Tarime: Mbunge aamua kupambana na Corona kwa vitendo, asambaza Sanitizer na vifaa vya kunawia Jimbo zima

Tarime: Mbunge aamua kupambana na Corona kwa vitendo, asambaza Sanitizer na vifaa vya kunawia Jimbo zima

Kuna mbunge wa upinzani aliwahi kukamatwa kwa kwenda kutoa msaada shuleni kisa hakuwa na kibali!Pia kule kagera kipindi cha tetemeko viongozi wa upinzani walizuiwa kwenda kutoa misaada!Ndio maana nikauliza kama hakukamatwa huyu mbunge!
Kama kweli kuna misaada kama hiyo iliyokataliwa kwa sababu tu msaada ulikuwa unatolewa na upinzani, hilo ni kosa linalobidi kukemewa. Kwa upande mwingine nilisikia wakati fulani mtu wa upinzani alitaka kutoa madawati kwenye kata fulani (sikumbuki wapi) serikali ikamkataza. Kilichokuja kugundulika ni kwamba madawati yaliyokataliwa yalikuwa hayakidhi kabisa kiwango kinachohitajika. Mtu huyo alitaka kiki ya kisiasa tu akaitangazia nchi na kuita waandishi wa habari waone 'msaada' anaotoa. Ni halali kwa Serikali kukataa misaada kama hiyo.
 
Kama kweli kuna misaada kama hiyo iliyokataliwa kwa sababu tu msaada ulikuwa unatolewa na upinzani, hilo ni kosa linalobidi kukemewa. Kwa upande mwingine nilisikia wakati fulani mtu wa upinzani alitaka kutoa madawati kwenye kata fulani (sikumbuki wapi) serikali ikamkataza. Kilichokuja kugundulika ni kwamba madawati yaliyokataliwa yalikuwa hayakidhi kabisa kiwango kinachohitajika. Mtu huyo alitaka kiki ya kisiasa tu akaitangazia nchi na kuita waandishi wa habari waone 'msaada' anaotoa. Ni halali kwa Serikali kukataa misaada kama hiyo.
Yaani dawati liwe chini ya kiwango kuliko jiwe analokalia mtoto?Huwezi kuwa serious
 
Heche wazo zuri lakini tatizo jina ila iko powa naziona hapa sirari na nyamongo tu kwa maana ya tarime vijijini
 
Huwezi kufanya hivyo kila siku,pesa anatoa wapi?Halafu mnataka wasiikosoe serikali,yaani kila kitu iwe sawa na wao wajikite kuhudumia wanamchi kwa fedha zao,hakuna siasa za hivyo duniani!
Tz kiujumla ujinga ni mkubwa kuliko tatizo lolote lile, na ndiyo maana imani yetu kubwa iko kwa serikali iloliyoko madarakani, imepelekea hata wawakilishi wetu majimboni wakihoji na kukosoa wakadhalilishwa wananchi tunaona sawa tu, yaani kiujumla matz hayajui maana siasa ya vyama vingi na hatujui kwanini vyama hivyo vipo
 
Tz kiujumla ujinga ni mkubwa kuliko tatizo lolote lile, na ndiyo maana imani yetu kubwa iko kwa serikali iloliyoko madarakani, imepelekea hata wawakilishi wetu majimboni wakihoji na kukosoa wakadhalilishwa wananchi tunaona sawa tu, yaani kiujumla matz hayajui maana siasa ya vyama vingi na hatujui kwanini vyama hivyo vipo
Kabisa,hatujiulizi kwanini nchi nyingi zimechagua mfumo wa vyama vingi na msingi wake ni nini!Tungelijua hilo nadhani mambo mengi yangebadilika sana!Sasa kama watu wanafikiri vyama vya upinzani ni sawa na Corona na kwamba vitokomezwe,hapo unapata picha ya ukubwa wa tatizo la uelewa hadi kwa viongozi!

Kumbe ndio wewe mkuu unayenishambulia sana kule MMU!😅😅😅😅😅
 
Tz kiujumla ujinga ni mkubwa kuliko tatizo lolote lile, na ndiyo maana imani yetu kubwa iko kwa serikali iloliyoko madarakani, imepelekea hata wawakilishi wetu majimboni wakihoji na kukosoa wakadhalilishwa wananchi tunaona sawa tu, yaani kiujumla matz hayajui maana siasa ya vyama vingi na hatujui kwanini vyama hivyo vipo
Wewe ni mzungu siyo? Ndiyo maana hata DM umeweka picha ya mzungu (Nguruwe) umekuwa brainwashed na hao wazungu au hujawahi kuishi kwao hao mabwana zako wazungu.
 
Back
Top Bottom