TANZIA: Mwanamuziki wa bongo fleva, Salum Mohamed maarufu kwa jina la Sam wa Ukweli afariki dunia

TANZIA: Mwanamuziki wa bongo fleva, Salum Mohamed maarufu kwa jina la Sam wa Ukweli afariki dunia

Hance Mtanashati

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2016
Posts
20,137
Reaction score
26,189
Msanii Sam wa ukweli hatunaye tena duniani, amefariki usiku huu hospitali ya Palestina iliyopo Sinza

Mwili wa Sam umepelekwa hospitali ya Mwananyamala kuhifadhiwa.

IMG_20180607_015717_171.jpg


Sam, alitamba na vibao vyake kama, ‘Lonely’, ‘Usiniache’, ‘Sina Raha’, ‘Hata Kwetu Wapo’ na nyinginezo ambazo zilimtambulisha na kufanya vizuri katika muziki wa Bongo Fleva.

Bwana alitoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.

=======



Msanii wa Bongo Fleva, Sam wa Ukweli amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Juni 7, 2018 baada ya kuugua na mwili wake kupelekwa katika hospital ya Mwananyamala.

Taarifa hiyo imethibitishwa na msambazaji wa nyimbo zake na Meneja wa ‘Team Mtaa kwa Mtaa’, Amri the Business ambaye aneeleza kwa masikitiko makubwa kuwa Sam amefariki dunia na kumtakia kupumzika kwa amani.

“Siamini kilichotokea muda huu ila sina jinsi, kwani woote safari ni moja, pumzika kwa amani Sam wa Ukweli, hakika nilikupenda kama ndugu yangu wakuzaliwa tumbo moja, #rip” amesema Amri the Business.

Pia, aliyekuwa mtayarishaji wa nyimbo za Sam wa Ukweli, Steve amesema Sam alikuwa akiumwa na walipomuuliza alisema ni UKIMWI wa kulogwa.

Baadhi ya Video zake

 
Yaaan kisa umeona insta sudy kapost huna hata habari kamili about kifo chake includin chanzo ushakimbiliaa kupost khaaaa watu bwana yaan wanaume wa siku hizi mmekosa uvumilivu chaaa......haya tuambieee chanzo!!!



Rest in Peace sam wa ukweli
 
Yaaan kisa umeona insta sudy kapost huna hata habari kamili about kifo chake includin chanzo ushakimbiliaa kupost khaaaa watu bwana yaan wanaume wa siku hizi mmekosa uvumilivu chaaa......haya tuambieee chanzo!!!



Rest in Peace sam wa ukweli
wachaga hatujalala mpaka muda huu
 
I see, nimeumia sana, Sam wa ukweli hakuwa na maringo, hadi mimi wa uswekeni huku kijijini nilikuwa ni,impigia simu tuna piga stori fresh kabisa, duuu!!, acha nifute namba yake, Apumzike kwa amani, sote tunapita.
Kwani alikuwa superstar mpaka aringe??sam alikuwa msanii
 
Back
Top Bottom