Task TRA force Bado wananyanyasa watu, wavamia Bar ya Mpo Africa wabeba kreti za bia Usiku huu

Task TRA force Bado wananyanyasa watu, wavamia Bar ya Mpo Africa wabeba kreti za bia Usiku huu

Prof Koboko

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2020
Posts
350
Reaction score
2,550
Nchi hii sijui imelaaniwa wapi, ni juzi tu Rais wetu mpendwa Mama Samia aliwaonya Task forces TRA waache kutumia nguvu kudai kodi lakini usiku huu wamevamia Mpo Afrika bar iliyopo Temeke na kubeba crates za bia wakiwa wameambatana na polisi wengi wenye silaha.Hivi unapomvamia biashara ya mtu usiku huu na kubeba vitu vyake, kesho analipaje kodi?

Unashindwa nini kumwandikia mmiliki wa Bar barua kesho aje ofisini kumweleza tatizo lake ili ajue? Kuvamia biashara yake usiku wa manane na kuchukua bidhaa zake ndio utatuzi wa tatizo?

Mama Samia Rais wangu ulisemahutaki kodi ya dhuluma, hawa wametumwa na nani huyo asiyekusikia Mama?
Meneja wa TRA mkoa wa kodi wa Temeke na Kamishna mkuu wanatakiwa kufukuzwa kazi, huu tunahesabia kama uporaji wa mali za watu.
 
Unashindwa nini kumwandikia mmiliki wa Bar barua kesho aje ofisini kumweleza tatizo lake ili ajue? Kuvamia biashara yake usiku wa manane na kuchukua bidhaa zake ndio utatuzi wa tatizo?
Umejuaje kwamba hawajachukua hizo hatua za mwanzo ulizozitaja?

Umewasiliana nao tra ili kupata taarifa toka kwao?

Kama huyo mfanyabiashara anajua ana tatizo la kodi, kwa nini hajaenda huko tra kuwaeleza kinachoendelea kwenye biashara yake ili kwa pamoja wapange utaratibu mzuri wa kulipa kodi pole pole?

Kwenye nchi za dunia ya tatu ni wafanyabiashara wachache sana walio tayari kulipa KODI HALALI bila kulazimishwa.
 
Huo muda wa kukesha Bar hadi usiku wa manane mnautoa wapi? Tunapitia wakati mgumu kiuchumi kama nchi mmebaki kuendekeza anasa. Sasa hivi mlitakiwa muwe vitandani mnalala ili mudamke mapema asubuhi kazini vibaruani huko.

Safi sana TRA!
 
Umejuaje kwamba hawajachukua hizo hatua za mwanzo ulizozitaja?
Umewasiliana nao tra ili kupata taarifa toka kwao?..
Sasa ndiyo wavamie biashara na kubeba Makreti ya Bia usiku Wa manane?

Kama wamepitia hatua zote za mwanzo basi hatua sahihi ilipaswa waende na Kofuli lao kisha waifunge Baa na siyo kufanya uporaji Wa Mali za mwenye Baa..
 
Sasa ndiyo wavamie biashara na kubeba Makreti ya Bia usiku Wa manane?

Kama wamepitia hatua zote za mwanzo basi hatua sahihi ilipaswa waende na Kofuli lao kisha waifunge Baa na siyo kufanya uporaji Wa Mali za mwenye Baa..
Hao Ni majambazi sio TRA
 
Huo muda wa kukesha Bar hadi usiku wa manane mnautoa wapi? Tunapitia wakati mgumu kiuchumi kama nchi mmebaki kuendekeza anasa. Sasa hivi mlitakiwa muwe vitandani mnalala ili mudamke mapema asubuhi kazini vibaruani huko.

Safi sana TRA!
Night club
 
Mkuu Prof Koboko , kwanza asante kwa taarifa hii, itamfikia mhusika, ila vitu vingine ni kuelimishana tu, TRA Task Force haifanyi kazi usiku wa manane!, ukiona polisi wamevamia mahali usiku wa manane , ujue wana taarifa za kiinteligensia kuhusu uwepo wa mali za wizi, hivyo polisi wamefanya ambush na kuzikamata usiku huo huo na kuhifadhi ushahidi, wangesubiri hadi asubuhi, wangekuta manyoya!.

Hivyo tusubiri taarifa rasmi ya jeshi la polisi kuhusu tukio hilo.
P
 
Huo muda wa kukesha Bar hadi usiku wa manane mnautoa wapi? Tunapitia wakati mgumu kiuchumi kama nchi mmebaki kuendekeza anasa. Sasa hivi mlitakiwa muwe vitandani mnalala ili mudamke mapema asubuhi kazini vibaruani huko.

Safi sana TRA!
Upoyoyo unakusumbua.
Biashara ya bar ni kazi halali na pengine inaajiri dada zako

Sent from my G80 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu Prof Koboko , kwanza asante kwa taarifa hii, itamfikia mhusika, ila vitu vingine ni kuelimishana tu, TRA Task Force haifanyi kazi usiku wa manane!, ukiona polisi wamevamia mahali usiku wa manane , ujue wana taarifa za kiinteligensia kuhusu uwepo wa mali za wizi, hivyo polisi wamefanya ambush na kuzikamata usiku huo huo na kuhifadhi ushahidi, wangesubiri hadi asubuhi, wangekuta manyoya!.

Hivyo tusubiri taarifa rasmi ya jeshi la polisi kuhusu tukio hilo.
P
Ni kweli kabisa...
 
Back
Top Bottom