Serikali hii IMEMDHULUMU huyo jamaa mabilioni mengi sana. 15kg ni sawa na 75,000 carats (1 carat is equal to .0002kg)
Na bei ya carat moja kutokana na daraja la Tanzanite ndiyo hiyo hapo chini.
Tukichukia hata bei ya chini kabisa ya $300 kwa carat moja. Kwa 75,000*$300 angepata $22,500,000 times conversion rate ya 2,300 angestahili kupata shilingi 51.7 billions.
For richly colored AAA Tanzanite, 1ct is approximately worth $300-$425 per carat. 2ct sizes reach $450-$650 per carat. 3 carats and up will reach $650-$750 per carat. The changes taking place in Tanzania makes tanzanite a very good investment stone.
Hapana. Bei hiyo ni kwa a finished cut and polished stone.
Serikali imenunua rough stone ambayo bado haijakatwa wala kuwa polished. Lakini maswali ni mengi.
1. Nani Mnunuzi?
Tunaambiwa mnunuzi ni Serikali kupitia Wizara ya Madini na Benki Kuu ya Tanzania. Wizara ya Madini haijawahi kuwa mnunuzi wala muuzaji wa madini. Leo wamebeba jukumu hilo.
Imekuaje leo miezi michache kabla ya Uchaguzi, wizara hii imenunua Tanzanite ikisindikizwa na simu kutoka kwa Raisi kutoa pongezi? Je, kuna bajeti katika wizara hii inayoruhusu wizara kununua madini kutoka kwa wachimbaji wadogo na wakubwa?
Ni muhimu hili swali likajibiwa ili DEALERS na BROKERS wajue wana ushindani mpya kwenye soko la ununuzi wa madini.
Ni muhimu pia utaratibu huu wa wizara kununua madini ukawekwa wazi ili WAUZAJI na WACHIMBAJI wakajua soko lao ni pana. Inaonekana Wizarani bei ni nzuri.
2. Thamani ya Tanzanite
Thamani ya Tanzanite inatokana na ubora wa jiwe kwenye rangi, uchongaji wake na mwisho mwelekeo wa soko (demand and supply).
Swali ni, nani kathaminisha Tanzanite iliyouzwa? Ni muhimu kujua thamani hiyo ilizingatia jiwe ambalo limeshakatwa na linahitajika sokoni na kwa grade ipi?
Uthaminishaji huu ndiyo umezaa Bilionea. Uthaminishaji huu umefanywa na Wizara kuzingatia hii ni rough stones au cut & polished?
3. Muuzaji Laizer
Kama kuna makosa ya makusudi kwenye udhaminishaji na muuzaji huyu akalipwa bei ya juu zaidi, ni vizuri kufahamu na kufuatilia transactions za kwenye account itakayoingia hiyo Shilingi 7.8 bilioni.
4. Wizara inamuuzia nani na kwa bei gani?
Wizara imenunua jiwe kwa thamani ya Shilingi 7.8 bilioni. Ili ipate faida, inapaswa kuliuza kwa zaidi ya bei iliyonunulia. Hili ni jiwe ambalo bado halijakatwa wala kuwa polished.
Wizara itamuuzia nani na kwa bei gani? Ikipatikana hasara na kama kuna wizi katika biashara hii, nani anawajibika?