Tarehe 18 Mei 1985: Shirika la kijasusi la KGB kulikuwa na idara iliyojulikana kama Directorate K

Tarehe 18 Mei 1985: Shirika la kijasusi la KGB kulikuwa na idara iliyojulikana kama Directorate K

Nimemchana anachofanya sio poah angekua anakupa credit aisee ...... Kwa hyo hapo anaenda kujivutia pesa kiulain kwa kila kichwa 2500 telegram[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Hajakutukana, maana yule bwana ni mtata sana kama ukiingia anga zake [emoji28][emoji28]
 
18

Mwanamama Veronica price , pamoja na maafisa wa ngazi za juu wa M16 waliipitia form ya application ya SUNBEAM na hatimaye waliona Sasa huyu bwana akiwa nchini mwao itakuwa ni jambo la heri sana kwao. Lakini swala la ku approve visa application ya Oleg halikuwa jambo jepesi hata kidogo. Hii ni kwa sababu Oleg tayari alishakuwa suspect na mashirika mengi ya ulaya magharibi ikiwemo PET na wao M16. Afisa yoyote wa Russia aliyekuwa ana uhusiano na KGB hakupaswa kuingia ndani ya uingereza endapo . Kimbembe kikawa ni wizara ya mambo ya nje ya uingereza. Kwani lazima wizara hii ingejua rekodi zote za Oleg hususan kufanya kazi nchi za Scandinavia na ingezusha maswali mengi sana. Lakini ni maafisa wachache wa ngazi za juu wa M16 walitaka huyu bwana apewe ruhusa kuingia nchini humo. Swala likawa ni kwamba ofisi ya uhamiaji ingetoa visa ila ni kwamba ingezusha wasiwasi ikiwa bwana Oleg atapewa idhibati ya kuingia uingereza. M16 baada ya kuona kikwazo ni ofisi za uhamiaji za uingereza ni kikwazo wakaamua kucheza Dili na PET . M16 waliwaambia wenzao PET endapo ofisi ya wizara ya mambo ya nje ya uingereza ikitaka enquiries kuhusiana na SUNBEAM kufanya kazi nchi hizo za Scandinavia wao waseme kwamba alifanya na hakuwa suspect wa KGB kama ilivyojulikana mwanzo . Kwa kifupi PET na M16 Walikuwa wanafanya mchezo wa kufoji taarifa za Oleg Ili visa yake ipasishwe na aweze kuingia uingereza. Taratibu zilikamilka na hatimaye diplomatic visa passport ya Oleg ndani ya siku 22 ikawa tayari imekamamilika badala ya siku 30. Kiuhalisia mamlaka za uhamiaji za uingereza zilikuwa Zina doubt sana ila ndio hivyo , majasusi ni majasusi tu.[emoji1]. Hata maafisa wa Russia kwenye ofisi ya wizara ya mambo ya nje walishangazwa na ku DOUBT visa ya Oleg kuwa approved haraka sana baada ya yeye kwenda kuipokea kwenye ofisi za uhamiaji .
Mamlaka za urusi zilikuwa slow kiasi kwamba Oleg ilimpasa asubiri miezi 3 zaidi mbele kabla ya kupewa ruhusa rasmi kutoka nje ya Russia.
Hili swala lilizua mjadala kwa Oleg binafsi na kwa uingereza hususan M16. Ni kwamba KGB walikuwa wanakagua background ya bwana Oleg na historia yake kwa ujumla. Hii kazi ilikuwa inafanywa na kitengo Cha internal investigation wing . Muda mwingi aliotumia kuusubiri alikuwa anaperuzi ma file mbalimbali ya KGB.
Wanasema kwenye headquarters za KGB mfumo wa kutunza mafaili yenye Siri ulikuwa ni complex sana . Ni kwamba kila afisa hapo kitengoni alikuwa na sefu yake ya kuhifadhia ma file kutokana na kila idara . Na baada ya kila afisa kufunga sefu yake funguo zote zilikuwa zinawekwa kwenye boksi special la mbao .kila ufunguo ulikuwa na individual stamp ya kumtambulisha afisa na idara husika . Ni kwamba boksi hili lenye funguo lilipelekwa kwenye ofisi kuu inayosimamia idara mbalimbali na Kisha boksi lile linafungiwa kwenye ofisi kuu ya FCD . Hivyo usalama wa mafaili ya Siri ulikuwa ni kipaumbele . Hivyo Oleg katika harakati za kupekua pekua mafaili alikutana na taarifa za bwana Jack Jones . Huyu alikuwa ni kiongozi wa chama Cha wafanyakazi nchini uingereza na baadaye kiongozi wa chama Cha communist party nchini uingereza . Huyu bwana kwa mujibu wa report za faili lake alikuwa anaiuzia KGB taarifa za kamati kuu za chama na serikali kuanzia 1964 Hadi 1969.
Mwingine Oleg aliyemgundua kwenye mafaili hayo ni bwana bob Edwards mbunge wa chama Cha mrengo wa kushoto Cha labour ambaye alikuwa na uhusiano na Russia miaka ya 1920s na Aliwahi Kukutana na Stalin .na alikuwa kwenye payroll ya KGB akiwauzia informations.
Mtu mwingine aliyekuwa pia ni agent wa KGB alikuwa ni mbunge mstaafu na katibu mkuu wa chama Cha labour party ambaye alikuwa na mahusiano ya Siri na KGB. Ilisemekana alikuwa anapokea fedha kutoka kwa KGB ku support chama chake kama payment ya kuwauzia taarifa za Siri urusi. Na wote hao ambao Oleg aliwagundua walikuwa ni left wingers yaani wale wanaoamini mrengo wa kushoto au pro-soviet.
Pia Oleg aliweza kupata file Moja lenye kurasa 300 hivi zito likamvutia likiwa limepewa jina la BOOT.
Ukurasa wake wa kwanza ulianza kwa maneno haya " I , senior operational officer major Petrov, Ivan Alexeyevich, herewith open a file on the agent Michael Foot, citizen of the United kingdom, giving him pseudonym Boot".
Ni kwamba huyu Michael foot alikuwa ni mbunge mstaafu wa chama Cha labour , mwandishi na pia mpinzani wa Margaret thatcher katika kinyang'anyiro Cha uchaguzi mkuu Cha uwaziri mkuu wakati huo. Naye huyu bwana alikuwa kwenye payroll ya KGB na alikuwa anatumiwa na huyo Petrov . Kiongozi mkuu wa chama Cha upinzani Cha labour . Huyu Foot alikuwa ni mwanasiasa machachari sana. Kwa mfano uchaguzi wa 1979 nchini uingereza James Callaghan baada ya kubwagwa na margareth thatcher akashinda kiti Cha u PM ,alijiuzulu kwenye chama Cha labour na nafasi yake akaichukua huyu Michael foot mwezi November 1980. Kura za maoni zilionyesha chama Cha labour kilikuwa mbele kwa asilimia 10 nyuma ya chama Cha conservative kilichokuwa kinaongozwa na margareth thatcher. Na uchaguzi uliotarajiwa kufanyika mwaka 1984 ulionyesha kwamba Michael foot angekuwa prime minister wa U.k.ila alianguka. Repoti zilikuja kuonyesha baadaye kwamba Laiti angeshinda huyu bwana ingekuwa ni kashfa kubwa kwa P.M wa uingereza kuwa agent wa KGB.
Pia taarifa za huyu bwana zilionyesha alikuwa anapokea fedha kati ya euro 100 Hadi 2000 na hakuwahi julikana ni payment za Nini miaka ya 1960s .

Hizi taarifa zote bwana oleg aliweza kuzihifadhi kwa MATUMIZI YAKE YA BAADAYE.[emoji28][emoji28].
Everyone has a price tag Ulimakafu kuja huku
 
Huyo buyoye ni nyoko na mwizi hafu Huwa analipishwa watu kwanini asirepotiwe Kwa copyright infringement Hana haya kweli, hata story ya yoga aliiba pia
Ni swala la muda tu.
 
Ni swala la muda tu.
Inabidi watu waanze kumu report Kwa copyright infringement maana huo ni wizi wa kazi na nguvu za wengine pia aweke source. Mange kimambi kawakomesha wote waliokuwa wanatumia habari zake Tena huko Twitter au Instagram uki report inafanyiwe kazi, haiwezekani mtu atumie nguvu and energy yeye aibe bila kutaja hata source this isn't fair huku yeye akauze hizo habari
 
Sehemu 02.

SEHEMU YA PILI

Bwana Oleg Gordievsky alizaliwa ndani ya KGB ,ikamkomaza,ikamtwist vilivyo na almanusura imhuharibie maisha . Kufanya kazi ndani ya idara kubwa ya kijasusi ndani ya muungano wa Soviet,kwake ilikuwa ni heshima kubwa sana na ni kazi iliyokuwa kwenye damu yake. Kwani baba yake amefanya kazi ndani ya shirika Hilo maisha yake yote. Familia ya Gordievsky iliishi kwenye apartment za shirika Hilo na walipewa special treatment na favor maalumu kwa kuwa wao walikuwa ni familia ya kitengo.

Shirika la kijasusi la KGB(komitet gosudarstvennoy bezospasnosti) kwa kiswahili sanifu ni kamati ya ulinzi la kitaifa, ilikuwa ni taasisi imara ya usalama kuwahi kuundwa hapa duniani. Shirika Hili lilizaliwa kutoka kwenye kikundi kidogo Cha majasusi watiifu wa mzee Stalin. Kazi Yake ilikuwa kukusanya taarifa nje na ndani ya muungano wa Soviet ,kutoa ulinzi ndani ya taifa ,pamoja na maafisa wa ngazi za juu wa serikali ya kijamaa.

Kwa kifupi shirika Hili lilikuwa limetawala nyanja zote za kimaisha kwa wale wote waliokuwa wapo chini ya muungano wa ki Soviet.

Lilikuwa ni shirika lililoajiri na kupandikiza majasusi duniani kote kwa ajili ya ,kukusanya ,kuiba ,na pia kununua taarifa mbalimbali za Siri ikiwemo za kijeshi, kisiasa, silaha pamoja na taarifa za kisayansi na teknolojia. Inakadiriwa kipindi hicho shirika likiwa katika kilele Cha mafanikio ilikuwa na ma agent takribani milioni na zaidi.

Kwa upande wa nchi za kimagharibi hii taasisi ilitazamwa kama zana ya kuwatia watu hofu,kutii wasichokijua,kuwatesa na kuwanyanyasa raia wake kidhalimu. Ilitazamwa kama kundi la kimafia chini ya mwavuli wa kikomunisti lenye kusambaza propaganda za kijamaa zilizopitwa na wakati .

Lakini kwa waliokuwa wanaishi chini ya muungano wa ki Soviet wao walichukulia KGB kama mlinzi wao,alama ya uzalendo na Utiifu kwa taifa na mamlaka,pamoja na ngao ya kuwalinda Raia dhidi ya umagharibi. Kuwa memba wa KGB ilikuwa ni heshima na sifa na pia alama ya ufahari kwa wakati huo.

Hivyo basi bwana Oleg hakuwa na la kupingana nalo zaidi ya kufuata nyendo za mshua wake bwana Anton lavrentyevich Gordievsky, na kuwa afisa wa KGB.

Baba yake Oleg kabla ya kuwa afisa wa KGB ,alikuwa ni mwalimu .lakini baada ya mapinduzi ya mwaka 1917 akaamua kujiunga na kuwa mwanachama rasmi wa chama Cha kikomunisti. Kilichomfanya baba yake Oleg kujiunga na ukomunist ni itikadi za mzee Stalin , ambazo zilikuwa Kali.
Alijiunga na chama Cha NkVD( baadaye sana ilimezwa ndani ya KGB) au taasisi ya kikomunisti kwa ustawi wa watu. Lengo la hii taasisi au chama ni kulinda maslahi ya kikomunisti ,kutoa ulinzi na vilevile kusambaza propaganda pamoja na kupambana na maadui wa urusi. Mzee Stalin alitangazia umma kwamba maadui wa urusi ni mabepari , mashoga,majasusi wa utawala uliopita,wayahudi , maofisa wa serikali wenye mrengo wa kibepari n.k. Hivyo bwana Anton alijitolea kwa udi na uvumba katika kulinda itikadi za kikomunisti. Alijitolea kufundisha propaganda kwenye kambi za kijeshi na taasisi za elimu . Tuseme kwa kifupi alikuwa ni mwenezi kama polepole.
Na katika kipindi hicho watu walianza kuonja ladha ya ukomunisti .watu walipotezwa, wengine walinyang'anywa Mali ,kufungwa na pia wengine walilazimishwa kuhama nchi. Na kubwa zaidi wengi walikufa na njaa kutokana na uzalishaji kuzorota mashamba na maghala kuchukuliwa na serikali. Japo mzee Anton alikuwa ni mwanachama mtiifu kwa chama na serikali lakini nafsi ilikuwa inamsuta.
Alimwoa Olga nikolayevna gornova mrembo wa miaka 24 aliyekuwa anafanya kazi kwenye ofisi za takwimu. Walihamia Moscow kwenye apartments zilizokuwa spesho kwa ajili ya maafisa wa NkVD. Mtoto wao wa kwanza aliitwa Vasili aliyezaliwa 1932. Mtoto wao wa pili alizaliwa miaka sita baadaye yaani 1938,aliyeitwa Oleg antonyevich Gordievsky tarehe 10 October.
Mtoto wao wa tatu aliitwa marina aliyezaliwa miaka Saba baadaye. Kwa kifupi ilikuwa ni familia ya kitengo. Watoto walikuwa vizuri na pia stahiki na treatment za kutosha walizipata kutoka serikalini kwa kuwa ni familia ya KITENGO. Familia ilikuwa na kulelewa katika itikadi za kijamaa ,na watoto walikuwa watiifu na wazalendo kwa serikali ya kisoviet. Waswahili wanasema kila familia Ina Siri zake . kwa nje familia ya mzee Anton ilionekana ni familia Bora na iliyostawi sana na majirani kuweza kuwa admire. Haikuwa hivyo. Mzee Anton nafsi ilikuwa inamsuta sana kwa mabaya aliyokuwa anayafanya kipindi Cha Stalin anashika hatamu. Mfano kupotezwa kwa watu,uporaji wa mashamba na vifo vilivyotokana na njaa.hii ilimsumbua sana nafsini mwake lakini alikausha na Siri yake moyoni. Mkewe , Olga hakuwahi kuukubali ukomunisti lakini atafanyaje ndio anaishi kwenye ndoa yenye itikadi hizo. Sababu ya kuchukia ukomunisti ni kwamba baba yake alinyang'anywa mashine zile za upepo za kuvuta maji ardhini na serikali,pia kaka yake alikamatwa kwa kosa la kupinga sera ya umiliki na kilimo Cha kwa pamoja na kupelekwa huko Gulag Jimbo lililoko mashariki mwa Siberia na kupotelea huko mazima. Pia aliwahi shuhudia majirani zake kipindi hicho wakifuatwa usiku na watu wasiojulikana na kuondoka nao asiwaone tena.


View attachment 2588392
Familia ya mzee Anton kushoto na wanao wawili marina na Oleg wakiwa na umri wa miaka kumi hivi

View attachment 2588393
Watoto wa mzee Anton Vasili,mdogo wao wa kike marina na Oleg Gordievsky.


Oleg na Vasili walitofautiana kwa umri wa miaka sita hivi.na walikuwa kipindi Cha vita. Kwa mfano Vasili akiwa mdogo, alishuhudia mateka wa kivita wa kijerumani wakipanga gwaride mitaa ya Moscow na kulazimishwa kutembea umbali mrefu wakinyanyaswa na kudhihakiwa kama wanyama. Baba Yao mara nyingi alisafiri sehemu mbalimbali za nchi kueneza propaganda za kikomunisti. Kwa upande wa Oleg ,yeye alikuwa ni mtu wa kujifunza na kusoma vitabu. Kwa umri wake mdogo alijifunza kusoma katekisimu ya ki orthodox yenye mrengo wa kikomunisti. Pia alikuwa ni mtu wa kujifunza lugha na hatimaye alionyesha uwezo mkubwa katika kujifunza kijerumani. Baba yake Oleg alikuwa kila akirudi lazima aje na magazeti yenye itikadi za kikomunisti hivyo akawa na wasaha wa kuyasoma. Ingawaje alikuwa anasoma vitabu vya propaganda dhidi ya magharibi alivutiwa na maswala, kadhaa ikiwemo lugha za huko. Rasmi Sasa Oleg alivyofika umri wa utineja akajiunga tuseme UVCCM ya huko iliyojulikana kama KOMSOMOL.
Oleg alikulia kwenye familia yenye upendo baba yake akiwa mwanachama rasmi wa KGB,na mama yake pia akiwa mke wa afisa ,mama wa nyumbani, lakini ndani ya mioyo Yao Hawa wanandoa wawili walikuwa wanafeki tu kwa nje lakini ndani mwao kulikuwa na vidonda kuhusu madhila ya mfumo mzima wa kikatili wa kikomunisti.hakuna aliyewahi jionyesha kwamba anadukuduku lake dhidi ya mfumo.
Kwa kipindi hicho Cha utawala wa Stalin familia ya Anton Gordievsky waliamini kwamba unaweza ukawa mtiifu kwa serikali ya kikomunisti , lakini ukawa una amini jambo lingine kwa Siri sana Japo ilikuwa ni jambo la hatari ya maisha. Kwa mfano hapa kwetu uwe mtiifu kwa serikali ya ccm lakini ndani ni mwanachama mtiifu kabisa wa upinzani.

Umahiri wa Oleg ulidhihirika akiwa na UVCCM Yao ya KOMSOMOL kwa kupewa medali ya silver kama kijana mwenye akili , shupavu,mwenye bidii katika michezo na vilevile mzalendo haswa kwa nchi yake .licha ya hayo yote Oleg Gordievsky alijifunza kuishi maisha ya aina mbili.
Daah
 
19

Hili faili la Michael foot a.k.a agent BOOT lilifunua mambo mengi kidogo kwa upande wa bwana Oleg. Report mbalimbali zinasema kwamba huyu Michael foot alikuwa anapokea baadhi ya taarifa na majasusi wa urusi azitumie katika kampeni zake , hususan kuishawishi uingereza kuachana na kusitisha matumizi ya nuclear (. Nuclear disarmament ) . Kumbuka huyu bwana alikuwa ni mwanachama wa mrengo wa kushoto hivyo sera zake kipindi Cha kampeni aligusia kuitoa uingereza katika matumizi ya nuclear. Sera hizi alikuwa anapewa na urusi ,Kwa maana urusi au Soviet haikutaka nchi za magharibi kujizatiti katika kujijenga na kujilinda kupitia silaha za nuclear. Kwao waliona kama ni tishio. Repoti iliendelea kudokeza kwamba foot alitoa list ya wanasiasa ambao ni pro- Soviet kwa Russia na hivyo wangekuwa wanapewa fund na urusi ya kujiimarisha kisiasa na pia kuwapa Hela za matanuzi kipindi Cha holiday. Lengo la hizi fund lilikuwa ni kuwashawishi viongozi hao wawe na ushawishi katika kupinga matumizi ya nuclear ambao nchi za magharibi zilikuwa zimejikita katika kujiimarisha kiulinzi kutokana na tishio la umoja wa kisoviet enzi ya vita baridi. Pia bwana foot alitoa taarifa za maoni ya chama chake Kwa KGB kuhusiana na mtazamo wa uingereza kwenye maswala tata yaliyokuwa yanagonga vichwa kwa wakati huo ,kama uvamizi wa marekani nchini Vietnam,mauaji ya Kennedy na athari za kisiasa, na pia agenda kuu za mkutano wa Geneva kuhusu vita ya Korea 1954 . Nao KGB wangemtumia bwana foot katika kuyaeleza haya yote kwenye vikao vya chama na kitaifa kwa mtazamo ambao ungeegemea upande wa Russia. Kwa kifupi foot hata baadhi ya hotuba kuhusiana na maswala mtambuka wakati huo alikuwa akiandikiwa kwa msaada wa KGB. Alikuwa akitumika kueneza propaganda za Russia pasipo yeye kufahamu.
Mwaka 1967 bwana foot aliwapinga Russia hadharani kwa kitendo Chao Cha kuivamia Czechoslovakia. Russia wakaacha kumtumia na kuamua kumpuuzia. Lakini baadaye Russia wali resume tena mahusiano na foot baada ya kuchaguliwa na labour party kama kiongozi mkuu wa upinzani na ambaye alitarajiwa atapambana thatcher kwenye debe la kuwania u prime minister uchaguzi uliotarajiwa kufanyika. Ripoti mbalimbali baadaye zilisema kwamba endapo hizi taarifa za foot kuwa na mahusiano na KGB zingejulikana na mahasimu wake wa kisiasa hususan wa conservative , wangetumia kama fimbo ya kumchapa na kumpoteza kisiasa mazima . lakini bahati aliangushwa kwenye uchaguzi mkuu uliofuata wa 1984.
Kumbuka hili file bwana Oleg Gordievsky alilisoma mwaka 1981.



Tarehe 2 April 1982, nchi ya Argentina ilivamia visiwa vya faulkland vilivyokuwa chini ya uingereza kusini mwa bahari ya Atlantic. Huyu bwana foot alitaka hatua zichukuliwe za haraka kuhusiana na uvamizi huo wa Argentina. Margaret thatcher alituma kikosi kazi kudili na wavamizi huo. Hili tukio liliwachukiza sana Urusi hususan KGB na kupelekwa mwanamama huyu kuchukiwa na Urusi (Hadi Leo hii), kwa hatua zake za kuzima uvamizi huo. Kwani Moscow waliamini uingereza wangekuwa defeated katika kuuzima uvamizi huo. Russia walipanick sana katika tukio hili ,kwa maana hata Michael foot aliafiki kwa mpinzani wake wa kisiasa mwanamama thatcher kuchukua jitihada za kuzima uvamizi huo.
Ni kwamba uingereza au Britain kwa wakati huo ilikuwa katika vita baridi . Oleg alikuwa ameshachagua upande wake tayari [emoji39].





Baada ya Moscow kufanya clearance kwa Bwana Oleg , hatimaye mwaka tarehe 28 June 1982 alikwea pipa la shirika la ndege la Aeroflot Hadi London akiwa na mkewe Leila na wanao wawili. Ni kwamba akili ilikuwa inawaza mambo mengi ikiwemo taarifa za kijasusi alizozikusanya miezi minne akiwa anasubiri approval ya kusafiri.
Kifupi alikuwa amebeba kichwani mwake taarifa nyeti sana kwa wakati huo ikiwemo za agent boot au Michael foot . Na pia taarifa za majasusi wote walioko Jiji la London.
Lakini wanasema msaliti anakuwa na msaliti wake .



Tuachane na Oleg kidogo.tusonge Hadi marekani.


Aldrich Ames alikuwa ni afisa wa CIA ,mwenye maisha ya kawaida Lakini asiyekuwa na furaha kutokana na pandashuka ndani ya ndoa yake.
Huyu bwana kazi aliyopewa ya kuwaajiri na kuwatumia majasusi wa Soviet ndani ya mexico haikuwa na matokea yaliyotarajiwa na maboss wake ndani ya Langley Virginia makao makuu ya idara hiyo.Hakuthaminiwa ,na pia malipo hayakuwa mazuri na ndio ilifanya hata ndoa yake kuingia matatizoni. Alikuwa mzembe na careless sana kiasi Cha maboss wake kutomzingatia sana.
Huyu bwana alizaliwa huko river falls , Wisconsin mwaka 1941. Baba yake alikuwa ni academian na baadaye akawa anafanyia CIA kazi huko Burma.
Huyu Ames alikuwa ni mtu intelligent na pia Mtu mwenye ndoto kubwa za kuwa mbali kimaisha. Alijiunga na chuo Cha Chicago ila baadaye akaacha ,na kuanza kufanya part-time kama muigizaji. Baadaye alirudi na kupata degree yake ya kwanza na kujiunga na junior officer training course ndani ya CIA kwa kupitia connection ya mshua wake. Hii course ililenga kuongeza idadi ya majasusi kutokana na uhitaji mkubwa uliokuwepo wakati huo.
Alitumwa huko uturuki ambapo ndio palikuwa ndio center ya vita ya kijasusi kati ya west na east. Hii ni kwa sababu pia hapo uturuki palikuwa na military base ya marekani . Karibu na urusi kabisa .
Huko kazi yake ilikuwa ni kupandikiza majasusi wa Soviet na kukusanya taarifa kupitia wao. Pia kipindi Cha uvamizi wa Czechoslovakia na Russia , alikuwa na kazi ya kuchapisha vipeperushi vilivyoandikwa " Remember 68" lengo la hivi vipeperushi ni kuvimwaga kwenye dustbin kuwakumbusha waturuki kwamba nao wanaweza kuwa huenda nao watavamiwa na urusi kama walivyofanya kwa Czechoslovakia .
Mwaka 1972 alirudi Washington na akatumia miaka nne zaidi kujifunza ki Russia na kufanya kazi kwenye idara ya Soviet-east European department. Hii idara haikumvutia hata kidogo.
Hii ni kutokana kwamba kipindi hiki CIA ilikuwa inapigwa msasa kutokana na kashfa zilizokuwa zinaandama kitengo kwa wakati huo.
Kashfa zilizokuwa zinaandama shirika hili ni kwamba , ilisemekana Richard Nixon kwa wakati huo alipanga kuitumia CIA kuvuruga uchunguzi wa serikali kutokana na skendo maarufu wakati huo iliyomwandama ya WATERGATE SCANDAL. Pia serikali ya marekani ilikuja kubaini kazi chafu za taasisi hiyo ya usalama na kutaka kufanyike uchunguzi wa kina, tuhuma ikiwemo kupanga mauaji , matumizi ya binadamu kwenye kufanya tafiti (human experimentation), tuhuma za CIA kushirikiana na mafia,na vilevile tuhuma za kuwadukua watu pasipo ridhaa Yao. Sasa hizi kashfa ziliandama CIA kwa miaka 20 baadaye. Hii ilifanya mkurugenzi wake kwa wakati huo kujiuzulu aliyejulikana kama bwana James angleton pamoja na top staff wa shirika Hilo. CIA ndio kipindi ilianza kupoteza mvuto sana . Na hiyo tumbua tumbua ilikuwa ni bumpyride kwa maafisa wengi lakini haikumgusa Ames . Ilisemekana kwamba CIA ingetengamaa baada ya Miaka kumi baadaye ili iweze kurudi kwenye mstari na kupambana na KGB Ili liweze kuwa na ushawishi duniani.
Mwaka 1976 alipelekwa kikazi huko new York na baadaye akatumwa kikazi huko mexico 1981.
Wakuu wa CIA walianza ku notice tabia yake ya ulevi kupitiliza ,na kulalama kila wakati. Ila hakukuwahi pendekezwa aachishwe kazi.
Baadaye alimwoa Nancy segebarth. Kama Oleg tu ,ndoa yake ilikuwa na mvutano sana.
Akiwa meksiko kikazi hakuambatana na mkewe. Alikuwa akijihusisha na mahusiano na wanawake wengi .
Mwaka 1982 alikutana na mwanadada Rosario casas dupuy wa miaka 29 mwenye asili ya Colombia na ufaransa. Alikuwa mfanyakazi wa ubalozi wa Colombia hapo Mexico city.na ndipo walikutana na Ames kwenye diplomatic dinner party.
 
Nimemwona yaani we acha tu ,mpaka picha za humu kazipeleka kule yaani..dah...kwamba waende wakaisome telegram [emoji28][emoji28]
kwa jina naitwa Fortunatus Buyobe au ukipenda niite ndimu mkata shombo.

Kwanza naomba nijibu hoja yako moja kwa haraka sana bila kuikawiza

1. Kwamba nimekukopy na hadi nimechukua picha zako. Swali ni, ni wewe ndiye umezipiga picha hizi? Kama sio unajimilikishaje hakimiliki?

2. Kwa msisiti mkubwa ni kwamba sijakunukuu, siwezi kukunukuu na uwezo wangu wa kuandika tayari upo dhahili (mnyonge mnyongeni haki yake mpeni) ni kwamba members humu humu watapika consistency yako ya uandishi. Wataangalia chapisho lako la jana, la leo na la keshokutwa kisha kila kitu kitakuwana baina yako nami.

3. Hapa ndio pa muhimu zaidi. Bwana Oleg Gordievsky habari zake zimeandikwa sehemu nyini sana.

Naomba niseme wewe Story yako umeicopy hapa na kuitafsiri kwa kiswahili 👇


So hii ni open source document don’t own any rights na mbaya zaidi hukuwa mbunifu bali umecopy neno hadi neno.

Mimi bwana Oleg nimemsoma kulitia mwandishi BEN MACYNTYRE aliyefanya naye mahojiano. Hata hizo picha unazodai kuwa ni zako umezitoa kwenye hints za kitabu chake cha A SPY AND TRAITOR hivyo HUNA CHOCHOTE KILICHO CHAKO.

Mimi nina vyangu. My flow, Mpangilio wa matukio, na haya hayajionyeshi kwenye hii stotu tu bali na nyingine nyingi.

Karibu Telegramm utakuta story hii inaitwa THE MOLE, mle ndani imeanza na kina Aimes, Hanssen na ikaishia na Oleg. Sasa jiangalie. Ungekuwa na Identity ya kueleweka ningekushitaki
E1F41C00-1094-42B3-AA58-F04CFBDA1471.png
F74A5D34-8C38-416F-B175-7035FDC30424.jpeg
69AD5A3E-307E-4A3D-8CAA-9DC23D821E23.jpeg
 
kwa jina naitwa Fortunatus Buyobe au ukipenda niite ndimu mkata shombo.

Kwanza naomba nijibu hoja yako moja kwa haraka sana bila kuikawiza

1. Kwamba nimekukopy na hadi nimechukua picha zako. Swali ni, ni wewe ndiye umezipiga picha hizi? Kama sio unajimilikishaje hakimiliki?

2. Kwa msisiti mkubwa ni kwamba sijakunukuu, siwezi kukunukuu na uwezo wangu wa kuandika tayari upo dhahili (mnyonge mnyongeni haki yake mpeni) ni kwamba members humu humu watapika consistency yako ya uandishi. Wataangalia chapisho lako la jana, la leo na la keshokutwa kisha kila kitu kitakuwana baina yako nami.

3. Hapa ndio pa muhimu zaidi. Bwana Oleg Gordievsky habari zake zimeandikwa sehemu nyini sana.

Naomba niseme wewe Story yako umeicopy hapa na kuitafsiri kwa kiswahili [emoji116]


So hii ni open source document don’t own any rights na mbaya zaidi hukuwa mbunifu bali umecopy neno hadi neno.

Mimi bwana Oleg nimemsoma kulitia mwandishi BEN MACYNTYRE aliyefanya naye mahojiano. Hata hizo picha unazodai kuwa ni zako umezitoa kwenye hints za kitabu chake cha A SPY AND TRAITOR hivyo HUNA CHOCHOTE KILICHO CHAKO.

Mimi nina vyangu. My flow, Mpangilio wa matukio, na haya hayajionyeshi kwenye hii stotu tu bali na nyingine nyingi.

Karibu Telegramm utakuta story hii inaitwa THE MOLE, mle ndani imeanza na kina Aimes, Hanssen na ikaishia na Oleg. Sasa jiangalie. Ungekuwa na Identity ya kueleweka ningekushitaki

Mwanaume anajiitaje ndimu mkata shombo[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Wanaumeeeee hapa kuna mwenzenu kweli?[emoji2094][emoji2094][emoji2094][emoji2094]
 
19

Hili faili la Michael foot a.k.a agent BOOT lilifunua mambo mengi kidogo kwa upande wa bwana Oleg. Report mbalimbali zinasema kwamba huyu Michael foot alikuwa anapokea baadhi ya taarifa na majasusi wa urusi azitumie katika kampeni zake , hususan kuishawishi uingereza kuachana na kusitisha matumizi ya nuclear (. Nuclear disarmament ) . Kumbuka huyu bwana alikuwa ni mwanachama wa mrengo wa kushoto hivyo sera zake kipindi Cha kampeni aligusia kuitoa uingereza katika matumizi ya nuclear. Sera hizi alikuwa anapewa na urusi ,Kwa maana urusi au Soviet haikutaka nchi za magharibi kujizatiti katika kujijenga na kujilinda kupitia silaha za nuclear. Kwao waliona kama ni tishio. Repoti iliendelea kudokeza kwamba foot alitoa list ya wanasiasa ambao ni pro- Soviet kwa Russia na hivyo wangekuwa wanapewa fund na urusi ya kujiimarisha kisiasa na pia kuwapa Hela za matanuzi kipindi Cha holiday. Lengo la hizi fund lilikuwa ni kuwashawishi viongozi hao wawe na ushawishi katika kupinga matumizi ya nuclear ambao nchi za magharibi zilikuwa zimejikita katika kujiimarisha kiulinzi kutokana na tishio la umoja wa kisoviet enzi ya vita baridi. Pia bwana foot alitoa taarifa za maoni ya chama chake Kwa KGB kuhusiana na mtazamo wa uingereza kwenye maswala tata yaliyokuwa yanagonga vichwa kwa wakati huo ,kama uvamizi wa marekani nchini Vietnam,mauaji ya Kennedy na athari za kisiasa, na pia agenda kuu za mkutano wa Geneva kuhusu vita ya Korea 1954 . Nao KGB wangemtumia bwana foot katika kuyaeleza haya yote kwenye vikao vya chama na kitaifa kwa mtazamo ambao ungeegemea upande wa Russia. Kwa kifupi foot hata baadhi ya hotuba kuhusiana na maswala mtambuka wakati huo alikuwa akiandikiwa kwa msaada wa KGB. Alikuwa akitumika kueneza propaganda za Russia pasipo yeye kufahamu.
Mwaka 1967 bwana foot aliwapinga Russia hadharani kwa kitendo Chao Cha kuivamia Czechoslovakia. Russia wakaacha kumtumia na kuamua kumpuuzia. Lakini baadaye Russia wali resume tena mahusiano na foot baada ya kuchaguliwa na labour party kama kiongozi mkuu wa upinzani na ambaye alitarajiwa atapambana thatcher kwenye debe la kuwania u prime minister uchaguzi uliotarajiwa kufanyika. Ripoti mbalimbali baadaye zilisema kwamba endapo hizi taarifa za foot kuwa na mahusiano na KGB zingejulikana na mahasimu wake wa kisiasa hususan wa conservative , wangetumia kama fimbo ya kumchapa na kumpoteza kisiasa mazima . lakini bahati aliangushwa kwenye uchaguzi mkuu uliofuata wa 1984.
Kumbuka hili file bwana Oleg Gordievsky alilisoma mwaka 1981.



Tarehe 2 April 1982, nchi ya Argentina ilivamia visiwa vya faulkland vilivyokuwa chini ya uingereza kusini mwa bahari ya Atlantic. Huyu bwana foot alitaka hatua zichukuliwe za haraka kuhusiana na uvamizi huo wa Argentina. Margaret thatcher alituma kikosi kazi kudili na wavamizi huo. Hili tukio liliwachukiza sana Urusi hususan KGB na kupelekwa mwanamama huyu kuchukiwa na Urusi (Hadi Leo hii), kwa hatua zake za kuzima uvamizi huo. Kwani Moscow waliamini uingereza wangekuwa defeated katika kuuzima uvamizi huo. Russia walipanick sana katika tukio hili ,kwa maana hata Michael foot aliafiki kwa mpinzani wake wa kisiasa mwanamama thatcher kuchukua jitihada za kuzima uvamizi huo.
Ni kwamba uingereza au Britain kwa wakati huo ilikuwa katika vita baridi . Oleg alikuwa ameshachagua upande wake tayari [emoji39].





Baada ya Moscow kufanya clearance kwa Bwana Oleg , hatimaye mwaka tarehe 28 June 1982 alikwea pipa la shirika la ndege la Aeroflot Hadi London akiwa na mkewe Leila na wanao wawili. Ni kwamba akili ilikuwa inawaza mambo mengi ikiwemo taarifa za kijasusi alizozikusanya miezi minne akiwa anasubiri approval ya kusafiri.
Kifupi alikuwa amebeba kichwani mwake taarifa nyeti sana kwa wakati huo ikiwemo za agent boot au Michael foot . Na pia taarifa za majasusi wote walioko Jiji la London.
Lakini wanasema msaliti anakuwa na msaliti wake .



Tuachane na Oleg kidogo.tusonge Hadi marekani.


Aldrich Ames alikuwa ni afisa wa CIA ,mwenye maisha ya kawaida Lakini asiyekuwa na furaha kutokana na pandashuka ndani ya ndoa yake.
Huyu bwana kazi aliyopewa ya kuwaajiri na kuwatumia majasusi wa Soviet ndani ya mexico haikuwa na matokea yaliyotarajiwa na maboss wake ndani ya Langley Virginia makao makuu ya idara hiyo.Hakuthaminiwa ,na pia malipo hayakuwa mazuri na ndio ilifanya hata ndoa yake kuingia matatizoni. Alikuwa mzembe na careless sana kiasi Cha maboss wake kutomzingatia sana.
Huyu bwana alizaliwa huko river falls , Wisconsin mwaka 1941. Baba yake alikuwa ni academian na baadaye akawa anafanyia CIA kazi huko Burma.
Huyu Ames alikuwa ni mtu intelligent na pia Mtu mwenye ndoto kubwa za kuwa mbali kimaisha. Alijiunga na chuo Cha Chicago ila baadaye akaacha ,na kuanza kufanya part-time kama muigizaji. Baadaye alirudi na kupata degree yake ya kwanza na kujiunga na junior officer training course ndani ya CIA kwa kupitia connection ya mshua wake. Hii course ililenga kuongeza idadi ya majasusi kutokana na uhitaji mkubwa uliokuwepo wakati huo.
Alitumwa huko uturuki ambapo ndio palikuwa ndio center ya vita ya kijasusi kati ya west na east. Hii ni kwa sababu pia hapo uturuki palikuwa na military base ya marekani . Karibu na urusi kabisa .
Huko kazi yake ilikuwa ni kupandikiza majasusi wa Soviet na kukusanya taarifa kupitia wao. Pia kipindi Cha uvamizi wa Czechoslovakia na Russia , alikuwa na kazi ya kuchapisha vipeperushi vilivyoandikwa " Remember 68" lengo la hivi vipeperushi ni kuvimwaga kwenye dustbin kuwakumbusha waturuki kwamba nao wanaweza kuwa huenda nao watavamiwa na urusi kama walivyofanya kwa Czechoslovakia .
Mwaka 1972 alirudi Washington na akatumia miaka nne zaidi kujifunza ki Russia na kufanya kazi kwenye idara ya Soviet-east European department. Hii idara haikumvutia hata kidogo.
Hii ni kutokana kwamba kipindi hiki CIA ilikuwa inapigwa msasa kutokana na kashfa zilizokuwa zinaandama kitengo kwa wakati huo.
Kashfa zilizokuwa zinaandama shirika hili ni kwamba , ilisemekana Richard Nixon kwa wakati huo alipanga kuitumia CIA kuvuruga uchunguzi wa serikali kutokana na skendo maarufu wakati huo iliyomwandama ya WATERGATE SCANDAL. Pia serikali ya marekani ilikuja kubaini kazi chafu za taasisi hiyo ya usalama na kutaka kufanyike uchunguzi wa kina, tuhuma ikiwemo kupanga mauaji , matumizi ya binadamu kwenye kufanya tafiti (human experimentation), tuhuma za CIA kushirikiana na mafia,na vilevile tuhuma za kuwadukua watu pasipo ridhaa Yao. Sasa hizi kashfa ziliandama CIA kwa miaka 20 baadaye. Hii ilifanya mkurugenzi wake kwa wakati huo kujiuzulu aliyejulikana kama bwana James angleton pamoja na top staff wa shirika Hilo. CIA ndio kipindi ilianza kupoteza mvuto sana . Na hiyo tumbua tumbua ilikuwa ni bumpyride kwa maafisa wengi lakini haikumgusa Ames . Ilisemekana kwamba CIA ingetengamaa baada ya Miaka kumi baadaye ili iweze kurudi kwenye mstari na kupambana na KGB Ili liweze kuwa na ushawishi duniani.
Mwaka 1976 alipelekwa kikazi huko new York na baadaye akatumwa kikazi huko mexico 1981.
Wakuu wa CIA walianza ku notice tabia yake ya ulevi kupitiliza ,na kulalama kila wakati. Ila hakukuwahi pendekezwa aachishwe kazi.
Baadaye alimwoa Nancy segebarth. Kama Oleg tu ,ndoa yake ilikuwa na mvutano sana.
Akiwa meksiko kikazi hakuambatana na mkewe. Alikuwa akijihusisha na mahusiano na wanawake wengi .
Mwaka 1982 alikutana na mwanadada Rosario casas dupuy wa miaka 29 mwenye asili ya Colombia na ufaransa. Alikuwa mfanyakazi wa ubalozi wa Colombia hapo Mexico city.na ndipo walikutana na Ames kwenye diplomatic dinner party.

Boss tuendelee usijibu negative comments
Watu tunafatilia tuwekee vitu leo weekend muda wa kusoma upo
 
kwa jina naitwa Fortunatus Buyobe au ukipenda niite ndimu mkata shombo.

Kwanza naomba nijibu hoja yako moja kwa haraka sana bila kuikawiza

1. Kwamba nimekukopy na hadi nimechukua picha zako. Swali ni, ni wewe ndiye umezipiga picha hizi? Kama sio unajimilikishaje hakimiliki?

2. Kwa msisiti mkubwa ni kwamba sijakunukuu, siwezi kukunukuu na uwezo wangu wa kuandika tayari upo dhahili (mnyonge mnyongeni haki yake mpeni) ni kwamba members humu humu watapika consistency yako ya uandishi. Wataangalia chapisho lako la jana, la leo na la keshokutwa kisha kila kitu kitakuwana baina yako nami.

3. Hapa ndio pa muhimu zaidi. Bwana Oleg Gordievsky habari zake zimeandikwa sehemu nyini sana.

Naomba niseme wewe Story yako umeicopy hapa na kuitafsiri kwa kiswahili [emoji116]


So hii ni open source document don’t own any rights na mbaya zaidi hukuwa mbunifu bali umecopy neno hadi neno.

Mimi bwana Oleg nimemsoma kulitia mwandishi BEN MACYNTYRE aliyefanya naye mahojiano. Hata hizo picha unazodai kuwa ni zako umezitoa kwenye hints za kitabu chake cha A SPY AND TRAITOR hivyo HUNA CHOCHOTE KILICHO CHAKO.

Mimi nina vyangu. My flow, Mpangilio wa matukio, na haya hayajionyeshi kwenye hii stotu tu bali na nyingine nyingi.

Karibu Telegramm utakuta story hii inaitwa THE MOLE, mle ndani imeanza na kina Aimes, Hanssen na ikaishia na Oleg. Sasa jiangalie. Ungekuwa na Identity ya kueleweka ningekushitaki
Broo punguza vitisho,alaf pia na wewe umezidi nakumbuka kuna story kama sio ya UMUGHAKA sijui n nani nayo uliitoa humu ukawa unairusha kule kwako,alaf pia umshtak mtu kwa kipi kaka?hii kuburudika tuu au kuna kingine?

Ukweli n kwamba umeona jamaa anatoa hii story ukaamua kwenda kuitafuta ukaipa kichwa kingine ili watu watoe 2.5k per monthly,na naimani hakuna mwenye hati miliki ya hii story kwan hata wewe mwenyewe umeikopi mahali,
 
Back
Top Bottom