Tatizo la masikio: Fahamu kuhusu sehemu za sikio, magonjwa, ushauri na tiba

Tumia Boric acid, ikibuma tmia Marijuan, Mimi nilitumia Majani ya Ba ngi na nikapona. unakamulia juice au unaloweka na unaweka tone 2, au
 
Usaha unapotoka,kichwa hakiumi hata,hata kkichefu chefu wala maumivu
 
Mke wangu naye alisumbuliwa na tatizo hilo, katika kuhangaika hangaika tukaambiwa atumie mafuta ya kuku wa kienyeji au ya kondoo, ametumia ya kondoo sasa hivi usaha unatoka kwa mbali sana, alikuwa ananyunyuzia tone Moja tu kwa siku kwa kuwa inasemekana ni dawa kali sana ukiweka matone mengi ngoma ya sikio inapasuka
 

TIBA MBADALA YA MAGONJWA YA MASIKIO



Sikio (Ear) limegawika katika sehemu tatu kuu. Sehemu ya nje ya sikio, sehemu ya kati ya sikio na sehemu ya ndani ya sikio.

Kuna aina mbili ya matatizo ya masikio nayo ni:

i. Otitis media : ambayo hutokea katika sehemu ya kati ya sikio na mara nyingi huwatokea watoto wachanga na watoto wadogo.

ii. Otitis externa: ambayo hutokea katika sehemu ya ndani ya sikio na mara nyingi huwatokea waogeleaji, na hutokea zaidi wakati wa baridi.

Ishara za Matatizo ya masikio kwa Otitis media
i. Kuumwa na kuchomwa kwa sikio

ii. Kutokwa na uchafu ndani ya sikio

iii. Kutosikia kwa ghafla

iv. Homa

Sababu za Otitis media:
· Sababu kubwa ya maradhi hayo ni kuziba kwa bomba la sikio(Eustachiantube), kutokana na baridi, allergy pamoja na kuingia takataka. Hii inababisha maji maji ya sikio kujaa maji hayo nayo husababisha uvimbaji wa (ear drum) sikio.

Sababu za Otitis externa
· Hii husababishwa na baketeria au fungi, maji maji yanayoingia ndani ya sikio ndio sababu kuu ya kufanya bakteria na fungi kuzaana pia Skin allegies husababisha maradhi hayo.

Na sababu nyengine ni ulaji mbovu wa chakula pamoja na upungufu wa usafi wa mwili.

DAWA ZA KUJITIBU MARADHI YA MASIKIO:

i. Nyunyiza juisi ya Kitunguu saumu katika sikio linalouma

ii. Nenda Hospitali ukapigwe bomba ili maji na uchafu upate kutoka

iii. Pasha moto mafuta ya Zaituni (Olive oil) na yasubiri yapowe na ujitie drops mbili hadi 3

iv. Na usafishe masikio yako kila baada ya kutoka kukoga.

KUTOKWA NA USAHA SIKIONI:
Ikiwa utaweka kitu kama ujiti wa kiberiti au mfano wake sikioni, unaweza kusababisha jeraha kwenye sikio na damu kuanza kutoka. Baadae usaha unaweza kutungwa sehemu ya jeraha na kutoka kidogokidogo. Lakini pia mashambulizi ya bacteria sikioni yanaweza kusababisha kutokwa na usaha.

TIBA ZA MAUMIVU YA MASIKIO NA KUTOKWA NA USAHA:



Chukua maji masafi ujazo wa kijiko kimoja cha chai halafu uchukue chumvi kidogo kiasi cha vidole viwili uchanganye ndani ya maji hayo kisha hayo maji uchanganye na asali kijiko kimoja kidogo cha chai. Weka tone moja ya dawa hii ndani ya sikio lenye kuuma au kutokwa na usaha kutwa mara tatu
 
classmate wangu aliwahi kuugua hivyo enzi za primary badae akawa hatoki usaha nilipomuuliza katumia dawa gani akasema walichemsha kuku then mafuta ya kuku ndo wakawa wanadondoshea sikioni kwasasa sijui alipo so sijui kama kuna dawa nyingine alitumia
Mafuta ya kuku ni dawa kwa masikio yatokayo usaha, na mara nyingi sababu inakuwa ni kupigwa vibao vya masikio/taya, hivyo baada ya muda matatizo kama hayo hutokea.
 
Ulikuwa wapigwa vibao vya masikio/taya kipindi upo mdogo?

Kwanini usiombe kibali MHA upate ruhusa ya kwenda hospitali?

Kama tatizo ni pesa, pia waweza muona Raisi wenu mama Biella akusaidie jinsi gani waweza pata msaada wa matibabu.

Ukiwa waendelea kusubiri namna ya kwenda hospitali nje ya hapo ulipo, jaribu kutumia mafuta ya kuku, itakusaidia pia.
 
Muombe ushauri mama ako, si ulikataaa dawa za kienyeji??,
 
Asante kwa elimu yako,

Doctor,kipondi napatwa na tatizo hili miaka iliyopita kweli zilitokea dalili zote tajwa japo juu,lakn baada ya muda na mpaka Leo masikio yote mawili yanapotoa usaha huwa hayatowi maumivi kwa maana ya kuuma au kchwa kuhuma hata dalili yoyote tofauti tu na uchafu masikioni,
 
Daka kinyonga chukua mkia wake ingiza sikioni hakikish kinyonga humuui
 
Wana jamiiforums aaante kwa ushahuri wenu
Na ninataka ushahuri zaidi juu ya tatizo langu

Tatizo langu Mara ya kwanza kunitokea niliangaika nalo sana kias kwamba kila dawa ninayoshauriwa mtaani kwetu nilitumia
kila nilipokuwa naenda hospitali nilikuwa nawalazimisha madokta kunifanyia vipomo vya maskio,maana nilikuwa nikienda na nkiwabia historian ya ugongwa wangu Mara nyingi walikuwa tu na mzoea ya kunibadlishia dawa.
Lakini daktar alipokuwa ananipima masikio alikuwa haono chochote na kuniambia maskio yako sawa

Sasa huwa najihuliza chanzo cha huu uchafu ni nini kias tatzo halitibiki

Kutoka na hilo mama yangu aliachana kabisa kunipeleka hospital na kuanza kunitafutia dawa za kienyeji.
Kla mtu alokuja na ushauri wake na tuliohupokea nilihufanyia kazi,nikaanza kutumia bila mafanikio na sikutaka tena kuendelea nazo.

NB: masikio yangu yanapotoa uchafu,huwa hayaumi wala kutoa maumivu yoyote
 
Pole sana... Umesema uliwahi tumia dawa za hospital lakini hukuzipenda ukaachana nazo.? Nadhani hapo haukuwa sawa rudi tena hospital na usizembee kwenye dawa.
 
Tumia dawa yangu niliyo kupa ushauri utapona.
 
Pole sana... Umesema uliwahi tumia dawa za hospital lakini hukuzipenda ukaachana nazo.? Nadhani hapo haukuwa sawa rudi tena hospital na usizembee kwenye dawa.
hapana,ujanielewa dawa nilitumia lakn hapakuwepp na mafanikio,nlihitji vipimo na dawa zaidi lakin hapa kwetu kambin hakuna vipomo na dawa za kutosha,zle zilizpkiwepo hospitalini kwetu nilizitumia sana mpaka tukabadili dawa za kienyeji
 
Unaishi mkoa gani?kuna mti wa matunda kanda ya ziwa unaitwa masungwi haya ni matunda ni mwisho kijana unayachukua kama moja unalichoma kwenye moto linatoa maji unaweka matone mawili inawasha na kuuma ila baada ya hapa utasimuliaga tu
 
Mkuu pole sana ila jitahidi kufika hospital haraka... niliwahi kuomba msaada pia kupitia jukwaa hili kwakweli wana jf wapo mbele sana kusaidia embu pitia posti yangu usome ushauri mbali mbali

Masikio yangu yote yametoboka ngoma
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…