Tatizo la kula udongo: Fahamu visababishi, madhara yake na mbinu za kuacha

Tatizo la kula udongo: Fahamu visababishi, madhara yake na mbinu za kuacha

Wanajukwaa naombeni msaada wenu nna tatizo la kupenda sana kula udongo. Natamani sana kuacha lakini nimeshindwa kabisa.

Siipendi hii hali kwa sababu nasikia ni hatari kiafya japo sijui ni kwa kiwango gani...
Je, ulifanikiwa kupona tatizo lako? Ulitumia dawa gani?
 
Habari, naomba mnijuze kitu maana ninahofu mwenzaenu, m ni muathirika wa kula udogo ,yaan ni zaidi ya miaka kumi Sasa nimejaribu kuacha Sana lakini imekuwa ngumu ,Sasa najiuliza mmh ninapatag kinyesi kigumu ,vipi kuhusu wale wanaofanya mapezi kinyume na maumbile ,huku nyuma sehemu ya haja kubwa si kunakuwaga kumepanuka?

Vipi kwa mtu anayekula udongo c kinyesi kinakuwa kigumu sana haiwezi kuwa athari ni sawa na ya mtu anayefanya kinyume na maumbile? Naogopa maana Kuna wakat hadi naskia sehemu ya hajakubwa kunawasha mno jaman, msinipopoe ,jibuni tu kistaarabu nami niondokane na janga hili
 
Habari, naomba mnijuze kitu maana ninahofu mwenzaenu, m ni muathirika wa kula udogo ,yaan ni zaidi ya miaka kumi Sasa nimejaribu kuacha Sana lakini imekuwa ngumu ,Sasa najiuliza mmh ninapatag kinyesi kigumu ,vipi kuhusu wale wanaofanya mapezi kinyume na maumbile ,huku nyuma sehemu ya haja kubwa si kunakuwaga kumepanuka? Vipi kwa mtu anayekula udongo c kinyesi kinakuwa kigumu sana haiwezi kuwa athari ni sawa na ya mtu anayefanya kinyume na maumbile? Naogopa maana Kuna wakat hadi naskia sehemu ya hajakubwa kunawasha mno jaman, msinipopoe ,jibuni tu kistaarabu nami niondokane na janga hili
Kama umeshindwa kuacha kula udongo uwe na tabia ya kula papai Mara kwa mara
 
Habari, naomba mnijuze kitu maana ninahofu mwenzaenu, m ni muathirika wa kula udogo ,yaan ni zaidi ya miaka kumi Sasa nimejaribu kuacha Sana lakini imekuwa ngumu ,Sasa najiuliza mmh ninapatag kinyesi kigumu ,vipi kuhusu wale wanaofanya mapezi kinyume na maumbile ,huku nyuma sehemu ya haja kubwa si kunakuwaga kumepanuka? Vipi kwa mtu anayekula udongo c kinyesi kinakuwa kigumu sana haiwezi kuwa athari ni sawa na ya mtu anayefanya kinyume na maumbile? Naogopa maana Kuna wakat hadi naskia sehemu ya hajakubwa kunawasha mno jaman, msinipopoe ,jibuni tu kistaarabu nami niondokane na janga hili
ULAJI WA UDONGO NA MADHARA YAKE:

Kwa kawaida ulaji wa udongo husababishwa na mambo yafuatayo:

1.Upungufu wa madini ya chuma na zinc mwilini.
Hii ni kutokana na lishe duni au kupoteza damu nyingi wakati wa hedhi au upungufu wa madini chuma kutokana ugonjwa wa minyoo na safura.

2.Unywaji chai yenye majani ya chai au kahawa wakati wa kula,ambayo huzuia madini ya chuma kufyonzwa au kuharibiwa inapoingia mwilini.

3.Upungufu wa dawa ya kuyeyusha chakula tumboni (hydrochloric acid) pia husababisha tatizo hili.

MADHARA YA KULA UDONGO:

Kula udongo na vitu vingine ambavyo si chakula kunaweza kusababisha madhara ya kiafya kama ifuatavyo:

*Kwa kuwa udongo unaweza kuwa na sumu za dawa za mimea na mbolea kama vile lead, dioxin na madini mengine yenye hatari yanayopatikana kwenye udongo uliochafuliwa, hivyo inaweza kusababisha matatizo ya kiafya mwilini mwako.

*Husababisha mikwaruzo, michubuko na kupata majeraha ya ndani kwenye utumbo.

*Ugonjwa wenye homa na maumivu makali unaojulikana kama appendicitis ambao tiba yake ni upasuaji.

*Kupata minyoo aina ya safura.

*Kukosa choo na tumbo kuuma kwa siku nyingi bila sababu.

*Bawasiri
*Saratani ya utumbo

*Kwa kuwa mara nyingi udongo huchafuliwa kwa vinyesi na mikojo ya binadamu, ndege na wanyama kama mbwa nk, basi hali hii husababisha udongo kubeba vimelea vya magonjwa.

NIFANYAJE ILI NIWEZE KUACHA KULA UDONGO??

Ifuatayo ni namna ya kukabiliana na tatizo hilo:

*Kula vyakula vyenye madini chuma na zinc kwa wingi kama vile maharage, korosho, mboga za majani hasa spinach, mayai, nyama, samaki, mbegu za maboga na matunda

*Kutibu minyoo kwa kumeza dawa za minyoo angalau mara moja kwa mwezi.

*Kunywa juice ya spinach na karoti bilauli moja kutwa mara tatu kila siku.

*Kunywa supu ya mbogamboga na mchele.

ANGALIZO

Usinywe vinywaji vyenye caffeine wakati wa kula chakula.
 
Habari, naomba mnijuze kitu maana ninahofu mwenzaenu, m ni muathirika wa kula udogo ,yaan ni zaidi ya miaka kumi Sasa nimejaribu kuacha Sana lakini imekuwa ngumu ,Sasa najiuliza mmh ninapatag kinyesi kigumu ,vipi kuhusu wale wanaofanya mapezi kinyume na maumbile ,huku nyuma sehemu ya haja kubwa si kunakuwaga kumepanuka? Vipi kwa mtu anayekula udongo c kinyesi kinakuwa kigumu sana haiwezi kuwa athari ni sawa na ya mtu anayefanya kinyume na maumbile? Naogopa maana Kuna wakat hadi naskia sehemu ya hajakubwa kunawasha mno jaman, msinipopoe ,jibuni tu kistaarabu nami niondokane na janga hili
Huwa unaota ndoto za nyoka?
 
Mwanadamu ameumbwa kwa udongo na hata ulaji wako wa udongo ni kukumbuka chimbuko lako.

Pia suala la kupanuka puru lako hilo inatokana na kusukumiwa moto na si udongo.
 
Kama unashindwa kuacha kula 'udogo' nakushauri anza kula ukubwa.

Kama ilivyoelezwa kwenye posti namba 3, kitendo cha kula vitu ambavyo havina asili ya chakula ni ishara ya mambo kutokuwa sawa upande wa mwili.

Hivyo, suala la msingi lilikuwa ni kufahamu kwa nini inakutokea hivyo:
1: Upungufu wa madini
2: Upungufu wa vitamins
3: Tatizo la mfumo wa saikolijia/afya ya akili

Baada ya hapo, kinachofuata ni kurekebisha tatizo husika huku ukijifunza kuachana na mwenendo wako uliokuwa nao. Hapo huwa ni rahisi sana kufikia lengo.

Naomba uonane na wataalamu wa afya ili kung'amua tatizo ni nini hasa na usaidiweje.
 
Namshukuru Allah nimeacha kula udongo,maana nilikuwa nautafuna kwa siku natumia 500+kwaajili ya udingo,hata kula nilikuwa sitamani....nikila udongo nikinywa na maji naridhika,

Kuna dr akaniambia kila nikihisi hamu ya kula udongo basi nitafune dagaa,nashukuru sina tena hamu ya udongo
 
Mimi nilikuwa nakula japo sio mwingi lakini nilikuwa nakula mpaka nilipopata mimba nikachukia mpka leo sina hamu.
 
Back
Top Bottom