Mheshimiwa Rais wangu Mpendwa, na Kipenzi cha Wengi Tanzania na Duniani kwa ujumla... hakika niwie radhi manake na mimi nilikomaa kishenzi, eti #TokaChato... aaaaaaaaaaargh!
Mambo yenyewe kama ndo haya, we endelea tu baba kujifungia huko huko manake huyu Azrael kama simuelewi elewi hivi!! Mbona dizaini kama kuna watu anawalia timing, na akikuta channel hazisomi, ndo pale anakimbilia Aga Khan, kwa hasira anafyatua yeyote anayepita jirani yake!
Usirudi mjini baba, manake kuna wengine hapa JF eti walikuwa wanakuhesabia siku, na kwamba eti leo ndo umeshamaliza siku 28, na kwamba eti kwa mujibu wa sheria za utumishi, likizo inayozidi siku 28 ni likizo ya uzazi!!
Potelea mbali, we waambie ndiyo, una likizo ya uzazi... kwani ndo utazaa kweli bhana!!