Tatizo la kuwashwa mwilini baada ya kuoga: Fahamu chanzo, ushauri na tiba

Tatizo la kuwashwa mwilini baada ya kuoga: Fahamu chanzo, ushauri na tiba

Jamani mimi pia nina hili tatizo, lakini mimi nikioga bila kujisugua na dodoki sipati muwasho wowote yawe maji ya chumvi sijui ya moto au baridi, lakini nikitumia tu dodoki kujisugua sehemu yeyote cha moto nitakipata kwa muda wa dakika tano mpaka pale nitakapo jifuta maji vizuri na kupaka mafuta, mwenye utashi na hili swala anisaidie tafadhali.

Hilo dodoki litakuwa linachuna ngozi yako,tafuta kitu cha kujisugulia soft.

Mimi kuwashwa kwa maji inatokezea tena sana kwa maji ya moto, na ya baridi hayaogeki huku uzunguni, hivyo huweka balance ya maji si moto wala baridi.
 
Ndugu zangu huu ni mwaka wa 10 tangu tatizo la kuwashwa kila nikioga linianze nishazunguuka mpaka sasa nimechoka yoyote anae weza kunisaidia jinsi ya kupona naomba anisaidie

Pole sana ndugu yangu, ninakushauri uonane na specialist wa ngozi anaweza akakusaidia katika Hospitali ya Muhimbili.
 
Hilo tatizo linanisumbua sana asante kwa majibu
 
Siku mbili hizi nimefanya ka research kadogo kuhusu miwasho, nadhani hiyo yako inaweza kuwa inasababishwa na ngozi kuwa dry so ukitoka kuoga jipake mafuta fasta na pia ukijifuta na taulo usijisugue fanya kama una ji sponge kwa kugusia gusia kwenye mwili.

Mkuu we ndo umetoa jibu sahihi, mi mwenyewe tatizo hilo ninalo ila kwa njia iliyoiandika hapo juu sasa hali ni shwari
 
Mm na kushauriana acha kwanza sabun unayo tumia kuogea tumia sabun ya kipande kwanza then utagundua nn tatizo. Mfano mm nilikuwa nawashwa sana baada ya kuoga nimehangaika sana lkn nimegundua tatizo ni sabun ya protex ninaaleji nayo tangu niache. Kutumia. Nipo poa
 
Sodata, ushauri wa sabuni ni kweli kabisa, katabia kakubadirisha sabuni upelekea miwasho,jaribu kutumia aina moja ya sabuni,hata hivyo sabuni inayoleta muwasho ukiendelea nayo mwishowe ngozi yako ita-adapt na muasho kupotea,kingine jaribu kupaka mafuta hasa ya mgando pale unapotoka tu kuoga nayo inasaidia sana,ahsante,
 
Habarini za saa hizi wapendwa katika Mungu aliye hai,

Husika na kichwa hapo juu. Nimekuwa na tatizo hili la kuwashwa mwili mzima hadi mistari ya uvimbe kama nimetambaliwa na mdudu hujitokeza kwa miaka minne sasa, naumia mnoo!

Kwa matitabu niliyowahi kufanya ni ya St. Joseph hospital MOSHI mwaka 2015 hii haikuzaa matunda, niligongwa sindano nyingi lakini haikisaidia.

Matibabu mengine ni mitishamba flani hivi nilinunua sokoni mgandini(TANGA) mwaka Jana haikusaidia nayo, yani ndo tatizo linazidi nawashwa mpaka najisikia vibaya kufika mahali hadi nauchukia mwili wangu so saaad!!!.

Naombeni sana tena sana msaada wa nini nifanye kuondokana na shurba hii jamani.


Thanks in advance.
 
Ekenywa hospital ni jibu lako. Ni hospitali ya allergy.
 
Ekenywa hospital ni jibu lako. Ni hospitali ya alegy.
Iko wapi mkuu,nitafurahi kama litatatuliwa tatizo langu walah,sijui nitatoa shukria kubwa iliyoje,Naumia sana ukiona hivyo.
 
Kimbilia kwa Yesu atakuponya. Tafuta watumishi wakuombee ndio suluhisho
Nshaombewa pia mkuu especially my Mom ana upako sana every neighborhood use her prayer and win lkn mm bado kwa kweli.
 
Unawashwa wakati wa kulala au muda wote
Muda wote ila mchana ni nadra unakuta labda kutwa nzima nikawashwa Mara mbili tatu,lakini usiku Mungu aliye juu anajua mateso ninayopa,yani najigeuzageuza mpaka mwili unawaka moto na ina-persist mpaka masaa sita,silali mkuu please help God will pay you in return.[emoji24]
 
Niliwah kupata hilo tatizo, ila mimi ilikuwa ni minyoo ya tumboni.
Nikikaa muda mrefu sana bila kumeza dawa za minyoo huwa linarudi.

Kipindi sijapata solution nilitamani nitoke duniani maana nlikuwa sina. Amani.
 
Kama Ukienda na matibabu ya dunia (hospital) wakashindwa. Mtafute Yesu Kristo, Damu ya Yesu. Kwa huyu jamaa hakuna linaloshindikana.Gharama zake ni Uwe na Imani tu kwake. tatizo lako litakwisha.
 
Back
Top Bottom