KERO Tatizo la umeme kukatika limekithiri mkoa wa Mtwara

KERO Tatizo la umeme kukatika limekithiri mkoa wa Mtwara

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Hivi karibuni tatizo la kukatika kwa umeme mkoa wa Mtwara limekuwa kubwa na kero kwa wananchi.

Mkoa wenye gas asilia na makaa ya mawe lakini tatizo la umeme limekithiri. Najiuliza wakazi wa Mtwara wameongezeka kiasi kwamba Tanesco wanazidiwa au tatizo nini.

Umeme unaweza kukatika zaid ya mara tano ndani ya Lisa limoja alafu ni ile unakatika dk 1 unawaka dk inayofuata.

Ukirudi dk 10 nyingi unakatika tena yaani vifaa vya umeme vinaungua kila leo. Waziri mwenye dhamana na Serikali kwa ujumla liko ndani ya uwezo wenu kutatua hii kero.

Wanaoathirika ni wapiga kura wenu ambao hawana uwezo wa kununua majenereta.
 
Kumekuwa na changamoto ya umeme kukatika mara kwa mara Michiga -wilaya ya Nanyumbu Mtwara hasa nyakati za usiku kulala giza imekuwa kawaida , wakazi hatujui shida ni nini! Kama ni mgao tujue tu.
 
Back
Top Bottom