TCRA: Laini zote ambazo hazijasajiliwa kwa namba za NIDA zitafungwa kufikia Desemba 31, 2019

TCRA: Laini zote ambazo hazijasajiliwa kwa namba za NIDA zitafungwa kufikia Desemba 31, 2019

Kulikuwa na haja ya taasisi hizi mbili (NIDA na TCRA ) kukaa pamoja ili kuona namna kuendesha zoezi pamoja kabla kutangaza tarehe ya mwisho, kuliko wanavyopishana kama ziko chini ya serikali mbili tofauti
 
Mamlaka hiyo imesema kwamba hakuna laini ya simu itakayofungwa kabla ya tarehe hiyo.

Aidha, imesema wananchi wanatakiwa kwenda kusajili laini zao kwa kutumia vitambulisho vya uraia, na kuthibitisha usajili huo kabla ya muda uliowekwa kwa kuwa hakutakuwa na mabadiliko ya kuzifunga.

Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu, Kaimu Meneja Mawasiliano wa TCRA, Semu Mwakanjala, alisema hadi sasa laini za simu milioni 20 zimesajiliwa.

“Hakuna mabadiliko yaliyotolewa ikifika Disemba 31, mwaka huu, laini zote ambazo hazijasajiliwa kwa namba ya Nida (Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa) na kuthibitisha kwenye mifumo zitafungwa, tunawakata wananchi wasajili haraka,” alisema.

Aidha, alisema hakuna mtoa huduma atakayeruhusiwa kufunga au kukatisha mawasiliano ya mtumiaji yeyote kabla ya muda uliopangwa.

Jana kwenye baadhi ya makundi songezi (WhatsApp) baadhi ya watumiaji wa laini za simu walilalamika kukosa mawasiliano kwenye baadhi ya laini kwa kile kilichoelezwa kuwa zimezimwa kwa kuwa hawajasajili.

Mei mwaka jana, serikali ilitangaza ulazima wa usajili wa laini za simu, na kwamba ifikapo mwishoni mwa mwaka huu zitafungwa.

IPP Media

Kwanini wasiruhusu hata hizi Passport mpya kutumika kusajiri laini. Kuna fingerprint there. Itasawasaidia walioko nje kusajiri laini zao, kuwa na mawasiliano wakifika Tanzania instead of waiting three weeks bila simu.
 
Back
Top Bottom