TBS: Kuanzia 01 Machi 2021, utaratibu wa kukagua magari kutoka nje ya nchi, utafanyikia hapa nchini

TBS: Kuanzia 01 Machi 2021, utaratibu wa kukagua magari kutoka nje ya nchi, utafanyikia hapa nchini

Panga Pangua, Anzisha, Bomoa...., kila siku ni kubadilisha badilisha
450908765.jpg
 
Kama ni mzoefu wa kuagiza magari, pamoja na gharama nyingine lakini pia kunakuwa na gharama ya ukaguzi, kwa Japan inakuwa around dola 100 mpk 300 kutegemea na gari. Na ilikuwa usipokuwa na cheti cha inspection unapigwa faini hapa bongo. Naona TRA wanazitaka hizo dola badala ya kuwaachia wajapan nk.

Lkn pia wale wajapan ili wafanye biashara walikuwa wana customize vyeti vya ukaguzi vyote vinakuwa qualified hata kama gari halistahili kwa matumizi ya binadamu na mazingira.
 
Mi sioni cha ajabu hapa.
Kwa kuwa, hata sasa hivi ukiagiza gari kutoka Japan, lazima likaguliwe, na utalipia gharama ya kukaguliwa na kampuni ambayo imepata kibali kutoka Tanzania. Tena unalipa kwa $ kati $100 hadi $300 kama mdau alivyosema hapo juu.

Kilichobadilika ni kuwa badala ya kulipia na kukaguliwa Japan, sasa utalipia na kukaguliwa hapa.

Mi naona ni jambo nzuri. Kwanini tuiingizie hela ya ukaguzi Japan badala ya hiyo hela ibaki Tanzania?

Kwanini uangaike ku badilisha hela ya TSh kwenda $ kwa ajili ya kulipia ukaguzi Japan ambapo $ ni gharama badala ya kulipia kwa TSh?
 
Shirika la Viwango Tanzania (TBS) linawataarifu waagizaji na wauzaji wa magari kutoka nje ya nchi kuwa kuanzia tarehe 01 mwezi Machi, 2021, utaratibu wa kukagua magarikutoka nje ya nchi utafanyika baada ya kuwasili hapa nchini (Destination Inspection).Hivyo,magari yote yatakayosafirishwa kuanzia tarehe tajwa hapo juu yatakaguliwa katika bandari yaDar-es-Salaam.

Kwa sasa TBS inakagua magari kutoka nje ya nchi kupitia mawakala watatu(3) kutoka Japan na mmoja(1) kutoka Dubai ambao mikataba yao itakoma hivi karibuni.

Hivyo vyeti vya ukaguzi vitakavyotolewa na mawakala tajwa kwa magari yatakayosafirishwa kuanzia tarehe 01 mwezi Machi, 2021 havitatambulika na TBS.

Aidha,magari yatakayopimwa bandarini na kutokidhi matakwa ya kiwango yatahitaji kufanyiwa matengenezo nje ya bandari na kisha kuletwa na kupimwa tena kwenye yadi ya UDA mkabala na Bandari ya Dar es salaam.

Shirika litaendelea kuhakikisha kuwa magari yote yaliyotumika nakuingizwa nchini yanakidhi matakwa ya kiwango cha magari yaliyotumika.

Kwa taarifa zaidi kuhusu utaratibu huu mpyausisite kuwasiliana na:-

Mkurugenzi Mkuu,

Shirika la Viwango Tanzania (TBS),

SLP 9524,

Dar es Salaam.
View attachment 1682017

Wanatanua wigo wa kukusanya kodi.
 
Mi sioni cha ajabu hapa.
Kwa kuwa, hata sasa hivi ukiagiza gari kutoka Japan, lazima likaguliwe, na utalipia gharama ya kukaguliwa na kampuni ambayo imepata kibali kutoka Tanzania. Tena unalipa kwa $ kati $100 hadi $300 kama mdau alivyosema hapo juu.

Kilichobadilika ni kuwa badala ya kulipia na kukaguliwa Japan, sasa utalipia na kukaguliwa hapa.

Mi naona ni jambo nzuri. Kwanini tuiingizie hela ya ukaguzi Japan badala ya hiyo hela ibaki Tanzania?

Kwanini uangaike ku badilisha hela ya TSh kwenda $ kwa ajili ya kulipia ukaguzi Japan ambapo $ ni gharama badala ya kulipia kwa TSh?
Sema itasababisha msongamano mkubwa na hivyo kuchelewesha clearance ya magari
 
Mi sioni cha ajabu hapa.
Kwa kuwa, hata sasa hivi ukiagiza gari kutoka Japan, lazima likaguliwe, na utalipia gharama ya kukaguliwa na kampuni ambayo imepata kibali kutoka Tanzania. Tena unalipa kwa $ kati $100 hadi $300 kama mdau alivyosema hapo juu.

Kilichobadilika ni kuwa badala ya kulipia na kukaguliwa Japan, sasa utalipia na kukaguliwa hapa.

Mi naona ni jambo nzuri. Kwanini tuiingizie hela ya ukaguzi Japan badala ya hiyo hela ibaki Tanzania?

Kwanini uangaike ku badilisha hela ya TSh kwenda $ kwa ajili ya kulipia ukaguzi Japan ambapo $ ni gharama badala ya kulipia kwa TSh?
Mpumbavu
 
Shida sio ukaguzi maana hata kabla magari yalikuwa yanakaguliwa kabla ya kuwa shipped. Tatizo litakuwa ukiritimba, lazima kubambikiwa, kulipishwa X2 na kucheleweshewa huduma vitakuwa vipaumbele vyao.

Tutaona!
 
Nachokiona hapa ni urasimu kuongezeka pamoja na ucheleweshwaji wa magari na wizi wa vifaa kama yatakaguliwa uchochoroni.

Gharama nayo ni heri iwekwe public watu wajiandae mapema.

Nimeona kuna wakala wao ana-charge $295 kwa ajili ya pre-ship inspection huko Japan, hope nao hawatakuwa mbali na hapo.
 
Hapa naona vitu vifuatavyo;

1. Hata kama gari itakuja nzima, utaambiwa ni mbovu. Linatakiwa likatengenezwe. Kuna vifaa vitachomolewa halafu utavikuta kwenye garage zao uuziwe mara ya pili.

2. Watalazimisha wapeleke garage zao. Bei zitakuja za ajabu. Usishangae ukaambiwa ulipe 500K kwa kitu ambacho ungetengeneza kwa 200K.
IMG_ul14fj.jpg
 
Back
Top Bottom