Tanzanite iliyonunuliwa na Serikali yavunja rekodi kwa ukubwa duniani | Inaweza kutumika kukuza Sekta ya Utalii

Af yakae makumbusho ya taifa au sio
 
Napinga hoja, siungi hoja mkono, tanzanite tayari ni brand kubwa hakuna kubadilisha hilo zaidi ya kuwekeza kwenye promotion zaidi
 
Watanzania kwa mapendekezo tu hawajambo, wengine watakuja kusema yapewe jina la mheshimiwa sana!
 
Yaani wananzengo mna mshawasha na hayo majiwe duh!

Wazo lako ni zuri sana ila unadhani kwa njaa ya hela iliyopo kwa serekali sasa hivi wataweza kukaa na Bilioni 8 zipo tu kwenye kioo watalii wanazitazama? Hiyo miradi na mabombadia yaliyoagizwa we huyaoni?
 
Wamenyamaza labda walipewa hela yao...ila kulia na kucheka zote ni kelele.. .. ..walipatwa!
Umenifanya nikumbuke wakulima wa korosho.

Apo hata akipewa ataombwa bilion 1 kufadhili CCM . Mda si mrefu ataibukia ikulu ili wakamdende vizuri.
 
Yamekuja kipindi kizuri kweli kweli, na tukumbuke mawe yametoka ardhi ya Tz ambayo ni ya serikale.
 
Nadhani wazo la kuifanya kivutio cha utalii limesikika.



 
Wazo zuri, ila sasa ulinzi wake sasa si unajua tena wabongo kwa mishemishe? Unaweza kuta wajanja wameibuka nayo na kubadilisha na kanya boya (just thinking loud).

Nina swali lingine hivi hiyo bei aliyopata dogo ndiyo market price ya dunia? Yaani the same stones huko majuu inaweza kuuzwa kwa bei hiyo au ya juu zaidi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…