Tarehe 18 Mei 1985: Shirika la kijasusi la KGB kulikuwa na idara iliyojulikana kama Directorate K

Tarehe 18 Mei 1985: Shirika la kijasusi la KGB kulikuwa na idara iliyojulikana kama Directorate K

We mtanzania humjui kwa ulimbukeni?Mtz yeye kutumia vitu vya kutoka nje,kwake ni sawa na kuwaringishia wengine kuwa ana mkwanja mnene na elimu ya kutosha eti!.[emoji23][emoji23][emoji23]
Hata hivyo muda mwingine lazima uangalie vitu vya ndani ni vipi?. Hizi energy za kukuua?.
 
Kwa shirika la kijasusi la KGB kulikuwa na idara iliyojulikana kama directorate K. Hii idara ilikuwa na kazi maalumu ya kufanya bugging , kile kitendo Cha kupandikiza vinasa sauti na video camera kwa Siri kwenye ofisi za walengwa maalumu waliokusudiwa , kusikiliza mawasiliano Yao ya simu au pia wakati mwingine kwenye makazi Yao binafsi.

Ilichukua nusu dakika kufungu vitasa viwili vya mlango wa mbele wa chumba namba 220 kwenye ghorofa ya nane katika mtaa wa Leninsky prospekt . Hili lilikuwa ni jumba la ghorofa lililokuwa linakaliwa na maofisa wa KGB pamoja na familia zao.

Kwa Siri sana wanaume waawili waliokuwa wamevalia overall pamoja na gloves kwa haraka haraka wangedhaniwa kuwa ni mafundi tu wa kawaida kwa ajili ya kufanya matengenezo madogo madogo katika jumba Hilo , lakini uhalisia haukuwa hivyo. Baada ya kufungua vitasa vya chumba hicho kwa ustadi na kuingia ndani wakaaanza kufanya kilichowaleta.wanaume hao wawili wakaaanza kuweka camera pamoja na vinasa sauti kwa Siri kwenye sehemu sehemu mbali mbali chumbani maeneo ambayo sio rahisi kushtukiwa. Vinasa sauti viliwekwa ukutani kwenye maiki za simu ya mezani ,pamoja na kwenye Kona za kitanda ,jikoni ,maliwatoni n.k.

Pia kamera ndogo za Siri ziliwekwa kwenye taa za kila Kona ya chumba hicho ,baada ya hapo wakavaa mask usoni na kuanza kunyunyiza vumbi lenye mionzi kwenye nguo na viatu vilivyokuwa kabatini katika Hali ambayo isingeweza kushtukiwa na mlengwa wao. Hili vumbi lingewasaidia ku track movements za huyo mlengwa wao popote aendapo kwa kutumia kifaa kilichojulikana kama Geiger counte. Baada ya kumaliza kilichowaleta wakaurudishia mlango na kuufunga kama walivyoukuta na wakatokomea.

Masaa machache baadaye ,afisa wa ngazi za juu wa KGB alishuka kwenye uwanja wa ndege wa Moscow na shirika la ndege la Aeroflot akitokea London. Kanali Oleg antonyevich Gordievsky alikuwa katika kilele Cha mafaniko ya kazi Yake katika idara ya KGB. Mpaka kufika kuwa afisa wa ngazi za juu kwenye shirika Hilo alipitia vyeo mbalimbali ,amefanya kazi kama balozi kwenye nchi za Scandinavia, uingereza pamoja na hapo Moscow.

Akiwa na miaka 46 aliteuliwa kuwa mwakilishi wa KGB kwenye ubalozi wa USSR hapo London. Kwa kuwa alikuwa jasusi mbobevu alipanda vyeo kwa haraka ndani ya idara kiasi kwamba akawa na uwezo wa kujua Siri nyingi za kijasusi (Disclassfied material) pamoja na mtandao wa kijasusi kwenye mataifa mbalimbali ikiwemo mataifa ya magharibi.

Mwenye muonekano wa mwili wa mazoezi,akiwa hana hofu Wala wasiwasi huku akitabasamu alikatiza katikati ya umati wa watu hapo uwanja wa ndege kwa ajili ya kutafuta teksi imuondoe hapo impeleke anapoishi.
Bwana Oleg afisa wa kijasusi mtiifu wa shirika la KGB aliyependwa na mabosi wake kama asset muhimu waliokuwa nayo kipindi hicho ,pia alikuwa ni JASUSI MTIIFU WA UINGEREZA. Kwa kifupi alikuwa ni double agent.

Akiwa afisa wa KGB tayari alikuwa ni mwajiriwa rasmi wa shirika la kijasusi la uingereza la MI6 kwa miaka takribani 12 .na alipewa jina jina la uficho (codename) la NOCTON.

Na baadaye ikaja semekana alikuwa ndiye JASUSI wa thamani sana enzi zile za vita baridi. Taarifa za Siri alizokuwa anazivujisha kutoka KGB na mipango ya Siri ya USSR zilibadilisha kabisa mkondo wa vita baridi kwa wakati ule. Bwana Oleg aliweza kutoboa Siri ikiwemo mikakati ya nyuklia za USSR..mtandao wa majasusi uliokuwa kwenye nchi za magharibi,pamoja na sera za nje za urusi kwa wakati huo kwa wakubwa wa MI6.

Taarifa alizokuwa anazivujisha bwana Oleg ziliwafanya MI6 na CIA ku share kwa pamoja baadhi ya taarifa, lakini ajabu ni kwamba DG na top officials wa MI6 hawakutaka kutoa identity ya Oleg kwa Margaret thatcher Wala Ronald Reagan waliemwajiri ndani ya Kremlin kwa maaana ya USSR kwa kuwapa sensitive Disclassfied informations. Na kulikuwa na sababu maalumu ya kufanya hivyo.
Pia mkewe bwana oleg hakuwahi kujua mumewe ni spy wa uingereza.

Lakini imekuwaje amekuja ghafla Moscow kwa kuitwa na wakubwa zake? . yaani ni kwa mfano balozi polepole kateuliwa balozi Tz Cuba, lakini ghafla hajamaliza hata miezi mitatu anaitwa nyumbani ghafla ,lazima hata kama ni wewe utajiuliza tu.

Lakini wanasema JASUSI ni jasusi tu . bwana Oleg aliweza kunusa hatari iliyokuwa mbele Yake ,akiwa anakatiza katikati ya watu hapo uwanja wa ndege baada ya kutua ndani ya nafsi yake alihisi upweke uliochanganyika na mashaka . Baada ya kukaguliwa nyaraka zake na hati ya kusafiria na wale maafisa wa passport uwanjani hapo alikabidhiwa akaagwa akaondoka.

Kikawaida kwa wakati huo afisa yoyote hususani mwakilishi akitokea nje ya nchi lazima kunakuwa na courtesy ya maafisa wenzake kuja kumpokea mwenzao airport lakini haikuwa hivyo. Akiwa anaangaza huku na kule asione dalili yoyote ya mapokezi alinotice jambo lisilo la kawaida, kulikuwa na wanaume na wanawake wamesimama hapa na pale uwanjani hapo pasipo jambo la muhimu waliokuwa walikilifanya zaidi ya kushangaa huku na huko.

Lakini bwana huyu akiwa ndani ya teksi alijiambia ikiwa KGB wanajua ukweli kumhusu yeye muda huo angekuwa tayari amewekwa chini ya ulinzi muda huo punde alipokanyaga ardhi ya Russia,aburuzwe Hadi kwenye cell za KGB ahojiwe,ateswe mwisho wa siku auliwe kwa kupigwa risasi ya kichwani .

Mpaka anaingia kwenye teksi Hadi kufika yalipo makazi yake mtaa wa Leninsky prospekt hakuwa anafuatiliwa kwa namna yoyote ile.alikwea lift Hadi ghorofa ya nane kwenye jumba Hilo kitasa Cha kwanza Cha mlango wake kilifunguka na Cha pili vilevile lakini kitasa Cha tatu Cha mlango kilikuwa locked bwana Oleg hakuwahi tumia kitasa Cha tatu kwa kuwa hakuwa na funguo zake, lakini ajabu ni kwamba alikuta kitasa kimefungwa na hapo hapo akahisi Kuna watu waliingia na kutoka wakajisahau wakafunga Hadi kitasa Cha tatu. Alikuwa sahihi . Alikuwa anatiliwa wasiwasi. The spy was being spied upon by his fellow spies.
Du kumbe ni tamthlia nilifikiri ni tukio la kweli. Basi wapenzi wa izi vitu endeleeni kuenjoy.
 
Kwa mbaaalii naanza kuona na kuamini hii stori ya Oleg Gordievsky kuwekwa humu j.f . Imewauma baadhi ya watu Hadi huko Twitter . Kwani Kuna ubaya gani niliofanya ku share hii stori na waungwana humu ? . Hii ni user generated forum mtu anaandika na ku share anachoona kinafaa na Mimi nikaona ni vyema ku share lengo ni kuburidika na kuelimika kwa pamoja . Wengine wananiponda huko inbox kwamba ni najifanya mjuaji n.k. wengine wanasema kwamba ni acknowledge source sijui nimeitoa wapi hii story..nani kasema sita acknowledge sources au mlihisi nimejitungia hii stori..
By the way business as usual siwezi acha kuendelea . Labda nipigwe ban.
Pole. I see itakuwa yule yule kenge anajaribu kuunda ile umbea wa kiswaz wa kukamulia ndimu kama alivyojiita
 
Daah...! Uko kama mimi tu. Unakuta baadhi ya picha zinafunguka,zingine zinagoma na bahati mbaya mimi mwenyewe naendelea kuvumilia tu,itakayokubali sawa,ikigoma sawa. Browser pia mimi imenishinda. Nilijua niko peke yangu. Kumbe ni kilo cha wengi. Sijajua kwa nini JF wanarudi nyuma badala kwenda na wakati?. Siku hizi wamekuwa kama ccm tu
Mkuu
Reset factory settings kisha ishi nayo
 
Kesi ya Sergei skripal

Tangu zamani za mwanafalsafa sun tzu , Ili uweze kushinda vita dhidi ya mpinzani wako ,ilipaswa kupata taarifa za Siri kumhusu huyo mpinzani. Taarifa hizi muda mwingine zinaweza kukupa insight kuhusiana na madhaifu ya mpinzani wako . Na kikawaida ukishajua madhaifu ya mpinzani wako basi utatumia udhahifu huo huo kumpiga na kumshinda . Hivyo hivyo kwa nchi mahasimu hufanya hivi katika kukusanya taarifa hizo za Siri. Ndipo linapokuja neno UJASUSI. Hivyo nchi huamua kutuma au kupandikiza watu maalumu kwa nchi Fulani Ili iweze kukusanya taarifa hizo za kijasusi lakini maisha Yao Huwa hatarini .

Tukija kwenye level ya kitaifa . Nchi huamua kukusanya taarifa za kijasusi dhidi ya nchi nyingine ,Ili kuweza kujua mipango yake na mikakati yake kwa lengo binafsi la nchi husika Ili iweze kujilinda na pia kunufaika kimaslahi.
Wakati wa vita baridi baina ya USA na USSR , nchi hizi zilikuwa zinajikita Zaidi katika kupata taarifa za siri dhidi ya mwenzake kutokana na shinikizo lililotokana na tishio la kutokea vita ya nyuklia. Hii ilianza punde tu baada ya kumalizika kwa vita kuu ya pili ya dunia .
Nchi hizi ziliamua kutumia mbinu mbalimbali walizoona Zinafaa katika kupata taarifa za kijasusi dhidi ya mwenzake . Mamlaka za serikali hususani bunge hutunga sheria Kwa ajili ya kuzipa ithibati organization za kijasusi Ili kukusanya taarifa hizo Kwa maslahi ya nchi au muda mwingine Kwa maslahi binafsi ya wanasiasa. Nchi ya uingereza kwa mfano ilianza hizi harakati za kukusanya taarifa za kijasusi au kiintelijensia kupitia shirika lake la kipindi hicho lililoitwa SIS Baadaye ikaitwa M16 tokea mwaka 1909. Lengo kuu lilikuwa kukusanya taarifa ambazo zingeisaidia kupunguza uwezekano wa nchi ya ujerumani kuvamia nchi za magharibi hususani washirika wa uingereza kijeshi. Vilevile USA iliamua kuanzisha harakati za ukusanyaji wa taarifa za kijasusi rasmi punde tu ilipoisha vita ya pili ya dunia . Kwa mfano bunge la congress wakati huo lilipitisha National security Act ya mwaka 1947 . Na sheria hii ilipopita likazaliwa shirika la kijasusi la CIA. Na pia Soviet waliunda shirika lao ukusanyaji taarifa za kijasusi lililoitwa Cheka punde tu baada ya mapinduzi ya mwaka 1917 ulioondoa utawala wa Czar. Mbali na hizi taasisi zilizoundwa kisheria katika kukusanya taarifa za kijasusi , ni kwamba muda mwingine hutumika kufanya mauaji kwa baadhi ya walengwa fulani fulani ambao huonekana ni tishio katika ulimwengu wa kijasusi au kwa nchi husika.
Walengwa Hawa Huwa ni waasi au double agent. Ni kwamba mtu huamua kuwa double agent kutokana na sababu fulani fulani ambazo muda mwingine huwa ni tamaa binafsi , shinikizo au mapenzi binafsi .....
Katika hili swala la uasi tunamwangalia bwana mmoja aliyeitwa Sergei skripal . Huyu alipewa sumu ambavo inasemekana ingepaswa kumuua taratibu yeye pamoja na bintiye anayeitwa Yulia kutokana na uasi .
Huyu Sergei skripal ni nani haswa?
Huyu bwana alizaliwa tarehe 23 June mwaka 1951 huko Soviet maeneo ya bahari ya Baltic . Alianza kuifanyia kazi shirika la kijasusi la jeshi la Russia lililoitwa GRU. Katika kutekeleza majukumu yake alitumwa kufanya kazi kwenye nchi ya Malta na baadaye uhispania. Lakini inasemekana kipindi cha utawala wa Boris Yeltsin , majasusi waliokuwa wanatumwa kufanya kazi za kijasusi nchi za nje hawakuwa wanapewa mkwanja kwa kipindi kirefu wakiwa Wanawajibika nje ya nchi . Huyu bwana akaamua kujiongeza na kutafuta fursa za kiuchumi ambazo zingemwezesha kuishi maisha aliyoyataka. Katika kutafuta fursa alijikuta anakutana na afisa mmoja wa M16 na akajitambulisha kama agent wa GRU. Sasa rasmi hapo akaamua kuwa double agent akiitumikia GRU shirika lililomwajiri na pia kuitumikia M16 ya uingereza kwa Siri kwa ajili ya kupata pesa . Kwa kifupi alikuwa anauza taarifa za nchi yake kwa nchi hasimu ya uingereza Alipewa jina la uficho la FORTWITH akiuza taarifa za kijasusi zenye thamani kubwa kwa uingereza. Lakini mwaka 2000 alijikuta Na changmoto ya afya hivyo ikamlazimu kurudi Russia kwa ajili ya matibabu na akakutwa na kisukari . Ilimlazimu kujiuzulu kama afisa wa GRU na kuamua kufanya kwenye ofisi ya serikali hususan kwenye maswala ya kiutawala lakini Shughuli za kijasusi aliendelea nazo kama kawaida. Na vilevile alikuwa bado yupo kwenye payroll ya M16 akipokea mkwanja kama kawaida . Lakini mwaka 2004 shirika la kijasusi la Russia la FSB lilimtimua kutokana na tuhuma dhidi yake za kuwa double agent na mwaka 2006 alikutwa na hatia mahakama ya kijeshi na kupigwa mvua ya miaka 13. Tuhuma dhidi yake ni kwamba alikuwa anawapa taarifa M16. Lakini kupitia msaada wa serikali ya marekani huyu bwana alisamehewa kupitia makubaliano maalumu ya kubadilishana wafungwa baina ya U.S.A na Russia na huyu bwana aliamua kwenda kuishi nchini uingereza kwenye mji mdogo wa Salisbury.
Huyu bwana aliamua kununua nyumba huko Salisbury na kuamua kuhamia yeye na mkewe liudmila pamoja na wanao wawili mwaka 2011.
Lakini ajabu ni kwamba mwaka 2012 alimpoteza mkewe na mwaka 2017 mwanae wa kiume Alexander nae alifariki. Aliyebaki ni mwanae wa kike ambaye Alikuwa anakuja kumtembelea mshua wake Mara kwa mara akitokea Russia. Kutokana na vifo vya wanafamilia Hawa WA kwake , aliamua kuishi maisha ya kawaida tu akiwa na paka wake mmoja kwa ajili ya kuondokana na upweke .
Mwaka 2018, mwaka mmoja tu tokea kifo Cha kijana wake huyu bwana skripal akiwa na bintiye walikutwa hawajitambui wamepoteza fahamu eneo la hifadhi la Salisbury Park. Ripoti za kiuchunguzi za awali kutoka vyombo vya usalama na habari zilitabanaisha na kusema shambulio Hilo lilikuwa ni jaribio ya mauaji dhidi ya huyu bwana na huenda pia hata mkewe na mwanae ilikuwa ni mauaji ya kupanga. Baada ya kupelekwa hospitali , bwana skripal na mwanae walikuwa hawajitambui kwa wiki kadhaa pasipo kujulikana sababu ni Nini zilizopelekea Hali hiyo kwa mujibu wa ripoti za kitabibu. Lakini baada ya kupata nafuu waliruhusiwa kutoka hospitali tarehe 9 April 2018. Kutokana na huyu bwana kuwa na hadhi yake , mamlaka za serikali ya uingereza ziliamua kufanya uchunguzi wa kina kuhusiana na tukio hili . Taarifa zilitoka na kudhibitisha bwana huyu na bintiye walipewa sumu iliyoitwa nerve agent ambayo pia baadaye Theresa May waziri mkuu wa uingereza wakati huo aliithibitisha bungeni kuwa ni sumu aina ya Novichok (A-234) .
The organization for the Prohibition of chemical weapons (OCPW) ni Taasisi iliyokuwa inahusika na udhibiti wa matumizi ya silaha za kemikali ziliamua kufanyia kazi hili swala na kutaka kujua chanzo Cha hii sumu ilifikaje hapo uingereza. Kupitia maabara ya
Defence science and technology laboratory(DSTL) sample zilichukukuliwa na ripoti ikathibitisha ni sumu ya Novichok with high purity na ilikuwa kwa wingi eneo la mlangoni kwenye nyumba ya skripal.
Kwa mujibu wa mshauri wa maswala ya ya kiusalama ya kitaifa bwana mark sedwil alisema kwamba kupitia uchunguzi uliofanywa na DSTL ,sumu hii ilikuwa kwa wingi kwenye eneo la kitasa Cha mlango wa mbele wa nyumba ya skripal. Na sumu hii ilikuwa katika Hali ya umajimaji . Hivyo huyu bwana akasema sumu hii hutumiwa na Russia na hivyo wao wanahusika Moja kwa Moja na tukio la majaribio la kumuua bwana skripal. Lakini kama kawaida Russia wakakanusha madai haya na kusema ni propaganda dhidi yao ya kutaka kuzorotesha mahusiano ya kidiplomasia.
Ripoti Zaidi kuhusiana na hili tukio la jaribio la mauaji dhidi ya skripal ilisema kwamba hata eneo walilokuwa skripal na bintiye mara ya mwisho kabla ya kukutwa na hii dhahama kulikuwa na kiwango kikubwa Cha sumu hii. Hivyo Ili kuzuia watu kuwa exposed na hii sumu serikali iliamua kuizingira nyumba hiyo na viwanja vya karibu na eneo Hilo kwa utepe wa crime scene Ili kufanya uchunguzi zaidi. Shirika la bbc lilisema serikali ilituma maafisa 250 wa kitengo Cha kupambana na ugaidi na maafisa wa kijeshi 180 katika kulizingira eneo Hilo kwa ajili ya uchunguzi wa kina.
Maafisa uchunguzi walianza kuchunguza kuanzia nyumba ya skripal,gari yake maeneo walikopita, mgahawa walioenda kula, Hadi kwenye benchi walikokuwa wamekaa na kukutwa wamepoteza fahamu akiwa bintiye.
Kulikuwa na mkanganyiko kuhusiana na chanzo Cha hii sumu ilikotoka mpaka kufika uingereza. Kwa mfano vyombo vya habari vilisema huenda sumu hii ilichanganywa kwenye baadhi ya vitu vya Yulia skripal alivyoondoka navyo Moscow kuja uingereza. Taarifa za vyombo vya habari vya U.S vikadai huenda sumu hii iliwekwa kwa Siri kwenye gari ya skripal.
Lakini kwa mujibu ya mwanahistoria katika maswala ya kiintelijensia anayeitwa Boris volodarsky alisema kupitia chapisho lake la mtandaoni la "the poison war"
Kwamba huenda sumu hii ilifika eneo Hilo alilokuwa akiishi skripal kupitia technical timu ya majasusi na kufanya Yao huku mlengwa akiwa ni skripal.
Hivyo serikali ya uingereza ikafanya jitihada zote za kujua walengwa waliofanya hili tukio ni kina nani .
Na kweli mamlaka za shirika la kijasusi la uingereza likiwasuspect Raia wawili wa Russia ambao ni Alexander Petrov na Ruslan boshirov ambao pia walihusishwa kuwa ni maagent wa GRU. Walituhumiwa katika kufanya jaribio la mauaji dhidi ya skripal. Kwa mujibu wa ripoti za kiutafiti kuhusiana na hili swala huyu Alexander Petrov jina lake halisi alitambulika kama Alexander mishkin ambaye alikuwa ni daktari na Ruslan boshirov alitambulika rasmi kama kanali Anatoliy chepiga na wote walikuwa wanafanyia Kazi shirika la kijasusi la Russia tokea 2010. Kwa mujibu wa ushahidi uliopatikana nchini uingereza inasemekana huyu Chepiga alikuwa akijihusisha na operesheni za Siri muda mrefu na inawezekana yeye ndio aliyefanya tukio hili la kujaribu kutaka kumuua huyu skripal kwa sumu ya Novichok. Na inasemwa operesheni hii ilitolewa order kutoka kwenye mamlaka ya juu kabisa ya Russia.kremlin office.
Mamlaka za uingereza zilituma ombi la kuwakamata watu hawa na kuletwa uingereza kwa ajili ya kuja kujibu tuhuma dhidi yao. Na ilisema tukio hili ni kinyume na UN charter kutokana na matumizi ya nguvu kudhuru na ilitaka majibu ya kisheria kutokana na tukio hili kutoka kwa Russia.
Russia kama kawaida Yao wakakaza.
Sumu hii ya Novichok kwa mujibu wa ripoti za OCPW inasemwa ni miongoni mwa sumu zilizokuwa zinatengenezwa huko Russia miaka ya 1980s kipindi hicho Cha vita baridi. Na inasemekana ni sumu inayoathiri mfumo wa ufahamu mwilini na huweza kupenya kupitia ngozi . Na ikianza kufanya reaction mwilini inapelekea mfumo wa upumuaji kushindwa kufanya kazi na kupelekea kupoteza fahamu.
Sumu hii mara ya kwanza ilianza kutengenezwa huko ujerumani kipindi cha vita ya pili ya dunia, baadaye Russia ikachukua formula yake na kuanza kuitengeneza miaka hiyo ya 1980.
Bwana skripal na bintiye baada ya kuruhusiwa kutoka hospitali ,Sasa wanahifadhiwa kwa Siri kwenye eneo mojawapo ndani ya uingereza chini ya ulinzi mkali japo bado maisha Yao yapo hatarini.
Kutokana na Russia kukataa kuwakabidhi washukiwa kwenye mamlaka za uingereza kwa ajili ya kujibu tuhuma, serikali ya nchi hiyo pamoja na U.S iliamua kuwatimua maafisa wa Russia kwenye nchi hizo kutokana na hili sakata. Huku Russia iliendelea kukanusha.

Tukirudi nyuma kutokana na hili swala la ukusanyaji taarifa za kijasusi kwa nchi Moja dhidi ya nyingine , ni kwamba Hawa maagent wanaoenda field hukutana na dhahama nyingi sana ikiwemo kuuliwa .
Kwa mfano skripal , changamoto yake ya kukosa pesa akiwa field katika kukusanya taarifa za kijasusi kwa ajili ya nchi yake , ikabidi kuuza taarifa kwa nchi hasimu . Ilimgharimu uhai wa Memba wa familia yake na yeye almanusura kuuliwa .
Hivyo naweza kusema maagent huhatarisha maisha Yao pamoja na wale wapendwa wao kwa maslahi ya usalama wa nchi, na vilevile maslahi ya WANASIASA waliopo madarakani.



skynews-sergei-skripal-yulia-skripal_4365630.jpg

Sergei na bintiye Yulia skripal




Skripal_Russia_poison_AP18282305332603-300x213.jpg

Watuhumiwa wanaoshutumiwa kwenye mpango wa kumuua bwana Sergei na bintiye Yulia kwa sumu ya Novichok


UJASUSI SIO KAZI YA KILA MTU KUWEZA KUIFANYA , LINAPOKUJA SWALA LA MASLAHI YA TAIFA


Credit : google
 
Back
Top Bottom