Tatizo la Ajali za Barabarani Litatumaliza Watanzania. Je, Kweli Serikali Haiwezi Kufanya Kitu?

Kumbuka hiyo ndo nguvu kazi unapungua yaani walipa Kodi hao ni kitu kidogo cha kufikiria kwa wenye mamlaka lakini mtu akiona familia yake iko salama anapotezea kama vile walokufa mifugo tu
 
Kumbuka hiyo ndo nguvu kazi unapungua yaani walipa Kodi hao ni kitu kidogo cha kufikiria kwa wenye mamlaka lakini mtu akiona familia yake iko salama anapotezea kama vile walokufa mifugo tu
Umeongea jambo la msingi sana
 
Mpaka kila mtu akifahamu nafasi yake
Ni kweli chief,kulaumu nafsi ya tatu (askari wa usalama barabarani,miundombinu mibovu,vilevi n.k) haitoshi, jambo kuu na la msingi ni kujali usalama wako kwanza. Mathalani unapanda gari chakavu, dereva anaendesha huku kashaugwida ugimbi, kunyamazia dereva akiendesha bila kutii sheria za usalama na mengine ya kufanana na hayo.
 
Wazi mkuu
 
Ila Jeshi la polisi usalama barabarani hawakwepi lawama moja kwa moja. Linalo jukumu kubwa la kuhakikisha usalama wa raia barabarani ikiwamo kuhakikisha vyombo vya moto chakavu visiingie barabarani, dereva anaendesha kwa kufuata sheria na bila kutumia vilevi na mengineyo! Ila badala yake wote tunaona mambo ya hovyo tu wanayofanya.
Tunaendelea kungoja siku ile ambayo atatokea amiri Jeshi aliyechoshwa na huu uozo wao atoe kauli ambayo itawarudisha kwenye mstari sio mambo ya kubrashi viatu.Wanyooke kama rula na sisi tutapone.
 
Kabsa Mkuu
 
polisi wanapojaribu kuwa wakali watu wanaleta siasa.juzi kuna traffic kapigwa kapasuliwa uso kisa kusimamisha gari na kutaka kuwashusha abiria waliokuww wamepangwa kwenye coridor isiyo na siti ndani ya bus.
kilichonisikitisha zaidi ni mpaka wanaharakati wetu tunaoamini wameenda shule na wameelimika kule X wanashangilia kwamba ni dalili kwamba raia uoga unawatoka sasa,wanapiga askari wajinga wajinga,sawa.

ujinga wa watanazania wengi umewafanya kuwa shamba la kuvunia umaarufu kwa wajanja,mtaji wa kisiasa kwa wanasiasa wahuni,kichaka cha wahalifu kujificha,na ngazi ya kupanda kuufuata ukwasi kwa wenye nia hiyo.

ni bongo tu magari yatakimbizana kuwahi kufika kituo B ukute kuna watu walibeti nani mshindi.

ni bongo tu bodaboda ataendesha piki piki kichwa wazi akikimbia sana huku anapigiwa miruzi,abiria wake akiulizwa kwanini havai kofia anasema ina chawa.

ni bongo tu,ambapo speaker atasisitiza mabus yasafiri usiku pamoja na maroli na yeye hapandi mabus,akijua kabisa barabara zenyewe ni metre 6 tu two way.

bongo tu kosa la barabarani fine ni elfu 30 hata ukiendesha umelewa,huna break,au tyre vipara unawezalipa fine yakaisha,kwa wenzetu kuna makosa hawataki kabisa kihela chako utaenda mahakamani.

kifupi tuna kazi ya kumuomba Mungu atulinde halafu tuna kazi ya kuwa makini pia.wenzetu wameamua tu kuwa makini moja kwa moja na kushughulika na wanayoyaweza.
 
Maua yako mkuu 🌹
 
Tuanze na ripoti kamili za ajali. Ajali itolewe taarifa kamili kutoka kwenye 'tume' maalumu. Na sio tume iwe ndio utaratibu wa kawaida wa polisi na usalama barabarani kuhusiana na ajali.

Baada ya hiyo ripoti yenye majibu kamili wa ajali na jinsi ilivyotokeatokea na uhisika wa wote waliowajibika kuanzia fundi wa gereji aliyetengeneza breki, mmiliki aliyegoma kurekebisha kioo, dereva ambaye hakukata kona labda wooote (hadi nafasi ya wahanga kutovaa mikanda, helmenti na kujaa) kila mmoja na uhusika wake WAWAJIBISHWE!
 
Ukweli ni kwamba Sheria ya Usalama Barabarani Sura ya 168 inahitaji marekebisho makubwa sana.
Mfano tu;
Baraza la Taifa la Usalama barabarani litaongozwa na Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti na wajumbe wasiopungua 10 wanaoteuliwa na waziri anayehusika na masuala ya usalama barabarani. Kazi kubwa ya Baraza ni kutoa mwongozo juu ya kuongeza maarifa na njia mbali mbali zitakazoweza kuimarisha hali ya usalama barabarani.
Hili baraza linatakiwa lichaguliwe na watumiaji wa barabara sio waziri kwa sababu waziri kuja kukutana na ajali ni nadra sana!​
 
Media hazitumiki vizuri kunufaisha jamii, elimu elekezi ya Matumizi ya Barabara (pamoja usalama katika sector nyingine,) sio lazima itolewe chuoni, media zinasaidia kwa sababu udereva ni maisha endelevu kama media zenyewe.
 
Media hazitumiki vizuri kunufaisha jamii, elimu elekezi ya Matumizi ya Barbara (pamoja usalama katika sector nyingine,) sio lazima itolewe chuoni, media zinasaidia kwa sababu udereva ni maisha endelevu kama media zenyewe.
Media zetu zipo busy kuonesha nyimbo na shows pekee mkuu
 
Kipindi nimechapisha andiko hili kuna watu waliniambia kuwa halina point wala mashiko!
Kinachoendelea sijui ni kitu gani!? 😔
Tanzania Traffic mna kazi kubwa sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…