mcTobby
JF-Expert Member
- Feb 16, 2018
- 4,072
- 12,119
- Thread starter
- #281
13
Wiki tatu baadaye bromhead na Oleg walikutana kwa Siri sana kwenye local bar iliyoko uchochoroni kwenye Giza Giza . Na mpaka wanafika eneo Hilo walihakikisha hakukuwa na dalili za kufuatiliwa (dry-cleaning) . Mazungumzo Yao yalikuwa ni kama business talk tu ya kawaida Lakini tangu mwanzo lugha baina ya Hawa jamaa wawili ilikuwa ni kipengele sana hususan kwenye kujadili Mambo seriously kidogo. Oleg kingereza kilikuwa hakipandi, alikuwa anajua kijerumani na ki danish na kirussia ,yeye mwenzake alikuwa anajua kingereza tu huku lugha nyingine ni za kuungaunga.
Bromhead alimwambia tu Oleg kwamba muda mfupi ujao ataondoka Copenhagen (alitarajiwa kupangiwa majukumu mengine) hivyo , jukumu la kukutana naye angemwachia ofisa mwenzake hapohapo Denmark ambaye pia ni muongeaji mzuri wa lugha ya kijerumani. Vilevile huyu bwana alipaswa kumwonyesha eneo ambalo ni SAFE HOUSE kwa ajili ya kukutana . Eneo ambalo sio rahisi kushtukiwa kuliko hiyo ya kukutana kwenye bar au hotelini . Na vilevile angepewa funguo za nyumba hiyo ikiwemo na usafiri wa siri. Kweli ndani ya week bwana Oleg alionyeshwa nyumba hiyo na bromhead iliyokuwa Mitaa ya Charlottenund.
Bromhead alimwelezea huyu bwana swala la yeye kuwapa infos za urusi lilijulikana na maafisa wachache sana wa PET , vilevile hata M16 ni maafisa wa ngazi wa juu wachache wanaofahamu uwepo wake kama agent SUNBEAM. Na hawajui jina lake halisi ni nani . Idara za ujasusi zina amini sana Siri haiuwi kwa mtu mmoja maana ni hatari na vilevile haipaswi watu wengi waijue. Hivyo Siri Ili iwe Siri kikundi kidogo sana Cha watu kinapaswa kufahamu. Ndivyo ilivyokuwa kwa file la bwana Oleg. Kwa sababu bromhead alimsisitizia lazima iwe Siri maana yawezekana Kuna agents walioko ndani ya PET au M16 wakasanukia mpango wakamrepoti huko Moscow ikawa ni kizaazaa.
Alijulikana kwa codename SUNBEAM tu na sio jina lake halisi. Alimwakikishia usalama wake kwa kiasi fulani.
Baada ya hapo bromhead aliagana na Oleg akimtakia kila la heri na kurudi makao makuu M16 huko London kwa maboss wake.
Baada ya kutua tu London boss wa bromhead alimuuliza maswala kadhaa kuhusu asset hiyo muhimu . Lengo ni kutaka kuhakikisha mipango Yao inaenda sawia kuhusiana na swala la bwana Oleg jasusi wa KGB kuwafanyia kazi mashirika ya kijasusi ya magharibi hususani M16.
Wanasema kwamba kuhamisha file la KAZI kwenye idara za ujasusi kutoka kwa agent mmoja kwenda kwa mwingine sio kazi nyepesi hata kidogo na inachukua mchakato sana . Kwa maana file la Oleg au SUNBEAM lilikuwa ni file zito kidogo na ilihitajika juhudi za ziada maana one mistake inge compromise kila kitu ikiwemo maisha ya Oleg yawe hatarini na kuwe na mgongano au Mgogoro wa kidiplomasia baina ya west na Urusi.
Hivyo January 1 1975 bromhead alirudi kwa siri sana huko Denmark akipitia Sweden akitumia utambulisho fake Hadi mwonekano wake. Lengo la safari hii ni kwamba alikuja kukutana na agent mwenzake wa M16 aliyeitwa Philip Hawkins kwa ajili ya kumkabidhi file la Oleg aweze ku deal naye. Baada ya hapo bromhead alikutana na Oleg kwenye safe house kwa ajili ya kutambulishana na Hawkins ,baada ya mazungumzo ya hapa na pale bromhead aliondoka. Ikawa kwamba Oleg na Hawkins wangeshirikiana.
Tujadili,[emoji116][emoji116][emoji116][emoji116]
Swali ni kuwa kwanini mtu huamua hufanya ujasusi, inakuwaje mtu anahatarisha usalama wa hata familia yake, au anaamua kuacha kazi yenye kipato kizuri na kuwa jasusi ,Na Je Nini kinafanya mtu kuamua kufanyia ujasusi idara nyingine na kuisaliti idara iliyomwajiri..?
Wanasema ujasusi Huwa unakuja na shepu ya kila aina . Mwingine anaweza kuingia kwenye ujasusi kwa kusukumwa na itikadi,siasa na pia uzalendo. Wengine huingia huko kwa ajili ya kulipiza kisasi, wengine kulaghaiwa kingono ,kitapeli ,ujinga na pia sifa na majigambo ya kutaka kuonekana (kujipendekeza) . Pesa ikiwa kama kichocheo tu.
Bwana Pavel sudoplatov ambaye alikuwa ni KGB spy master enzi za Stalin aliwahi kusema kwenye kuajiri Hadi mtu kujiunga kuwa jasusi ni kwamba: nanukuu " search for people who are hurt by fate or nature-the ugly, those suffering from an inferiority complex,craving power and influence but defeated by unfavourable circumstances... .......In cooperation with us, all these find a peculiar compensation. The sense of belonging to an influential and powerful organization will give them a feeling of superiority over the handsome and prosperous People around them".
Hapa kwa tafsiri ya harakaharaka na isiyo rasmi ni kwamba mtu kujiunga na kuwa jasusi mzuri ni kuwatafuta wale ambao wako broken hawana mvuto ,wanaosumbuliwa na kutokujiamini ila wanataka kulazimisha kukubalika na wenye njaa na madaraka .wakiwekwa kitengoni watafanya vizuri na pia watafanya kazi kwa kujiamini kuliko wale wenye mvuto au wenye elimu kubwa kuwaliko wao hivyo watajihisi wenye nguvu wakiwa kitengoni [emoji39][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28].
Kwa mujibu wa KGB wanasema kwamba Kuna kanuni ya Hadi mtu kuwa jasusi MICE.
M-money
I-ideology
C-coersion
E-ego
1. Kwamba pesa inamfanya mtu awe tayari kujiunga na idara au kuuza Siri za nchi yake kwa vipande kadhaa vya shekeli. Money talks even there's great moment of silence.
2. Ideology au itikadi (capitalism vs communism) . Hata hapa kwetu huenda walioko huko kitengoni TISS ni matunda ya itikadi za ujamaa za Nyerere [emoji2][emoji2].
3.coercion.Hii ni labda mtu analazimishwa kufanya ujasusi kwa kulazimishwa pasipo ridhaa Yake. Mfano kushikiliwa mateka kwa familia yake ,mke na watoto au watoto tu. Haya hutokea . Au labda kutishiwa kuuawa endapo asipofanya kazi za kitengo.
4.Ego- nafikiri hii ni sababu ya kisaikolojia zaidi , kiburi ,kujifanya much know wa kila kitu ,kutaka kuonekana wewe ndio wewe ,yaani wewe ndio kusema ,ni sababu mojawapo watu kujiunga humo . Na hapa ndio pale wale hata kama kweli kaajiriwa kitengoni aonekane au ajulikane na kila mtu Ili aogopwe."UNAJUA MIMI NI NANI?" wako kwenye hiki kipengele [emoji38][emoji38][emoji38].
Na wanasema wapweke huwa ni rahisi kuwa majasusi wazuri na vilevile wengi wa majasusi ni wapweke wa kutupwa.. Kuna ukweli kiasi fulani.
Baadhi ya Wanasaikolojia wanasema kwamba mpaka jasusi wa nchi Moja kuisaliti nchi yake kuamua kuifanyia kazi nchi nyingine inawezekana ni mgongano kati ya inner world and outer world Kwa maana ya Mgogoro wa nafsi. Hili yawezekana kwa bwana Oleg. Kiitikadi alikuwa ni mcommunist Lakini baada ya kutoka nje ya Russia na kwenda kufanya kazi na kuonja ladha ya umagharibi kiitikadi alikuwa compromised . Mfumo aliokuwa akiutumikia ulikuwa wa kinyonyaji na katili kuliko mfumo alioenda kuukuta kwenye dunia nyingine. Je hii ilikuwa ni Sababu ya Oleg kuamua ku switch kuwa jasusi wa KGB na kuwafanyia kazi west?.
na pia dunia ya nje iliyoamua Oleg kuwa double agent labda ni mpasuko wa kiitikadi kati ya West na east pale aliposhuhudia ujenzi wa ukuta wa Berlin.
Na pia the inner world au tuseme Mgogoro wa nafsi , kutaka kulipiza kisasi kutokana na madhila ambayo familia yake ilipitia hususan mama yake alivyoteswa na mfumo wa kikomunisti zamani zile za Stalin . Hakukuwa na majibu ya uhakika kwenye hili.
Wiki tatu baadaye bromhead na Oleg walikutana kwa Siri sana kwenye local bar iliyoko uchochoroni kwenye Giza Giza . Na mpaka wanafika eneo Hilo walihakikisha hakukuwa na dalili za kufuatiliwa (dry-cleaning) . Mazungumzo Yao yalikuwa ni kama business talk tu ya kawaida Lakini tangu mwanzo lugha baina ya Hawa jamaa wawili ilikuwa ni kipengele sana hususan kwenye kujadili Mambo seriously kidogo. Oleg kingereza kilikuwa hakipandi, alikuwa anajua kijerumani na ki danish na kirussia ,yeye mwenzake alikuwa anajua kingereza tu huku lugha nyingine ni za kuungaunga.
Bromhead alimwambia tu Oleg kwamba muda mfupi ujao ataondoka Copenhagen (alitarajiwa kupangiwa majukumu mengine) hivyo , jukumu la kukutana naye angemwachia ofisa mwenzake hapohapo Denmark ambaye pia ni muongeaji mzuri wa lugha ya kijerumani. Vilevile huyu bwana alipaswa kumwonyesha eneo ambalo ni SAFE HOUSE kwa ajili ya kukutana . Eneo ambalo sio rahisi kushtukiwa kuliko hiyo ya kukutana kwenye bar au hotelini . Na vilevile angepewa funguo za nyumba hiyo ikiwemo na usafiri wa siri. Kweli ndani ya week bwana Oleg alionyeshwa nyumba hiyo na bromhead iliyokuwa Mitaa ya Charlottenund.
Bromhead alimwelezea huyu bwana swala la yeye kuwapa infos za urusi lilijulikana na maafisa wachache sana wa PET , vilevile hata M16 ni maafisa wa ngazi wa juu wachache wanaofahamu uwepo wake kama agent SUNBEAM. Na hawajui jina lake halisi ni nani . Idara za ujasusi zina amini sana Siri haiuwi kwa mtu mmoja maana ni hatari na vilevile haipaswi watu wengi waijue. Hivyo Siri Ili iwe Siri kikundi kidogo sana Cha watu kinapaswa kufahamu. Ndivyo ilivyokuwa kwa file la bwana Oleg. Kwa sababu bromhead alimsisitizia lazima iwe Siri maana yawezekana Kuna agents walioko ndani ya PET au M16 wakasanukia mpango wakamrepoti huko Moscow ikawa ni kizaazaa.
Alijulikana kwa codename SUNBEAM tu na sio jina lake halisi. Alimwakikishia usalama wake kwa kiasi fulani.
Baada ya hapo bromhead aliagana na Oleg akimtakia kila la heri na kurudi makao makuu M16 huko London kwa maboss wake.
Baada ya kutua tu London boss wa bromhead alimuuliza maswala kadhaa kuhusu asset hiyo muhimu . Lengo ni kutaka kuhakikisha mipango Yao inaenda sawia kuhusiana na swala la bwana Oleg jasusi wa KGB kuwafanyia kazi mashirika ya kijasusi ya magharibi hususani M16.
Wanasema kwamba kuhamisha file la KAZI kwenye idara za ujasusi kutoka kwa agent mmoja kwenda kwa mwingine sio kazi nyepesi hata kidogo na inachukua mchakato sana . Kwa maana file la Oleg au SUNBEAM lilikuwa ni file zito kidogo na ilihitajika juhudi za ziada maana one mistake inge compromise kila kitu ikiwemo maisha ya Oleg yawe hatarini na kuwe na mgongano au Mgogoro wa kidiplomasia baina ya west na Urusi.
Hivyo January 1 1975 bromhead alirudi kwa siri sana huko Denmark akipitia Sweden akitumia utambulisho fake Hadi mwonekano wake. Lengo la safari hii ni kwamba alikuja kukutana na agent mwenzake wa M16 aliyeitwa Philip Hawkins kwa ajili ya kumkabidhi file la Oleg aweze ku deal naye. Baada ya hapo bromhead alikutana na Oleg kwenye safe house kwa ajili ya kutambulishana na Hawkins ,baada ya mazungumzo ya hapa na pale bromhead aliondoka. Ikawa kwamba Oleg na Hawkins wangeshirikiana.
Tujadili,[emoji116][emoji116][emoji116][emoji116]
Swali ni kuwa kwanini mtu huamua hufanya ujasusi, inakuwaje mtu anahatarisha usalama wa hata familia yake, au anaamua kuacha kazi yenye kipato kizuri na kuwa jasusi ,Na Je Nini kinafanya mtu kuamua kufanyia ujasusi idara nyingine na kuisaliti idara iliyomwajiri..?
Wanasema ujasusi Huwa unakuja na shepu ya kila aina . Mwingine anaweza kuingia kwenye ujasusi kwa kusukumwa na itikadi,siasa na pia uzalendo. Wengine huingia huko kwa ajili ya kulipiza kisasi, wengine kulaghaiwa kingono ,kitapeli ,ujinga na pia sifa na majigambo ya kutaka kuonekana (kujipendekeza) . Pesa ikiwa kama kichocheo tu.
Bwana Pavel sudoplatov ambaye alikuwa ni KGB spy master enzi za Stalin aliwahi kusema kwenye kuajiri Hadi mtu kujiunga kuwa jasusi ni kwamba: nanukuu " search for people who are hurt by fate or nature-the ugly, those suffering from an inferiority complex,craving power and influence but defeated by unfavourable circumstances... .......In cooperation with us, all these find a peculiar compensation. The sense of belonging to an influential and powerful organization will give them a feeling of superiority over the handsome and prosperous People around them".
Hapa kwa tafsiri ya harakaharaka na isiyo rasmi ni kwamba mtu kujiunga na kuwa jasusi mzuri ni kuwatafuta wale ambao wako broken hawana mvuto ,wanaosumbuliwa na kutokujiamini ila wanataka kulazimisha kukubalika na wenye njaa na madaraka .wakiwekwa kitengoni watafanya vizuri na pia watafanya kazi kwa kujiamini kuliko wale wenye mvuto au wenye elimu kubwa kuwaliko wao hivyo watajihisi wenye nguvu wakiwa kitengoni [emoji39][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28].
Kwa mujibu wa KGB wanasema kwamba Kuna kanuni ya Hadi mtu kuwa jasusi MICE.
M-money
I-ideology
C-coersion
E-ego
1. Kwamba pesa inamfanya mtu awe tayari kujiunga na idara au kuuza Siri za nchi yake kwa vipande kadhaa vya shekeli. Money talks even there's great moment of silence.
2. Ideology au itikadi (capitalism vs communism) . Hata hapa kwetu huenda walioko huko kitengoni TISS ni matunda ya itikadi za ujamaa za Nyerere [emoji2][emoji2].
3.coercion.Hii ni labda mtu analazimishwa kufanya ujasusi kwa kulazimishwa pasipo ridhaa Yake. Mfano kushikiliwa mateka kwa familia yake ,mke na watoto au watoto tu. Haya hutokea . Au labda kutishiwa kuuawa endapo asipofanya kazi za kitengo.
4.Ego- nafikiri hii ni sababu ya kisaikolojia zaidi , kiburi ,kujifanya much know wa kila kitu ,kutaka kuonekana wewe ndio wewe ,yaani wewe ndio kusema ,ni sababu mojawapo watu kujiunga humo . Na hapa ndio pale wale hata kama kweli kaajiriwa kitengoni aonekane au ajulikane na kila mtu Ili aogopwe."UNAJUA MIMI NI NANI?" wako kwenye hiki kipengele [emoji38][emoji38][emoji38].
Na wanasema wapweke huwa ni rahisi kuwa majasusi wazuri na vilevile wengi wa majasusi ni wapweke wa kutupwa.. Kuna ukweli kiasi fulani.
Baadhi ya Wanasaikolojia wanasema kwamba mpaka jasusi wa nchi Moja kuisaliti nchi yake kuamua kuifanyia kazi nchi nyingine inawezekana ni mgongano kati ya inner world and outer world Kwa maana ya Mgogoro wa nafsi. Hili yawezekana kwa bwana Oleg. Kiitikadi alikuwa ni mcommunist Lakini baada ya kutoka nje ya Russia na kwenda kufanya kazi na kuonja ladha ya umagharibi kiitikadi alikuwa compromised . Mfumo aliokuwa akiutumikia ulikuwa wa kinyonyaji na katili kuliko mfumo alioenda kuukuta kwenye dunia nyingine. Je hii ilikuwa ni Sababu ya Oleg kuamua ku switch kuwa jasusi wa KGB na kuwafanyia kazi west?.
na pia dunia ya nje iliyoamua Oleg kuwa double agent labda ni mpasuko wa kiitikadi kati ya West na east pale aliposhuhudia ujenzi wa ukuta wa Berlin.
Na pia the inner world au tuseme Mgogoro wa nafsi , kutaka kulipiza kisasi kutokana na madhila ambayo familia yake ilipitia hususan mama yake alivyoteswa na mfumo wa kikomunisti zamani zile za Stalin . Hakukuwa na majibu ya uhakika kwenye hili.