Tatizo la Yanga ni Engineer Hersi ..wamuangalie anawaangusha

Tatizo la Yanga ni Engineer Hersi ..wamuangalie anawaangusha

Timu imecheza mechi ngapi?wachezaji hawa wamekaa pamoja kwa muda gani?acha uchochezi bwana
Nani anayejipa kazi ya kuandaa timu kama sio wao GSM? Laiti kama angekuwa watu makini wangekuwa serious na uandaaji wa timu kwenye pre season kwa kujikita kutafuta mechi za kirafiki za kimataifa. Hao Azam tu wameenda Zambia na wamecheza mechi za kirafiki zaidi ya mbili ndio mpira unavyotaka sio blah blah za wiki ya mwananchi badala ya kuandaa timu.
 
Hivi Yanga mmempa kazi ya kusajili wachezaji na makocha huyu Engineer Hersi kwa kigezo kipi? Kwa sababu ukiangalia hana uzoefu wa kutosha katika sekta hii. Huyu mtu anasajili wachezaji almost wote free agents na mbaya zaidi ni wachezaji ambao asilimia kubwa sio wa kuweza kuipa yanga ubingwa.

KOCHA NABI:
Hivi ulikuwa na ulazima GSM na Hersi kumleta Coach ambaye hana uwezo wa kuzungumza kiengereza na mbaya zaidi hana uzoefu wa soka la Afrika mashariki. Huyu Kocha hana maajabu hata huko Al Merrikh walimfukuza baada ya mechi chache sana.
Binafsi naona ukanda wetu huu wa CECAFA bado tuna makocha wazuri sana .


Je, Yanga waliona kitu gani kwa kocha huyu asiyejua hata Kuongea na wachezaji?


WACHEZAJI :
Embu angalia wale wachezaji wa Yanga waliosajiliwa misimu hii yote tangu Hersi ameanza kusajili wengi hawadumu na wanabadilishwa kila msimu. Kifupi Yanga hawana kamati bora ya usajili zaidi ya kumtegemea Hersi.

Wachezaji wote wapya waliokwama kwa sababu wameondoka bila mazingira mazuri huko walipotoka. Hii ni ka sababu ni free agents na Klabu zimepuuzia kutoa vibali vyao mapema.

USHAURI:
1. Engineer Hersi abaki kama muwezashaji na suala la kusajili wachiwee watu wenye uzoefu.
2. Yanga watafute scouts ambao wanawalipa na wnaweza kupata wachezaji wazuri sana wa Kigeni na nafuu kuliko hawa mediocore wa AS VITA.
PhD ya Msolla ( Masikini ) haina Ubavu mbele ya mwenye Bachelor yake Hersi ( Tajiri )
 
Tatizo la Hersi ni ten percent,kala milioni 20 kwa mukoko na kisinda jumla 40 yule kipa mdaka mishale kapiga 15 hao nina ushahidi
 
IMG-20210915-WA0012.jpg
 
Tatizo kila anayejua kusoma,kuandika na kuongea ashakuwa Kocha,scounts muwekezaji yaani anajua kila kitu.Imefungwa Barcelona 8-0 itakuwa Yanga cha ajabu mno ni nini kama hujui mpira kaa kimya waache wanajua wawekeze ubaki kuwa mshabiki tu ....tusipende kuwakatisha taama watu kama Hersi mwisho tutakosa wanamichezo huko mbele sababu ya watu kama nyie
Sio kila anaye wekeza au kupenda soka ni mtu wa soka, mimi nakubaliana na mtoa mada Engineer Hersi sio mtu wa soka ingawa anapenda soka. Haya mambo yanawatu wake.
 
Timu imecheza mechi ngapi?wachezaji hawa wamekaa pamoja kwa muda gani?acha uchochezi bwana
Hilo ni kosa la nani sasa!!!!? Wanaoendesha timu wameshindwa kupanga mipango mizuri ndo mana unaona Nabi kupewa siku 25 za preseason badala ya wiki 6, walipeleka timu Morocco kufanya nini!?? Huu mwaka wa ngapi GSM yupo yanga, bado anajenga timu kila msimu wanasajili wachezaji wapya zaidi ya kumi unategemea nini!? Yanga ijifunze kwa Simba jinsi ya kuendesha timu inavyotakiwa sio kwenda na mihemko..
 
Back
Top Bottom