tathmini ya matokeo mapya ya form 4

ufaulu O-level unashuka wakati ufaulu A-level unapanda....sielewiiii....
 
Mkuu bado sielwi,mbona dogo alikuwa na 4 ya 28,sshv ana zero?

Nimeshituka aisee niliposoma comment yako maana walichosema hawaendi kusahihisha upya bali wanachofanya ni kurekebisha grade na kutumia zilizotumika mwaka jana hivyo ningetarajia mtu either matokeo yake yangebaki vilevile au kidogo kungekuwa na changes, sasa kwa huyu mbona ni msiba na kinachotakiwa hapo ikiwezekana ni ku-appeal maana wanaofanya hii kazi ni wanadamu hivyo kukosea inawezekana lakini pia si vibaya kujiridhisha
 

Kaka asante kwa maelekezo. Sasa mbona kuna kijana jirani yangu alikuwa na Div 4 point 28 sasa hivi kapata Div 4 ya point 33 ? Nadhani kuna somo alikuwa na D sasa hivi ni F? Pathetic!
 
Kaka asante kwa maelekezo. Sasa mbona kuna kijana jirani yangu alikuwa na Div 4 point 28 sasa hivi kapata Div 4 ya point 33 ? Nadhani kuna somo alikuwa na D sasa hivi ni F? Pathetic!

Ila hata mie hapa inashangaza kweli maana kwa logic ya haraka haraka na kwa maelezo waliyoyatoa wakati wanafanya hili zoezi moja kwa moja utaona kuna mawili either Div na point inabaki vilevile au inaongezeka na si kushuka maana kama ingekuwa wametumia grade za zamani yaani D ni 21 alafu ikaonekana kwamba walikosea walitakiwa watumie D kuanzia 30 hapa ndio tungesema kwamba kuna ambao wangeshuka tena na zero zingeongezeka, cha kufanya hapo ni ku-appeal ili kujua tatizo ni wapi maana waliofanya hili zoezi ni binadamu na huenda kukawa na tatizo la ku-insert formula kama kipindi kile walivyofanya kosa dogo la Islamic knowledge ambalo lilileta shida kidogo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…