Tarehe 18 Mei 1985: Shirika la kijasusi la KGB kulikuwa na idara iliyojulikana kama Directorate K

Tarehe 18 Mei 1985: Shirika la kijasusi la KGB kulikuwa na idara iliyojulikana kama Directorate K

20


Akiwa nchini mexico bibiye Rosa hakujua Aldrich Ames ni jasusi. Lakini baadaye alikuja kugundua kwamba huyu bwana ake mpya ni spy na ameoa hii ilileta mtafaruku kidogo , kutokana na shinikizo la huyu mchepuko Aldrich alimwahidi angemuacha mkewe Nancy kwa talaka. Lakini utaratibu wa kuchukua maamuzi ya kumtaliki Nancy yalikuwa ni ya gharama sana ukilinganisha na kiasi Cha mshahara wa afisa huyo as per CIA salary scale alikuwa akipokea tu Dola elfu kama arobaini na kidogo kwa mwaka kipindi hicho. Kutokana na huyu Rosa kuwa ni mwanamke wa matanuzi , Aldrich alimwahidi angeacha kazi CIA na kuamua kutafuta kazi yenye mshahara mkubwa ku meet standard za mrembo huyo . Maamuzi haya ya kumsikiliza huyu mchepuko yalimgharimu maisha yake yote........




Turudi kwa bwana SUNBEAM..

Ubalozi wa Russia au Soviet ulikuwa maeneo ya Kensington palace gardens viungani mwa Jiji la London. Nyumba aliyofikia Oleg na familia yake haikuwa mbali sana na ofisi za ubalozi wa Soviet .
Ilikuwa ni nyumba yenye vyumba viwili mitaa hiyo ya Kensington .
Siku chache baada ya kufika alitembea Hadi mtaa wa nyuma ya ubalozi wake akiwa amevaa kofia ambayo sio rahisi kutambulika hadi kwenye kibanda Cha simu . Alibonyeza namba kadhaa alizokuwa Nazo alizopewa na guscott miaka michache nyuma akiwa Copenhagen. Baada ya ku dial hizo namba,alisikia upande wa pili wa simu sauti ikisema "hello , welcome to London, ,thank you for calling. We look forward to seeing you...." Hii ilikuwa ni sauti ilyorekodiwa ya bwana guscott ikimkaribisha Oleg London na rekodi ile ilitaka wakutane mwezi July tarehe nne.
Sasa ni rasmi Oleg alikuwa mikononi mwa M16 ndani ya uingereza .
Mkewe na wanawe wali adapt maisha ya uingereza kwa haraka sana.
Kipindi Oleg anawasili aliyempokea alikuwa ni balozi ambaye alikuwa ni secretary wa ubalozi huo wa Soviet aliyeitwa Arkadi Vasilyevich guk . Huyu bwana aliwasili hapo ubalozini miaka miwili nyuma. Mkomunisti kindakindaki na Cha pombe wa vodka ile mbaya. Hapo London alikuwa anakula na kunywa made in Russia peke Yake.
Alitambulishwa kwa wafanyakazi wenzake wa hapo ubalozini na orientation za hapa na pale.
Baadaye Oleg alikuja kugundua huu ubalozi ni ofisi yenye manungu, kujipendekeza,masengenyo, vinyongo na wivu na kila aina ya ushenzi miongoni mwa wafanyakazi wake wote aliowakuta .

Baadaye Bwana Oleg alianza harakati namna ya kuwasiliana na M16 ,na hatimaye tarehe nne July akapiga Tena namba zile alizopiga mara ya kwanza ila kwenye kibanda tofauti Cha simu . Na mara hii bwana Geoffrey guscott alipokea . Walipanga kukutana mchana huo eneo ambalo sio rahisi kwa manjagu wa KGB kuwepo . Walipanga kukutana kwenye hotel ya holiday inn mtaa wa Sloane. Na kweli Oleg alifika na kumuona guscott aliyekuwa amekaa na mwanamama mmoja wa makamu kidogo. Huyu mama alijulikana kama Veronica price. Walisalimiana na Kisha wakasimama na kutoka wakienda moja kwa Moja nje ya hotel hiyo kupitia mlango wa nyuma. Oleg aliwafuata pasipo kusema neno.nyuma ya hotel kulikuwa na park ya magari . Kulikuwa na gari inasubiri hapo ikiwa imepakiwa tokea hapo usiku wa jana yake aina ya ford wakaingia ndani ya gari Hilo lililokuwa na plate number ambazo sio rahisi ku track. Guscott na Oleg walikaa siti za nyuma wakaanza maongezi wakijuliana Hali ,huku mwanamama Veronica price akiendesha. Walikuwa wakiongea ki Russia pasipo huyo mama kujua Nini wanaongea. Veronica price aliendelea ku drive gari Hadi Bayswater zilipokuwa nyumba kadhaa . Nyumba hizi zilichaguliwa kama safe house na M16 kwa ajili ya bwana Oleg. Zilikuwa umbali wa mwendo wa gari masaa mawili kutoka ubalozi wa Soviet hapo London.

Hii sehemu ilikuwa fupi sana boss
Ongezea weekend ni ndefuuu
 
Na marafiki zangu ni wa Irish aisee wakija bongo wakienda supermarket wananunua bidhaa made in Irish Kwa kuzitafta na wanafurahia kabisa huku Tanzania sijui kwanini hatupendi kununua vitu made in Tanzania tunapenda vya nje
We mtanzania humjui kwa ulimbukeni?Mtz yeye kutumia vitu vya kutoka nje,kwake ni sawa na kuwaringishia wengine kuwa ana mkwanja mnene na elimu ya kutosha eti!.[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Ni hovyo kweli yani hata story ya yoga alijifanyaga yake na kutoza watu ili kupata updates baada ya yoga ku stop updates na yeye aka stop, heri mleta mada ana share humu free Kwa wote kujifunza Sasa huyu mwizi anatoza wengine
Hivi yoga kapotelea wapi? Bi dada alinikamata vyema ghafla akapotea nami nikawa mvivu kufuatilia Habari za Mr. born town.
 
kwa jina naitwa Fortunatus Buyobe au ukipenda niite ndimu mkata shombo.

Kwanza naomba nijibu hoja yako moja kwa haraka sana bila kuikawiza

1. Kwamba nimekukopy na hadi nimechukua picha zako. Swali ni, ni wewe ndiye umezipiga picha hizi? Kama sio unajimilikishaje hakimiliki?

2. Kwa msisiti mkubwa ni kwamba sijakunukuu, siwezi kukunukuu na uwezo wangu wa kuandika tayari upo dhahili (mnyonge mnyongeni haki yake mpeni) ni kwamba members humu humu watapika consistency yako ya uandishi. Wataangalia chapisho lako la jana, la leo na la keshokutwa kisha kila kitu kitakuwana baina yako nami.

3. Hapa ndio pa muhimu zaidi. Bwana Oleg Gordievsky habari zake zimeandikwa sehemu nyini sana.

Naomba niseme wewe Story yako umeicopy hapa na kuitafsiri kwa kiswahili [emoji116]


So hii ni open source document don’t own any rights na mbaya zaidi hukuwa mbunifu bali umecopy neno hadi neno.

Mimi bwana Oleg nimemsoma kulitia mwandishi BEN MACYNTYRE aliyefanya naye mahojiano. Hata hizo picha unazodai kuwa ni zako umezitoa kwenye hints za kitabu chake cha A SPY AND TRAITOR hivyo HUNA CHOCHOTE KILICHO CHAKO.

Mimi nina vyangu. My flow, Mpangilio wa matukio, na haya hayajionyeshi kwenye hii stotu tu bali na nyingine nyingi.

Karibu Telegramm utakuta story hii inaitwa THE MOLE, mle ndani imeanza na kina Aimes, Hanssen na ikaishia na Oleg. Sasa jiangalie. Ungekuwa na Identity ya kueleweka ningekushitaki
Na ile story ya dada Yoga mbona uliikopi na kuipeleka twitter?
 
Hivi yoga kapotelea wapi? Bi dada alinikamata vyema ghafla akapotea nami nikawa mvivu kufuatilia Habari za Mr. born town.
Nakwambia I think plan ilivokuwa inaendelea born town akagundua mchezo na kuudhibiti mapema ikiwemo new CEO kufatiliwa ma file yake ikiwemo machafu so imebidi new CEO awe mdogo ka piritoni,;ila kuja Kwa Paka nchini Kuna jambo
 
21


Baada ya kufika safe walianza kutambulishana rasmi sasa kila mmoja akawa familiar na mwenzake .
Guscott alimwambia Oleg eneo hili ndio ingekuwa ni kama safe house na wangekutana hapa mara kwa mara kwa kila walipopata wasaha wa kukutana na Oleg angetoa umbea wake kwa M16 pasipo kugundulika au kufuatiliwa .
Maafisa wa M16 kipindi oleg akiwa kwao walikuwa wameandaa mpango mkakati wa kumtorosha bwana Oleg na familia yake nchini urusi endapo angekuja kuhisiwa na KGB anaifanyia uingereza kazi kwa Siri Na walitarajia hili lingetokea. Huo mpango ulipewa jina la operation PIMLICO. hivyo wakawa wanampa kama briefings za mpango huo uliokuwa kwenye makaratasi.
Ni kwamba hapo kabla M16 hawakuwahi kuwa na access ya kumtumia jasusi wa KGB ndani ya uingereza anayefanya kazi under official diplomatic cover. Hivyo Sasa kwakuwa Oleg alikuwa ndani ya uingereza waliamua kumbadilisha jina la uficho la SUNBEAM na kupewa jina la NOCTON . Asili ya jina hili ni Kijiji kilichoko huko Lincolnshire uingereza. Kulikuwa na sababu ya kumbadilisha jina la uficho.
Wanadai kwamba Japo M16 na M15 ni mashirika pacha lakini kila mmoja alikuwa anafanya kazi kivyake na kwa namna anavyojua yeye .. kwa mfano shirika la M15 lilikuwa Lina deal sana na domestic surveillance ndani ya uingereza, pia lilikuwa na wajibu katika kuwafuatilia nyendo za maafisa wa ki Soviet hapo London. Hivyo M16 wa wakaona M15 wangeweza ku compromise mpango wa kumtumia Oleg kuwapa taarifa . Wakaamua kuwashirikisha baadhi ya maafisa wachache sana wa ngazi za juu wa M15 ikiwemo D.G. Lengo la kuwashirikisha Hawa M15 ni kulinda asset Yao inayowapa info asije akagundulika na maafisa wengine wa kitengo na mpango uka leak. Huu mpango wa mashirikiano baina ya haya mashirika pacha kishughulika na hili swala la Oleg au NOCTON waliupa jina la uficho la LAMPAD.
Baada ya hayo yote baada ya kupeana briefings za hapa na pale baina ya Oleg na maafisa hao wa M16 wakaagana na kuondoka. Ni kwamba Oleg alipaswa kuwa katika safe house hiyo na kuwapa infos makachero hao wa uingereza kila ilipopatikana nafasi
Oleg pia alianza kuwapa infos za baadhi ya maafisa wa M16 Waliokuwa wanawafanyia kazi Soviet. Kwa mfano hapo nyuma ndani ya M15 kulikuwa Kuna afisa mstaafu aliyeitwa Roger Hollis ilisemekana alikuwa ni mole ndani ya shirika Hilo na alikuwa anavujisha taarifa nyeti kwa KGB, lakini kwa mujibu wa taarifa za Siri alizokuwa Nazo Oleg ni kwamba mchawi hakuwa huyo Hollis Bali alikuwa ni afisa mwingine mstaafu wa M16 aliyeitwa John cairncross aliyekuwa ni mole wa Soviet mwaka 1964.
Pia Oleg Kutokana na kufukunyua ma file ya KGB ,aligundua kwamba kulikuwa Kuna agent aliyeitwa ELLI ambaye M16 hawakuwahi mjua hapo kabla ,aliyepandikzwa na Soviet mwaka 1946 na alikuwa anaitwa Leo Long na alikuwa amepandikizwa kwenye chuo Cha Cambridge akitoa Siri kwa Soviet wakati wa vita ya pili ya dunia. Pia Oleg aliendelea kutema Siri ,kwamba hata aliyekuwa mtaalamu na injinia wa mabomu ya nyuklia aliyekuwa anaifanyia kazi
Idara ya kijeshi ya Britain's wartime atomic bomb research aliyeitwa Bruno pontecorvo alikuwa anauza taarifa za Siri za kijeshi kwa urusi wakati huo. Pia Oleg aliwapa infos za wanasiasa hususan wa chama Cha labour party walioko madarakani waliokuwa kwenye payroll ya KGB .Hizi infos zilitua mezani kwa M16 na zikakaliwa kikao na maafisa wa ngazi za juu waliokuwa wanajua hili swala la NOCTON. Taarifa hizi Ziliwashtua na vilevile kuwashangaza.
Katika taarifa hizi zote , M16 waliamua kuipa uzito taarifa kuhusu Michael foot kiongozi wa upinzani wa chama Cha labour ambaye alitarajiwa kuchuana na margaret thatcher kwenye uchaguzi wa 1984. M16 waliona endapo Michael Foot angeshinda uchaguzi uliotarajiwa na hizi taarifa kuwekwa public , ingeleta Mgogoro mkubwa wa kikatiba kwa taifa la uingereza na ingekuwa kashfa kubwa ya kisiasa. Hili swala wakapewa M15 Kwa ajili ya kuchukua hatua zaidi walizoona ingemfaa. D.G wa M15 akalifikisha hili swala la tuhuma za foot mezani kwa katibu mkuu wa bunge (chief secretary) sir Robert Armstrong . Huyu alikuwa ni mshauri mkuu wa P.M wa uingereza na vilevile alikuwa na jukumu la maswala mazima katika kusimamia kamati za usalama na intelejensia kwa taifa la uingereza. Amewahi kuhudumu hapo nyuma kama principal private secretary kwa mawaziri wakuu kama Harold Wilson na Edward heath. Alipofikishiwa hizi taarifa aliamua kuziminyia chini kwa kuona hizi tuhuma zipo kisiasa zaidi. Akaona asilifikishe kwa Margaret thatcher. Huyu bwana Armstrong alikuwa ni miongoni mwa washauri walioaminika na margaret thatcher. Armstrong aliona ngoja kwanza asimwambie kuhusu hizi tuhuma za mpinzani wake wa kisiasa Michael foot. Ripoti zinadai endapo Armstrong angemwambia Margaret thatcher , thatcher angetumia hizo tuhuma kumkaanga Michael Foot kwenye kampeni. Kifupi Armstrong hakuwahi mwambia yoyote tuhuma za Michael Foot hata kwenye chama Cha conservative, labour au hata marafiki wa uingereza kama marekani. Swala likabaki kwa M16 , endapo Michael foot akishinda uchaguzi mkuu ingeleta mtafaruku kidogo ,na ingebidi Hadi malkia wa uingereza apewe taarifa . Lakini kama bahati Michael foot a.k.a agent BOOT hakushinda uchaguzi huo.

Mwaka 1982 joto la Vita baridi lilikuwa limepanda sana kwa pande zote east na west .. Kremlin waliamini kwamba nchi za magharibi hususani uingereza wangeanzisha vita halisi.
 
IMG_20230501_102619_151.jpg

Huyu ni sir. Robert Armstrong.aliyekuwa cabinet secretary na mshauri wa karibu wa Margaret thatcher.


IMG_20230501_102519_874.jpg

Leila akiwa na wanawe wawili maria na Ana nje ya mkahawa mmoja mtaa wa Trafalgar square huko London.

IMG_20230501_102508_460.jpg

Jengo la ubalozi wa Soviet hapo London mtaa wa 13 Kensington palace gardens.
 
Back
Top Bottom