Tatizo la Machinga, Tulikosea, Tunakosea, Tutaendelea kukosea!

MTAZAMO

JF-Expert Member
Joined
Feb 8, 2011
Posts
19,675
Reaction score
33,583
Ndugu zangu Watanzania,

Kuna sehemu tulikosea, tunakosea na tutaendelea kukosea. Wimbo wa Machinga kufanya biashara maeneo yasiyo rasmi kama yupo anayefikiri ni wimbo wa juzi basi ana upungufu wa akili. Nani hapa ambaye anaweza kukataa kuwa kwa mfano mitaa ya Kongo ilivyo leo pako hivyo miaka mingi mno na hakuna kilichobadilika zaidi ya majengo mapya?

Serikali za awamu zote zilikuja na njia mbalimbali ambazo zingine ziliishia kuchoma fedha ambazo hazikutoa matunda yoyote ikiwemo Machinga complex kule Karume. Hivi pamoja na wastani wa wasomi nchi hii kupanda sana hadi leo tunapambana na machinga badala ya kupambana na kile kinachozalisha machinga? Mnataka kuleta usafi,mpangilio wa nchi zingine kwa muonekano wao wa nje bila kuja na takwimu za namna walivyoweza kuacha maeneo yao ya katikati ya jiji bila machinga! Tuleteeni ushahidi ufuatao ili tujue hayo madesa ya kusifia nchi za wenzetu ni sahihi kuyatumia hapa;

1) Ushahidi jinsi walivyokuwa na tatizo la machinga kama letu
2) Kama walitatua kwa kuwatimua maeneo yao, au ...
3) Namna walivyoendesha zoezi la kuhamisha machinga kwa namna yenye mfanano na Kariakoo

Pamoja na Rais wa awamu iliyopita kuwa Mkali mno lakini swala la machinga alijua hana suluhisho la kweli na serikali haina mkakati wa maana akaona hakuna haja ya "kuliamsha dude" ambalo hana suluhisho na mbaya zaidi kitu kinachogusa maisha ya watu. Hivi ni nani anapenda kukaa kwenye lile jua la Kariakoo?, Hivi nani anapenda kukaa kwenye zile barabara pengine na mtoto huku gari zikigusa makalio yako? Tusicheze na maisha ya watu kama hatujajipanga! Tunasikiliza watu ambao wana njia za kujipatia kipato na mbaya zaidi kelele zao ni kubwa kuliko wanyonge hawa ambao kelele zao za manunguniko zitaishia kwenye kuta za nyumba zao!

Hakuna serikali ya awamu yoyote imewahi kufanikiwa kwenye hili zoezi la machinga. Naomba sana viongozi wetu tutafute namna ya kutatua tatizo hili kwa hekima. Kweli Kariakoo ni tatizo kubwa lakini si la jana wala juzi hatuwezi kulitatua kwa short cut. Wale ni mama zetu, dada zetu, Kaka na baba zetu wanaohangaika tena kwa mahitaji ya chini sana pengine familia ipate ugali tu. Ile Kariakoo ndio centre ya biashara kubwa kwenye ukanda wetu huu na muingiliano ni mkubwa, ule muingiliano ndio unaovutia machinga pia kujipatia riziki.

Swala la Machinga si la kuamka na kutangaza waondoke maeneo ya Kariakoo, Ile Kariakoo ilivyo hakuna sehemu Machinga atastahili kuwepo HAKUNA! Hao wachuuzi si wa kupanga mafremu, Hao wanaenda penye watu! Hao wenye maduka pia ndio wanawapa bidhaa wakasaidie kuuza. Ni mfumo wa biashara ambazo haufutiki kwa kuwafukuza tu, ni utaratibu ambao kwa kushirikiana nao hao wamachinga tunapaswa KUWAELEWA na kutafuta suluhisho la kudumu.

Mungu atusaidie hekima, busara za viongozi ziwaongoze kusitisha zoezi la kuwaondoa wale wamachinga na kujiuliza why walifeli awamu zote na nini kipya kifanyike.

"Our life of poverty is as necessary as the work itself. Only in heaven will we see how much we owe to the poor for helping us to love God better because of them" Mother Teresa
 
Hata wewe hapo kama ni Potential Machinga unategemea nini ?

Kila mwaka wanaongezeka huwezi kuwa na sustainable solution zaidi ya kuwapunguza machinga (tusiendelee kuwazalisha) / i.e. Reduce their Numbers.... How ?

That's a Topic for another Day.....
 
Kwa sababu hizo hizo tutazotumia kuondoa machinga Kariakoo zipo maeneo mengi hapa Dar kama pale mwenge na majiji mengine. Hili si tatizo la Kariakoo pekee bali ni mfumo wa biashara ambao umechangiwa na tatizo la ajira. Bila kutatua chanzo hatutokomesha hili tatizo labda tutaibua watu ambao watatafuta kipato kwa njia zingine ambazo zitakuwa mbaya zaidi ya umachinga.

Mfano kwasasa bodaboda zimeokoa vijana wengi ingawa pia zimeleta matatizo mengi. Sasa hata kuwadhibiti wavae helmet tumeshindwa! Bodaboda pia ni bomu ambalo lazima kuwe na mkakati wa kuwasaidia hawa vijana.
 
Kuwafukuza sidhani kama ni suluhisho.ila kama ni suluhisho wasitumie mabavu,kuna mbinu mia saba za kumfukuza mtu sehem
 
Mfano kwasasa kuna uhaba wa House girls kuliko sababishwa na elimu bure na maafisa elimu kufatilia kila mtoto anakwenda shule. Hili la Machinga kwasasa ni kama limekuwa rasmi ndio maana hadi wanapewa vitambulisho na kulipia 20,000. Hivi vitambulisho vimelenga machinga ambao kwa nature ya biashara yao hawakai maeneo yaliyotengwa.

Hapo hapo wafanyabiashara wanawatumia kuwauzia vitu vyao ikiwemo mfano Azam ice cream, ni umachinga ule na wale hawakai sehemu maalum! Hili swala linahitaji mjadala wa mapana na sio siasa wala mihemko.
 
Machinga ni zao la informal business sector ambao ndo mfumo wa biashara uliokithiri nchini. Low formalization of businesses + high unemployment rate = machinga kila sehemu.
 
Watu ambao hawawezi kusoma alama za nyakati. Kule gine walioasi na kupindua wanashangiliwa, kutiwa hamasa na nguvu na machinga wa gine.
 
Our life of poverty is as necessary as the work itself. Only in heaven will we see how much we owe to the poor for helping us to love God better because of them" Mother Teresa[emoji1545][emoji1545][emoji1545][emoji1545][emoji1545][emoji1534][emoji1534][emoji1534][emoji1534]
 
Mtu wa falsafa ushakamata kitu [emoji109]
 
Tatizo umasikini tumeugeuza siasa, tunafunga mgodi unaoajiri watu elfu nne, kisa tunadai dollars 50m, tunaweka tozo la miamala badala yake ajira zaidi ya laki tano zinapotea and no one cares, kisa tunao polisi wakupiga watu, nao polisi wanalalamika kesi zimepungua yaani wanakufa njaa
 
Mie najiuliza hawa vijana wanaokesha kwenye night clubs wakisubiri kurudisha maghetoni machangudoa wakizeeka itakuwaje? Hao old age citizens tutamudu health care zao?
 
Rc makala aangalie ataondoka na machinga hali ukiwa mbaya wanasiasa watamgeuka
 
Nakubaliana na afande kiondo wakati tunajenga shule na zahanati tujenge pia na mahabusu na vituo vya polisi kwani hizo shule sanasana zitaongeza weledi kwenye uhalifu. Unamsomesha mtu ambaye hatakaa kwenye formal life, unategemea nini? Eti akajiajiri? Mtu kawa sg wa sadc hataki kujiajiri anaenda kwenye ubunge akaanze kubishana na akina musukuma,
 
Mie najiuliza hawa vijana wanaokesha kwenye night clubs wakisubiri kurudisha maghetoni machangudoa wakizeeka itakuwaje? Hao old age citizens tutamudu health care zao?
Nyi ndo mumejenga hizo night club, tukiacha kwenda mnalaumu
 
Viongozi wetu watambue ya kuwa pale wanapopewa dhamana ya uongozi basi jukumu lao kubwa ni kutafuta njinsi ya kutatua changamoto zinazowakabili wananchi wanaowaongoza. Kwa kuwa pindi wanapoomba kibali kwao ili waweze kuchaguliwa, huwa wanajinadi kwa ahadi likuki.

Pindi wanapokabidhiwa dhamana za uongozi, viongozi wengi hupata vipato vikubwa, marupurupu kibao na hata wengine kupewa misamaha ya kodi ili kuwafanya wasiwe na changamoto binafai za kifedha ili wajikite katika kutafuta suluhu za changamoto zinazowakabili wananchi.

Changamoto za ajira kwa vijana na hata milundikano yao katika miji na majiji mbalimbali duniani ili kutafuta fursa zilizopo katika sekta isiyokuwa rasmi ni jambo ambalo linafahamika kijamii na kiuchumi. Hii inatokana na wengi wao kukosa fursa rasmi, mitaji na stadi sahihi za maisha.

Kwa hapa nchini Tanzania, viongozi wetu wa chama tawala hawakwepi lawama juu ya milundikano ya machinga amboao wanaendesha biashara zao pasipo kuwa na mpangilio wowote ule. Milundikano hii yenye kuikwaza sekta rasmi wala haikuanza leo, bali imechochewa kupitia tamaa za wanasiasa.

Uendeshaji wa biashara zote, yaani zilizo rasmi na hata zisizo rasmi, ni lazima zisimamiwe na sheria ndogo ndogo, yaani "by laws" zinazotungwa na utekelezaji wake kusimamiwa na manispaa za miji na majiji. Sheria hizi zinapaswa kuheshimiwa kwa sababu ndizo zenye kuweza kuweka mipangilio ya watu kufanya shughuli zao pasipo kubughudhi watu wengine.

Viongozi wa juu wa nchi wanapokosa utashi wa kisiasa, huishia kuvuruga mifumo kupitia kufanya siasa. Ndiyo! Nasema ni siasa rahisi kwa kuwa kiongozi wa juu pasipo kujali anavuruga ama anakwaza ufanisi wa watendaji wa manispaa, yeye kutokana na maslahi binafsi ya kisiasa anawageuza vijana kama ndiyo mtaji wake wa kisiasa.

Hatuwezi kuwaacha machinga wakiendelea kuongezeka kila kukicha, huku tukiogopa kuwaelimisha kuhusu umuhimu wa wao kutii sheria na hata kuzingatia maeneo stahiki ambayo yametengwa ili waweze kufanya shughuli zao.

Ni jukumu la serikali kuhakikisha kwanza wanawatengea machinga maeneo yao rasmi ambayo yatawawezesha kufanya shughuli zao. Pili inapaswa elimu sahihi ilitolewe kwao kuhusu umuhimu wa wao pia kutiiia ili wasiweze kuwabughudhi watu wengine.
 
Mawazo yako nayakubali it's absolutely correct, sasa tutumie approach ipi kutatua ulio ya ainisha? Tutumie thumb rule au bottom up approach?
 
Ni Uzi bora sana hongera Mtazamo na wachangiaji wengine... Mimi nadhani tungeanza na upashanaji hbr chanya na kuangalia Kwa undani sana tija ya VETA NA SIDO na ikibidi kuwekeza zaidi ltk maeneo haya.. Wakati unapita sana in lzm kabisa kuwekeza / Kutafuta technologia rahisi kwa maisha ya Watz tukiwa na mtaji wa ardhi AMANI na nguvukazi watu...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…