Tarehe 9-12-1961 ilikukuta wapi?

Tarehe 9-12-1961 ilikukuta wapi?

Heri ya siku ya uhuru wadau.

Nikikumbuka siku ya tarehe 09/12/1961 naona ni kama juzi tu kumbe ni miaka kibao imepita.

Nakumbuka siku hiyo tulivyochinja mbuzi nyumbani kusherekea uhuru, nakumbuka mvua kubwa ilivyonyesha mpaka kusababisha maji kujaa ziwa Victoria kupita kingo zake.

Kweli wakati ni ukuta.

Mkuu unakumbuka nini siku hii?
Shikamoo bro mkubwa?
 
Heri ya siku ya uhuru wadau.

Nikikumbuka siku ya tarehe 09/12/1961 naona ni kama juzi tu kumbe ni miaka kibao imepita.

Nakumbuka siku hiyo tulivyochinja mbuzi nyumbani kusherekea uhuru, nakumbuka mvua kubwa ilivyonyesha mpaka kusababisha maji kujaa ziwa Victoria kupita kingo zake.

Kweli wakati ni ukuta.

Mkuu unakumbuka nini siku hii?
Kuna mtu aliwahi kusema...wajinga nao huzeeka
 
Hata ningekuwa nakufahamu kwa jina halisi siwezi kukuchukia. Ila ulimbukeni na uongo uache


Have a fabulous weekend!!
Hamna shida mkuu
I never lie in my words
Ila shikilia hapo hapo huenda ipo siku tutaongea kwa heshima zaidi
Thanks for that
Umenishambulia bila kosa lolote na bado unaniita muongo sasa huo ukweli uanike hapa
Hata kama nipo huko ningesema tu niko mahali flani maana hakuna anaenitafuta
Be happy
 
Nilikuwa duniani, ila sikumbuki hilo tukio maana unajua tena waswahili kila leo ni sherehe wala hujui nini kinaendelea

Sherehe tangu uhuru mpaka leo ndio maana hata maendeleo ni zero
Niliona ni ujinga kuishi huko nikasepa baada ya kuona maduka ya ushirika ya Nyerere wameanza kuuza ngano unalazimishwa na sabuni
Ila miaka 10 ya kwanza ya Uhuru tulikuwa bado tuna mentality za kizungu maana watu walikuwa wanajielewa sana na akili kibao
Baba alikuwa mfanyabiashara na supplier mkubwa kwa wazungu, Gari lake lilikuwa Land Rover nakumbuka mwaka 1967 alinunua ila kulikuwa na wakulima wawili pia walikuwa na Peugeot kabla ya mzee hao walikuwa nazo kabla ya Uhuru

Maisha zamani yalikuwa matamu asikuambie mtu yaani mswahili tajiri tena anatamba na Gari?
Hapo ndio wenye roho ya korosho wakaingia madarakani na kuona wao waanze nao badala ya kuwahamasisha waendeleze biashara zao
Mahasidi wametufanya hivi ila poleni sana
Hakukua na smartphone, intaneti, computer , magari mazuri, miundombinu mizuri. Huo utamu uliletwa na nini au unaongea according to you.
 
Miaka 60 za uhuru ila bado tuko vile vile kila kitu loh Nyerere kauua hi nchi.
Nyerere kaondoka madarakani mwaka 85, aliongiza nchi kwa kutegemea kilimo, mifugo na viwanda. Hakuchimba madini ukiondoa Alma's na Tanzanite, Wala hakuchimba gesi pamoja na kwamba akijua uwepo wake. Aliuaje uchumi wa Tanzania, uchawa wenu ndio umeua nchi.
 
Hamna shida mkuu
I never lie in my words
Ila shikilia hapo hapo huenda ipo siku tutaongea kwa heshima zaidi
Thanks for that
Umenishambulia bila kosa lolote na bado unaniita muongo sasa huo ukweli uanike hapa
Hata kama nipo huko ningesema tu niko mahali flani maana hakuna anaenitafuta
Be happy

Mimi nimemaliza Mkuu.
 
Heri ya siku ya uhuru wadau.

Nikikumbuka siku ya tarehe 09/12/1961 naona ni kama juzi tu kumbe ni miaka kibao imepita.

Nakumbuka siku hiyo tulivyochinja mbuzi nyumbani kusherekea uhuru, nakumbuka mvua kubwa ilivyonyesha mpaka kusababisha maji kujaa ziwa Victoria kupita kingo zake.

Kweli wakati ni ukuta.

Mkuu unakumbuka nini siku hii?
Nilikuwa sijazaliwa Ila Kuna kipindi mvua ilinyesha Bibi yangu akaniambia mvua Kama hii ilinyesha wakati wa Uhuru.
 
Kipindi hicho nilikua kama sekretarieti wa anga za juu huko nakumbuka nimekaa zangu ofisini nikaitwa nipeleke barua adress ya baba wa taifa

Nikaona hii barua mbona huyu mu white man kanipa kwa masikitiko makubwa hivi njiani nikapaki mandolin nikachungulia

Kumbe ilikua mikeka ya betpawa minne
Mmoja wa moja kwa moja mwingine wa double chance sijui kwanini alinipa kwa huzuni vile inawezekana ilichanika hakucash aut😂😂😂
 
Heri ya siku ya uhuru wadau.

Nikikumbuka siku ya tarehe 09/12/1961 naona ni kama juzi tu kumbe ni miaka kibao imepita.

Nakumbuka siku hiyo tulivyochinja mbuzi nyumbani kusherekea uhuru, nakumbuka mvua kubwa ilivyonyesha mpaka kusababisha maji kujaa ziwa Victoria kupita kingo zake.

Kweli wakati ni ukuta.

Mkuu unakumbuka nini siku hii?
Tarehe hiyo baba yangu alikuwa bize na mishemishe za elimu ili aje kuchomoza maishani.

Mie nilikuwa bado mbinguni
 
Unapayuka tu nikikwambia uniambie mode of function ya hicho kifaa unajua au unabwabwaja?..au ndo akili yako ilipoishia?

Bila shaka lugha hujui ulipata D au F.

Maarifa madogo!!
Nimekuuliza jambo dogo kijana unaanza matusi.Ndiyo kwenye familia yenu mnavyotukana namna hiyo.Una A+ ya weledi wa matukano.
 
Hakukua na smartphone, intaneti, computer , magari mazuri, miundombinu mizuri. Huo utamu uliletwa na nini au unaongea according to you.
Mkuu kweli barua ilikuwa ukiandika na kupeleka posta itachukua hata mwezi kumfikia uliemuandikia ila Habari za vifo tulikuwa tunapata haraka sana kwa njia ya simu ya upepo telegraphy ambapo anakuja postman na kuwataarifu msiba
Kulikuwa na magari mkuu ila kwa wakati huo yalikuwa yanatamba na kukufikisha unapotaka pia kulikuwa na reli pia
Yalikuwa mazuri kwa wakati huo maana hata population ilikuwa ndogo
 
Nimekuuliza jambo dogo kijana unaanza matusi.Ndiyo kwenye familia yenu mnavyotukana namna hiyo.Una A+ ya weledi wa matukano.

Wala sijakutusi, ila ni wewe kujipa umaamuma kwa jambo ambalo ni obvious sasa hapo carbon 14 dating inakuja vipi kwamba wewe ulishindwa kuelewa kile ambacho namaanisha ?

Ile ni lugha tu kama kiswahili kilikupiga chenga hasa isimu ya lugha basi sina msaada kwa kweli.
 
Heri ya siku ya uhuru wadau.

Nikikumbuka siku ya tarehe 09/12/1961 naona ni kama juzi tu kumbe ni miaka kibao imepita.

Nakumbuka siku hiyo tulivyochinja mbuzi nyumbani kusherekea uhuru, nakumbuka mvua kubwa ilivyonyesha mpaka kusababisha maji kujaa ziwa Victoria kupita kingo zake.

Kweli wakati ni ukuta.

Mkuu unakumbuka nini siku hii?
Walichinja kuku home nikaenda kucheza narudi nakutana na mguu wa kuku
 
Back
Top Bottom