwa siku kadhaa kulingana na uhitaji wa rangi.
Muhogo ukaa juani kati ya siku 2 hadi 5 kutegemea mapenzi ya mtumiaji na kiwango cha jua.
Ili muhogo uwe mweusi sana utaanikwa kwa siku 2 au 3 tu.
Kisha uandaliwa sehemu ya kuvundikia kwa kutumia majani ya mzima au mgomba kwa kutandazwa chini kwa urefu usiopungua nchi 3 toka chini,kisha unyunyiziwa maji hayo majani na kupangwa muhogo juu yake,kisha unyunyiziwa maji huo muhogo uliopangwa na kisha unafunikwa na majani juu na pembeni kiasi cha kuweza kutengeneza joto kali,na unyunyiziwa maji tena juu ya hayo majani funikia.Baada ya hapo usubiriwa kwa siku 5 hadi 7 ndiyo unakuwa tayari.Utolewa na kuanikwa juani mpaka unakauka kabisa na unakuwa tayari kwa kuhifadhiwa,kuchemshwa kama kitafunwa au kusagwa kuwa unga.

Mikoa wanaofanya hivi ni Tabora,Shinyanga,Mwanza na Mara.
 
MATOWOLWA asili ya utengenezaji wake ni mkoa wa Tabora hasa wilaya ya Sikonge.Ni njia iliyotumiwa tangu zamani na wahenga wa mkoa huo ikiwa ni njia ya kuhifadhi chakula kwa muda mrefu.Matowolwa uweza kuhifadhika kwa miaka hata zaidi ya mitatu bila ya kuharibika wala kubunguliwa.Na ndiyo njia bora zaidi inayokuwezesha kuhifadhi zao la viazi vitamu kwa muda mrefu zaidi.
MICHEMBE/MAKEWE ni njia nyingine inayotumiwa na makabila ya mikoa ya Tabora,Shinyanga na Mwanza ya kuhifadhi viazi vitamu kwa muda mrefu japo hivi vikikaa sana uweza kubunguliwa na wadudu.Nadhani asili ya utengenezaji wa aini hii ni mkoa wa Shinyanga.
N.B
Mkoa wa Tabora unaweza kuwa ndiyo mkoa unaoongoza kwa njia za kuhifadhi mazao ya chakula na mbogamboga kwa muda mrefu zaidi kwa njia za asili.
Unyamwezini utapata mboga za majani zilizo kaushwa kama Nsansa (majani ya kunde yaliyo chemshwa na kisha kuanikwa),Nswalu (Mlenda wa asili uliokaushwa na kusagwa),Ntwili (Karanga zilizokaangwa na kusagwa),Uyoga ulikaushwa kwa jua,Ntole (nyanya chungu za asili)pia ukaushwa kwa jua na kuhifadhiwa.
Nyama uweza kuhifadhiwa kwa kubanikwa au kupakwa chumvi na kuanikwa juani au kuhifadhi nyama mbichi kwa kulowekwa kwenye asali kwa muda wa hadi mwaka.
Duh! Kumbe kuna mikoa ina utajiri wa maarifa katika uhifadhi salama na asili wa chakula na hatufahamu chochote kile kuihusu, umenifumbua macho kuanza kuifuatilia mikoa hii hususani Tabora kujifunza kitu katika tamaduni na njia bora za uhifadhi vyakula kwa kipindi kirefu pasina gharama kubwa kitu ambacho ni muhimu kwa taifa katika nyakati mbaya au za dharura kujihakikishia utoshelevu na usalama wa vyakula, siyo tu wananchi kuitegemea serikali kwa kila kitu linapokuja suala la akiba ya chakula katika nyakati ngumu yenyewe tu ndiyo iwatunzie kisha iwagawie bali hata wao kuwa na maarifa muhimu kama haya yakuweza kuwavusha ni msaada mkubwa kwa nchi na kipimo tosha kwa jamii iliyostaarabika ya kiafrika.
 
Ugali wa muhogo usiokuwa mweupe kabisa(Nyange/Makopa),utokana na njia moja ya kutengenezwa.
Kwanza ni aina ya muhogo wenyewe,mara nyingi muhogo unaotengezwa unga huwa ni muhogo mchungu usioweza kuchemshwa na kuliwa ukitolewa tu shambani.
Ugali huu wa muhogo wenye rangi za weusi,utengenezwa kwa njia ya KUVUNDIKA.
Muhogo utolewa shambani na kumenywa na kisha kuwekwa juani kwa siku kadhaa kulingana na uhitaji wa rangi.
Muhogo ukaa juani kati ya siku 2 hadi 5 kutegemea mapenzi ya mtumiaji na kiwango cha jua.
Ili muhogo uwe mweusi sana utaanikwa kwa siku 2 au 3 tu.
Kisha uandaliwa sehemu ya kuvundikia kwa kutumia majani ya mzima au mgomba kwa kutandazwa chini kwa urefu usiopungua nchi 3 toka chini,kisha unyunyiziwa maji hayo majani na kupangwa muhogo juu yake,kisha unyunyiziwa maji huo muhogo uliopangwa na kisha unafunikwa na majani juu na pembeni kiasi cha kuweza kutengeneza joto kali,na unyunyiziwa maji tena juu ya hayo majani funikia.Baada ya hapo usubiriwa kwa siku 5 hadi 7 ndiyo unakuwa tayari.Utolewa na kuanikwa juani mpaka unakauka kabisa na unakuwa tayari kwa kuhifadhiwa,kuchemshwa kama kitafunwa au kusagwa kuwa unga.

Mikoa wanaofanya hivi ni Tabora,Shinyanga,Mwanza na Mara.
Asante sana mkuu, sijui nikushukuru vipi kwa darasa lako maridhawa maana masomo kama haya hatuyapati shuleni bali ni maarifa tunayoyaishi na kuyaacha yaishilie zake pasipo kunukuliwa mahali popote pale kwa vizazi vijavyo, mwisho wa siku sayansi hii ya asili ya uandaaji vyakula ya kiafrika kabisa ambayo ni niyakuvutia na yenye kuakisi uasilia wetu tunaipoteza na kuifukia kabisa, kizazi kijacho kitaishia kutusoma kama mababu ambao hawakuwaachia urithi wowote vizazi vyao kuhusu asili na tamaduni zao, licha ya kwamba walikuwa wasomi na siyo kama kizazi cha enzi za ukoloni.
 
Kula kifamilia/kujumuika pamoja kijamii
Screenshot_20230808-094917~2.jpg
Screenshot_20230808-094850~2.jpg
Screenshot_20230808-094833~2.jpg
Screenshot_20230808-102809~2.jpg
Screenshot_20230808-094035~2.jpg
 
Back
Top Bottom