Tathmini zinasema Lissu ana nguvu nje ya chama kwa wapiga kura za Urais wa nchi, kwa nini aliamua kugombea ndani ya chama ambako ni dhaifu?

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
16,859
Reaction score
28,112
Kwa maoni yangu, Lissu angejikita katika kujiimarisha katika kugombea nafasi ya urais (japo asingeshinda).

Hata watu wake wa karibu wanasema Lissu ana nguvu sana nje ya chama kwa wananchi wa kawaida ambao wanapiga kura za urais. Kwa nini aliamua kujidhoofisha kwa kugombea Uenyekiti wa chama, hatimaye kusababisha mpasuko? Angebaki na umakamu, na kama angekuwa Rais (hatakuwa Rais) Uenyekiti ungekuja tu

Mpasuko huo unadhoofisha hata nguvu yake katika kugombea nafasi ya urais kwa sababu mahasimu wake ndani ya chama wanamsubiri wahujumu kura zake za urais. Ni mtandao mkubwa wa mahasimu wake ndio anautegenea ulinde kura zake za Urais. Watamshughulikia vilivyo.

Kama sasa hivi tu anawatukana, akiwa Rais? Hakika watapambana kuhakikisha hawi Rais japo ni chadema mwenzao.

Nadhani alipata washauri wasio sahihi, na sasa atakuwa na majuto, japo hatajionyesha hadharani.

Sasa hivi Mbowe yupi atawapa chadema fedha kufadhili urais wa mtu anayemtukana? Mbowe atawekeza kwa wabunge tu, naa Lissu ataachwa ajijue.
 
Lini na wapi Lissu amemtukana mtu? Kueleza machafu yanayofanyika Chadema siyo matusi bali anaonyesha dhamira kuwa akipewa nafasi ya kuongoza chama atakisafisha. Tatizo maccm mumezoea zile siasa za huyu ni mwenzetu hata akijinyea mtasema amejamba tu.
 

Mwenzenu katika imani anawaasa:

 
Maswali ni yetu tukupe majibu au ni yake akupe majibu?
 
Hopeless topic.
 
CDM hawezi kuwa jinga hivyo ndugu.

Ndiyo maana hata mwamba na chawa wake si wenzetu!
Wakati chama kinaanzishwa ulikuwa bize kufanya kilimo cha bangi Tarime, hebu kaa kule, na hii ndio dawa, sogeza kalio sindano iingie
 
"Mbowe atawekeza kwa wabunge tu"
Hii sentensi imekaa kijasiriamali mno.
 
Kama ana nguvu nje ya chama huyu ndo tunamuhitaji, chama kitaungwa mkono vizuri zaidi
 
Mbowe must go
 
Kama wakifanya hizo siasa za kukomoana ndani ya chama chao na wakapambania ubunge tu, huo ushenzi utawagharimu hawataambulia mbunge hata mmoja labda wapewe wawili watatu kama maridhiano tu ccm iwaachie isikabe mpaka penati. Nani atawapa kura, bora kuwapa kura ccm tu waendelee kutawala.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…