Tathmini yangu fupi ya utendaji wa Marais wetu; Inaonesha Mkapa alikuwa Rais wa daraja la juu sana

TRA wenyewe wanaaema wameanzishwa 1995,unadhani ilianzishwa ili isifanye kazi!?
 
Wewe jamaa una chuki flani mpaka unaonekana mpumbavu
 
TRA kaanzisha mwinyi,31/7/1995
His predecessor, President Mwinyi, had already taken the initial steps by setting up the Presidential Commission of Enquiry into Public Revenues in 1991; which had recommended the establishment of the Tanzania Revenue Authority (TRA). This was established, and commenced full operations in July 1996, after President Mkapa had taken office. Dailynews.

Uko sahihi mkuu.
 
Ilikua rasmi 31/7/1995,ni matokeo ya SAP
 
Ilikua rasmi 31/7/1995,ni matokeo ya SAP
Kweli kabisa mkuu,

Structural Adjustment Programme SAP ya taasisi za Breton Wood (Wakwe zetu). SAP imeondoa serikali nyingi Ikulu barani Afrika hasa baada ya kuhatamia Multipartism. Afrika ni daraja la kuvusha matajiri na kutosa majini maskini.

Poor people walk distance in search for food to eat rich people walk distance to digest the food.
 
Mzungu anaogopa mwafrika akiwa huru mosi atakosa malighafi,pili afrika itakua dola kubwa kwa kuwa Ina rasilimali nyingi,unaona China leo anakula nao meza moja,kisa rasilimali
 
Kwahiyo iundwe taasisi ya Madawati
Baadae iundwe taasisi ya Madarasa
Hatimae iundwe taasisi ya Upungufu wa Chaki
Sasa mkuu baadae itaundwa taasisi ya taasisi zilizoundwa
bafae taasisi ya mall za serikali
 
Mzungu anaogopa mwafrika akiwa huru mosi atakosa malighafi,pili afrika itakua dola kubwa kwa kuwa Ina rasilimali nyingi,unaona China leo anakula nao meza moja,kisa rasilimali
Mkuu,
Hiyo ni empirical fact umetoa. Afrika pekee ina nusu ya rasilimali zote za dunia. Tusipojipanga, hawa watu watatutawala milele. Wakati fulani najaribiwa kutamani uongozi wa kizazi cha kwanza cha Afrika baada ya uhuru maana hawa walimng'oa mkoloni na kutengeneza agenda na mfumo wa kuanzia, vizazi vya uongozi vilivyofuata vikajikinai na Uafrika.
 
Kabla ya 1996 kodi zilikua zinakusanywa ila idara ya makusanyo ya kodi ilikua ni kitengo pale wizara ya fedha.

Kumeongezeka sana ufanisi wa ukusanyaji kodi toka kuanzishwa kwa TRA.
Lakini mpaka sasa TRA iko chini ya wizara ya fedha. Yaani kama kitengo fulani, au?
 
Ubinafsishaji wa hovyo na Rais aliepo madarakani atangazwe mshindi hata kwa tofauti ya kura moja hiyo sheria ilipitishwa wakati wake.
 
Huyu ndie yule wa biashala mpaka ndani ya Ikulwu.
 
Rais Mkapa ndiye muasisi wa TRA, kabla ya hapo kulikuwa na idara chini ya wizara ya fedha ikijulikana kama income tax, ambayo ufanisi wake wa kukusanya kodi ulikuwa dhaifu sana....

The Tanzania Revenue Authority (TRA) was established by Act of Parliament No. 11 of 1995, and started its operations on 1st July 1996. In carrying out its statutory functions, TRA is regulated by law, and is responsible for administering impartially various taxes of the Central Government.
 
started its operations on 1st July 1996
Mkuu Matuja,
Ina maanisha iliishaanzishwa huko nyuma lakini ikaanza operesheni July 1996. Wakati inaanzishwa Mkapa alikuwa Waziri, Mkapa amekuja kuwa Rais Nov 1995 alipokula kiapo, ndani ya Nov - Dec 1995 (mwezi mmoja) hakuanzisha TRA bali alikuwa ndiyo ametingwa kusuka/kuunda safu yake ya serikali ya ngwe yake ya kwanza ya awamu ya 3. Ndiyo maana hadi 1996 akaja kuiboresha na kuanza operesheni July. Hapa ni suala tu la timing.
 
Mkuu Douglas, pengine kama una kumbukumbu ya mswaada wa sheria kupelekwa kabla ya bunge kuvunjwa July 1995 sio vibaya ukashirikisha jukwaa ili kuwa na uelewa wa pamoja.

Ila pia kuna uwezekano hoja ya kuasisiwa TRA ilipelekwa bunge la 1995 Nov wakati tayari Mkapa akiwa Rais. Hata hivyo chombo kinachoitwa Mamlaka ya mapato (TRA), imekuwa chombo rasmi 1996; kwa msingi huo kabla ya tarehe hiyo hapakuwa na TRA isipokuwa shughuli za kukusanya mapato ilikuwa chini ya idara iliyojulikana kama "income tax"
 
Kwahiyo iundwe taasisi ya Madawati
Baadae iundwe taasisi ya Madarasa
Hatimae iundwe taasisi ya Upungufu wa Chaki
Sasa mkuu baadae itaundwa taasisi ya taasisi zilizoundwa
Ndugu balimar hoja hapa si kuundwa taasisi ya madawati hoja ni kutengeneza mfumo unaotatua changamoto katika hali endelevu kwa mf awamu ya tano mwanzoni tulinunulishwa madawati na tukaambiwa tatizo la madawati limekwisha kana kwamba tumesahau au hatujui kuwa madawati huharibika lakini pia idadi ya wanafunzi huongezeka ilikuwa hivyo kwa vyumba vya madarasa nyumba za waalimu na maabara.
Kwa watu mnaotumia bongo vizuri lazima mbuni njia ya kujibu hizi changamoto katika Hali endelevu na sio zima moto
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…