TANZIA: Aliyekuwa Mume wa Irene Uwoya, Ndikumana Hamad Katauti amefariki dunia

Miss Natafuta

JF-Expert Member
Joined
Sep 16, 2015
Posts
27,031
Reaction score
49,928
Habari ya kusikitisha, ni Kwamba wachezeaji wawili nchini Rwanda wamefariki Usiku wa kuamkia leo kila mmoja akiwa nyumbani kwake. Hategekimana Bonaventure aka Gangi na Mume wa zamani za Irene Uwoya, Ndikumana Hamad Katauti Wamefariki dunia. Ndikumana alikuwa kocha msaidizi wa timu ya soka ya Rayon Sports ambayo inaongoza kwa kuwa na mashabiki wengi nchini Rwanda.

Uongozi wa timu hiyo umesema jana Katauti alifanya mazoezi na wachezaji wake akiwa buheri wa afya. Mwili wake umekutwa nyumbani kwake mjini Kigali akiwa amefariki dunia. Haijajulikana kifo chake kimesababishwa na nini kwani hakuwa mgonjwa na wala hajafanya ajali. Mwili wake umepelekwa monchwari ya kiislamu ya dispensari ya Rwampala kwa maombi ya familia yake kwani miili ya waislamu haihifadhiwi katika monchwari za kawaida kwa mujibu wa imani zao.

Mungu ampe malazi mema peponi.

Siku ya Harusi ya Irene Uwoya aka Oprah na Ndikumana Hamad ‘Katauti’


Huyu ni Mtoto wa Irene aliyezaa na Ndikumana, Krish Ndikumana

Ndikumana alizaliwa 10/05/1978.
ujumbe wake wa mwisho kwa irene
 
habari ya kusikitisha, mume wa zamani za Irene Uwoya, Ndikumana Hamad Katauti amefariki dunia. Alikuwa kocha msaidizi wa timu ya soka ya Rayon Sports ambayo inaongoza kwa kuwa na mashabiki wengi nchini Rwanda. Uongozi wa timu hiyo umesema jana Katauti alifanya mazoezi na wachezaji wake akiwa buheri wa afya. Mwili wake umekutwa nyumbani kwake mjini Kigali akiwa amefariki dunia. Haijajulikana kifo chake kimesababishwa na nini kwani hakuwa mgonjwa na wala hajafanya ajali. Mwili wake umepelekwa monchwari ya kiislamu ya dispensari ya Rwampala kwa maombi ya familia yake kwani miili ya waislamu haihifadhiwi katika monchwari za kawaida kwa mujibu wa imani zao. Mungu ampe malazi mema peponi.
 
Nimeleta Uzi ukafutwa,Apumzike kwa Amani.
 
Dah! So sad... Soka na michezo mingine migumu ina pesa lakini naona kwa kiasi fulani inasababisha matatizo makubwa kiafya. Wanamichezo wamekuwa wakifa ghafla bila kuonesha dalili za kuugua kabisa...

Anyway, R.I.P jembe...
 
Kwahiyo kale kadogo ndo kamemsababishia kifo?Vifo vingine vinadhalilisha uanaume wako, mara ya mwisho niliona insta ameandika anaenjoy na bebi wake[emoji3]. Anyway tukutane mbinguni, R.I.P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…