Tatizo la umeme: Awamu ya tano haiwezi kukwepa lawama labda tu kama madai hayana ukweli

Acheni upumbavu jamani!

Jk alikuwa na mgao wa umeme wa kufa mtu!

Magufuli hakuwa na mgao kabisa wa umeme...!

Samia kaingia tu tayari mgao, hebu twambieni huyu mnaemlaumu yeye alikuwa anatumia mitambo ipi?
Sio tu hakuwa na mgao pia alizima mitambo ya IPTL ya akina singa singa na rugemalila na walinyimwa leseni ya kuendesha biashara yao ya kuuzia umeme Tanesco.
Hizi blaah blaah za Waziri na wapambe ndio hujuma zile zimeshaanza ili kurejesha biashara ya IPTL ya kukusanya hela za kugawana kwenye viroba!
 
Vision ya Magufuli ilikuwa ni umeme wa bei nafuu wa maji ambao ungeongezea huu uliopo kwa kiwango kikubwa tu. Hata tungetengeneza wa gas ila wa maji uwepo kwanza!

Halafu kupungua kwa maji sio kosa sababu system ya hydropower inafanya kazi kwa kukusanya maji mengi sehemu moja kabla hayajaachiliwa kusukuma turbines kwenye poromoko!
 
Kuna kenge watakuja kukukejeli haya ndio mambo wengi hawaelewi! Magufuli hakuwa mjinga kama ambavyo wengi wanataka kuaminisha umma. When it came to infrastructures na project benefit analysis jamaa alikuwa ni mwamba.
 
Usimamizi mbovu
 
Kwahiyo sasa hivi haupigi mwingi
 
Kipindi cha magufuli umeme ulikuwa unakatika kama kawa ,thread zipo kibao humu ,sema ndiyo TANESCO wasingeweza kutangaza.
Unakatika ila sio kwa siku nzima au zaidi ya siku! Marekebisho ya muda mchache umeme unakuwa umerudi. Sababu ni za msingi kama ni transformer imebutuka replacement ya haraka watu wanaendelea na huduma.
 
We waache waneng'eneke tu..

Muda utaongea
 
Acha uongo Mimi naishi Tanzania usitete ujinga haitakusaidia
 
Unakatika ila sio kwa siku nzima au zaidi ya siku! Marekebisho ya muda mchache umeme unakuwa umerudi. Sababu ni za msingi kama ni transformer imebutuka replacement ya haraka watu wanaendelea na huduma.

Hapo sawa maana baadhi wanaconclude kwamba ulikuwa haukatiki kabisa.
 
Nani anapambana kumtetea?

Magu atajitetea mwenyewe kwa matendo yake.

Yani watu wameshindwa kutoa huduma ya umeme alafu lawama anatupiwa Magu ambae tulipata umeme wa uhakika kipindi chake chote?
 
Uzuri watanzania sio wajinga na wapumbavu kama bavicha
 
Tofauti, lakini yanatokea kipindi kimoja.....Why hayo matatizo yote yatokee kipindi kimoja? Kwa nini miaka yote hayajatokea kwa pamoja namna hii? Lazima kuna common cause inayounganisha hayo matatizo dunia nzima
Kukosa kwao umeme hakuhalalishi na sisi tukose umeme huku.

Hao sababu zao ni tofauti kabisa tena za kisomi, hizi za hapa kwetu ni za kipumbavu.
 
Kwa hiyo wewe unamwamini.nani akisema kuna kitu flani basi unamwamini lakini kwa tanzania huamini?
Binafsi, huwa siamini mwanasiasa yeyote na ndo maana posts zangu ni nadra sana ukute natoa reference kutoka kwa wanasiasa!!

Kinyume chake, naifahamu Power Master Plan, na kuna siku hapa niliweka sehemu yake!

Kwa mfano, baada ya kujenga bomba, ilitakiwa pajengwe vituo 4 vya kuzalisha umeme pale Kinyerezi kwa sababu gesi ilishavutwa!!

Katika vituo 4 hivyo, JK alijenga kituo kimoja, na kingine kikawa kwenye mchakato! Ilitarajiwa Magu akiingia amalizie vituo 3 vilivyobaki!! Hadi umauti unamkuta, alijenga kimoja TU ambacho tayari mchakato wake ulishaanza, vingine vyote akapiga chini na kuhamia kwenye Bwawa la Nyerere ambalo tulitakiwa KUANZA MWANZO!!

What do you expect?

Na ingawaje watu mnaleta masihara sana, hadi sasa umeme wa gesi ni 57% ya umeme WOTE uliopo kwenye grid ya taifa!! Ulishawahi kujiuliza endapo Magu angejenga vituo vyote, hivi sasa kungekuwa na umeme kiasi gani kwenye grid ya taifa?!

Huku mkishangilia umeme wa maji, huku mkidanganywa kwamba mgao wa wakati wa JK ulitokana na watu kuziba maji, lakini ukweli ni kwamba umeme wa maji ni 36.6% TU!

Hapa chini ni Ripoti ya Wizara ya Nishati zama za JPM....


Kumbe, ingawaje nchi ilikuwa inategemea zaidi umeme wa gesi, lakini bado tukatelekeza mradi wa ujenzi wa vituo vipya vya kuzalisha umeme pale Kinyerezi!!

Sasa unatarajia nini ile 36.6% tunayotegemea kutoka kwenye chanzo cha maji, inapokumbwa na changamoto ya ukame?! Au unakataa kwamba hakuna ukame?! Au unakataa kwamba vyanzo vya maji vimepungua?!

Na huyo aliyewahi kusema "tuna umeme mwingi" alizingatia kwamba kila siku wateja wapya wa umeme wanazaliwa, na matumizi ya umeme yanaongezeka?!
 
Sasa hiyo so ndo Kinyerezi II ambayo nimekuambia ndiyo alijenga JPM, bila shaka kwa sababu alikuta tayari mchakato umeshaanza!!

Je, Kinyerezi III na Kinyerezi IV ilishajengwa?
 
JPM, tuombee kwa Mungu, unatamani urudi duniani ila mapenzi ya Mungu yalishatimia. Ama kweli tunakukumbuka kwa mazuri.
 
Kukosa kwao umeme hakuhalalishi na sisi tukose umeme huku.

Hao sababu zao ni tofauti kabisa tena za kisomi, hizi za hapa kwetu ni za kipumbavu.
Sababu ipi ya kipumbavu? Ukisema sababu ya Climate change ya kipumbavu (Which means kutumia umeme wa maji ni upumbavu) then hoja ya Zitto ina mashiko
 
Kukosa kwao umeme hakuhalalishi na sisi tukose umeme huku.

Hao sababu zao ni tofauti kabisa tena za kisomi, hizi za hapa kwetu ni za kipumbavu.
Na ninaweza kusema kuwa ni Upumbavu wa CCM wote, kwani haiwezekani miaka 60 yote (Haijalishi nani alikuwa Rais au Serikalini) wameshindwa kutafuta chanzo kingine cha umeme zaidi ya hiki kimoja wanachokitegemea!! Ni upumbavu wa Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete na Magufuli pamoja na wasaidizi wao wote waliounda serikali zao!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…