Tarehe 18 Mei 1985: Shirika la kijasusi la KGB kulikuwa na idara iliyojulikana kama Directorate K

Tarehe 18 Mei 1985: Shirika la kijasusi la KGB kulikuwa na idara iliyojulikana kama Directorate K

kwa jina naitwa Fortunatus Buyobe au ukipenda niite ndimu mkata shombo.

Kwanza naomba nijibu hoja yako moja kwa haraka sana bila kuikawiza

1. Kwamba nimekukopy na hadi nimechukua picha zako. Swali ni, ni wewe ndiye umezipiga picha hizi? Kama sio unajimilikishaje hakimiliki?

2. Kwa msisiti mkubwa ni kwamba sijakunukuu, siwezi kukunukuu na uwezo wangu wa kuandika tayari upo dhahili (mnyonge mnyongeni haki yake mpeni) ni kwamba members humu humu watapika consistency yako ya uandishi. Wataangalia chapisho lako la jana, la leo na la keshokutwa kisha kila kitu kitakuwana baina yako nami.

3. Hapa ndio pa muhimu zaidi. Bwana Oleg Gordievsky habari zake zimeandikwa sehemu nyini sana.

Naomba niseme wewe Story yako umeicopy hapa na kuitafsiri kwa kiswahili 👇


So hii ni open source document don’t own any rights na mbaya zaidi hukuwa mbunifu bali umecopy neno hadi neno.

Mimi bwana Oleg nimemsoma kulitia mwandishi BEN MACYNTYRE aliyefanya naye mahojiano. Hata hizo picha unazodai kuwa ni zako umezitoa kwenye hints za kitabu chake cha A SPY AND TRAITOR hivyo HUNA CHOCHOTE KILICHO CHAKO.

Mimi nina vyangu. My flow, Mpangilio wa matukio, na haya hayajionyeshi kwenye hii stotu tu bali na nyingine nyingi.

Karibu Telegramm utakuta story hii inaitwa THE MOLE, mle ndani imeanza na kina Aimes, Hanssen na ikaishia na Oleg. Sasa jiangalie. Ungekuwa na Identity ya kueleweka ningekushitaki
Kwahiyo sababu picha hakupiga yeye ndio uhalalishe wewe kuzitumia baada ya yeye kuleta hii story humu? Jaribu kuwa na Akili basi kijana. We huelewi hata kufanya transcription kutoka kwenye SL kuja TL ni kazi ngumu na ambayo mwandishi anastahili credits zake halafu wewe unachukulia tu simpo?? Acha Upumbavu wa dhahiri kiasi hicho.
 
Broo punguza vitisho,alaf pia na wewe umezidi nakumbuka kuna story kama sio ya UMUGHAKA sijui n nani nayo uliitoa humu ukawa unairusha kule kwako,alaf pia umshtak mtu kwa kipi kaka?hii kuburudika tuu au kuna kingine?

Ukweli n kwamba umeona jamaa anatoa hii story ukaamua kwenda kuitafuta ukaipa kichwa kingine ili watu watoe 2.5k per monthly,na naimani hakuna mwenye hati miliki ya hii story kwan hata wewe mwenyewe umeikopi mahali,
Hivi Hana kazi nyingine za kufanya huyu Hadi awe anakopy habari na kuziuza buku jero?
Mbona atafika mbinguni kachoka sana
 
Ni hovyo kweli yani hata story ya yoga alijifanyaga yake na kutoza watu ili kupata updates baada ya yoga ku stop updates na yeye aka stop, heri mleta mada ana share humu free Kwa wote kujifunza Sasa huyu mwizi anatoza wengine
Niliona twitter yeye anabadili heading tu ila content zinafanana na baada ya kusoma huku kaenda twitter chapu kuandika
 
SEHEMU YA 3

Stalin alikufa mwaka 1953.Aliyemfuata baada ya yeye kufariki alikuwa ni Nikita khrushchev. Miaka mitatu tu toka afariki Stalin aliyemfuata alianza kuuponda utawala wake kwa kuwa ulikuwa wa kimabavu akiwa anahutubia mkutano mkuu wa 20 wa chama .Baba yake Oleg alipigwa na butwaa sana na akaamini huenda ndio itikadi za kijamaa zinaenda kufa kutokana na sera za Nikita. Kwani wafungwa wa kisiasa waliachiliwa,masharti ya censorship yakalegezwa n.k. Hiki ni kipindi ambacho mambo ya umagharibi na uhuru ulianza na raia wakaanza kuona hafueni . Kwa upande wa mzee Anton hakufurahishwa( mlinda legacy[emoji1]) lakini kwa mwanaye ilikuwa ni ahueni.
Akiwa na miaka 17 Oleg alijiunga na Moscow state institute of international relations. Huko alivutiwa na maisha ya chuo . Alijihusisha pia na deep discussion kuhusu sera za nchi yake za usosholisti
.kwa kifupi alianza kuamini katika mrengo wa kibepari(hakuonyesha waziwazi).lakini asijue kwamba mle chuoni kulikuwa na spies wa KGB. Akaonywa kiaina na wenzake. Na pia alikuja kugundua mambo hayajabadilika kabisa . Hii ni baada ya urusi kuivamia Czechoslovakia, raia wa huko wakiandamana kupinga kuwepo kwao ndani ya umoja wa Soviet. Lakini maadamano yalizimwa na ikapelekea umwagaji mkubwa wa damu.

Hiki chuo kilikuwa ni chuo Cha hadhi ya juu sana kwa wakati huo kiasi kwamba Henry Kissinger aliwahi kukiri mwenyewe na kusema ni "Russian Harvard". Chuo hiki kilikuwa chini ya wizara ya mambo ya nje ilikuwa ndio tunaweza kusema breeding ground ya wanadiplomasia, wanasayansi,wachumi,wanasiasa na zaidi training center ya majasusi wa KGB.
Akiwa hapo Oleg alijikita kwenye masomo ya historia, geography,uchumi pamoja na mahusiano ya kimataifa,yote ya haya masomo yakiwa yamejikita katika itikadi za kikomunisti. Taasisi hii pia ilikuwa inafundisha lugha 56 zaidi ya chuo chchote duniani kwa wakati huo. Kujifunza lugha chuoni hapo ilikuwa ni njia na sababu ya kupata ajira nje ya nchi kwa mwana KGB. Na pia ni kwa sababu kilikuwa special kwa ajili ya ujasusi.Oleg kwakuwa alijifunza kijerumani tokea akiwa mdogo aliamua kujifunza kingereza,lakini kaka yake akamlazimisha asomee kiswedish ambaye tayari ni mwajiriwa rasmi wa KGB . Kwani alimsisitizia kujifunza lugha hiyo kutampa mwanya wa kufanya kazi nchi za Scandinavia.
Chuoni hapo alikuwa anasoma magazeti ya nje hususan magharibi Japo yalikuwa machache lakini kulimpa mwanga Fulani wa duniani huko.
Akiwa na miaka 19 Oleg na rafiki yake wa chuo kwa wakati huo aliyeitwa stanislav kaplan walianza mazoezi ya kujijenga miili Yao . wakaaanza kufanya cross-country running kama sehemu ya kuweka mwili fiti.hii ilikuwa ni sehemu ya course hapo chuoni. Huyu rafiki yake alikuwa anasoma kozi fupi za kufanya tracking mwenye asili ya Czechoslovakia. Yeye tayari alikuwa na degree yake tayari aliyoipata kwenye chuo Cha Charles mjini Prague. Na kuja kwake hapo chuoni ni kwamba alichaguliwa kama wale the best and gifted students ndani ya muungano wa Soviet.
Kwa kuwa walikuwa ni marafiki walikuwa wanashare baadhi ya mambo na namna gani hawakuwa wanavutiwa na mfumo wa taifa lao kwa maana walihisi kama wamefungwa akili na propaganda za nchi Yao. kwa kuwa walikuwa ni vijana rijali na wenye muonekano wa kuvutia ,walikuwa ni Magnet kwa wanawake wengi hususan walipokuwa wakipata maakuli kwenye mkahawa mmoja kitingoji Cha Gorky park. kwa hiyo kukaa hapo waliweza kujirusha na bebezi.
kaka wa Oleg ,Vasili yeye tayari alikuwa ameajiriwa ndani ya KGB kama illegal ndani ya kundi kubwa la majasusi waliosambazwa duniani.
huyu Vasili alikuwa ni majasusi kwenye kundi la illegal au kwa kirusi ni Nelegal.
Iko hivi wanasema urusi kulikuwa na aina mbili za majasusi .legal na nelegal. Kuna wale wanatumwa kukusanya taarifa za Siri kwenye nchi Fulani wakijifanya wafanya biashara,wafanya kazi kwenye mashirika ya msaada, wahisani,walimu, waandishi wa habari n.k. . Na wanakuwa na majina feki, passport feki na utambulisho batili. Hawa ikitokea wamekamatwa ina kula kwao mazima na nchi inawakana kama raia wao endapo wamekamatwa . Kwa kifupi wanakuwa hawana formal cover na ni sleeper agents. Sasa Kuna wale ambao ni legal , Hawa wanakuwa na diplomatic cover. Hawa ni wale ambao ni wafanyakazi wa ubalozini (consular staff) akiwemo na balozi mwenyewe [emoji1]. Hawa ikitokea wanahusishwa na ujasusi/uhaini kwenye nchi Fulani mara nyingi hawawezi kushtakiwa wanakuwa declared persona non grata na kufukuzwa na nchi hiyo ndani ya masaa 24 au 72. Hawa Sasa wanakuwa na formal/diplomatic cover .
Kwa hiyo bwana Vasili yeye alikuwa ni illegal aliyeajiriwa mwaka 1960 na FCD (First chief directorate). ndio aliyemshauri bwana mdogo asomee lugha ya kiswedi. Na ndie aliemtambulisha mdogo wake kitengoni kwa mabosi wake wa kitengoni FCD. Hichi kitengo ndani ya KGB kilikuwa kinajihusisha na ujasusi wa nje ya urusi.
Mwaka 1961 bwana Oleg Gordievsky alipata mwaliko wa ghafla na akapewa maelekezo aende kwenye jumba Moja karibu na makao makuu ya KGB lililoko mitaa ya Dzerzhinsky.


View attachment 2591897
Bwana Oleg kwenye miaka yake akiwa chuoni.
View attachment 2591901
Oleg akiwa kwenye sare za KGB
Hatari sana
 
Boss tuendelee usijibu negative comments
Watu tunafatilia tuwekee vitu leo weekend muda wa kusoma upo
Naunga mkono asijibu hoja mbovu za huyo ndimu, in short ni troublemaker !
Sio kwenye uzi huu tu amekua mtatanishi bali ni nyuzi nyingi.

Ukitaka kujua anacopy ona comment alivyo ijibia , ipo mbali sana . Hii inaonyesha anaufutilia huu uzi.
 
Ingekuwa sikuheshim
Broo punguza vitisho,alaf pia na wewe umezidi nakumbuka kuna story kama sio ya UMUGHAKA sijui n nani nayo uliitoa humu ukawa unairusha kule kwako,alaf pia umshtak mtu kwa kipi kaka?hii kuburudika tuu au kuna kingine?

Ukweli n kwamba umeona jamaa anatoa hii story ukaamua kwenda kuitafuta ukaipa kichwa kingine ili watu watoe 2.5k per monthly,na naimani hakuna mwenye hati miliki ya hii story kwan hata wewe mwenyewe umeikopi mahali,
Ingekuwa sikuheshumu ningekujibu. Hebu leo acha shetani apitie mbali.
 
Ingekuwa sikuheshim

Ingekuwa sikuheshumu ningekujibu. Hebu leo acha shetani apitie mbali.
Kama hukopi hii story huku na kuipakapaka rangi kwa viswaga vyako uchwara kabla ya kuipaste kwenye telegram yako mbona story haiendelei kule sasa? Iendeleze tuone hiyo creativity yako unayojitapa nayo sasa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
20


Akiwa nchini mexico bibiye Rosa hakujua Aldrich Ames ni jasusi. Lakini baadaye alikuja kugundua kwamba huyu bwana ake mpya ni spy na ameoa hii ilileta mtafaruku kidogo , kutokana na shinikizo la huyu mchepuko Aldrich alimwahidi angemuacha mkewe Nancy kwa talaka. Lakini utaratibu wa kuchukua maamuzi ya kumtaliki Nancy yalikuwa ni ya gharama sana ukilinganisha na kiasi Cha mshahara wa afisa huyo as per CIA salary scale alikuwa akipokea tu Dola elfu kama arobaini na kidogo kwa mwaka kipindi hicho. Kutokana na huyu Rosa kuwa ni mwanamke wa matanuzi , Aldrich alimwahidi angeacha kazi CIA na kuamua kutafuta kazi yenye mshahara mkubwa ku meet standard za mrembo huyo . Maamuzi haya ya kumsikiliza huyu mchepuko yalimgharimu maisha yake yote........




Turudi kwa bwana SUNBEAM..

Ubalozi wa Russia au Soviet ulikuwa maeneo ya Kensington palace gardens viungani mwa Jiji la London. Nyumba aliyofikia Oleg na familia yake haikuwa mbali sana na ofisi za ubalozi wa Soviet .
Ilikuwa ni nyumba yenye vyumba viwili mitaa hiyo ya Kensington .
Siku chache baada ya kufika alitembea Hadi mtaa wa nyuma ya ubalozi wake akiwa amevaa kofia ambayo sio rahisi kutambulika hadi kwenye kibanda Cha simu . Alibonyeza namba kadhaa alizokuwa Nazo alizopewa na guscott miaka michache nyuma akiwa Copenhagen. Baada ya ku dial hizo namba,alisikia upande wa pili wa simu sauti ikisema "hello , welcome to London, ,thank you for calling. We look forward to seeing you...." Hii ilikuwa ni sauti ilyorekodiwa ya bwana guscott ikimkaribisha Oleg London na rekodi ile ilitaka wakutane mwezi July tarehe nne.
Sasa ni rasmi Oleg alikuwa mikononi mwa M16 ndani ya uingereza .
Mkewe na wanawe wali adapt maisha ya uingereza kwa haraka sana.
Kipindi Oleg anawasili aliyempokea alikuwa ni balozi ambaye alikuwa ni secretary wa ubalozi huo wa Soviet aliyeitwa Arkadi Vasilyevich guk . Huyu bwana aliwasili hapo ubalozini miaka miwili nyuma. Mkomunisti kindakindaki na Cha pombe wa vodka ile mbaya. Hapo London alikuwa anakula na kunywa made in Russia peke Yake.
Alitambulishwa kwa wafanyakazi wenzake wa hapo ubalozini na orientation za hapa na pale.
Baadaye Oleg alikuja kugundua huu ubalozi ni ofisi yenye manungu, kujipendekeza,masengenyo, vinyongo na wivu na kila aina ya ushenzi miongoni mwa wafanyakazi wake wote aliowakuta .

Baadaye Bwana Oleg alianza harakati namna ya kuwasiliana na M16 ,na hatimaye tarehe nne July akapiga Tena namba zile alizopiga mara ya kwanza ila kwenye kibanda tofauti Cha simu . Na mara hii bwana Geoffrey guscott alipokea . Walipanga kukutana mchana huo eneo ambalo sio rahisi kwa manjagu wa KGB kuwepo . Walipanga kukutana kwenye hotel ya holiday inn mtaa wa Sloane. Na kweli Oleg alifika na kumuona guscott aliyekuwa amekaa na mwanamama mmoja wa makamu kidogo. Huyu mama alijulikana kama Veronica price. Walisalimiana na Kisha wakasimama na kutoka wakienda moja kwa Moja nje ya hotel hiyo kupitia mlango wa nyuma. Oleg aliwafuata pasipo kusema neno.nyuma ya hotel kulikuwa na park ya magari . Kulikuwa na gari inasubiri hapo ikiwa imepakiwa tokea hapo usiku wa jana yake aina ya ford wakaingia ndani ya gari Hilo lililokuwa na plate number ambazo sio rahisi ku track. Guscott na Oleg walikaa siti za nyuma wakaanza maongezi wakijuliana Hali ,huku mwanamama Veronica price akiendesha. Walikuwa wakiongea ki Russia pasipo huyo mama kujua Nini wanaongea. Veronica price aliendelea ku drive gari Hadi Bayswater zilipokuwa nyumba kadhaa . Nyumba hizi zilichaguliwa kama safe house na M16 kwa ajili ya bwana Oleg. Zilikuwa umbali wa mwendo wa gari masaa mawili kutoka ubalozi wa Soviet hapo London.
 
Back
Top Bottom