Tatizo la Tanzania halikuwa ujamaa wala vita vya Kagera bali ombwe la uongozi

Nyerere aliipotezesha Dira moja kwa moja hii nchii na tumeshindwa kujipapatua hadi hii leo
NYERERE alipewa uwaziri mkuu, hatimaye uraisi wa nchi, Kwasababu alionekana ana sifa za kuwa kiongozi mkuu wa Tanganyika na hatimaye TANZANIA kuliko watu wote waliokuwepo wakati wake akiwemo na babu wa baba yako.
Nasisitiza acha UTOTO, DOLA nyingi(empires), zimeanguka DUNIANI (Greece, Roman, Britain, nk) na Mifumo mingi imeanguka DUNIANI(Ukabaila, utumwa, ujamaa,nk), Je, hizo DOLA na hiyo Mifumo iliongozwa na NYERERE?( Kwahiyo, kuanguka kwa TANZANIA ni jambo la kawaida sana).

IFIKE wakati, sisi kama taifa tuamue nini cha kufanya ili tusonge mbele ili tufikie mafanikio tunayodhani kuwa tulistahili kuyapata. Tuache kukaa kwenye vijiwe kumlaumu MAREHEMU aliyeachia madaraka miaka 40 iliyopita bila kuuza rasilimali muhimu za nchi yetu( ardhi, mafuta , gesi, hifadhi, n.k). UJERUMANI imeendelea sana DUNIANI licha ya vita vya Dunia ilivyopigana na DUNIA nzima( Sasa mtu aliyeondoka madarakani mwaka 1985, anakuathiri vipi wewe?, Mbona akili yako Iko chini sana). Cha ajabu hata wengine ni wazee kabisa halafu wanashindwa kutafakari juu ya Hilo.

Kwahiyo, matatizo yetu ya leo hayatokani na NYERERE bali uvivu wetu sisi wenyewe( mfano: Akina Mulokozi , Diamond, Bakhressa, Dewji, Mengi, GSM, nk, wanafanya vizuri katika kutengeneza fedha).
NB: Ukianza kumtupia mtu matatizo yako, hutafanya jitihada ya kujitoa kwenye matatizo yako.
 
Watanzania huwa tunapenda majibu marahisi kwenye maswali magumu.

Huwa tunapenda kusingizia haya yafuatayo kwenye umasikini wetu, hasahasa anguko na mdororo
NYERERE ALIJIPIGA PINI MWENYEWE KWA KUFUATA MFUMO WA (SERIKALI YA KIJAMAA NA UMMA WA KIJAMAA) MFUMO SAHIHI NI (SERIKALI YA KIJAMAA NA UMMA WA KIBEPARI) kwa sasa tanzania tunafuata mfumo potovu sana kuliko hata wa Nyerere wa (SERIKARI YA KIBEPARI NA UMMA WA KIBEPARI) huu ni mfumo mbaya sana serikali inakuwa mali ya wahuni wachache na kuwa ni mradi wao na familia zao
 
Badala ya kufanya jitihada ujikwamue kwenye umasikini wako, umekalia kumsema NYERERE, kana kwamba nchi zote DUNIANI hazina matatizo ya kuanguka kiuchumi na hatimaye kuinuka na kufanya vizuri.
Kushindwa kwa TANZANIA kuwa na uchumi wa juu hakujasababishwa na NYERERE kumesababishwa na watanzania wenyewe.
Mfano: Tungekuwa na ubunifu wa juu unaotuwezesha kutengeneza bidhaa mbalimbali na kuziuza nje ya nchi na uzalishaji mkubwa wa ndani tusingekuwa nchi masikini. Na NYERERE aliachia ngazi madaraka ya nchi hii mwaka 1985( miaka 40 iliyopita). Kama mtoto alizaliwa wakati huo Sasa hivi ni Mzee. Kwahiyo, matatizo yetu yamesababishwa na uvivu wetu na kukosa ubunifu na siyo NYERERE.( Mfano: Akina Mulokozi, Diamond, Bakhressa, Dewji, Mengi, GSM, nk, Hawa ni matajiri katika nyakati zetu hizi).
Tukianza kumtupia matatizo yetu mtu hatutafanya jitihada ya kuyaondoa.
Tubadilike tuanze kutengeneza historia zetu, badala ya kuficha UVIVU WETUkwa watu waliondoka madarakani zaidi ya miongo 4 iliyopita ( 40 years ago).
 
Kama kawaida watanzania hutafuta sababu za kufeli,,hivi Nyerere katoka miaka 40 iliypita ambapo Tanzania hatukuwa na hata na simu za mkononi Wala lami Wala umeme vijijini,,Sasa tuliozaliwa miaka 50 iliyopita tumeifanyia nini nchi hii
 
Tatizo la nchi hii ni CCM tu. Mengine yote ni blah blah. Waliondoa miiko ya uongozi, wakaua Azimio la Arusha, Waliua kila kitu kwa kuiba na kugawana, wakaiingiza CCM kwenye vyombo vya ulinzi, ili kupata ulinzi wao milele.
 
Kadri ninavyoendelea kujifunza kuhusu hii dunia ndiyo nazidi kuamini kuwa system ya uchumi wa dunia ipo rigged. Wakubwa/mkubwa akitaka uendelee utaendelea. Akitaka usiendelee hautaendelea. Hakika, "And the weak suffer what they must."

 
Tatizo la Tanzania ni kukataa mawazo ya OSCAR KAMBONA kwa miaka ile
 
Malcolm, mtu akikubishia lazima atakuwa mchawi. Pamoja na kuujuwa ukweli, tusiokuwa wanasiasa (wataalam na wananchi wa kawaida) tunaponzwa na unafiki kiasi kwamba tunashindwa kuchukua maamuzi sahihi dhidi ya hawa wanasiasa. Na viongozi wa kisiasa wanatumia udhaifu wetu huo kufanya wanavyotaka. Tumeruhusu siasa itawale taaluma.
 
Umeandika jambo zito sana ambalo naamini wachache watakuelewa. Uchina wameliweza hili (SERIKALI YA KIJAMAA NA UMMAH WA KIBEPARI), na mpaka sasa naamini hata Marekani ilifanikiwa sana ilipotumia huu mfumo tokea mwaka 1933 hadi 1953. Huu mfumo kitaalamu tunasema, The Ownership is capitalist, but the Distribution of wealth is socialist. Roosevelt's New Deal made sure that, America as state was pursuing Market Forces, without leaving anyone behind, through a safety-net of the Welfare State.

Huwezi kujenga Ujamaa bila kuzingatia masoko yanasema nini. Mwishowe utapanga uchumi (Economic Planning) bila kuzingatia kwamba watu huwa wanabadilika hivyo uhitaji wa masoko hubadiliki, hasahasa katika utoaji wa huduma na uuzaji wa bidhaa. Urusi walipanga uchumi wao vizuri miaka ya 1970's (The Brezhnev Era) na ikakadiliwa kwamba ndani ya miaka 30 wanaweza kuwapita Wamarekani, ila wakaanguka vibaya. Msomi nguli kutoka Uingereza wa masomo ya Ujamaa Prof Anthony Giddens, ambaye aliwahi kuwa mshauri wa Waziri Mkuu wa Uingereza, Tony Blair anasema hivi:


"In hindsight, we can be fairly clear why the Soviet Union, far from surpassing the US, fell dramatically behind it, and why social democracy encountered its own crises. The economic theory of socialism was always inadequate, underestimating the capacity of capitalism to innovate, adapt and generate increasing productivity. Socialism also failed to grasp the significance of markets as informational devices, providing essential data for buyers and sellers. These inadequacies only became fully revealed with intensifying processes of globalization and technological change from the early 1970s onwards." The Third Way: Renewal of Social Democracy, Pg 4

Kuhusu hoja yako ya (SERIKALI YA KIJMAA NA UMMAH WA KIBEPARI), ambapo Serikali inatakiwa kuingilia uchumi wa kibepari ili mambo yasiharibike, Prof Giddens alienda mbali na kuchambua mfumo wa The Welfare State barani Ulaya, hasa kwenye nchi zinazofuata mfumo wa Social Democracy na kusema haya yafuatayo ambayo nanukuu:


"Social democratic regimes in practice have varied substantially, as have the welfare systems they have nourished. European welfare states can be divided into four institutional groups, all of which share common historical origins, aims and structures:
  • the UK system, which emphasizes social services and health, but tends also to have income dependent benefits.
  • Scandinavian or Nordic welfare states, having a very high tax base, universalist in orientation, providing generous benefits and well-funded state services, including health care.
  • Middle European systems, having a relatively low commitment to social services, but well-resourced benefits in other respects, financed mainly from employment and based upon social insurance contributions.
  • Southern systems, similar in form to the Middle European ones, but less comprehensive and paying lower levels of support.
Old-style social democracy saw free market capitalism as producing many of the problematic effects Marx diagnosed, but believed these can be muted or overcome by state intervention in the marketplace. The state has the obligation to provide public goods that markets cannot deliver or can do so only in a fractured way. A strong government presence in the economy, and other sectors of society too, is normal and desirable, since public power, in a democratic society, represents the collective will. Collective decision-making, involving government, business and unions, partly replaces market mechanisms. "

Hivyo Ujamaa utafanya kazi endapo utaruhusu masoko yafanye kazi yenyewe, huku serikali ikipewa nguvu ya kuhakikisha kwamba Ubepari hauvuki mipaka na kuvuruga taasisi za nchi. Hili ndilo Mengitsu alifanikiwa kulifanya kwenye baadhi ya taasisi za nchini Ethiopia kama sekta ya anga. Uchina nao wamefanikiwa sana kwenye hili kuliko nchi yoyote ile duniani, hadi kufikia hatua State Owned Enterprises (SOEs) zao zinatoa gawio kutokana na faida kubwa mno.

Yote haya yamewezekana kwasababu kisheria mifumo ya kitaasisi, inajiendesha yenyewe kitaalamu, bila wanasiasa kuingilia moja kwa moja. Hapa Tanzania tulifanya Ujamaa bila kuzingatia masoko. Tukaenda mbali na kutengeneza Mfumo wa kisheria (A Legal System) ambayo ilihakikisha kwamba watanzania hawawezi kujenga jamii ya kimasoko ambayo inazalisha bila kupewa maelekezo na serikali ambayo inapanga (Planning) kila kitu.

Ukishindwa kuelewa jinsi mfumo wa sheria wa Tanzania uliotengenezwa na Mzee Nyerere unavyoharibu na kuathiri mfumo mzima wa Uchumi wa nchi, utahisi kwamba kila kitu kiko sawa na kumzungumzia marehemu ni upumbavu. Lakini, ili tutoke hapa tulipo kama nchi ni lazima kufahamu haswa nini kilisababisha sisi kufika hapa, tatizo kubwa haswa ni lipi, na tunawezaje kujikwamua.
=================================================================

Like Dorian Gray, Tanzania's Government altogether with their populace are dysmorphic and scopophobic, they've never had the courage and boldness of staring at themselves at the mirror and appreciate their flaws. Nothing strikes a nerve to an ordinary Tanzanian like gazing at his own flaws and imperfections.
 

Acha kukariri mkuu
 
MIMI MWENYEWE NINA MASIKITIKO MAKUBWA SANA KUONA UWEZO WA WATANZANIA KATIKA KUELEWA MAMBO ...Mfano unakuta mtu anaponda Ujamaa au mwingine anaponda ubepari ! Huo ni ushahidi wa kukosa uwezo wa kiakili katika kufikiri .....ujamaa na ubepari ni vitu vyema tu kama utajua vinatakiwa kuwa katika FORMATION GANI ...KUNA FORMATION 4 ZA UJAMAA NA UBEPARI NAZO NI

1) SERIKALI YA KIBEPARI NA UMMA WA KIBEPARI
2) SERIKALI YA KIJAMAA NA UMMA WA KIJAMAA
3) SERIKALI YA KIBEPARI NA UMMA WA KIJAMAA
4) SERIKALI YA KIJAMAA NA UMMA WA KIBEPARI



Mfumo sahihi hapo ni NO 4 ...

Nyerere alijikwamisha kwa sababu alitumia mfumo NO 2...

Baada ya Nyerere akaja Mwinyi naye alikosea kwa kutumia mfumo NO 1 walio tumia mfumo NO 1 ni Kikwete ..Mkapa ..na sasa Samia ...mfumo huu huwa mbaya sana..


Kwa JPM alijitahidi kuipeleka nchi katika mfumo sahihi ambao ni mfumo NO 4
 
Kabisa ndugu, Nyerere alitengeneza mifumo kutokana na wakati uliokuwepo kuweka nchi kuwa na umoja nakuvuka vizingiti vya nyakati hizo. Sasa nijukumu letu kuchukua alipoishia na kutengeneza mifumo mipya kulingana na wakati huu wetu sisi. Sasa kuanza kumlaumu mzee miaka sijui mingapi ilopita wakati wewe huna uloweza Fanya kuleta changes ni aibu. Mwenzio alipambana na wakoloni wewe CCM tu wandengereko wenzio umewashindwa unaanza kumshushia mzee heshima. Nihuzuni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…